Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Jaji Othman, awe chachu ya mabadiliko ya Katiba mpya - CHADEMA
na Janet Josiah
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman, kuendeleza mapambano ya kudai na kuandikwa kwa Katiba mpya ambayo katika kipindi hiki imezua mjadala mkali. Jaji Othman aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, juzi na kuapishwa jana katika viwanja vya Ikulu, kuchukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhan, ambaye anastaafu kwa mujibu wa sheria kuanzia leo.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, Erasto Tumbo, alisema chama chao kinaamini kuwa Jaji Othman ataendeleza mjadala huo kama alivyouanza Jaji Ramadhan ambaye alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa umefika wakati sasa Watanzania wakatoa maoni kuhusu uwepo wa Katiba mpya.
CHADEMA inamtaka Jaji Othman asiwe kikwazo katika mjadala huo, ila inamtaka awe msaada katika zoezi hili linaloendelea ili kuwapa Watanzania haki yao ya msingi ambayo tunaamini wameidai kwa muda mrefu, alisema Tumbo.
Tumbo alisema kutokana na wadhifa mkubwa aliopewa na Rais kama Jaji Mkuu wa Tanzania na kuongoza mahakama kama mhimili wa tatu wa dola, anayo kila sababu ya kukabiliana na changamoto alizozikuta ukiwamo mjadala huo.
Alisema miongoni mwa changamoto hizo ni ile ya mahakama kufanya maamuzi ya kukubali kuwepo kwa mgombea binafsi, hoja ambayo ilimfanya Jaji Ramdhan apate kigugumizi na kuirudisha bungeni ambako ilishindikana.
Kabla ya uteuzi huo Jaji Othman alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa na mtetezi wa Haki za Binadamu Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.
Jaji Othman alizaliwa Januari Mosi, 1952 na ana shahada ya kwanza ya sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na shahada ya uzamili (MA) kutoka Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.
Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.
na Janet Josiah
Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, Erasto Tumbo, alisema chama chao kinaamini kuwa Jaji Othman ataendeleza mjadala huo kama alivyouanza Jaji Ramadhan ambaye alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa umefika wakati sasa Watanzania wakatoa maoni kuhusu uwepo wa Katiba mpya.
CHADEMA inamtaka Jaji Othman asiwe kikwazo katika mjadala huo, ila inamtaka awe msaada katika zoezi hili linaloendelea ili kuwapa Watanzania haki yao ya msingi ambayo tunaamini wameidai kwa muda mrefu, alisema Tumbo.
Tumbo alisema kutokana na wadhifa mkubwa aliopewa na Rais kama Jaji Mkuu wa Tanzania na kuongoza mahakama kama mhimili wa tatu wa dola, anayo kila sababu ya kukabiliana na changamoto alizozikuta ukiwamo mjadala huo.
Alisema miongoni mwa changamoto hizo ni ile ya mahakama kufanya maamuzi ya kukubali kuwepo kwa mgombea binafsi, hoja ambayo ilimfanya Jaji Ramdhan apate kigugumizi na kuirudisha bungeni ambako ilishindikana.
Kabla ya uteuzi huo Jaji Othman alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa na mtetezi wa Haki za Binadamu Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.
Jaji Othman alizaliwa Januari Mosi, 1952 na ana shahada ya kwanza ya sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na shahada ya uzamili (MA) kutoka Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.
Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.