CHADEMA yapata meya, naibu wake

Kisendi

JF-Expert Member
Jan 29, 2009
699
178
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), jijini Mwanza kimemteua Diwani wa Nyakato, Josephat Manyerere, kuwa mgombea wa umeya wa jiji hilo, huku nafasi ya unaibu ikichukuliwa na Charles Machinchibera wa Mahina.

Uteuzi huo ulifanyika juzi baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya wilaya mbili za Nyamagana na Ilemela, chini ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.

Chama hicho pia kimefanikiwa kupata madiwani wanne wa viti maalumu jijini hapa, ambao ni Neema Mafuma na Pendo Mboya kutoka Nyamagana, wakati Ilemela madiwani walioteuliwa kwenye viti maalumu ni Lucy Kambulwa na Gladness Kiwia.

Kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilipata madiwani watatu wa viti maalumu na kufikisha idadi ya madiwani 12 huku CHADEMA ikiwa na madiwani 15.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha uteuzi, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Mwanza, Wilson Mushumbusi, alisema wagombea wa umeya na unaibu waliteuliwa na chama baada ya kukidhi vigezo vinavyotakiwa.

Waliokuwa wakiomba kuteuliwa kugombea nafasi hiyo ya umeya wa Jiji la Mwanza, ambao pia wameachwa katika uteuzi huo ni Chagulani Adams na Henry Matata.

Vigezo vilivyotumika ni uzoefu katika usimamizi wa taasisi, uongozi wa chama au vyama, uadilifu na uaminifu katika kusimamia mali za umma, uelewa wa sera na ilani ya chama hicho na umri katika chama.

Akizungumzia mchakato wa uundaji wa Jiji la Mwanza, Dk. Slaa alitoa angalizo kuwa ni lazima wananchi watumikiwe kwa masilahi ya umma na si mtu binafsi.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), jijini Mwanza kimemteua Diwani wa Nyakato, Josephat Manyerere, kuwa mgombea wa umeya wa jiji hilo, huku nafasi ya unaibu ikichukuliwa na Charles Machinchibera wa Mahina.

Uteuzi huo ulifanyika juzi baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya wilaya mbili za Nyamagana na Ilemela, chini ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.

Chama hicho pia kimefanikiwa kupata madiwani wanne wa viti maalumu jijini hapa, ambao ni Neema Mafuma na Pendo Mboya kutoka Nyamagana, wakati Ilemela madiwani walioteuliwa kwenye viti maalumu ni Lucy Kambulwa na Gladness Kiwia.

Kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilipata madiwani watatu wa viti maalumu na kufikisha idadi ya madiwani 12 huku CHADEMA ikiwa na madiwani 15.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha uteuzi, Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Mwanza, Wilson Mushumbusi, alisema wagombea wa umeya na unaibu waliteuliwa na chama baada ya kukidhi vigezo vinavyotakiwa.

Waliokuwa wakiomba kuteuliwa kugombea nafasi hiyo ya umeya wa Jiji la Mwanza, ambao pia wameachwa katika uteuzi huo ni Chagulani Adams na Henry Matata.

Vigezo vilivyotumika ni uzoefu katika usimamizi wa taasisi, uongozi wa chama au vyama, uadilifu na uaminifu katika kusimamia mali za umma, uelewa wa sera na ilani ya chama hicho na umri katika chama.

Akizungumzia mchakato wa uundaji wa Jiji la Mwanza, Dk. Slaa alitoa angalizo kuwa ni lazima wananchi watumikiwe kwa masilahi ya umma na si mtu binafsi.




Nawaomba saana Chadema Mkoani mwanza wajitahidi kuyafanya kwa vitendo yale yote aliyokuwa akiyaahidi mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, kubwa hasa la kuanza nalo ni kuwasomesha watoto toka elimu ya msingi na sekondari bure. Kama Tarime na Karatu iliwezekana sehemu ambazo hazina rasilimali kama mwanza, sioni kwa nini Mwanza washindwe. Wajipange vizuri tu kukusanya na kudhibiti mapato yote na kuhakikisha yanafanya kazi ilokusudiwa. Wakifanikiwa mwanza basi 2015 Chadema itaiteka kanda nzima ya ziw toka Mwanza hadi Tabora.

KAMA TARIME WALIWEZA KWANINI MWANZA WASHINDWE?????????

 
LAbda sielewi lakini mie nilidhani sera kubwa kubwa za chadema zilikuwa za kitaifa mfano ya kulipia gharama ya wanafunzi mashuleni.
Kwa sasa kutaka wanafunzi wa Mwanza wasome bure ni kinyume na sera ya chma kinachoongoza nchi ambacho ni CCM.
 
Kisendi bwana!! eti Chadema wamepata meya, sema wameteua mgombea wa u-meya, unaweza kushangaa ndani ya hao madiwani 15 wa CDM wengine wanaunga mkono CCM, si unajua kura ni siri ya mtu?... wanaweza kukisaliti CHADEMA halafu wote humu ndani mkabaki vinywa wazi.....Hapana, haka ni kautabiri tu ila kakiwa kweli msishangae wandugu.............
 
LAbda sielewi lakini mie nilidhani sera kubwa kubwa za chadema zilikuwa za kitaifa mfano ya kulipia gharama ya wanafunzi mashuleni.
Kwa sasa kutaka wanafunzi wa Mwanza wasome bure ni kinyume na sera ya chma kinachoongoza nchi ambacho ni CCM.


Katika halmashauri ya Jiji la Mwanza, CCM ni chama cha upinzani.
 
Back
Top Bottom