Joss
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 765
- 191
Kwa mujibu wa katiba yetu,mshindi wa nafasi ya urais akitangazwa hakuna chombo chenye mamlaka ya kuhoji.Kwa namna hiyo basi nawashauri viongozi wa Chadema,kama sheria inaruhusu wawasilishe pingamizi mahakamani juu ya usitishwaji wa kutangaza matokeo halafu wafungue kesi ya uchakachuaji wa kura.Naamini kwa muda wote tangu kukamilika kwa majumuisho ya kura kwenye majimbo watakuwa wamekusanya ushahidi wa kutosha kuhusiana na uchakachuaji.
Ushahidi mwingine unaweza kuwa wazi kwa kuwa fomu zote zilizosainiwa na mawakala pamoja na wasimamizi zipo.Pia yaweza angalia idadi ya wapiga kura kutofautiana na matokeo yanayotolewa na NEC.
Chondechonde,msituangushe wapiga kura maadam mmeyakataa matokeo na mnatakwimu zote basi mwende mbele.Sisi tupo nyuma yenu.
Jumuiya za kimataifa zimekuwa na upofu katika kufanya tathimini halisi ya uchaguzi na jinsi umafia wa uchakachuaji ulivyofanyika hivyo naomba sana tusiwategemee kutoa tamko lolote.
Mungu awe pamoja nasi !!!!
Ushahidi mwingine unaweza kuwa wazi kwa kuwa fomu zote zilizosainiwa na mawakala pamoja na wasimamizi zipo.Pia yaweza angalia idadi ya wapiga kura kutofautiana na matokeo yanayotolewa na NEC.
Chondechonde,msituangushe wapiga kura maadam mmeyakataa matokeo na mnatakwimu zote basi mwende mbele.Sisi tupo nyuma yenu.
Jumuiya za kimataifa zimekuwa na upofu katika kufanya tathimini halisi ya uchaguzi na jinsi umafia wa uchakachuaji ulivyofanyika hivyo naomba sana tusiwategemee kutoa tamko lolote.
Mungu awe pamoja nasi !!!!