CHADEMA yajiondoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Waziri Jafo awashangaa kususia uchaguzi

Wapo watu waliojiweka mkao wa kula 2020, kumbuka hata Mzee Lowassa alidandia jahazi na kumpiga kikumbo Dr. Slaa lakini mwisho wa siku haikuwa vile alitaka iwe.
Hebu jibu hili swali Kada Mwenzangu "wangeshiriki unadhani nani angenufaika??"
 
jibu ni wale wote waliotaka kukitumia chama kama jahazi la kuwavusha 2020 na kutwaa ubingwa ambao kiukweli sio wao. kila siku tunasema Chadema ina wenyewe, na wenyewe wameshasoma alama za nyakati kama kuna watu wanataka kukiondoa chama nje ya dhumuni lake la kuanzisha na kukimbia nacho kusikojulikana.

Tunacho kiona sasa, ni chama kujiweka kwenye "sleeping mode", kujirudisha nyuma na kujikosesha nguvu kwa makusudi ili kisiwe kivutio kwa wale wanotala kukitumia kwa manufaa yao. Wimbi la bahari likishapita, basi ni rahisi kujiamsha na kuanza kuendeleza ajenda ya awali au hata ikiwezekana mpya na yenye mvuto zaidi.

Msipate shida, Tiss wapo na nyie wapambe mpo, anzisheni chama mnachotaka kama mnaona hivi vyama vibaraka vilivyopo havina mvuto. Lakini wananchi tunajitambua hatuko tayari tena kushiriki siasa na chaguzi za kishenzi.
 
Hebu jibu hili swali Kada Mwenzangu "wangeshiriki unadhani nani angenufaika??"
Mkuu, ungepeda niseme wananchi, lakini nashindwa kutumia hilo neno. Maana kama wanufaika wangekuwa ni wananchi, wasingetumia uwamuzi ambao sio wa kidemokrasia wa kususa uchaguzi.

Wanufaika wapo na wanajijua, kitendo hichi cha kujitoa kinapunguza nguvu kwa yeyote alitetegema madiwani au wenyeviti wa mitaa na vijiji kujenga hoja kwa wanachama au hata wananchi kwa ujumla ili kuvuka 2020.
 
Mwananchi wa kawaida ni lazima atoe ushirikiano kwa serikali ya mtaa kwa sababu vinginevyo anaweza kujikwamisha katika kutimiza mambo yake muhimu.

Mabwanyenye ndio aghalabu kutumia Huduma za serikali ya mtaa kwani wenyewe wana consultants na mawakala katika kila jambo hata jumuiya hawasali lakini Kanisani wanakaa viti vya mbele kabisa.

Inawezekana kukawa na uonezi kweli katika maeneo fulani ya uchaguzi lakini kule uswahilini kutotoa ushirikiano kwa serikali yako ya mtaa ni jambo ambalo haliwezekani.

Tusidanganyane

Maendeleo hayana vyama!
 
Mwananchi wa kawaida ni lazima atoe ushirikiano kwa serikali ya mtaa kwa sababu vinginevyo anaweza kujikwamisha katika kutimiza mambo yake muhimu.

Mabwanyenye ndio aghalabu kutumia Huduma za serikali ya mtaa kwani wenyewe wana consultants na mawakala katika kila jambo hata jumuiya hawasali lakini Kanisani wanakaa viti vya mbele kabisa.

Inawezekana kukawa na uonezi kweli katika maeneo fulani ya uchaguzi lakini kule uswahilini kutotoa ushirikiano kwa serikali yako ya mtaa ni jambo ambalo haliwezekani.

Tusidanganyane

Maendeleo hayana vyama!
Hii inanikumbusha hata 2015 walikataa matokeo na kutokumtambua JPM, matokeo yake wakajikuta hata shughuli zao za kawaida za bungeni na nje ya Bunge zinakwama. Kwenye siasa za vyama vingi huwezi kuikwepa serikali, ni lazima utashirikana nayo utake usitake.
 
Msipate shida, Tiss wapo na nyie wapambe mpo, anzisheni chama mnachotaka kama mnaona hivi vyama vibaraka vilivyopo havina mvuto. Lakini wananchi tunajitambua hatuko tayari tena kushiriki siasa na chaguzi za kishenzi.
Mnalaumu mtu asie na hatia, siku postmortem ikifanywa mtakuja kuona ukweli uko wapi.
 
Kiukweli mi sijapendezwa na Hali ya mambo ilivyo , wangewaacha Tu wapinzani na sio kuwanyanyasa kias hiki, Mbowe amefanya maamuzi Bora Sana kuwah kutokea, JPM namkubali Ila Kwa hili totaly wrong
 
CHADEMA kama chama kikubwa cha siasa, nategemea wawe na viongozi wao na wanachama huko huko mitaani. Hawa ndio askari wa kutegemewa kuikomboa nchi.

Hao viongozi waliopo makao makuu ya chama na mikoana/wilayani ndio wanaotakiwa kusimamia zoezi la ukombozi kwa kuwa na mipango thabiti ya kuelekeza mapambano sehemu zote nchini.

Ni swala la kuwa na mpangilio mzuri tu wa kazi.

Ukombozi wa nini unazungumzia wewe???!!!
 
Ni maamuzi sahihi 💯
Mmewatendea haki Wananchi
Huu ndio Upinzani
Safari ya Kuipigania Demokrasia ndio imeanza kama viongozi wa upinzani ndio mnakuwa imara zaidi.
Tutafika ng'ambo ile yenye matumaini
 
77414550_429484467740078_516728448588705826_n.jpeg
 
Mbowe ni mwanaCCM damudamu alipandikizwa kufanya mission ya kuipandisha na kuiua CHADEMA amefanikiwa maana Chadema itaenda Makumbusho kama CuF, NCCR MAGEUZI
 
Kwani hata ikifa wewe nini kinakuwasha?kama mmebaki peke yenu machozi ya nini!au mtakosa buku 7 za bando?

Naona baada ya majahili wa CCM kuharibu na kuutia najisi uchaguzi wa serikali za mitaa, wanafanya juhudi za ziada za kutakatisha uovu wao!!!!!
 
Back
Top Bottom