CHADEMA Yampitisha Mshimbe Mgombea Zanzibar; Yatoa Taarifa kuhusu maamuzi ya Kamati Kuu

Mzee heshima mbele
Mimi sitaki details nyingi ila mazungumzo na Ikulu lazima yawekwe wazi kila baada ya wao kukutana la sivyo hali ya CUF inatutisha. Hali na siasa sio siri lazima washika dau wapewe ni nini CDM wanafuata ikulu na kila hatua ili kutoa maswali na wasiwasi, kumbuka kule mwenye Ikulu ni CCM na CCM sio mwema hata kidogo kwa demokrasia ya TZ haipendi wala haitaki anajaribu kumrubuni yeyote kwa gharama yeyote.

Sasa ulitaka ujue nini kilizungumzwa Ikulu? nilidhani watu wengi walikuwa wanataka picha sasa picha inaonekana hazitoshi tena. Ila tusubiri tuone je Kikwete atateua tume ya kupitia Katiba bila kubadilisha sheria na je itaanza kazi kabla ya mabadiliko ya sheria Bungeni? Huo ndio mstari uliochorwa.
 
Sasa ulitaka ujue nini kilizungumzwa Ikulu? nilidhani watu wengi walikuwa wanataka picha sasa picha inaonekana hazitoshi tena. Ila tusubiri tuone je Kikwete atateua tume ya kupitia Katiba bila kubadilisha sheria na je itaanza kazi kabla ya mabadiliko ya sheria Bungeni? Huo ndio mstari uliochorwa.

Mkuu Mwanakijiji ni kwamba ukishaumwa na nyoka hata unyasi unaukimbia!! Usiri katika mazungumzo una historia mbaya hapa nchini ndio maana watu wanaogopa! Na mara nyingi usiri huwa hauna mwisho mwema kwa wale ambao hawana dola. Mwezi November 2011 walipokutana pande zote zilisaini communique lakini sasa tunaona vipande vipande vya taarifa.
 
Watanzania bwana, sasa watu mko kwenye mapambano, majenerali wamekaa na kupanga mikakati na kufanya mazungumzo; wanakuja kwa wapiganaji na kuwaambbia yale ambayo ni muhimu kw awapiganaji na kuonesha njia ya kuelekea ushindi. Wapiganaji wanaanza kuuliza details za kila kitu kilichozungumzwa? really?

Unless wanaotaka hivyo siyo wapiganaji isipokuwa wajumbe wa adui ambao wangependa kujua taarifa za ndani. CHADEMA wametoa taarifa inatosha kwa wakati huu mambo ya gharama zote n.k huwezi kuweka kila kitu hadharani ukiweka hesabu zako zote wazi adui zako wanaweza kujua una nguvu kiasi gani. Hawa wanaosema wanataka details zaidi hutawaona wakidai CCM iweke zaidi taarifa zake. why not?

Wewe hujawaelewa wapiganaji?! Wanataka taarifa ya mapato na matumizi kwa takwimu kwa vita iliyokwisha piganwa huko nyuma. Sio vita ijayo, wapiganaji wanataka kujua vita iliyopita iliwagharimu kiasi gani.
 
Moja: Taarifa haijitoshelezi, mfano-Kulitokea nini huko Uzini mpaka sasa ufanyike uchaguzi na uteuzi wa mgombea wa chadema? Mwakilishi aliyechaguliwa 2010 amefariki au kavuliwa uanachama?Mbili: Vyama vyetu vijifunze kutumia fedha kwa umakini. Hii itatupa moyo kwamba hata wakiingia madarakani hawatatapanya mali na raslimali za watanzania. Chadema wana pesa sana siku hizi kiasi cha kufanyia mikutano New Africa Hotel? Mi nilidhani wangebana sana matumizi ili sehemu ya mapato yao yaelekezwe kijijini kuimarisha chama!!?

Wewe kweli bongo lala hujui nini kilitokea Uzini! Kama hujui ilipaswa kuuliza kwanza badala ya kutoa conclusion kuwa taarifa haijitoshelezi!
 
Yaani nimeisoma hii taarifa nilichopata zaidi ni lugha tamu ya porojo kuliko utendaji, kweli hilki ni chama maini na si makini !

Inaonyesha hata usivyo makini kutumia nafasi katika mtandao, una-quote habari kuu! Kweli wewe ni maini!
 
aahahaha.chadema imeingia kwenye Uchaguzi kwa nia ya kusindikiza wenyeji. akifika nyjiani atarudi kwao
Demokrasia inaruhusu usipojaribu huwezi kujipima. After all mwanya wa vyama vingine vya upinzani kujipenyeza katika siasa za Zenji umeanzakuonekana. Watapanua tu!
 
Mkuu Mwanakijiji ni kwamba ukishaumwa na nyoka hata unyasi unaukimbia!! Usiri katika mazungumzo una historia mbaya hapa nchini ndio maana watu wanaogopa! Na mara nyingi usiri huwa hauna mwisho mwema kwa wale ambao hawana dola. Mwezi November 2011 walipokutana pande zote zilisaini communique lakini sasa tunaona vipande vipande vya taarifa.

Kweli tupu
 
Sasa ulitaka ujue nini kilizungumzwa Ikulu? nilidhani watu wengi walikuwa wanataka picha sasa picha inaonekana hazitoshi tena. Ila tusubiri tuone je Kikwete atateua tume ya kupitia Katiba bila kubadilisha sheria na je itaanza kazi kabla ya mabadiliko ya sheria Bungeni? Huo ndio mstari uliochorwa.

MMM
Siasa ni watu na viongozi wana wakilisha kundi kubwa la watu wanaofanya kazi usiku na mchana tena kubwa zaidi kuliko hata viongozi wa kitaifa. Kila mwanachama na mshika dau wa CDM anajua kunamazungumzo na Ikulu kuhusu katiba, katiba sio ya viongozi ni yetu sote. Mjadala unaoendelea ikulu ni kwa ajili yetu sisi wananchi/wanachama. Sasa hiyo siri ni kwaajili ya nani? Je hayo mazungumzo yakishindikana ni nani nguvu ya umma ni sisi au ni wao sita au kumi waliokwenda Ikulu? Ni kweli hatuna haki ya kujua?

Kumbuka walikwenda mara ya kwanza tumeshuhudia mswada ukitiwa saini kwa mbwembwe ni kipi kipya au kiini macho na uchelewashaji huku unalainishwa?

Hatuhitaji makubwa ila tunataka kujua nini kinazumzwa na tutegemee nini ili wakituhitaji tujue ? Hata CUF ilianza na ukimya leo ndoa takatifu. Najua Viongozi wetu wa CDM ni makini ila ni wanadamu.
 
Back
Top Bottom