Uchaguzi 2020 CHADEMA yatangaza kusudio la kuweka Mgombea Urais wa Zanzibar

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,601
217,993
TAMKO LA KUTANGAZA NIA KUWANIA NAFASI YA RAIS WA ZANZIBAR KUPITIA CHAMA CHA DEMO ( 425 X 640 ).jpg

Taarifa hii imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho upande wa Zanzibar Mh. Salum Mwalimu Mjini Zanzibar alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari.

=====

TAMKO LA KUTANGAZA NIA KUWANIA NAFASI YA RAIS WA ZANZIBAR KUPITIA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatangaza kusudio la kusimamisha mgombea katika nafasi ya Rais wa Zanzibar katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu na hivyo inafungua milango kwa wanachama wake wenye sifa kutangaza nia.

Hii ni mara ya kwanza kwa CHADEMA kutangaza rasmi kuweka mgombea katika nafasi hiyo ya juu ya nchi kwa upande wa Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar Salum Mwalim ametoa tangazo hilo katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika leo Jumamosi June 06, 2020 katika Ofisi Kuu ya Chadema , Kisiwandui Zanzibar.

“Tunawatangazia rasmi wanachama wetu wenye sifa na ambao wana nia ya kugombea nafasi ya Urais wa Zanzibar waandike kwa Katibu Mkuu wa chama na kuwasilisha barua hizo ofisi ya Makao Makuu Zanzibar wakati wowote kuanzia leo hadi Juni 15, 2020 Saa Kumi na Nusu Alasiri”

“Chama kimejipima na kutafakari kwa kina na kimeona kwamba sasa ni wakati mufaka kuwapa nafasi wanachama wake wenye ndoto na uwezo wa kugombea nafasi hiyo kutimiza ndoto zao”

Kwa sasa ni kutanga nia zao kwa chama na kwamba baada ya hapo utafuata mchakato wa uchukuaji wa Fomu za ndani ya chama ambapo maelekezo yake pamoja na utaratibu mzima utakaofuata utatolewa baadae. Kwa watakaowasilisha taarifa zao wataruhusiwa kutangaza kusudio lao hilo kwa Umma kupitia vyombo vya habari.

Chama kinawahimiza wanachama wote wenye Sifa, Vigezo na Maadili kama ilivyoanishwa kwenye Kanuni za chama Sura ya Kumi (10) katika Katiba ya Chama ya Mwaka 2006 Toleo la 2016 na matakwa ya Katiba ya Zanzibar kujitokeza.
”Niwatake wanachama wetu wote kufuguliwa kwa mlango huu usiwe chanzo cha kuvuruga umoja na mshikamano ambao umekuwa thabiti ndani ya chama chetu Zanzibar.”

Pamoja na tangazo hili, chama chetu kipo tayari kuendeleza ushirikiano na vyama na kulinda nia na shabaha ya ushirikiano huo bila kuathiri malengo ya vyama vyetu kwa masilahi ya kila M-Zanzibari katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Aidha, tunaendelea kuwasisitiza wanachama wetu walioonesha nia ya kugombea nafasi za Udiwani, Uwakilishi na Ubunge kwa Unguja na Pemba kuendelea na taratibu za chama na kwamba milango bado ipo wazi kwa ambao bado hawajafanya hivyo.

Chama kinawatakia kheri wanachama wake, pamoja na wafuasi na wapenzi na kwa pamoja tunawataka kuendelea kujipanga kukiletea chama ushindi katika uchuguzi Mkuu wa Oktoba .

Imetolewa na:
Ofisi ya Naibu Katibu Mkuu
Zanzibar
 
Wasisahau kuwa sas hivi tume ipo chini ya TISS- uvccm ambao wote ni chato die hard. Mwaka huu atakayetoboa ujue ni kidume. Magu atakuwa anagaw majimbo kama karanga. Na wakishajazana bungeni watakuambia chaguo la Mungu libadilishiwe katiba.
 
Ha ha ha chadema Zanzibar kina mwanachama mmoja tu tapeli salum Mwalimu mkazi wa kinondoni dar es salaam naibu katibu mkuu chadema Zanzibar mkazi wa kinondoni Dar es Salaam aliyewahi gombea ubunge Kinondoni Dar es Salaam
 
Wasisahau kuwa sas hivi tume ipo chini ya TISS- uvccm ambao wote ni chato die hard. Mwaka huu atakayetoboa ujue ni kidume. Magu atakuwa anagaw majimbo kama karanga. Na wakishajazana bungeni watakuambia chaguo la Mungu libadilishiwe katiba,
Bila tume huru, taratibu, na uwanja sawa wa kisiasa, upinzani hauambulii kitu.
 
Nilikuwa nakukumbusha tu kwamba dhambi ya ubaguzi haijawahi kumwacha mtu salama , Lyatonga Mrema alishawahi kuwa mbunge wa Temeke baada ya kumshinda mvaa Hereni aliyekuwa ofisa wa ikulu
Safari hii Mbowe mkazi wa kinondoni mwambieni Hana chake hai ubunge asahau
 
Ha ha ha chadema Zanzibar kina mwanachama mmoja tu tapeli salum Mwalimu mkazi wa kinondoni dar es salaam naibu katibu mkuu chadema Zanzibar mkazi wa kinondoni Dar es salaam aliyewahi gombea ubunge kinondoni dar es salaam
Itakuwa aibu Kubwa sana na hapo eti salumu mwalimu ndio akagombee
 

Taarifa hii imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho upande wa Zanzibar Mh. Salum Mwalimu Mjini Zanzibar alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari.

NOTE : nafasi ya ushirikiano na vyama vingine makini vyenye nia ya dhati ya kung'oa ccm madarakani ingali bado ipo.
Tatizo cdm wabinafsi sana. Wanajiona wao ndio wapinzani wakati wasaanii watupu
 
Safari hii Mbowe mkazi wa kinondoni mwambieni Hana chake hai ubunge asahau
Awamu hii akileta makanyagio yake Hai lazima tumpopoe mawe. Japo kaanza kuwaweka sawa viongozi wa makanisa ya kilutheri.
Hai leo kuna maeneo maji tunapata kwa wiki mara moja. Mbunge wetu wa kutusemea shida zetu ye yupo zake Dar.
 
NI VIZURI WANGEUNGANA NA ACT ILI KUWA NGUVU MOJA
Chadema wajinga CUF iliamua kuungana na chadema sababu CUF walikuwa na nguvu Sana Zanzibar lakini Tanzania bara hawakuwa ma nguvu wakasacrifice Duni Haji ajiunge chadema ili chadema iwe na nguvu Zanzibar na CUf iwe na nguvu bara

Matokeo Baada ya chadema kupata wabunge wengi kikaota ndevu na kuanza dharau kwa waliowafikisha Hapo walipo akiwemo Lowasa na Seif na Duni Haji hawakujua kuwa muungano wa Lowasa na Seif sharriff Hamd ulikuwa muungano wa the CCM frustrated people .Seif alitimuliwa CCM Na Lowasa akapigwa chimi CCM kugombea uraisi mmoja akawa Chadema Lowasa the fristrated akaungana na the frustrated mwingine wa CUF maslim.Seif kuunga alliance ya kuipiga chini CCM ambayo wanahisi iliwafrustarate ndoto zao hewa wakitumia UKAWA Kama fimbo!!!

Kilichotokea walikuwa fustrated more kupindukia kwenye uchaguzi mkuu na ndani ya vyama walivyokuwa vya CUF na Chadema!!
Seif na Duni Haji na wafuasi wao wakatimka alliance ya chadema na kukimbilia ACT wazalendo kwa Zitto Kabwe ambaye alitimuliwa na chadema !!!

Sahau ACT wazalendo kuungana na chadema sababu wote mliwaumiza Chadema kuanzia Zitto Kabwe ,Duni Haji nk pambaneni na hali zenu . Chadema Wana short sighted leaders !!! Safari hii mtatupwa nje.Nobody wants to join you matapeli nyie wa kisiasa
 

Taarifa hii imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho upande wa Zanzibar Mh. Salum Mwalimu Mjini Zanzibar alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari.

NOTE : nafasi ya ushirikiano na vyama vingine makini vyenye nia ya dhati ya kung'oa ccm madarakani ingali bado ipo.
"Nafasi ya ushirikiano na vyama vingine makini ingali ipo" Mh ina maana mlichotufanyia tukiwa Ukawa hatukijui?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom