Chadema wapi Halima Mdee?

Endeleaaa

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
1,485
738
Pengine nipo nyuma kitaarifa. wana JF na chadema kwa ujumla sijamuona mh. Mbunge Halima Mdee kwa muda. Mdee alikuwa changamoto nyingine ndani ya Bunge baada ya Zitto lakini kwa sasa hasikiki wala kuonekana. Chadema kulikoni. Watanzania wengine tungefurahia kujua kulikoni.

Kwa wanaojua wasifu wa huyu mwanadada aliyekuwa mwiba kwenye kikao cha bajeti cha mwaka jana tushushieni na wengine tumjue vizuri zaidi

Demokrasia Daima...
 
EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Community Development Diploma 2004 2005 DIPLOMA
University of Dar es Salaam Degree 1999 2003 GRADUATE
Kilakala High School A-Level Education 1996 1998 HIGH SCHOOL
Zanaki Secondary School O-Level Education 1992 1995 SECONDARY
Mlimani Primary School Primary Education 1985 1991 PRIMARY

--------------------------------------------------------------------------------
CERTIFICATIONS
Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
No items on list

--------------------------------------------------------------------------------
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
Ministry of Labour, Employment and Youth Development Development Officer 2004 2005

--------------------------------------------------------------------------------
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA Member of Parliament of Tanzania 2003 Todate


http://www.parliament.go.tz/bunge/Mp_Cv3.asp?PTerm=2005-2010&fpkey=340&vusername=GUEST")
 
Una maanisha kuwa yupo huku JF? LOL na inakuwaje kama yupo RSA na ni mwakilishi wa watu..anajigawaje kuhudhuria bunge nk, au labda pengine ana likizo? Just curious

nakuliliaTanzania, not just curious. You have right to ask, sababu anakula pesa kutoka kwa tax payer.
 
Yeye Ni Mpinzani Bwana Hamuwezi Kumuuliza Hata Kidogo Kwani Nyie Ni Wageni Hapa Tanzania ?

Mpinzani Akifanya Faulo Aachwe Tu Afanye Anachotaka
 
Kwani kwenda kusoma ni faulo? kuna mamia na maelfu mangapi ya waajiriwa wa serikali ambao sio wabunge wa upinzani, sio tu wanalipiwa ada ya shule bali mishahara yao yote inaendelea kulipiwa na tax payers? hizi ni hoja nyepesi sana. Sina hakika kama hiyo masters analipiwa na serikali, lakini hata kama yeye hatakuwa wa kwanza eti. Sidhani kama kutokuwepo kwake bungeni kwa sababu ya kutafuta elimu ni suala la kujadiliwa humu. Naamini ukosefu wa daktari pale Muhimbili kwa sababu ya kusomea Phd Ulaya ambayo inalipiwa na tax payers unanigusa zaidi kuliko kutokuwepo kwa Halima Mdee bungeni....
 
hili Chadema mmechemsha mkipewa uwakilishi wa wananchi ndio mnajua kuna ksasa tukisema kwa hili hakuna tofauti na hao CCM mnabisha kwa hoja ipi? acheni ubinafsi ukikubali kutetea watu watumikie kama unaona elimu kwanza nenda class
 
hili Chadema mmechemsha mkipewa uwakilishi wa wananchi ndio mnajua kuna ksasa tukisema kwa hili hakuna tofauti na hao CCM mnabisha kwa hoja ipi? acheni ubinafsi ukikubali kutetea watu watumikie kama unaona elimu kwanza nenda class

Kweli wewe ni mshamba wa kijijini! Kada pinzani ni mshamba wa mjini, inabidi mkutane mtoane ushamba shamba wenu!
 
Una maanisha kuwa yupo huku JF? LOL na inakuwaje kama yupo RSA na ni mwakilishi wa watu..anajigawaje kuhudhuria bunge nk, au labda pengine ana likizo? Just curious

.....mbunge wa singida LAZARO MALANDO...yule bw mdogo muda mwingi anautumia kula nondos marekani ...na akiwa na muda anahudhiria vikao bungeni..

degree za uzamili mbona hazina kokoro..mtu anaweza kula masters RSA ...na research akafnyia tanzania so muda mwingi akawa bongo...anakuwa anaenda college kila baada ya muda kufanya mitihani na kuhudhuria some lectures...hili jambo la kawaida kabisa kwa watu wa masters na phd...tatizo ni bachelors ..na hata ikiwa hiyo za correspondence zipo.....pia siku hizi kuna masters za executives ambazo ni convenient zaidi..kwa watu busy..

mwacheni binti ale nondo
 
.....mbunge wa singida LAZARO MALANDO...yule bw mdogo muda mwingi anautumia kula nondos marekani ...

..umenikumbusha wewe,huyu tapeli aliyetapeli watu Iowa na wa kujipendekeza kwa mama mkapa yuko wapi siku hizi? na anakula nondo gani hizo za masters maana hata degree ya kwanza alikuwa hajamaliza maana nasikia anasema ana degree,hii sampuli ndio viongozi wa bongo yaani kanyaboya tupu,mungu atusaidie tuu.
 
nakuliliaTanzania, not just curious. You have right to ask, sababu anakula pesa kutoka kwa tax payer.

Mtanganyika, thanks for ur not. Well, vile sina facts nyingi kuhusu hiyo safari yake ya bondeni, nani anamlipia nk, na kuna arrangements gani, ndo nikaona bora kwanza niwe curious kupata informations zaidi then niweze kutoa kwa mapana mawazo yangu
 
.....mbunge wa singida LAZARO MALANDO...yule bw mdogo muda mwingi anautumia kula nondos marekani ...na akiwa na muda anahudhiria vikao bungeni..

degree za uzamili mbona hazina kokoro..mtu anaweza kula masters RSA ...na research akafnyia tanzania so muda mwingi akawa bongo...anakuwa anaenda college kila baada ya muda kufanya mitihani na kuhudhuria some lectures...hili jambo la kawaida kabisa kwa watu wa masters na phd...tatizo ni bachelors ..na hata ikiwa hiyo za correspondence zipo.....pia siku hizi kuna masters za executives ambazo ni convenient zaidi..kwa watu busy..

mwacheni binti ale nondo

PM, heshima mbele mkuu,

Hakuna tatizo na kula kwake hiyo Masters, ila kwa vile hapa imetolewa taarifa kuwa yupo RSA, anasoma, ndo tunahoji, je ni kwa taratibu zipi, anapata muda wa kuhudhuria bunge? Kumbuka huyu ni mbunge, mwakilishi wa watu

Jingine ni hizo masters za correspondence..without prejudice, nisingependa Mh Halima aingie kwenye mkumbo wa PWU kama unakumbuka....so tunaweza kuomba kujua, kama anasomea nini na anafata utaratibu upi...full time ama part time, anagawaje muda wake?

Ninakumbuka Mh Mbowe anasome UK...Mzee Sumaye kamaliza juzi juzi pale Havard ...so hakuna tatizo kabisa kwa mtu yeyote kujiendeleza kielimu...ila in which framework?
 
..Halima Mdee hawakilishi jimbo lolote la Uchaguzi.

..kama mahudhurio yake yatakuwa mabaya kutokana na kuwa shuleni basi Spika anaweza kumuadhibu, ikiwa ni pamoja na kumtoa ubunge.

..Hata Amina Chifupa nasikia alikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu kimoja hapa Bongo.

..Hata Monica Mbega aliacha unaibu waziri wa fedha na ubunge na kwenda masomoni UK.

..Hata Emmanuel Mwambulukutu aliteuliwa Ubalozi RSA akiwa Mbunge ktk Bunge la Jamhuri.
 
David Tarimo ni mmoja wa ma-Partners au Wakurugenzi wa Kampuni ya PricewarhouseCoopers na David Tarimo ni Mshauri mkuu wa mambo ya Kodi kwa makampuni yote Makubwa ya Madini hapa Tanzania. Mapato ya Kampuni ya PricewaterhouseCoopers kwenye kitengo chao cha ushauri wa Kodi ni zaidi ya dola million 3 kwa mwaka na kiasi hicho hutoka sana sana kwa Fees kwenye makampuni hayo ya Madini. ya Kahama Mining; Geita Gold; Tuwaluka, Barrick Gold, Bugwazi, Mwadui Williamson; na mengineyo. Nafasi ya David katika tume iyo inaweza kuleta conflict of interest aidha atakosana au kuwaudhi wateja wake hao makaburu au atajaribu kuwasaidia.
 
..umenikumbusha wewe,huyu tapeli aliyetapeli watu Iowa na wa kujipendekeza kwa mama mkapa yuko wapi siku hizi? na anakula nondo gani hizo za masters maana hata degree ya kwanza alikuwa hajamaliza maana nasikia anasema ana degree,hii sampuli ndio viongozi wa bongo yaani kanyaboya tupu,mungu atusaidie tuu.

Ehhee, hii sasa ni issue. Ebu nipe nyeti zaidi za huyu bwana, ningependa kujua zaidi. Sikujua kuwa kumbe hata degree hakumaliza, basi bongo tuna kazi. Inakuwaje watu matapeli wanapenya kwenye sehemu nyeti katika taifa letu?
 
Back
Top Bottom