CHADEMA wateka desemba 9, CCM washindwa kujinadi maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Sherehe za uhuru wa "TANGANYIKA" zimedoda. Mitaani watu hawana habari kwani wanaona mafanikio ya uhuru yamekuwa neema kwa wachache huku wengi wakiachwa kwenye wimbi la ujinga,maradhi na umasikini kinyume na ilivyotarajiwa na waasisi wa uhuru mnamo tar.9.12.1961. Bila shaka yoyote, waasisi wa taifa la Tanganyika haswa Mwl.Nyerere waliweka misingi ya kujenga taifa lenye usawa,uzalendo,mshikamano na uchapaji kazi ili kuleta maendeleo ya uchumi kwa watu wote na kuinua hali ya maisha ya watu. Ashakum si matusi, CCM wakawa wana wapotevu waliorithi nyumba yenye misingi mizuri na kuanza kuibomoa.Ndipo miiko ya uongozi ilipofutwa na maadili yake, viwanda vikafa kwa sera mbovu na hata kilimo kusuasua. Leo hii CCM (Wajamaa) hunadi Kilimo Kwanza huku somo la kilimo katika shule zetu likipewa kisogo.CCM wako busy na CHADEMA na kusahau kujinadi japo kwa machache waliyofanya, wamepoteza dira!
 
Imenishangaza sana, headline za Magazeti leo ni Mandela na Dr.Slaa CHADEMA, utafikiri sio siku ya uhuru.....kama Ni Strategy ya media CDM wameshinda........sorry nilikuwa namaanisha kushinda na sio kushindwa.....
 
Imenishangaza sana, headline za Magazeti leo ni Mandela na Dr.Slaa CHADEMA, utafikiri sio siku ya uhuru.....kama Ni Strategy ya media CDM wameshindwa...

He kwahiyo unamaamisha cdm wangezunguka kwenye media wawakumbushe kuwa leo ni siku ya uhuru, amka basi unyanyue akili zako uweke kichwani
 
Haki sawa; Katika tasnia ya habari kuna msukumo wa mambo yanayofanya habari ipewe kipaumbele.CCM wameshindwa kutumia fursa hii na kuuthibitishia umma kwamba wanaendesha nchi kwa mfumo wa bora liende.Unadhani wangebuni kitu na kukizindua siku kama ya leo media zisingeandika? They have a very poor PR campaigns to discover headlines making opportunities.Na hii yote ni matokeo ya laana ya ufisadi inayoua ubunifu!
 
Last edited by a moderator:
Hivi leo kumbe sikukuu ya uhuru dah!

Uhuru wa bendera hatusherekei upuuzi, watanganyika tuendelee kutafuta uhuru wa kweli, tuchape kazi.

Waacheni wapumbavu waadimishe uhuru wa gwaride ..mpavu zao!!
 
Hivi leo kumbe sikukuu ya uhuru dah!

Uhuru wa bendera hatusherekei upuuzi, wanganyika tuendelee kutafuta uhuru wa kweli, tuchape kazi.

Waacheni wapumbavu waadimishe uhuru wa gwaride ..mpavu zao!!

Na hii nayo ni sera ya CHADEMA?
 
Hivi leo kumbe sikukuu ya uhuru dah!

Uhuru wa bendera hatusherekei upuuzi, wanganyika tuendelee kutafuta uhuru wa kweli, tuchape kazi.

Waacheni wapumbavu waadimishe uhuru wa gwaride ..mpavu zao!!
Utakufa hivyo hivyo huku watz na ccm yao wakisherehekea uhuru wa nchi yao
 
Mungi; Mkuu habari za siku? Mtaani kwetu watu hawana muda kabisa na sherehe, kwanza wanahoji inakuwaje tusherehekee uhuru wa nchi ambayo CCM hawaitaki kama ambayo walijinasibu wakipinga serikali tatu kwenye katiba mpya?
 
Last edited by a moderator:
Hivi leo kumbe sikukuu ya uhuru dah!

Uhuru wa bendera hatusherekei upuuzi, wanganyika tuendelee kutafuta uhuru wa kweli, tuchape kazi.

Waacheni wapumbavu waadimishe uhuru wa gwaride ..mpavu zao!!

Wa upumbavu huu wa michagadema ndio mana slaa amepigwa kigoma
 
Mungi; Mkuu habari za siku? Mtaani kwetu watu hawana muda kabisa na sherehe, kwanza wanahoji inakuwaje tusherehekee uhuru wa nchi ambayo CCM hawaitaki kama ambayo walijinasibu wakipinga serikali tatu kwenye katiba mpya?
Kamuokoeni slaa anapigwa kg
 
Tanganyika bado inatawaliwa na hivyo haipo kabisa,sasa kusherehekea kitu ambacho hakipo ni akili kweli?
Tuitafute Tanganyika kwanza ndio tupate sababu ya kusherehekea
 
Kamuokoeni slaa anapigwa kg

Dr. Slaa hawezi kupigwa na washenzi, kakindi kadogo cha kipumbavu kinatafuta umaarufu eti Slaa anpigwa!!!!
Hata mungemwua bado isingewasaidia kurudisha spirit ya watu nyuma, sana sana mngechochea moto wa mapinduzi
 
tamuchungu; Punguza munkari Mkuu, labda utupe ufafanuzi kidogo juu ya maswala matatu haya; 1.Kwanini msisimko wa sherehe za uhuru wa Tanganyika hupungua kwa kasi kila mwaka? 2.Kwanini vyombo vya habari havijatoa kipaumbele kuhusu jambo hili zaidi ya yahusuyo CHADEMA na msiba wa Mzee Madiba? 3.Ni kwa kadri gani ujamaa na kujitegemea unaenziwa ukilinganisha na sera mpya kama ubinafsishaji,utandawazi na uwekezaji? Karibu tena!
 
Last edited by a moderator:
Siku ya uhuru tayari imeshapoteza mvuto wake labda kwa wafungwa waliopo Magerezani ambao wanasubiri msamaha wa rais ndiyo wataiona faida kwao.
 
You remind me of the 9. 12.1961: nishasahau kabisa cuz kila kitu kwenye media ni CDM NA DR.SLAA. Hii ina maanisha uhuru bado haujapatika ndio maana watu wako busy kuutafuta kupitia CDM,ccm nao wako busy kutetea ujinga ili waendelee kuwa madarakani kwa kuwapumbaza watu wasione madhaifu yao. Wanakesha wakiropoka hili na lile kuhusu dr.slaa na CDM, WAMESAHAHAU WAJIBU WAO KWA MTANZANIA.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom