Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Watch TBC Live toka Bungeni!
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekubali yaishe, wanamtambua JK kama Rais, Wanampongeza!
Mbowe ameomba reconciliation for the sake of Umoja wa Kitaifa.
Big Up kwa Freeman Mbowe, sio siri mimi binafsi nilikuwa simuheshimu sana Mbowe nikimuona kama spoon fed leader.
Kuanzia sasa ni heshima mbele! Huo ndio uanamume, kukubali kushindwa na kukubali yaishe!
Mbowe amewashukuru wapiga kura kwa kura walizoipigia Chadema!.
Hiki Mbowe alichokifanya Bungeni, ndicho Dr. Slaa alichotakiwa kukifanya ile siku ya kutangazwa matokeo!
Nilisema that was a golden missed opportunity. Sasa Mbowe amerekebisha makosa ya Dr. Slaa. Chadema sasa inarudi juu!
Kuna posti niliwahi kuiposti kuwa Chadema hawajajipanga, nilishambuliwa piga ua. Sasa nasema Chadema imeanza kujipanga. Big up!.
Kwanza mlibanaaa... mwisho mmeachia... I'm glad I was damm right!
Chadema sasa tusonge mbele, hata mimi nikirudi uraiani, naweza kufikiria kujiunga Chadema, kuimarisha nguvu!
Asante sana Freeman Mbowe!.
Update 1: Angalizo!.
Kuna kitu kinaitwa expressly na impliedly!
Expressly ni kwa Mbowe kutangaza kwamba sasa Chadema inamtambua Rais!
Impliedly ni pale Mbowe alipompongeza rais, akamsifu, akamshukuru na bla bla bla nyingi za kusifu na kutukuza na kuonyesha spirit ya reconciliation.
mkubali msikubali, Chadema imemtambua Rais JK impliedly na wamekubali yaishe zaidi ya hapo ni ubishi tuu, vinginevyo Mbowe afanya Press Conference afafanue na kukazia kutomtambua JK!
Pasco.
Mimi simtambui, simpongezi huyo JK.