Mtondoli
Member
- Nov 9, 2021
- 70
- 174
Inawezekana mkanipinga kama ilivyokawaida yenu huwa hampendi kuambiwa ukweli. Chadema hii ni ya vijana waoga sana sana, wako Dkt. Slaa CHADEMA walikuwa wakitangaza maandamo yanakuwa maandamano kweli. Watu walikuwa wanasafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine kushiriki maandamano. Si kwamba vitisho havikuwepo la hasha vilikuwepo, polisi walikuwepo,matumizi ya bullet yalikuwa zaidi ya sasa.
Nilikuwepo Arusha kwenye maandamo yaliyokuwa yameitishwa na chadema, viongozi walikuwa mstari wa mbele wakiwa na vitambaa vyeupe nakumbuka Dkt. Slaa aliongoza hayo maandamano, akiwemo Freeman Mbowe, Godbess Lema, Mzee Ndesamburo, watu walisafiri kutoka mikoa yote Tanzania kuja kusapoti maandamano hayo.
Nchi ilizizima huku polisi wakiendelea kupiga mikwara ya kutisha kabisa, umati wa watu ulifunga barabara karibia kila sehemu, watu walifunga maduka wakaja kuungana na wanamageuzi wenzao chadema, kama ilivyo ada polisi walianza kurusha risasi ovyo na mabomu ya machozi, wengine walipata kipigo akiwemo na mke wa Dkt. Slaa, Josephine Mushumbusi aliumizwa vibaya Sana
Kuna vijana walikufa na wakazikwa kishujaa na bendera za chama zikapepea nusu mlingoti. Hiyo haikuwatisha maandamano yaliendelea kila mahari. Nasema nyinyi vijana wa sasa hamuisaidii demokrasia mkiwa waoga namna hiyo
Kwa suala la Mbowe mpaka leo pangekuwa hapatoshi, nani wa kuwa mstari wa mbele kututia morali ya kutokuogopa vitisho vya polisi? Hayupo ni Dkt. Slaa peke yake ndie angethubutu, CHADEMA mmepoteza watu muhimu sana kwa ajili ya mkate wa siku moja, mrudisheni Dkt Slaa mtaona jinsi mpinzani anavyotakiwa awe.
Nilikuwepo Arusha kwenye maandamo yaliyokuwa yameitishwa na chadema, viongozi walikuwa mstari wa mbele wakiwa na vitambaa vyeupe nakumbuka Dkt. Slaa aliongoza hayo maandamano, akiwemo Freeman Mbowe, Godbess Lema, Mzee Ndesamburo, watu walisafiri kutoka mikoa yote Tanzania kuja kusapoti maandamano hayo.
Nchi ilizizima huku polisi wakiendelea kupiga mikwara ya kutisha kabisa, umati wa watu ulifunga barabara karibia kila sehemu, watu walifunga maduka wakaja kuungana na wanamageuzi wenzao chadema, kama ilivyo ada polisi walianza kurusha risasi ovyo na mabomu ya machozi, wengine walipata kipigo akiwemo na mke wa Dkt. Slaa, Josephine Mushumbusi aliumizwa vibaya Sana
Kuna vijana walikufa na wakazikwa kishujaa na bendera za chama zikapepea nusu mlingoti. Hiyo haikuwatisha maandamano yaliendelea kila mahari. Nasema nyinyi vijana wa sasa hamuisaidii demokrasia mkiwa waoga namna hiyo
Kwa suala la Mbowe mpaka leo pangekuwa hapatoshi, nani wa kuwa mstari wa mbele kututia morali ya kutokuogopa vitisho vya polisi? Hayupo ni Dkt. Slaa peke yake ndie angethubutu, CHADEMA mmepoteza watu muhimu sana kwa ajili ya mkate wa siku moja, mrudisheni Dkt Slaa mtaona jinsi mpinzani anavyotakiwa awe.