*CHADEMA YA MBOWE NA MFANO WA UDIKTETA "AT ITS OWN BEST"*
Tribute to David Silinde et. al.
Na Mwamba Wa Kaskazini
Leo naanza kwa methali ya huko majuu kwamba "what goes around, comes around"
Chadema kwa miaka minne hii wamekuwa wakitekeleza demokrasia yao vizuri tu chini ya Serikali ya Awamu ya Tano; wakifanya vikao vyao vya chama, wakikutana na wanahabari na wakihudhuria Bunge, ikiacha mengine mengi, lakini bado wamekuwa wakiipaka nchi natope kuwa ni ya kidikteta!
Sasa kweli lisemwalo sana kama halipo basi linakuja na limekuja kivingine; yaliyowakuta wote waliokwenda kinyume na Mbowe hayajatosha kuwaonesha udikteta wa Mbowe na Chadema sasa leo mmejionea.
Leo kisa cha wabunge kadhaa wa Chadema kutokubaliana na uamuzi wa kiimla wa Mbowe wa kuwataka waondoke Bungeni eti kisa Corona, na kisha wabunge hao wakaanza kusakamwa na wapambe wa Mbowe ni uthibitisho sasa kuwa Mbowe ni mpinzania dikteta anayesubiri tu kuwaangamiza watu zaidi!
Kwanza uamuzi wake wa kuwazuia wabunge kwenda kazini kwao (Bungeni) hata mimi ningekuwa mbunge nisingeutekeleza; ni wa kisanii na kibabaishaji.
Yani unawatoa wabunge Bungeni palipowekewa kila aina ya kinga dhidi ya Corona halafu unawaacha wakusanyike baa jioni ambako hata maji tiririka hakuna
Wabunge wengi wa Chadema wameonekana wakizurura mitaani Dodoma, wengine wakienda majimboni na kujichanganya na wananchi-hapa wanajilinda nini?
Mtoto wa Mbowe alipata Corona (na madaktari wa Serikali katika hospitali ya Serikali ndio wakamhudumia hadi akapona), alipata Bungeni??
Lakini Mbowe wakati akiwaingiza mkenge wabunge wake wasipate kipato na hata kufubaa kisiasa kwa kutoingia Bungeni, ni Mbowe huyo huyo wafanyakazi wa taasisi zake binafsi zinazomuingizia hela hajawapeleka "karantini." Kawaacha wamuingizie hela, aendelee kupiga hela!
Wafanyakazi wa gazeti lake la Tanzania Daima, wako kazini, wafanyakazi wake kwenye hotel za familia yake za Aishi Machame wako kazini, ila wabunge wa Chama chake eti anawazuga waondoke Bungeni "wakajikarantini."🤦🏽🤦🏽Huyu bogus sana.
Sasa leo nakupa "tribute" Silinde kwa kujivua nafasi zako za uongozi wa Chadema hasa za kibunge (ila ubunge haujajivua mwanangu safi, kwa nini ukose kiinua mgongo chako bana miaka mitano ishafika).
Wewe ni shujaa mwingine mpinga udikteta wa ndani ya Chadema. Wewe ni limbuko la wengi.
Ndio ni wewe!
Sent from my iPhone using JamiiForums
Tribute to David Silinde et. al.
Na Mwamba Wa Kaskazini
Leo naanza kwa methali ya huko majuu kwamba "what goes around, comes around"
Chadema kwa miaka minne hii wamekuwa wakitekeleza demokrasia yao vizuri tu chini ya Serikali ya Awamu ya Tano; wakifanya vikao vyao vya chama, wakikutana na wanahabari na wakihudhuria Bunge, ikiacha mengine mengi, lakini bado wamekuwa wakiipaka nchi natope kuwa ni ya kidikteta!
Sasa kweli lisemwalo sana kama halipo basi linakuja na limekuja kivingine; yaliyowakuta wote waliokwenda kinyume na Mbowe hayajatosha kuwaonesha udikteta wa Mbowe na Chadema sasa leo mmejionea.
Leo kisa cha wabunge kadhaa wa Chadema kutokubaliana na uamuzi wa kiimla wa Mbowe wa kuwataka waondoke Bungeni eti kisa Corona, na kisha wabunge hao wakaanza kusakamwa na wapambe wa Mbowe ni uthibitisho sasa kuwa Mbowe ni mpinzania dikteta anayesubiri tu kuwaangamiza watu zaidi!
Kwanza uamuzi wake wa kuwazuia wabunge kwenda kazini kwao (Bungeni) hata mimi ningekuwa mbunge nisingeutekeleza; ni wa kisanii na kibabaishaji.
Yani unawatoa wabunge Bungeni palipowekewa kila aina ya kinga dhidi ya Corona halafu unawaacha wakusanyike baa jioni ambako hata maji tiririka hakuna
Wabunge wengi wa Chadema wameonekana wakizurura mitaani Dodoma, wengine wakienda majimboni na kujichanganya na wananchi-hapa wanajilinda nini?
Mtoto wa Mbowe alipata Corona (na madaktari wa Serikali katika hospitali ya Serikali ndio wakamhudumia hadi akapona), alipata Bungeni??
Lakini Mbowe wakati akiwaingiza mkenge wabunge wake wasipate kipato na hata kufubaa kisiasa kwa kutoingia Bungeni, ni Mbowe huyo huyo wafanyakazi wa taasisi zake binafsi zinazomuingizia hela hajawapeleka "karantini." Kawaacha wamuingizie hela, aendelee kupiga hela!
Wafanyakazi wa gazeti lake la Tanzania Daima, wako kazini, wafanyakazi wake kwenye hotel za familia yake za Aishi Machame wako kazini, ila wabunge wa Chama chake eti anawazuga waondoke Bungeni "wakajikarantini."🤦🏽🤦🏽Huyu bogus sana.
Sasa leo nakupa "tribute" Silinde kwa kujivua nafasi zako za uongozi wa Chadema hasa za kibunge (ila ubunge haujajivua mwanangu safi, kwa nini ukose kiinua mgongo chako bana miaka mitano ishafika).
Wewe ni shujaa mwingine mpinga udikteta wa ndani ya Chadema. Wewe ni limbuko la wengi.
Ndio ni wewe!
Sent from my iPhone using JamiiForums