CHADEMA yashinda uwenyekiti mji mdogo Usa River leo

kombah

Member
Nov 1, 2010
52
38
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa CHADEMA kata Ndugu Paulo,amesema Kamanda Malisa ameshinda kwa kishindo katika uchaguzi huo na kumuangusha mgombea wa wa CCM ndugu Tom wa kitongoji cha Llima Sioni. Pamoja na utundu uliotumika wa CCM kuongeza madiwani watatu nao wapige kula lakini juhudi zao ziligonga mwamba na Ndugu Malisa kutoka kwenye ukumbi akiwa kidedea.Pia jopo hilo limemchagua makamu mwenyekiti nao ikaenda kwa CHADEMA na kuchaguliwa ndugu Richard Mkungu kwa kula nyingi na kumbwaga Richard wa CCM kitongoji cha Usa Madukani. Kwahiyo pia nafasi ya makamu wa mwenyekiti ikaenda CHADEMA.
 
Naona makamanda mmeamua kushuka ngazi za vijjiji! maana udiwani hamna chenu!

Wape hongera mwenyekiti na katibu wa chama taifa nguvu yao kwa uchaguzi wa mwenyekiti imezaa matunda.
 
Mfa maji haishi kutapa tapa
Naona makamanda mmeamua kushuka ngazi za vijjiji! maana udiwani hamna chenu!

Wape hongera mwenyekiti na katibu wa chama taifa nguvu yao kwa uchaguzi wa mwenyekiti imezaa matunda.
 
Ushindi wa CHADEMA ukanda wa Arusha is no longer interesting news to me. Nitafurahi siku mtakapokuwa mnaongelea ushindi wa CHADEMA Mtwara, Lindi, Zanzibar, Tanga, Tabora, Dodoma etc. Lakini kwa Arusha wala haitushitui hata kama madiwani wote wangekuwa ni wa CHADEMA. Maana ipo dhahiri kwamba Arusha ni ngome ya CHADEMA.
 
Ushindi wa CHADEMA ukanda wa Arusha is no longer interesting news to me. Nitafurahi siku mtakapokuwa mnaongelea ushindi wa CHADEMA Mtwara, Lindi, Zanzibar, Tanga, Tabora, Dodoma etc. Lakini kwa Arusha wala haitushitui hata kama madiwani wote wangekuwa ni wa CHADEMA. Maana ipo dhahiri kwamba Arusha ni ngome ya CHADEMA.
Nadhani ulipaswa kutumia akili kidogo kujua kwamba ili kujiimarisha mapambano yoyote yale lazima yawe na base, kama huna mzizi wa kusimamia lazima utanyauka tu, kwahyo ni muhimu sana kwa cdm kuendelea kufanya vizuri arusha..na baada ya hapo mbeya, mwanza, dar, na kisha tanga, lindi, mtwara na baadae unguja na pemba na nchi nzima
 
Back
Top Bottom