Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,100
- 5,649
Kutokana na unafiki,uongo,kejeli na jaziba za wanaCHADEMA ,wabunge na wafuasi wao katika wiki iliyopita imedhihirisha hawana uwezo wa kuongoza nchi hii yenye kila aina ya changamoto.Nitafafanua baadhi ya uongo wa WANACHADEMA;
Mosi,Walimshambulia sana Mh.Simbachawene(NW-Nishati) kwa uzushi ati amefumaniwa na kukatwa mkono huko SINGIDA.Wameumbuka kwa uongo uliokubuhi,nikajiridhisha kuwa hiki chama ni cha Waongo,kwani 100% ya wanaJF ambao ni CHADEMA walitumia simu na mitandao ya kijamii kusambaza uongo huu.
Pili,Jazba ya muhuni mmoja anajiita Mchungaji,ndg.Msigwa,hafanani hatakujiita mchungaji kwa hasira alizonazo.Mahakama inafuata sheria na ushahidi zaidi kuliko hisia zako
nakushauri ukasome biblia vizuri;YA KAISARI mpe KAISARI na YA MUNGU mpe MUNGU,siasa ni busara zinatawala na uwezo wa kujenga hoja.
Tatu,Viongozi wenu wanafiki,hawajui kujenga hoja katika bajeti kwa kisingizio ati lazima wapinge kila kitu ndiyo maana ya upinzani....Jamani bungeni si sehemu ya kuigiza mambo ya DEBATE MOTION ni sehemu yakuishauri serikali nini kifanyike ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Nadhani wabunge wengi waCHADEMA wamepata ubunge kwa bahati mbaya....bado wanaweweseka pia elimu ndogo.
Rai yangu kwa wana CCM wote,mapinduzi ya kweli yapo ndani ya CCM na sikukimbilia upinzani,tuache uoga kuchambua mapungufu ya serikali ili tuimarishe chama chetu.
Hongera sana Mh.Mpina,Filikunjombe,Lugola,Mkono ,Mwakyembe,Zambi kwa kuonyesha njia,nawengine wafuate mfano huo.Serikali imewapa uhuru wa kujadili kila kitu kwa uwazi zaidi.
Pamoja na haya yote, Effective January 2016 watoto wa dada zako wataanza kupata huduma za chakula shuleni, na shemeji yako ataanza kufikiria kujenga nyumba yake mwenyewe ya kisasa kwa ajili ya familia yake na wewe utaweza kupata mkopo benki kwa riba isiyodhidi 10% na mama yako ataanza kununua sukari kwa bei isiyodhidi shilingi mia tano kwa kilo.