Uchaguzi 2020 CHADEMA: Wanachama 11 wachukua fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania

CHADEMA

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
488
2,468


Ikumbukwe kwamba waliotia nia ni wengi lakini ni wachache waliojitangaza hadharani , Sasa leo tega sikio ili usikie ni akina nani wengine Wazito sana waliotia nia ya kuomba Urais wa Tanzania kupitia Chadema .

Mungu ibariki Chadema

=======

----UPDATE----

Ndugu wanahabari

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinapenda kuutarifu Umma wa Watanzania kupitia mkutano huu kuwa jumla ya wanachama 11 wamejitokeza kutia nia ya kuwania uteuzi wa kupeperusha bendera, kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba, mwaka huu, ambao utahusisha pia nafasi za udiwani, uwakilishi na ubunge.

Wanachama hao ambao idadi yao na majina yao yanatangazwa rasmi kwa umma kupitia taarifa hii kwa vyombo vya habari, wamejitokeza, kila mmoja kwa wakati wake, ndani ya muda uliowekwa, kutangaza nia hiyo kwa kutekeleza Kifungu cha (1) cha Mwongozo wa Chama wa Kutangaza Kusudio la Kuwania Nafasi za Uongozi Kwenye Vyombo vya Uwakilishi Serikalini, kipengele cha (g), ambacho kinatamka;

"Kwa nafasi ya Uongozi wa Kitaifa ndani ya Chama na Urais taarifa za walio na kusudio la kugombea nafasi hizo zitawasilishwa kwa Katibu Mkuu na kujadiliwa na Kamati Kuu na kutolewa uamuzi kwa hatua zinazofuata."

Mtakumbuka kuwa mnamo, Juni 3, mwaka huu, Chadema kupitia tamko lililotolewa na Katibu Mkuu wa Chama, Mhe. John Mnyika, kilifungua rasmi mlango kwa mwanachama yeyote anayetaka kutia nia ya nafasi ya urais, kuandika barua ya kusudio lake Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chama.

Hadi mlango huo wa kutia nia unafungwa rasmi Juni 15, mwaka huu, saa 10.00 jioni, ikiwa ni jumla ya siku 12 baada ya kufunguliwa, wanachama waliotekeleza kanuni hiyo ni hawa wafuatao;

 Charles, Mwita Isaya
 Lissu, Tundu A.M
 Dkt. Majinge, Mayrose Kavura
 Manyama, Leonard Toja
 Mbowe, Freeman Aikaeli
 Mch. Msigwa, Peter Simon
 Adv. Mwanalyela, Gasper Nicodemus
 Nalo, Opiyo G.O.M
 Adv. Neo, Simba Richmund
 Nyalandu, Lazaro Samuel
 Shaban, Msafiri

Ndugu wanahabari

Ofisi ya Katibu Mkuu pia ilipokea barua iliyokuwa imeandikwa na vijana wa makundi mbalimbali ya waendesha bodaboda, kwa niaba ya mwanachama mmoja ambaye wao waliona anafaa kutia nia ya kuwania urais, lakini kwa kuwa barua hiyo haijakidhi matakwa ya kifungu hicho cha 1(g) cha mwongozo uliotajwa hapo juu, haijazingatiwa na hivyo hata jina la mwanachama huyo halijawekwa katika orodha ya watia nia wala hajatajwa hapa katika taarifa hii.

Hivyo basi, kufungwa rasmi kwa mlango huo wa kutia nia, kunaruhusu kuendelea kwa hatua zingine kwa mujibu wa taratibu za Chadema, kwa kuzingatia Katiba, Kanuni na Miongozo mbalimbali. Kwa mujibu wa mwongozo ulionukuliwa hapo juu, kwa sasa majina ya watia nia wote yatawasilishwa kwenye kikao cha Kamati Kuu ya Chama, ambayo nayo itatekeleza wajibu wake kwa hatua mbalimbali katika mchakato huu kwa kuzingatia ibara ya 7.7.16 ya Katiba ya Chadema.

Ni vyema pia tukawakumbusha wanahabari na wananchi wote wanaofuatilia mchakato huu kuwa, hatua hii ya kutia nia ilihusisha kuandika barua kwa Katibu Mkuu na si kuchukua na kurudisha fomu. Hatua nyingine zinazofuata zitatangazwa baadae.

Imetolewa leo, Jumatano, Juni 17, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema
1592399450385.png
1592399459650.png
 
Siku moja tu baada ya Lisu kutumia masaa 4 akiwahutubia watanzania na kuwapa sababu za kwa nini anatangaza nia ya kuwania urais wa Tanzania, huku nyuma Mbowe akaibuka na igizo la kuvamiwa na watu wasiojulikana, kisha kukanyagwa kanyagwa na kuvunjwa mguu wa kulia bila mtoto wake James aliyekuwa ndani kusikia chochote ,badala yake akasikia Joyce Mkuya aliyekuwa umbali wa kilomita 5!!
Lengo la hili igizo ilikuwa ni kufunika habari ya Lisu kuandikwa na vyombo vya habari.

Kana kwamba haitoshi Mbowe baada tu ya kuruhusiwa kutoka hospitali ,huku akichechemea akatangaza nia ya kugombea urais wa Tanzania!

Yani watanzania wakiwa na hamu ya kusikia report kutoka kwa Mbowe mwenyewe kwamba alivamiwaje, ilikuwaje ,badala ya kujibu hizo hoja ,yeye akaja na igizo jingine la kwamba kuna wazee wameenda nyumbani kwake kumshawishi awanie urais wa Tanzania!!.

Hivi Lisu unataka ufanyiwe nini ndiyo ujue kwa sasa hauhitajiki Chadema?
Haya maigizo ya mwenyekiti wako wa chama kufunika utangazaji wako nia hayajakuamsha tu?.

Shituka
 
Baada ya JPM kuchukua form. In absence of ccm makini hakuna Tanzania imara, wote walisubiri ccm aongoze ndiyo wengine wafuate hata matokea huwaga yanakuwa hivyo ni ccm kwanza wengine baadae.

"Wengine waoga, hawajiamini, hawana uthubutu, wanakimbia changamoto kama vile Corona"by JPM jana Dodoma
 
Ni kupoteza muda kujipa matumaini kwa mambo usiyoyaweza! Wenye akili wanahangaika Magufuri aoongezewe muda , nyinyi mnahangaika na kutafuta wagombea?
 
Siku moja tu baada ya Lisu kutumia masaa 4 akiwahutubia watanzania na kuwapa sababu za kwa nini anatangaza nia ya kuwania urais wa Tanzania, huku nyuma Mbowe akaibuka na igizo la kuvamiwa na watu wasiojulikana, kisha kukanyagwa kanyagwa na kuvunjwa mguu wa kulia bila mtoto wake James aliyekuwa ndani kusikia chochote ,badala yake akasikia Joyce Mkuya aliyekuwa umbali wa kilomita
5!
Wewe jamaa mkali wa kuandika riwaya hata Shigongo hakufikii..piga pesa kipaji unacho
 
Sawa CHEDEMA tupeni list yenu, na wana Lumumba tunaisubiri ya kwenu... Hiki ndicho kipimo sahihi cha demokrasia ndani ya vyama vyenu.
 
Baada ya JPM kuchukua form.
In absence of ccm makini hakuna Tanzania imara, wote walisubiri ccm aongoze ndiyo wengine wafuate hata matokea huwaga yanakuwa hivyo ni ccm kwanza wengine baadae.
"Wengine waoga, hawajiamini, hawana uthubutu, wanakimbia changamoto kama vile Corona"by JPM jana Dodoma
Bashiru kachapisha Fomu moja tu na yenyewe imeondoka, kama Membe unataka form, unatakiwa ukaombe kwa aliyechukua utoke copy.
 
Back
Top Bottom