Naipongeza ccm kwa serikali yake kuacha kung'ang'aania kuzika marehemu wasiowahusu. Wao na serikali wanashutumiwa na wafiwa kama wauaji cha kustaajabisha wanang'ang'ania kuzika eti wafiwa watapata ujiko kisiasa.Wana Jf,
Kama mtakumbuka waziri mkuu juzi alitoa kauli ya serikali kuwa itagharamikia mazishi ya waliofariki katika milipuko ya mabomu na risasi Arusha.
Taarifa iliyothibitishwa ni kwamba Ndugu wa Marehemu wote wawili wamekataa serikali kujihusisha na mazishi ya ndugu zao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti ndugu hao wamesikitishwa na kitendo cha kushawishiwa kuwakataa CHADEMA, wamesema wao wapo na CHADEMA kwa kuwa wao pia ni wafiwa katika tukio ambalo lilitokea kwenye mkutano wao.
Leo hii miili ya marehemu wote zimesafirishwa kwenda makwao Tanga na Tabora, ambapo Mbunge Rose Kamili ndiye aliyeshughulikia taratibu zote ikiwa pamoja na kulipia gharama za usafiri, chakula na malazi kwa wote waliosafirisha miili ya ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki.
Coster zote zimeondoka mapema leo kuelekea kwenye maziko.
Naipongeza ccm kwa serikali yake kuacha kung'ang'aania kuzika marehemu wasiowahusu. Wao na serikali wanashutumiwa na wafiwa kama wauaji cha kustaajabisha wanang'ang'ania kuzika eti wafiwa watapata ujiko kisiasa.
Hujanielewa mkuu, tuko pamoja..Hivi ni siasa zimefanya baadhi yetu kuwa Na roho Za paka kiasi hiki? .. Ni Siasa tu AMA kingine? Huyu hawezi kuwa Mtanzania Wala sidhani Kama ni binaadam inasadikiwa Kwamba kuna majini yamevaa miili ya watu nao ni member humu JF. You must be the one...