CHADEMA yashtuka kampeni chafu

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
CHADEMA yashtuka kampeni chafu


na Mwandishi Wetu



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetamba kunasa mtandao mpana unaoundwa na kundi la wanasiasa, wakiwamo wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na baadhi kutoka kambi ya upinzani, waliojiunga pamoja kukisambaratisha chama hicho.

Habari ambazo Tanzania Daima imezinasa kutoka ndani ya chama hicho cha upinzani zinaonyesha kwamba, tayari viongozi wakuu wa juu wa chama hicho cha upinzani wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, wameanza kufanya vikao vya siri wakikutana na watu mbalimbali wa ndani na nje ya chama hicho ili kuweza kukabiliana na mtandao maalumu ulioundwa kwa ajili ya kufanikisha ajenda hiyo.

Kwa mujibu wa habari hizo ambazo zimethibitishwa na mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu, zinaeleza kwamba tayari hatua kadhaa za kisiasa, kiutawala na kisheria zimeshaanza kuchukuliwa ili kudhibiti mpango maalumu wa siri unaoratibiwa na baadhi ya wanasiasa kutoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ndani ya kambi ya upinzani.

Habari zaidi zinaeleza kwamba moja ya sababu ya kuanza kuibuka kwa mkakati huo ni ushindani mkali wa kugombea kiti cha ubunge cha Tarime ambacho kiko wazi baada aliyekuwa akikishikilia, Chacha Wangwe (CHADEMA), kufariki dunia katika ajali ya gari mwishoni mwa mwezi uliopita.

Lissu, mmoja wa wanaharakati maarufu nchini, aliieleza Tanzania Daima jana kwamba, walikuwa wamefanikiwa kupata vielelezo kadhaa ambavyo wanakusudia kuvitumia ili kukabiliana na kishindo cha kundi hilo alilolitita kwa jina moja tu la ‘mtandao’, ambalo limejitoa mhanga kukimaliza chama hicho.

Kwa mujibu wa Lissu, mkakati wa kwanza ambao kundi hilo la mtandao limeamua kuutumia kuisambaratisha CHADEMA ni kwa kuanza kumpaka matope Mwenyekiti wao, Mbowe, na kumhusisha na kashfa za kila aina ili kumwondolea heshima kubwa aliyojijengea katika jamii kwa muda mrefu sasa.

‘‘Tumeshabaini mkakati mzima wa kutusambaratisha. Utakumbuka hawa jamaa walianza kumchokonoa Mwenyekiti (Mbowe) wakati ule walipomhusisha na deni la NSSF, wakakwama, baada ya hapo wakajaribu kutumia uamuzi wa chama kumsimamisha umakamu mwenyekiti marehemu Wangwe kutuvuruga, wakakwama pia. Sasa wamekuja na mbinu chafu ya kujaribu kukihusisha chama chetu na ajali na hatimaye kifo cha Wangwe, wakitumia hoja dhaifu na za kupikwa,” alisema Lissu.

Habari zaidi ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka ndani ya CHADEMA zinaonyesha kwamba, mbali ya mkakati huo wa siri kuhusisha makada maarufu wa CCM, kimebaini pia kuwapo kwa kundi la wanasiasa wachache wanaotoka katika vyama viwili vya siasa vya NCCR-Mageuzi na Tanzania Labour (TLP) (majina na nyadhifa zao tunazo), ambao nao wanatajwa kushirikiana na makada maarufu wa CCM katika kufanikisha mpango wa kuisambaratisha CHADEMA.

Taarifa za maandishi ambazo gazeti hili limeziona zinaeleza kwamba, chama hicho kimeweza kunasa mawasiliano na mazungumzo ya siri ambayo yalifanywa na viongozi wawili wa juu wa TLP na mhariri mmoja mwandamizi hivi karibuni, yaliyopangwa kuchapwa kwa namna ya kupindishwa katika gazeti moja la kila wiki linalotoka kesho Alhamisi.

‘‘Tunaweza kusema kwa uhakika kwamba tumenasa mazungumzo kati ya mhariri wa gazeti hilo la kila wiki na viongozi wawili wa juu wa chama cha ....(kinatajwa), yaliyofanyika nyumbani kwa mmoja wa viongozi hao ambayo yalijaribu kuzungumzia madai yanayomhusisha mwenyekiti (Mbowe) na kile kinachoitwa sherehe aliyofanya eti kusherehekea kifo cha Wangwe...suala hili linapaswa kukabidhiwa kwa wanasheria wetu ili walifanyie kazi na ikibidi kuchukua hatua za mara moja za kisheria dhidi ya wahusika hawa,’’ ndivyo linavyosomeka dokezo moja.

Tanzania Daima ilipowasiliana na Mbowe mwenyewe ili kujua iwapo alikuwa anazo taarifa hizo, hakuwa tayari kusema lolote zaidi ya kumweleza mwandishi wa habari hizi: ‘‘Tumejipanga sawasawa kuwaeleza Watanzania ukweli wote kuhusu mambo haya yote, ili wajue ni kitu gani kinafanyika, ni kina nani wanafanya na malengo yao ni yapi.”

Wakati CHADEMA ikikabiliana na tuhuma hizo zinazoelekezwa kwake, chama hicho kimeandika barua kwenda kwa Kituo cha Demokrasia (TCD) kikilalamikia habari zilizoandikwa na baadhi ya magazeti Jumapili iliyopita ambayo yaliandika habari za kumhusisha Mbowe na taarifa za kusherehekea kifo cha Wangwe.

Katika barua hiyo ya juzi Jumanne iliyosainiwa na Anthony Komu, ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya TCD, CHADEMA inaitaka taasisi hiyo kueleza ukweli wa kile kilichotokea nchini Afrika Kusini mara tu baada ya Mbowe kupata taarifa za msiba wa Wangwe.

Pamoja na mambo mengine, CHADEMA imeitaka TCD kuwaita wanasiasa wote waliokuwa katika ziara hiyo iliyoandaliwa na taasisi hiyo kuitwa na kueleza ukweli wa kile kilichotokea na iwapo kulikuwa na ukweli katika maelezo yanayodaiwa kutolewa na kiongozi mmoja wa TLP, Richard Lyimo, anayedaiwa kumwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) akilalamikia kile anachokieleza kuwa mwenendo wa Mbowe baada ya kupata taarifa za msiba wa Wangwe.

Wakati hayo yote yakitokea, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza nafasi za uchaguzi mdogo na ubunge katika Jimbo la Tarime, iliyoachwa wazi baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Wangwe.

Mbali ya uchaguzi huo, NEC pia imetangaza uchaguzi mdogo wa madiwani katika jimbo hilo, sambamba na chaguzi nyingine ndogo ndogo katika halmashauri na kata 33, katika mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mkurugenzi wa NEC, Rajabu Kiravu, alisema NEC imefikia hatua ya kuandaa uchaguzi mdogo katika Jimbo la Tarime baada ya kupokea taarifa rasmi kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, kuwa jimbo hilo liko wazi.

Kiravu alisema kwa mujibu wa sheria za uchaguzi, uchaguzi mdogo wa ubunge unatakiwa ufanyike baada ya siku 20 na isizidi 50 wakati uchaguzi mdogo wa madiwani, isizidi siku 30.

Kutokana na hali hiyo, Kiravu alisema tume imeandaa taratibu za uchaguzi katika Jimbo la Tarime, ambako Septemba 13, utafanyika uteuzi wa wagombea, wakati kampeni zitaanza Septemba 14 hadi Oktoba 11, mwaka huu na uchaguzi utafanyika Oktoba 12.

Akizungumzia chaguzi za kata, Kiravu alisema tume ilipokea taarifa za awamu mbili toka kwa waziri anayeshughulikia serikali za mitaa kuwepo kwa nafasi wazi katika kata 33 nchini.

Kiravu alisema taarifa ya awamu ya kwanza ilihusu kata 23, ambako uchaguzi wake utafanyika Septemba 21 mwaka huu.

Alizitaja halmashauri zitakazohusika katika uchaguzi huo na kata zake katika mabano kuwa ni pamoja na Mpanda (Katuma), Sengerema ( Nyamazugo, Busisi, Bupandwa), Geita (Kagu) Ukerewe (Bukindo) Muleba (Kibanda), Ngara (Kabanga) Bahi (Mundemu), Kigoma ( Nguruka) Urambo (Ushokora) Tabora (Ng’ambo, Malolo) Maswa ( Ipililo) Mvomero (Langali) Morogoro (Mtombozi) Manyoni (Kintiku) Songea (Wino) Tanga (Chongoleani Ngamiani Kati), Nachingwea ( Naipanga, na Nditi) pamoja na Tandahimba (Mahuta).

Alisema taarifa ya pili iliyohusu kata 10, uchaguzi wake utafanyika Octoba 12. Uchaguzi huo utafanyika Monduli ( Monduli juu na Elisalei) Singida ( Utemini) Serengeti ( Kisangura), Moshi ( Uru Mashariki) Magu ( Sukuma), Ludewa (Lupingu), Arusha ( Sombetini), Ludewa ( Lupingu), Arusha Mjini ( Sombetini), Mbarali (Rujewa) pamoja na Korogwe (Mnyuzi).

Aidha, Tume imetangaza watakaojaza nafasi za viti maalumu kuwa ni pamoja na Bura Venosa Stephano (Hanang), Anna Isikaka Sibajaje, (Mbeya), Neema Issa Nassoro (Arusha), Salima Abdul Mutungi (,Biharamulo), Theresia Peter Mushi (Moshi Mjini), Monica Shello Luvanda (Mufindi).

Wakati huo huo, Kiravu alisema tume imeendelea na zoezi lake la kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura na mpaka sasa mikoa 12, tayari imekamilisha kazi hiyo.

Alisema kwa sasa zoezi hilo linafanyika katika mikoa ya Shinyanga na Mara wakati mikao ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Dar es Salaam, uboreshaji wake utafanyika Septemba na Oktoba na kabla ya kazi hiyo kuhamia visiwani Zanzibar.
 
Kampeni chafu ni sehemu ya siasa,unapokuwa na madhaifu yako wenzio watayatumia vema kujinufaisha na kuyatangaza ipasavyo.
 
Kampeni chafu ni sehemu ya siasa,unapokuwa na madhaifu yako wenzio watayatumia vema kujinufaisha na kuyatangaza ipasavyo.

Siasa si mchezo mchafu ila inalazimishwa iwe hivyo na watu wenye nia zao mbaya. Kama ingekuwa ni kitu cha mchezo tu kisingekuwa kinasomewa na watu kugraduate.

Nakubaliana na wewe kuwa mtu anaweza kutumia weakness zako kukushambulia lakini hizo weakness ziwepo zisiwe za kutunga thats why hata mimi nawasupport chadema kwa kutambua kuwa kuna watu wana nia mbaya nao na sasa wanachukua hatua. Tena wamechelewa they have to act fast.

Maana penye ukweli utajionyesha tu.
 
Kampeni chafu ni sehemu ya siasa,unapokuwa na madhaifu yako wenzio watayatumia vema kujinufaisha na kuyatangaza ipasavyo.

Do we need kampeni chafu kwa manufaa ya wachache na kuacha Taifa lina angamia ? Kwa nini kuwekwe uchafu wa kampeni hizo pasipo na sababu ya maana ?

Nadhani Chadema must come clean kwenye hili mapema na wazidi kujjikita katika kufahamika na wajipange na uchaguzi mkuu na chaguzi zingine
 
MWENYEKITI wa TLP, Augustino Lyatonga Mrema juzi alikuwa kivutio katika mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mbeya Vijijini kwa tiketi ya CUF, Daudi Mponzi uliofanyika kwenye kiwanja cha stendi ya mabasi cha Mbalizi alipodai kuwa wamejitakia maisha ya shida kwa kuichagua CCM.


Alikuwa akihutubiua kwenye mkutano uliofurika mamia ya watu na kuhudhuriwa na viongozi wa vyama vinne vya siasa vya TLP na PPT Maendeleo ambavyo vimeamua kuungana na CUF kumpigia kampeni mgombea wake ili anyakue jimbo hilo lililoachwa wazi baada ya Richard Nyaulawa (CCM) kufariki mwishoni mwa mwaka jana.


Wananchi hao walianza kuonyesha kuvutiwa na Mrema mara aliposimama jukwaani wakati alipomshangilia na kupiga kelele kuonyesha kumkubali na bila kuchelewa waziri huyo wa zamani wa mambo ya ndani alianza hotuba yake kwa kuwaambia wananchi kuwa shida na maisha magumu waliyonayo wamejitakia.


"Hizi shida mnajitakia wenyewe msimlaumu Mwenyezi Mungu kwani Mungu amefanya kazi ya kuwaumba, lakini nyie mmefanya kazi ya kuichagua CCM na ndiyo maana mnabaki na malalamiko ya kusema 'Mungu nisaidie maisha ni magumu'. Naomba niwasisitizie kuwa hili si kosa la Mungu, ni kosa lenu kwa kuchagua chama ambacho kimejaa propaganda," alisema.


Mrema aliendelea kuwavutia wananchi hao aliposema kuwa alipokuwa naibu waziri mkuu alifanya kazi zake vizuri, ikiwa ni pamoja na kukamata ndege iliyokuwa na dhahabu zenye thamani ya Sh175 milioni, lakini waziri mkuu wa wakati huo hakufanya lolote zaidi ya propaganda.


Alisema kuwa ameamua kuiunga mkono CUF kwa sababu watendaji wake ni majasiri na wana uwezo mkubwa na kwamba CUF ni chama cha ukombozi hivyo kinastahili kuungwa mkono na wananchi wote, ikiwa ni pamoja na wa Mbeya Vijijini ambao alisema wanatakiwa kumpa kura za Mponzi.


Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa wananchi wa Mbeya Vijijini wana nafasi ya kubadilika na kumchagua mgombea wa CUF kuwa mbunge wa jimbo la Mbeya vijijini ili maisha yao yaweze kubadilika .
 
Last edited by a moderator:
Vita ya maneno CUF, Chadema tete H
Hussein Kauli

VITA ya maneno baina ya Chama cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) vimezidi kuingia katika hatua tete baada ya CUF kuwatuhumu wenzao kuwa ni chama kibaraka.


Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika jana kwenye viwanja vya Manzese Bakhresa, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa CUF, Ismail Jussa aliituhumu Chadema kuwa harakati zake za kupinga ufisadi hazina ukweli wowote.


"Masuala ya ufisadi wa rada, ununuzi wa ndege ya rais pamoja na suala la kampuni hewa ya ufuaji umeme nchini ya Richmond hayakuanza leo, bali yalikuwapo tangu utawala wa awamu ya tatu, lakini Chadema imeshupalia suala la ufisadi huku ikionekana kuwatetea mafisadi," alisema Jussa.


Alitoa mfano kuwa katika wakati huu wa vita dhidi ya mafisadi, mmoja wa wabunge wa chama hicho alipeleka gari mahakamani, ili likamsaidie usafiri mmoja wa watuhumiwa wa kesi za ufisadi.


Pia alidai kuwa mwenyekiti wa chama hicho alipopata safari za nje ya nchi mwaka 2008 ambaye aliambatana na mjumbe wa CUF, Mustafa Wandwi, katika safari hiyo alidai mwenyekiti huyo alimshawishi ajiunge na chama chake kwa kumuahidi kiasi cha Sh1 milioni.


Alihoji kama Chadema inarubuni watu kwa fedha ili wajiunge na chama chao, basi haiwezi kupambana na ufisadi sababu ni chama fisadi. Wakati huohuo, CUF imeishutumu serikali ya awamu ya nne kwa kushindwa kuwafikisha mahakamani wahusika wa kashfa ya Richmond, badala yake inawapeleka mahakamani watu wasiohusika na kashfa hiyo.


Shutuma hizo zimekuja baada ya serikali hiyo juzi kumfikisha mahakamani Naeem Gire, aliyedaiwa kuhusika na kashfa ya Richmond. Lakini chama hicho kimesema kigogo huyo wa Richmond hahusiki na kashfa hiyo.


Akizungumza kwenye mkutano huo, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Abdulkarim Atik alisema Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005 alisema urais wake hauna ubia na mtu yeyote.


Lakini mwelekeo wake katika kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi, wakiwemo wahusika wa Richmond, unatatanisha, jambo alilosema linaonyesha kuwa urais wake una ubia na watu fulani.


"Salamu kwa Kikwete.Rais Kikwete alipoingia madarakani alisema kuwa urais wake hauna ubia na mtu yeyote. Asiseme kwamba vigogo wanaohusika na Richmond hawapo", alisema Atik.


Aliongeza kuwa "kumfikisha mtu ambaye hahusiki na Richmond hakuonyeshi ukweli wowote katika kuwashughulikia wahusika wa kashfa hiyo". Atik alimgeukia Waziri Mkuu Mizengo Pinda akieleza kuwa naye haeleweki katika kuwashughulikia wahusika wa kashfa hiyo.


"Waziri Pinda kwa hili anapindisha mambo. Kuwashughulikia wahusika wa Richmond haitakiwi kuwa kificho kwa sababu Mheshimiwa Harrison Mwakyembe alishamaliza kila kitu kuhusu wahusika," alisema Atik.
 
CUF yawatema wabunge wenye kashfa

2005-04-30 08:47:45
Na Oswald Rutaihwa


Chama cha Wananchi (CUF), kimewaondoa kwenye orodha ya wagombea ubunge wa chama hicho katika uchaguzi mkuu wa Oktoba ,mwaka huu, wabunge watatu waliosimamishwa na Bunge la Jamhuri kufuatia kashfa ya kughushi hati za kusafiria na kuwapatia visa raia watatu wa Somalia.

Taarifa ya CUF iliyotolewa jana na kusainiwa na Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba ilisema pamoja na wabunge hao kupitishwa na vikao vya chini ili watetee nafasi zao, Baraza Kuu limewaondoa kwenye orodha ya wagombea na kulipongeza Bunge la Jamuhuri kwa hatua ya kuwasimamisha.

Aidha, Baraza Kuu limeiagiza Kamati ya Utendaji ya chama hicho kufanya uchunguzi kwa wabunge na wawikili pamoja na wanaowania nafasi hizo katika uchaguzi ujao kuona kama wapo wanaojihusisha na vitendo hivyo na kuchukua hatua.

Wabunge waliosimamishwa juzi na Bunge kutokana na kashfa hiyo ni pamoja na Karim Said Othman (Chambani), Khalifa Mohamed Issa (Mtambwe) na Khamis Ali Saleh (Magogoni).

'Baraza Kuu la uongozi wa Taifa la CUF limesikitishwa sana na kitendo cha wabunge hao kutumia vibaya nafasi zao na hadhi zinazoambatana na nafasi hizo na linalaani vikali kitendo chao ambacho kimekitia aibu chama,' ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliendelea kusisitiza, 'Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF linalipongeza Bunge na linakubaliana na hatua lililochukua ya kuwasimamisha ubunge wabunge hao na hatua nyingine zote zilizochukuliwa dhidi ya vitendo hivyo vilivyolidhalilisha Bunge na nchi Kimataifa.'

CUF kimesema hakihusiki na vitendo vya wabunge hao na kwamba hakikuwa na taarifa zozote juu ya vitendo hivyo.

'Baraza Kuu la Uongozi wa Taifa linatamka kwamba kitendo walichofanya wabunge hao ni chao binafsi, chama kinajitenga kabisa na vitendo hivyo,\' ilisisitiza taarifa hiyo.

Chama hicho kilisema kitawaita wabunge hao ili kuwapa nafasi ya kujieleza kuhusiana na kashfa hizo kabla ya kuamua kuchukua hatua za ziada za kinidhamu dhidi yao.

'Baraza Kuu la Uongozi wa Taifa linauhakikishia umma wa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwamba CUF kinalichukulia suala hili kwa uzito wake na kitalitumia kuweka mfano na kutoa mafunzo kwa wengine…,' ilisisitiza taarifa hiyo.

Habari zilizopatikana mara baada ya kikao cha Baraza Kuu lililokutana Jijini Dar es Salaam jana zilisema uamuzi wa kuwaondoa wabunge kwenye orodha ya wagombea baada ya kushinda kwenye kura za maoni katika majimbo yao ulifikiwa baada ya mvutano mkali miongoni mwa wajumbe kufuatia baadhi kutaka wabunge hao wavuliwe uanachama.

'Tulitaka tuwatimue maana wamekiabisha chama na wengi tulikuwa tunapendekeza hilo.

Ngoja tuone nini kitaamuliwa baada ya kuwaita wajieleze,' alisema mmoja wa wajumbe wa Baraza Kuu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Bunge lilifikia uamuzi wa kuwasimamisha wabunge hao hadi Agosti 5, mwaka huu.

Uamuzi huo unafuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge baada ya kupokea tuhuma dhidi ya Wabunge hao, kuzichunguza na kubaini wanahusika na kashfa hiyo.

Wanawake hao wa Kisomali wanaohusishwa na kashafa hiyo ya kupatiwa hati za kusafiria za Tanzania na kisha kupewa visa ya kuingia nchini Ujerumani ni pamoja na Sophia Ally Rage ambaye jina lake halisi ni Jawahir Elmi Abshir.

Wengine ni Fardhosa Musa Mohamed na Halima Abdallah Chambo wote wakiwa ni raia wa Somaria.

Uchunguzi wa kamati ya bunge ulibaini kuwa mbali ya wabunge hao kughushi hati kwa wanawake hao, pia waliudanganya Ubalozi wa Ujerumani na kuwawezesha kupatiwa Visa ili kufanikisha kwenda katika nchi hiyo.

Naye Namsembaeli Mduma anaripoti Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Adadi Rajabu amesema, Jeshi la Polisi haliwezi kuingilia suala la Wabunge watatu waliosimamishwa na Bunge la Jamhuri kwa kashfa ya kughushi hati za kusafiria kwa raia watatu wa Somali bila ya idhini ya Bunge.

Bw. Adadi alilieleza Nipashe ofisini kwake Jijini Dar es Salaam jana kuwa, ikiwa Bunge litatoa idhini, jeshi hilo litachunguza kashfa hiyo na kuchukua hatua za kisheria.

Alisema, hata kama kuna dalili zozote za kuwepo kwa makosa ya jinai katika kashfa hiyo, Jeshi la Polisi haliwezi kuchunguza na kuchukua hatua zozote za kisheria dhidi ya watuhumiwa bila idhini ya Bunge.

'Hadi sasa ofisi yangu haijapata malalamiko wala maelekezo yoyote kutoka katika Bunge kuhusu tuhuma za wabunge hao wa CUF, tunasikia tu katika vyombo vya habari.

Kiutaratibu na maadili ya kazi yetu, tunafanya upelelezi kugundua makosa ya jinai mara tu chombo hicho kinapotutaka tufanye hivyo,' alisema Bw. Adadi.

Kwa mujibu wa Bw. Adadi, Bunge lina mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa wenye makosa kwa kufuata taratibu lililojiwekea, endapo litaona kuwa adhabu inayotolewa itasaidia kukomesha tatizo.

Alisema, 'pengine Bunge litawasiliana nasi hapo baadaye au labda limeona adhabu lililotoa kwa watuhumiwa inatosha, tupo kazini wakati wote na hivyo tutafanya upelelezi pindi tutakapotakiwa kufanya hivyo.'

Aliongeza kuwa, kusimamishwa kwa wabunge hao, Bw. Khamis Ali Saleh (Mgogoni), Bw. Karim Said Othman (Chambani) na Bw.Khalifa Mohammed Issa (Mtambe), ni hatua za kiutawala za Bunge kwa ajili ya kurekebisha nidhamu.

'Suala hilo likikabidhiwa kwetu tutalishughulikia ipasavyo kwa kulipeleleza na kuwafikisha wahusika katika vyombo vya sheria mara moja endapo tutabaini kosa lolote la jinai,' Bw. Adadi alisisitiza.

Wabunge hao wanadaiwa kuwasaidia wanawake watatu raia wa Somalia kujipatia hati za kusafiria na viza ya kuwaruhusu kuingia nchini Ujerumani kwa njia ya udanganyifu.

Kufuatia kitendo hicho, Bunge liliwasimamisha wabunge hao kuhudhuria vikao vyake kuanzia juzi hadi Agosti 5, mwaka huu.

SOURCE: Nipashe
 
CUF yawatema wabunge wenye kashfa

2005-04-30 08:47:45
Na Oswald Rutaihwa


Chama cha Wananchi (CUF), kimewaondoa kwenye orodha ya wagombea ubunge wa chama hicho katika uchaguzi mkuu wa Oktoba ,mwaka huu, wabunge watatu waliosimamishwa na Bunge la Jamhuri kufuatia kashfa ya kughushi hati za kusafiria na kuwapatia visa raia watatu wa Somalia.

Taarifa ya CUF iliyotolewa jana na kusainiwa na Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba ilisema pamoja na wabunge hao kupitishwa na vikao vya chini ili watetee nafasi zao, Baraza Kuu limewaondoa kwenye orodha ya wagombea na kulipongeza Bunge la Jamuhuri kwa hatua ya kuwasimamisha.

Aidha, Baraza Kuu limeiagiza Kamati ya Utendaji ya chama hicho kufanya uchunguzi kwa wabunge na wawikili pamoja na wanaowania nafasi hizo katika uchaguzi ujao kuona kama wapo wanaojihusisha na vitendo hivyo na kuchukua hatua.

Wabunge waliosimamishwa juzi na Bunge kutokana na kashfa hiyo ni pamoja na Karim Said Othman (Chambani), Khalifa Mohamed Issa (Mtambwe) na Khamis Ali Saleh (Magogoni).

'Baraza Kuu la uongozi wa Taifa la CUF limesikitishwa sana na kitendo cha wabunge hao kutumia vibaya nafasi zao na hadhi zinazoambatana na nafasi hizo na linalaani vikali kitendo chao ambacho kimekitia aibu chama,' ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliendelea kusisitiza, 'Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF linalipongeza Bunge na linakubaliana na hatua lililochukua ya kuwasimamisha ubunge wabunge hao na hatua nyingine zote zilizochukuliwa dhidi ya vitendo hivyo vilivyolidhalilisha Bunge na nchi Kimataifa.'

CUF kimesema hakihusiki na vitendo vya wabunge hao na kwamba hakikuwa na taarifa zozote juu ya vitendo hivyo.

'Baraza Kuu la Uongozi wa Taifa linatamka kwamba kitendo walichofanya wabunge hao ni chao binafsi, chama kinajitenga kabisa na vitendo hivyo,\' ilisisitiza taarifa hiyo.

Chama hicho kilisema kitawaita wabunge hao ili kuwapa nafasi ya kujieleza kuhusiana na kashfa hizo kabla ya kuamua kuchukua hatua za ziada za kinidhamu dhidi yao.

'Baraza Kuu la Uongozi wa Taifa linauhakikishia umma wa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwamba CUF kinalichukulia suala hili kwa uzito wake na kitalitumia kuweka mfano na kutoa mafunzo kwa wengine…,' ilisisitiza taarifa hiyo.

Habari zilizopatikana mara baada ya kikao cha Baraza Kuu lililokutana Jijini Dar es Salaam jana zilisema uamuzi wa kuwaondoa wabunge kwenye orodha ya wagombea baada ya kushinda kwenye kura za maoni katika majimbo yao ulifikiwa baada ya mvutano mkali miongoni mwa wajumbe kufuatia baadhi kutaka wabunge hao wavuliwe uanachama.

'Tulitaka tuwatimue maana wamekiabisha chama na wengi tulikuwa tunapendekeza hilo.

Ngoja tuone nini kitaamuliwa baada ya kuwaita wajieleze,' alisema mmoja wa wajumbe wa Baraza Kuu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Bunge lilifikia uamuzi wa kuwasimamisha wabunge hao hadi Agosti 5, mwaka huu.

Uamuzi huo unafuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge baada ya kupokea tuhuma dhidi ya Wabunge hao, kuzichunguza na kubaini wanahusika na kashfa hiyo.

Wanawake hao wa Kisomali wanaohusishwa na kashafa hiyo ya kupatiwa hati za kusafiria za Tanzania na kisha kupewa visa ya kuingia nchini Ujerumani ni pamoja na Sophia Ally Rage ambaye jina lake halisi ni Jawahir Elmi Abshir.

Wengine ni Fardhosa Musa Mohamed na Halima Abdallah Chambo wote wakiwa ni raia wa Somaria.

Uchunguzi wa kamati ya bunge ulibaini kuwa mbali ya wabunge hao kughushi hati kwa wanawake hao, pia waliudanganya Ubalozi wa Ujerumani na kuwawezesha kupatiwa Visa ili kufanikisha kwenda katika nchi hiyo.

Naye Namsembaeli Mduma anaripoti Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Adadi Rajabu amesema, Jeshi la Polisi haliwezi kuingilia suala la Wabunge watatu waliosimamishwa na Bunge la Jamhuri kwa kashfa ya kughushi hati za kusafiria kwa raia watatu wa Somali bila ya idhini ya Bunge.

Bw. Adadi alilieleza Nipashe ofisini kwake Jijini Dar es Salaam jana kuwa, ikiwa Bunge litatoa idhini, jeshi hilo litachunguza kashfa hiyo na kuchukua hatua za kisheria.

Alisema, hata kama kuna dalili zozote za kuwepo kwa makosa ya jinai katika kashfa hiyo, Jeshi la Polisi haliwezi kuchunguza na kuchukua hatua zozote za kisheria dhidi ya watuhumiwa bila idhini ya Bunge.

'Hadi sasa ofisi yangu haijapata malalamiko wala maelekezo yoyote kutoka katika Bunge kuhusu tuhuma za wabunge hao wa CUF, tunasikia tu katika vyombo vya habari.

Kiutaratibu na maadili ya kazi yetu, tunafanya upelelezi kugundua makosa ya jinai mara tu chombo hicho kinapotutaka tufanye hivyo,' alisema Bw. Adadi.

Kwa mujibu wa Bw. Adadi, Bunge lina mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa wenye makosa kwa kufuata taratibu lililojiwekea, endapo litaona kuwa adhabu inayotolewa itasaidia kukomesha tatizo.

Alisema, 'pengine Bunge litawasiliana nasi hapo baadaye au labda limeona adhabu lililotoa kwa watuhumiwa inatosha, tupo kazini wakati wote na hivyo tutafanya upelelezi pindi tutakapotakiwa kufanya hivyo.'

Aliongeza kuwa, kusimamishwa kwa wabunge hao, Bw. Khamis Ali Saleh (Mgogoni), Bw. Karim Said Othman (Chambani) na Bw.Khalifa Mohammed Issa (Mtambe), ni hatua za kiutawala za Bunge kwa ajili ya kurekebisha nidhamu.

'Suala hilo likikabidhiwa kwetu tutalishughulikia ipasavyo kwa kulipeleleza na kuwafikisha wahusika katika vyombo vya sheria mara moja endapo tutabaini kosa lolote la jinai,' Bw. Adadi alisisitiza.

Wabunge hao wanadaiwa kuwasaidia wanawake watatu raia wa Somalia kujipatia hati za kusafiria na viza ya kuwaruhusu kuingia nchini Ujerumani kwa njia ya udanganyifu.

Kufuatia kitendo hicho, Bunge liliwasimamisha wabunge hao kuhudhuria vikao vyake kuanzia juzi hadi Agosti 5, mwaka huu.

SOURCE: Nipashe

Gazetyi la 2005 linawaboa vipi CHADEMA mbona haliusiani na kubomolewa kwa CHADEMA please au mimi nimeshindwa kuelewa
 
Nadhani hapa sisiemu watakuwa wanachekelea pembeni, Vita ya panzi neema kwa kunguru!
 
Vita vya Panzi, furaha ya Kunguru. Mwageni sera zenu jinsi mtakavyoikomboa nchi na wananchi mkipata fursa ya kuwa madarakani, sio kupambana wenyewe kwa wenyewe.
 
CCM inasubitri kutangaza ushindi tu kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu
 
Hata Ujambazi ulipungua Mrema ni kiongozi mwenye uchungu na Nchi yake nakaribia kusema alipendwa kama alivyokuwa akipendwa Sokoine ila vizuri havidumu.

Hivi Tambwe Hiza na Makamba ni kutoka kabila gani ?????
 
Wakati wake umekwisha sasa inabidi atafute kitu kingine cha kufanya vinginevy atabaki kuwa\ kivution kama hivyo.
 
Wakati wake umekwisha sasa inabidi atafute kitu kingine cha kufanya vinginevy atabaki kuwa\ kivution kama hivyo.

Unaweza kusema hivyo ikiwa umefilisika kimawazo na si msiasaji bali mtu wa jazba.
 
SO now is not Upinzani against CCM; its Upinzani against Upinzani; Hehehe very interesting; nilishangaa CUF wakikusanyana Dar badala ya rasilimali zao kuzipeleka Mbeya vijijini; ngoja tuone mwisho wake
 
MWENYEKITI wa TLP, Augustino Lyatonga Mrema juzi alikuwa kivutio katika mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mbeya Vijijini kwa tiketi ya CUF, Daudi Mponzi uliofanyika kwenye kiwanja cha stendi ya mabasi cha Mbalizi alipodai kuwa wamejitakia maisha ya shida kwa kuichagua CCM.


Alikuwa akihutubiua kwenye mkutano uliofurika mamia ya watu na kuhudhuriwa na viongozi wa vyama vinne vya siasa vya TLP na PPT Maendeleo ambavyo vimeamua kuungana na CUF kumpigia kampeni mgombea wake ili anyakue jimbo hilo lililoachwa wazi baada ya Richard Nyaulawa (CCM) kufariki mwishoni mwa mwaka jana.


Wananchi hao walianza kuonyesha kuvutiwa na Mrema mara aliposimama jukwaani wakati alipomshangilia na kupiga kelele kuonyesha kumkubali na bila kuchelewa waziri huyo wa zamani wa mambo ya ndani alianza hotuba yake kwa kuwaambia wananchi kuwa shida na maisha magumu waliyonayo wamejitakia.


"Hizi shida mnajitakia wenyewe msimlaumu Mwenyezi Mungu kwani Mungu amefanya kazi ya kuwaumba, lakini nyie mmefanya kazi ya kuichagua CCM na ndiyo maana mnabaki na malalamiko ya kusema 'Mungu nisaidie maisha ni magumu'. Naomba niwasisitizie kuwa hili si kosa la Mungu, ni kosa lenu kwa kuchagua chama ambacho kimejaa propaganda," alisema.


Mrema aliendelea kuwavutia wananchi hao aliposema kuwa alipokuwa naibu waziri mkuu alifanya kazi zake vizuri, ikiwa ni pamoja na kukamata ndege iliyokuwa na dhahabu zenye thamani ya Sh175 milioni, lakini waziri mkuu wa wakati huo hakufanya lolote zaidi ya propaganda.


Alisema kuwa ameamua kuiunga mkono CUF kwa sababu watendaji wake ni majasiri na wana uwezo mkubwa na kwamba CUF ni chama cha ukombozi hivyo kinastahili kuungwa mkono na wananchi wote, ikiwa ni pamoja na wa Mbeya Vijijini ambao alisema wanatakiwa kumpa kura za Mponzi.


Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa wananchi wa Mbeya Vijijini wana nafasi ya kubadilika na kumchagua mgombea wa CUF kuwa mbunge wa jimbo la Mbeya vijijini ili maisha yao yaweze kubadilika .

Siku hizi kawa mpiga debe wa wagombea wa upinzani?
 
Back
Top Bottom