CHADEMA Yabwagwa NA CCM KISUTU--DIWANI WAKI AVULIWA UDIWANI

Kachanchabuseta

JF-Expert Member
Mar 8, 2010
7,269
675
MATOKEO ya uchaguzi wa udiwani wa kata ya Kijitonyama, Kinondoni jijini Dar es Salaam yaliyomtangaza mgombea Uloleulole Athumani wa CHADEMA kuwa ni mshindi, yamebatilishwa na Mahakama ya Hakimu mkazi kisutu.

Uamuzi huo umetolea leo Mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Genvitus Dudu katika kesi ya kupinga matokeo hayo iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa kiti hicho kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo.

Dudu katika uamuzi wake alisema amesikiliza mashahidi wa pande zote mbili, mahakama imeona mdaiwa katika fomu ya
kugombea nafasi hiyo, aliandika jina la Uloleulole Juma Athumani wakati kwenye hati ya kisheria lipo jina la Juma Uloleulole Athumani.Alisema mahakama hiyo imeona kwamba hao ni watu wawili, inakubaliana na Bulembo (mdai) kuwa kungekuwa na hati ya kiapo inayoonyesha mdaiwa alibadilisha jina lake.

Alisema kutokana na kukosekana na hati hiyo, inatosha kumvua mdaiwa nafasi aliyokuwa nayo na pia katika hati ya kisheria anayotakiwa kutia saini mbele ya hakimu, mdaiwa imeweza kuleta mashaka kwa kuwa ina tarehe mbili tofauti.Alisema hati hiyo inaonesha mdaiwa alitia saini Agosti 14, mwaka 2010 na ya pili inaonesha hakimu alitia saini Agosti 18, mwaka 2010 mahakama inashindwa kuelewa kama kweli mdaiwa alitia saini mbele ya hakimu au la.

Aidha Hakimu huyo alisema wananchi wananyimwa haki yao kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria hawakuweza kujua vigezo vya mgombea kutokana na kwenda kinyume cha Sheria ya Uchaguzi mahakama hiyo inaona uchaguzi wa udiwani wa kata ni batili.Kutokana na hayo, alisema maombi ya mdai yamefanikiwa kwamba matokeo ya uchaguzi yaliyomtangaza mdaiwa ni mshindi ni batili.

Hata hivyo alisema mahakama hiyo haina mamlaka ya kumtangaza Bulembo kuwa ni mshindi na kusema uchaguzi urudiwe kwani mamlaka hayo yapo kwenye mamlaka nyingine.Bulembo alifungua kesi hiyo, akidai kutoridhishwa na matokeo hayo ya uchaguzi huku akiwa amewasilisha sababu sita.

Katika sababu hizo aliiomba mahakama itamke matokeo batili, atangazwe yeye ndiyo diwani au kufanyike kwa uchaguzi wa
wazi na huru.Hata hivyo mahakama ilisema pande zote mbili kama kuna ambaye hajaridhika na uamuzi huo anayo haki ya kukata rufani.
 
kha! Yeye ndio alitype majina yk au tume? Kinachotakiwa ni uchaguzi mpya si kumvua madaraka diwani wa cdm na kumvika hy guluguja wa ccm kwani ni dhahir kw ht wananch walimchagua wa cdm. Ht bungeni wanatamkaga ZUBERI ZITTO KABWE, ZITTO ZUBERI KABWE yt 2najua kw anayetajwa ni ZITTO KABWE.
 
huyu bulembo alilisha sana ubwabwa raia pale kwa mtogole. lakini mpaka mateja walienda kumpigia kura uloleulole... alikuwa na mvuto wa kisiasa kwa kweli!
 
What a lose! Tatizo lingine la mahakama zetu. Hawaangalii matakwa ya wananchi. Watu wamepiga kura na kumchagua diwani wao. Ingekuwa majina yaliwachanganya wapiga kura na kusababisha kuvuruga uchaguzi, hapo ningekubaliana nao. Lakini kurudia uchaguzi kwasababu ya typing error ambayo haikuathiri uchaguzi ni ufinyu wa fikra na woga wa kutoa maamuzi hasa kwa mahakama zetu ambazo kwa sasa zinaingiliwa sana na wanasiasa wa chama tawala. Poor Tz. U have a very long way to go!
 
kha! Yeye ndio alitype majina yk au tume? Kinachotakiwa ni uchaguzi mpya si kumvua madaraka diwani wa cdm na kumvika hy guluguja wa ccm kwani ni dhahir kw ht wananch walimchagua wa cdm. Ht bungeni wanatamkaga ZUBERI ZITTO KABWE, ZITTO ZUBERI KABWE yt 2najua kw anayetajwa ni ZITTO KABWE.

Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini.

Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.
 
Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini.

Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.

Huna jipya!!!!!
 
Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini.

Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.
Ukiwaona ditopile mzuzuri ilikuaje akapewa dhamana kesi ya mauaji?
 
Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini.

Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.

We mdada upo makini sana katika kuandika. Lakini katika hili ni wazi maneno ya Mbowe kuwa Mhimili huu unainigiliwa ni kweli
 
Mimi naamini kuna tofauti kubwa sana kati ya sheria na busara. Ni kweli hajatimiza matakwa ya kisheria hilo liko wazi.
Lakini tuwe wakweli, je hili kosa liliathiri vipi mchakato mzima wa upigaji kura? Pia nini hitaji la msingi la wapiga kura, ni mwakilishi wao au ni jina lake?
Nio maana nimesema hapa haijatumika busara hasa kwa mlalamikaji. Huyu ni mtu anayeguswa na maeldeleo ya jamii yake kweli? Endapo utaitishwa uchaguzi mwingine, ni nani atagharamikia.

Inavyooneka hoja ya mlalamikaji ni jina tu na tarehe za kula kiapo, sio vitu kama rushwa ambavyo vina influence kwa wapiga kura, vipi uchaguzi ukifanyika halafu watu wakamchagua yuleyule kwa kuwa wao wanahitaji kiongozi sio jina lake? Hatuoni kama haya ni matumizi mabaya ya fedha ya walipa kodi wenzake. Ama kweli siku hizi wanaotaka madaraka wapo kibinafsi zaidi kuliko wanavyotuaminisha. Mambo mengine aibu kweli.
 
haya kama mmeshinda fanyeni mabadiliko sio tu mnalidhika kwa kwenda mahakamani..
 
Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini.

Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.

nyege mbaya sana!
 
Me sioni kama jina ni tatizo ila naamini kwajinsi ulole anavyokubarika ata burembo atoe gari kwa kila mtu wa kata ya k*nyama awezi kushinda namjua bulembo
 
Maandiko ya kijinga namna hiyo ndio yanawakosesha haki, jaribu kuwa na nidham ya kuandika kwanza ndipo utapomuelewa Hakim kamaanisha nini. Kama wewe unashindwa kufata utaratibu wa kuandika uliofunzwa na Mwalim wako darasani ukaona kuandika utakavyo wewe ndio bora, ujuwe hayo ndio anayaongea Hakim "kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria", matakwa ya kisheria ni pamoja na namna ya kuandika karatasi za kutumia kisheria na mpaka "spacing na indent" hutumika zilizoainishwa kisheria, si kujiandikia tu utakavyo, msifikiri waliowawekea mitaala ya kuwafundisha namna ya kuandika walifanya makosa, wanajuwa huko mbele mtakumbana na nini. Wewe kwa jinsi ulivyoandika hufai hata kidogo kuitetea hii hoja hapa JF mliambiwa muwache kutumia namna hizo za maandishi, hamsikii.
MUWACHE NI Kihindi au kichina? YN MM NINGEKUA WW NINGEACHA KIHEREHERE CHA KUJIDAI NAJUA. we hujui na hujui km hujui hvy ww ni mpu.mbavu.
 
MUWACHE NI Kihindi au kichina? YN MM NINGEKUA WW NINGEACHA KIHEREHERE CHA KUJIDAI NAJUA. we hujui na hujui km hujui hvy ww ni mpu.mbavu.

Mie niite upendavyo wala hunishtuwi ndio kwanza unanipa hamasa ya kuendelea kuwapa darsa watu kama wewe. Naona darsa limekuingia, laiti lingekuwa halijakuingia usinge ng'aka. Kuhusu hayo maneno yako yaki sms, ni utawala wa JF ambao walitangaza hawayataki. Ukiendelea wanakuona humu, watakulamba ban halafu useme oohhh sijaambiwa. Ohhhooo shauri lako.
 
Mie niite upendavyo wala hunishtuwi ndio kwanza unanipa hamasa ya kuendelea kuwapa darsa watu kama wewe. Naona darsa limekuingia, laiti lingekuwa halijakuingia usinge ng'aka. Kuhusu hayo maneno yako yaki sms, ni utawala wa JF ambao walitangaza hawayataki. Ukiendelea wanakuona humu, watakulamba ban halafu useme oohhh sijaambiwa. Ohhhooo shauri lako.

sasa darsa ndio nini? Vibibi vingine bwana! Ndo nyie 20 years post menopause lakini bado mnavaa vimini,aafu mnalalama eti mabinti wa siku hizi wanavaa vibaya!
 
sasa darsa ndio nini? Vibibi vingine bwana! Ndo nyie 20 years post menopause lakini bado mnavaa vimini,aafu mnalalama eti mabinti wa siku hizi wanavaa vibaya!

Darsa ndio darsa, na nnadhani hata nawe umefaidika, hivi bado wanavaa? siye huko hatuko kabisa, siye tuko kwenye stara. Tunajistiri.
 
Back
Top Bottom