Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Baada ya chama cha mapinduzi kuelemewa na kashfa za wizi na ufisadi wa mali ya umma huku vijana wake na mawaziri wenye umri mdogo wakiwa wananuka rushwa na kuwa na vito vya thamani kwa haramu, sasa wamechanganyikiwa na kuanza kutaka kurubuni wananchi kuwa nao ni sawa na wao kwa kuanza kushindana kutumia usafiri wa masikini na watu wa kipato cha chini baada ya serikali ya CCM kuuza na kufilisi mashirika yote ya usafiri salama ndani na nje ya majiji kama UDA, reli, mabasi nk
Vijana hawa wakiongozwa na Mbunge wa bumbuli Bwana January Makamba na Mbunge wa tabora hamisi Kigwangala wameonekana wakipost kwa nyakati tofauti picha wakiwa wanatumia usafiri wa bajaj ili kuwaridhisha watanzania kuwa wako nao.
Kama kweli wana nia njema ya kusaidia masikini badala ya kuwasanifu wauze mali zao zote na magari yao wanunue magari ya wagonjwa ili yawasidie akina mama na wazee kufika hospitali mapema badala ya kuzalia njiani na watoto kufa.
Kama kweli wanauchungu na watanzania warudishe fedha za kifisadi walizozipata kutoka kampuni za madini, mikataba mibovu na posho haramu walizovuna tangia wakiwa watumishi wakawaida serikalini.
Kama kweli wanauchungu na wananchi wakaishi majimboni mwao na watoto wao watumie shule, hospitali na huduma zote za jamii zilizoko kule badala ya wao kugeuka kuwa kina masanja.
Inauma sana mtu mzima kuchezea akili za watu wenye shida za kweli na mahitaji. Umasikini wa Tanzania unaletwa na usanii wa viongozi kama hawa.
ni wajibu wa kila mtanzania kumwogopa kama ukoma kiongozi yeyote anayetumia umasikini wetu ili kututawala huyu ni mtu hatari sana kuliko njaa. Kwani njaa inaweza kukuuwa ila huyu atakutesa wewe na kizazi choko daima.
Tanzania hatuhitaji viongozi wanaofikiri kimasikini na kutaka kutushikamanisha na umasikini hatutaki. Wenzetu wanawaaminisha watoto wao wataweza mambo makubwa na hawataki watoto wao waishi maisha ya wazazi wao bali bora zaidi naz zaidi ila hawa viongozi wetu tena vijana wanataka tuamini kwenye umasikini, taabu, dhiki na ajali.
Naamini kiongozi ni mfano, kioo, mwanga, na njia ya jamii. simtaki kiongozi atakayeifundisha jamii umasikini kwa mtaji wa kupigiwa kura.
Raisi anayehubiri umasikini ni wa CCM ndio maana kila mara wanasema hawajui umasikini wetu.
Mmeuwa UDA mkaleta bajaj leo mnazisujudia : hatuzipendi tunazipakia kwa sababu hatuna jinsi.
Chief Mkwawa
Umasikini ukienziwe unadumu. kataa umasikini na kataa usanii wa Viongozi wa CCM
Vijana hawa wakiongozwa na Mbunge wa bumbuli Bwana January Makamba na Mbunge wa tabora hamisi Kigwangala wameonekana wakipost kwa nyakati tofauti picha wakiwa wanatumia usafiri wa bajaj ili kuwaridhisha watanzania kuwa wako nao.
Kama kweli wana nia njema ya kusaidia masikini badala ya kuwasanifu wauze mali zao zote na magari yao wanunue magari ya wagonjwa ili yawasidie akina mama na wazee kufika hospitali mapema badala ya kuzalia njiani na watoto kufa.
Kama kweli wanauchungu na watanzania warudishe fedha za kifisadi walizozipata kutoka kampuni za madini, mikataba mibovu na posho haramu walizovuna tangia wakiwa watumishi wakawaida serikalini.
Kama kweli wanauchungu na wananchi wakaishi majimboni mwao na watoto wao watumie shule, hospitali na huduma zote za jamii zilizoko kule badala ya wao kugeuka kuwa kina masanja.
Inauma sana mtu mzima kuchezea akili za watu wenye shida za kweli na mahitaji. Umasikini wa Tanzania unaletwa na usanii wa viongozi kama hawa.
ni wajibu wa kila mtanzania kumwogopa kama ukoma kiongozi yeyote anayetumia umasikini wetu ili kututawala huyu ni mtu hatari sana kuliko njaa. Kwani njaa inaweza kukuuwa ila huyu atakutesa wewe na kizazi choko daima.
Tanzania hatuhitaji viongozi wanaofikiri kimasikini na kutaka kutushikamanisha na umasikini hatutaki. Wenzetu wanawaaminisha watoto wao wataweza mambo makubwa na hawataki watoto wao waishi maisha ya wazazi wao bali bora zaidi naz zaidi ila hawa viongozi wetu tena vijana wanataka tuamini kwenye umasikini, taabu, dhiki na ajali.
Naamini kiongozi ni mfano, kioo, mwanga, na njia ya jamii. simtaki kiongozi atakayeifundisha jamii umasikini kwa mtaji wa kupigiwa kura.
Raisi anayehubiri umasikini ni wa CCM ndio maana kila mara wanasema hawajui umasikini wetu.
Mmeuwa UDA mkaleta bajaj leo mnazisujudia : hatuzipendi tunazipakia kwa sababu hatuna jinsi.
Chief Mkwawa
Umasikini ukienziwe unadumu. kataa umasikini na kataa usanii wa Viongozi wa CCM