CHADEMA washitukiwa wakitaka kuvuruga mkutano CCM

Masatu

JF-Expert Member
Jan 29, 2007
3,276
125
CHADEMA washitukiwa wakitaka kuvuruga mkutano

Habari Zinazoshabihiana
• Mwanry akamia kumfuatilia Mbowe 10.01.2007 [Soma]
• Polisi yachunguza kauli za Mbowe, Kabwe 07.09.2007 [Soma]
• mabadiliko ya jina la Wizara yaibua mjadala mkubwa 24.03.2006 [Soma]

*Wadaiwa kupanga kikundi cha kuzomea wana CCM

Na Francis Godwin, Iringa

MKUTANO wa viongozi wa CCM waliokuwa katika ziara ya kuelezea utekelezaji wa Ilani ya chama hicho mkoani wa hapa umeingia dosari baada ya kikundi cha wapinzani wakiongozwa na Katibu wa CHADEMA wa Mkoa, Bw. Paschal Bella, kuanzisha vurugu dakika za mwisho kwa lengo la kuvuruga mkutano huo.

Mbali ya tukio hilo, pia aliyekuwa kamishina wa NCCR -Mageuzi wa Mkoa wa Iringa, Bw. Hussein Mwaikambo, alirudisha kadi ya chama hicho kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Bw. Aggrey Mwanri na kujiunga CCM, kwa madai kuwa Upinzani hauna sera na ubinafsi umetawala katika vyama hivyo.

Bw. Bella na wenzake, walifikia hatua hiyo baada ya kada wa CCM, Bw. Shaibu Akwilombe, ambaye awali alikuwa kiongozi wa juu wa CHADEMA, kusimama katika jukwaa hilo na kuelezea upungufu ndani ya chama hicho.


Kutokana na hali hiyo, kikundi hicho kikiongozwa na kiongozi huyo kilipinga kwa sauti kubwa tuhuma za Bw. Akwilombe dhidi ya CHADEMA kuwa hazina ukweli wowote.

"Si kweli, mwongo huyo CHADEMA haiko hivyo... tunataka mjibu hoja za wapinzani dhidi ya mkataba wa mgodi wa Buzwagi, si kuishambulia CHADEMA," walisema wanakikundi hao.

Hata hivyo, kabla hawajaendelea makamanda wa CCM na baadhi ya wananchi waliwafuata na kuwaondoa kwa nguvu katika mkutano huo, huku baadhi yao wakitaka wawape kipigo kwanza ili liwe fundisho.

Kiongozi huyo wa CHADEMA na wenzake, waliokolewa na baadhi ya wasamaria wema kwa kuondolewa katika eneo la viwanja vya Mwembetogwa, ambako mkutano huo uliokuwa.

Ilidaiwa kuwa lengo la kikundi hicho kufika katika mkutano huo, lilikuwa ni kuwazomea viongozi hao, lakini kutokana na kuonywa na Katibu wa CCM wa Mkoa, Bw. Kilumbe Ng'enda kuwa atakayejaribu kufanya fujo katika mkutano huo atakiona cha moto, azma hiyo ilishindikana.

Baadhi ya wana CCM walililalamikia Jeshi la Polisi kwa kushindwa kuweka ulinzi wa kutosha katika mkutano mkubwa kama huo, tofauti na ilivyokuwa kwa wapinzani ambapo ulinzi ulikuwapo wa kutosha.

Wakati huo huo, uongozi wa CCM Taifa umesema jitihada za Rais Jakaya Kikwete katika kuliongoza Taifa zinaonekana kwa kila Mtanzania na wasio Watanzania katika kuiwezesha nchi kung'ara vyema ulimwenguni na kuwaonya wapinzani kuacha kuchafua jina lake.

Ulisema Rais hawezi kukurupuka kuwachukulia hatua wabadhirifu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) bila kuwa na uhakika wala uchunguzi wa kutosha kufanyika, kwani anaongoza nchi kwa kuzingatia misingi ya demokrasia tofauti na wapinzani wanavyotarajia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Bw. Aggrey Mwanri, alitoa onyo hilo wakati akizungumza na wakazi na wana CCM wa manispaa ya Iringa katika uwanja wa Mwembetogwa.




Kidogo kidogo ukweli utadhihiri.....
 
sasa tatizo ni nini? kwani kunamtu aliyesema kuwa wanaozomea wanatoka chama gani. Sisi tunachojua wananchi wale wale waliokuwa wanauzulia mikutano ya hadhara miaka ya nyuma na kuambiawa utumbo sasa wenginewo wamestuka na hawataki tena wameanza kuzomea.

na ukimwona mtu anazomea ujue basi amechoka na hicho chama na mara nyingi atakuwa ameshaamua kujiunga na chama kingine. usitegemee wewe, kada mpinzani kili time na mtu wa pwani(sijui bagamoyo) mnaweza kuzomea kwenye hiyo mikutano, la hasha, kwa sababu nyie mnakubariana na huo ufisadi na mko tayari kuutetea.

Sasa kidogo kidogo ukweli utadhirik, ukweli upi wakati sisi tunaoipinga serikali ndiyo tunazomea na tuna vyama vingine sasa kikiwamo chadema. Kwa akili yako ulidhani wanaozomea ni ccm kama ulidhani hivyo basi wewe ni wale mapungua... wanaozomea ni wananchi waliochoka
 
Hivi wapinzani siyo Watanzania? au ni watanzania nusu? Ni nani aliyesema kuwa ukiwa mwana CCM basi una haki za ziada?
 
eti wanaozomea ni wapinzani?hahahaha,just give me a break,
basi kama ule umati wote ambao huwa unazomea ni upinzani,basi mambo safi sanaaaaaaaaaa,kuna nguvu kubwa kwa upinzani.
 
hao hao wanapenda sana kutrivialize mambo,mbona hao "wapinzani" hawajaongea lolote pale ambapo "mamia" ya watu "walipofurika" JKN Airport "kumpokea" Muungwana baada ya ziara ndefu ya ughaibuni kwenda "kuitangaza" Tanzaia?Wakati "umati" ule ulikuwa umevaa kijani na njano?

CCM bwana too childish,yaani ni kama vile watoto...
 
hao hao wanapenda sana kutrivialize mambo,mbona hao "wapinzani" hawajaongea lolote pale ambapo "mamia" ya watu "walipofurika" JKN Airport "kumpokea" Muungwana baada ya ziara ndefu ya ughaibuni kwenda "kuitangaza" Tanzaia?Wakati "umati" ule ulikuwa umevaa kijani na njano?

CCM bwana too childish,yaani ni kama vile watoto...

Ibambasi kwa taarifa yako ule umati pia ulikuwa wa kupikwa.. watu wameokotezwa vijiweni wakakatiwa hela ya ugali na kuvaa tshirt kumlaki mhishimiwa saaaana! kwani asingekuta maadamano na umati ule asingejisikia kuwa ndiye mkuu!
 
Sasa kidogo kidogo ukweli utadhirik, ukweli upi wakati sisi tunaoipinga serikali ndiyo tunazomea na tuna vyama vingine sasa kikiwamo chadema. Kwa akili yako ulidhani wanaozomea ni ccm kama ulidhani hivyo basi wewe ni wale mapungua... wanaozomea ni wananchi waliochoka

Sasa na wasiowapinga serikali na ambao sio Chadema wakienda ktk mikutano wa Chadema na kufanya kazi ya kuzomea itakuwa siasa au SI HASA!
 
acheni ujinga na upofu hivi wapinzani wao hawazomewi kwakuwa wana uwezo wa Mungu kuzuia kuzomewa?

hivi nikija kwako ukanizomea nitasema ulikodi jirani yako kuja kunizomea? hautakuwa wewe?

acheni ujuaji CCM haina mvuto tena!

makamba anawapa nafasi ndugu zake atazomewa na kundi lake lote!

CCM pamoja na ruzuku yote ile mbona hawanunui watu wa kushangilia ili wawazidi chadema wanaozomea?

huu ni utoto hata nyie watu wenye upeo hadi kutumia mtandao leo hii mnaongea ujinga tu?

ninasema watu wa Tanzania baadhi yetu tumelaaniwa na hawa kina makamba na kikwete!

eti umewahi kusikia wapi chama tawala na serikali iliyopata ushindi wa asilimia 80 leo wanazomewa? hii ni aibu ya milele!

siku imefika sio nyingi maandamano yankuja tutajua kama kuandamana pia wamekodiwa!

wanafiki wote mtakwisha!
 
hawa chadema huchemka mara nyingi tu. hata bado wanalo mwaka huu. weshalikoroga ni kulinywa tu
 
Waheshimiwa waleta hoja, unajua siku za kati ya wiki ni za kazi, na ni vyema kuleta thread na hoja za maana kujadiliwa kama hazipo muache ili tupige mzigo kuikomboa Tanzania,

Hoja kama hizi zinatakiwa zije ijumaa jioni hivi,,, ili wakati wengine wanaenda kwenye ngwasuma, melody, TOT Plus, wengine tunachanganua mambo ya nnji hapa...
 
Hivi wapinzani siyo Watanzania? au ni watanzania nusu? Ni nani aliyesema kuwa ukiwa mwana CCM basi una haki za ziada?

hili ndio jambo ambalo nadhani wengi hawalijui, wanadhani kwamba ukiwa chadema, cuf ndio mpinzani ! sasa nauliza mpinzani ni nani ? yule anayepingana na sera za ccm au ? maana najua kuna wanaccm wengine wanapingana na sera za ccm vile vile, hata republican mccain anapingana na akina bush kila siku anapingana na bush na sio mpinzani !
 
hili ndio jambo ambalo nadhani wengi hawalijui, wanadhani kwamba ukiwa chadema, cuf ndio mpinzani ! sasa nauliza mpinzani ni nani ? yule anayepingana na sera za ccm au ? maana najua kuna wanaccm wengine wanapingana na sera za ccm vile vile, hata republican mccain anapingana na akina bush kila siku anapingana na bush na sio mpinzani !

wewe nawe na mccain! teh teh teh
 
Sasa na wasiowapinga serikali na ambao sio Chadema wakienda ktk mikutano wa Chadema na kufanya kazi ya kuzomea itakuwa siasa au SI HASA!

Masatu kazi unayo. Umebeba zigo lote walilokimbia akina tafiti, kulikoni, chinga, mgongo, and the likes. Unaweza kuzeeka kabla ya umri wako. Au nawe utakimbia kama wapiga debe wenzio?
 
"Si kweli, mwongo huyo CHADEMA haiko hivyo... tunataka mjibu hoja za wapinzani dhidi ya mkataba wa mgodi wa Buzwagi, si kuishambulia CHADEMA," walisema wanakikundi hao.

Misitari hapo juu inaonyesha kwamba hawa wanakikundi walitaka ijibiwe hoja ya buzwagi, si ngonjera kuhusu Chadema ambazo tayari wameshajibiwa kwamba hata ccm ni ya ukoo pia.

Binafsi nawaona hawa wanakikundi walikuwa wanawakilisha mawazo ya kitaifa si kichama. watanzania kwa sasa wanataka kujua serikali inasema nini kuhusu tuhuma za ufisadi na si ngonjera za mufilisi kina Akwilombe na Hizza.

Kila wanakoenda wimbo wao haubadiliki, hata wasikilizaji wanaboreka. siasa zinataka ubunifu wa Lugha si Ngonjera zile zile kila wakati. hata viongozi wanaondamana nao nadhani hawajui kwenda na wakati ama upeo wao wa kupambanua mambo ni mdogo. kwa maana nyingine wanatudhihirishia kwamba kasoro ya chadema ni kupeana uongozi basi, vinginevyo kwenye maeneo mengine Chadema ni safi.
 
Masatu kazi unayo. Umebeba zigo lote walilokimbia akina tafiti, kulikoni, chinga, mgongo, and the likes. Unaweza kuzeeka kabla ya umri wako. Au nawe utakimbia kama wapiga debe wenzio?

Tutabanana humu humu mpaka kieleweke!
 
Swala hapa sio kuzomea ila kuwakatalia pale CCM wanaposema uongo.Hivi wanaozomea bungeni wakati wapinzani wanawakilisha hoja huwa ni akina nani kama sio CCM.Kama ni mchezo mchafu CCM ndo mmeanza,sasa mnaona inauma kwa vile mlizoea "ndiyo mzee"
 
Back
Top Bottom