CHADEMA walinishangaza sana na bado wananishangaza

Mkuu MMP, inaumiza sana kuona kuwa katika nchi hii kuna watu tena kwenye nafasi muhimu katika ofisi za umma ni waongo na wanafiki hata kuliko shetani. Binafsi sijawahi kuvutiwa na Lowassa kiasi hicho, lakini kama kweli watu wana hasira na ufisadi wanawezaje kuchukuliana na kuridhika na Mwakyembe aliyetamka kwa kinywa chake kuwa kamati yake ilificha mambo ili kuilinda serikali ya kikwete? Chenge je, yuko wapi?! Hawa wanaochukia hivyo ufisadi lakini wako kimya kuhusu Lugumi! Kivuko feki cha Dar-Bagamoyo?! Ufisadi woote uliofanyika nchi hii kwa nini wanakuwa kimya na kubaki kudanganya umma kuwa ufisadi uko upinzani?! Na hata kama uko huko kwa nini wasiwachukulie hatua za haki?!

Kuna kitu nimejifunza kutokana na siasa za wenzetu na historia ya Demokrasia huko ilikoanzia Ugiriki. Hatua za mwanzo za Demokrasia zilibeba utambuzi wa makundi ya watu kwa ubaguzi (huko Ugiriki) kiasi ungejiuliza dhana yenyewe ya Demokrasia iko wapi ikiwa watu wanabaguliwa.

Miongoni mwa Wagiriki wa kipindi hicho cha kina Plato, ukisema mtu ilimaanisha MWANAUME HURU. Wanawake na watumwa hawakuwa na nafasi za kimaamuzi na sababu ziliwekwa wazi. Mtumwa kwao alikuwa ni kifaa tu kama vilivyo vifaa vingine kama jembe, nyundo na toroli. Mtumwa hana haja ya kufikiri zaidi ya kufanya lile analoambiwa na bwana wake. Kwa maana hiyo, kumpa nafasi ya kuamua au kuchagua mtu wa namna hiyo ilifananishwa na kumpa mbuzi karatasi ya kura.

Wanawake nao (kwa kipindi hicho) hawakuwa sehemu ya uchangiaji wa maamuzi sababu hawakuwa responsible kwa yatukiayo kwa uchaguzi wao. Kwa mifano hii, nikiingiza Tanzania kwenye nafasi ya jamii ya Wagiriki ya wakati ule, naona tulipaswa kufika huko.

Tunapoenda kupiga kura (hapa Tanzania) makundi yote yana haki sawa ya kuchagua...kigezo pekee ni umri. Lakini ukiangalia nani anaathirika vipi na maamuzi yanayofanywa na kura hizi za jumla utagundua kuna wanaoathirika zaidi ya wengine kwa kuwa tunatofautiana malengo na matarajio. Mtu anayekatwa P.A.Y.E anajua uchungu wa kodi, leo hii chaguo lake lenye tija linashindwa kwa wingi wa kura za watu waliohongwa khanga na Tshs 2000 pamoja na disko kwenye kampeni na kumuwekea kiongozi kwa kuwa tu 'ni haki ya kila Mtanzania' kupiga kura.

Mimi nikirudisha kumbukumbu nyuma miaka michache, ninaona picha ya WATUMWA waliopewa haki ya kuchagua Rais. Kuna uchaguzi hapa, watu walichagua kiongozi kwa ushabiki 'presidaa sura babuu, tusiharibu noti', na kweli washabiki hao walifanya hivyo kwa hamasa kubwa. Unajiuliza, wafanyabiashara, na wawekezaji wanaotaka kulinda mitaji yao nao wangechagua sura? Ingekuwa tumegawanywa makundi kwa ufahamu wetu, hata mchaguliwa angekuwa na amani kuona kura zake zimetoka kwa watu wa aina gani?

Hapa kuna shida Mkuu. Kuna kundi kubwa la watu wasiojua wanafanya nini, wasio na kumbukumbu na wasiotaka kufikiri wanatumia haki yao kuchagua. Baada ya kuchagua, malalamiko kila uchao lakini uchaguzi ukija ndio wao wataalam wa kuimba mipasho na kumsifia mgawa tshirt. Kila ninapowafikiri hawa, huwa namkumbuka Mungu wangu...tumaini langu la mwisho!
 
Hesabu rahisi ni kwamba 2005-2010 kura ziliongezeka mara 4.5 (2,700,000/600,000). Kwa debe la M4C lililopigwa 2010-2015 tulitegemea factor ya kuongezeka kwa kura iwe zaidi ya 4.5, kwa maana kura za upinzani zingekuwa zaidi ya 12,000,000 (2,700,000 x 4.5). Kwa hiyo Lowasa kapunguza kura za upinzani.
 
NLD inapewa kura 1,500,000 kweli akili ndogo.
Hahaaaa! Halafu mbaya zaidi, hana utashi au ujasiri wa kueleza NLD wamezipataje hizo 1.5 ml....!!!

Huwa najiuliza inawezekanaje binadamu kamili akakubali kupoteza au sijui niseme kufukia kwenye tope chafu uhuru wake wa kufikiri na uwezo wa kuona mambo yaliyo dhahiri kwa uhalisia wake.
 
Umesahau udini mliopandikiza na mlikua mnamuita padri.
Mara 'babu' 'kibabu kile' nk! Na hawahawa ndio wanahoji kwa nini wengine wamebadili mitazamo yao, ila hata siku moja hutawasikia wakieleza kwa nini wakati ule walikuwa wanamuona kama adui yao lakini sasa siyo adui tena! Hawahawa hutasikia wakihoji kwa nini kikwete hakumshitaki Lowassa na kiuhalisia aliwashawishi wananchi wa Monduli waendelee kumchagua Lowassa, lakini mwisho wa kampeni za mwaka jana akiwa rais anawaambia watanzania kuwa Lowassa ndiye mwenye richmond!!! Hawahawa hawahoji lolote kwa nini bunge lenye wingi wa wabunge wa ccm lilimchagua kuwa mwenyekiti wa moja ya kamati muhimu ya bunge!
 
Chadema chama cha mafisadi kwa sasa ndiyo maana mambo yao yote kwa sasa lazima yaamuliwe na mafisadi.
Zile hela alizogawa baba yako kwaajili ya kuwafunga mafisadi mbona mpaka sasa sijaona fisadi yeyote kutoka chadema aliyeshikwa au kushitakiwa? Naoma mpaka sasa walioshitakiwa ni kutoka ccm tu!
 
CHADEMA walinishangaza sana!!how can you compare Dr slaa versus Lowassa? good comparison was Dr slaa versus Dr Magufuli!!

Bado CHADEMA wananishangaza sana!eti lowassa amewasaidia chadema kupata kura nyingi ,majiji etc this is very wrong!! kwanza walipoteza vitu vingi mpaka sasa!!

simple mathematics hii hapa
1.2005: chama kimoja CHADEMA versus CCM :Mbowe about kura 600,000

2.2010:chama kimoja CHADEMA versus CCM :D Dr Slaa:kura about 2700000

3.2015:vyama 4 (UKAWA) versus CCM pekee. Lowassa about 6 million

kuwa hiyo 6000000:4(viama 4 ukawa)=1500000.
kuwa hiyo kama lowassa angesimama peke yake angepata kura milioni moja na nusu wakati Dr. Slaa alipata 2.7 million!!kuwa maana nyingine Dr. Magufuli alimshinda vibaya Lowassa!!na kama Dr. Slaa angegombea kushindana na Lowassa ,Dr. slaa angemshinda ile mbaya sana!!na Leo Dr. Slaa akirudi chama chochote bado ni tishio kuwa CCM lakini siyo Lowassa!!
Arithmetics is inapplicable in politics. Use qualitative tool to argue your case study.
 
CHADEMA walinishangaza sana!!how can you compare Dr slaa versus Lowassa? good comparison was Dr slaa versus Dr Magufuli!!

Bado CHADEMA wananishangaza sana!eti lowassa amewasaidia chadema kupata kura nyingi ,majiji etc this is very wrong!! kwanza walipoteza vitu vingi mpaka sasa!!

simple mathematics hii hapa
1.2005: chama kimoja CHADEMA versus CCM :Mbowe about kura 600,000

2.2010:chama kimoja CHADEMA versus CCM :D Dr Slaa:kura about 2700000

3.2015:vyama 4 (UKAWA) versus CCM pekee. Lowassa about 6 million

kuwa hiyo 6000000:4(viama 4 ukawa)=1500000.
kuwa hiyo kama lowassa angesimama peke yake angepata kura milioni moja na nusu wakati Dr. Slaa alipata 2.7 million!!kuwa maana nyingine Dr. Magufuli alimshinda vibaya Lowassa!!na kama Dr. Slaa angegombea kushindana na Lowassa ,Dr. slaa angemshinda ile mbaya sana!!na Leo Dr. Slaa akirudi chama chochote bado ni tishio kuwa CCM lakini siyo Lowassa!!


2015Vyama 4(ukawa) versus ccm,ccmpolisi, NEC hata hizoulizosema ni aibu tu.
 
Nchi hii haina utawala wa sheria? Km lowasa ni fisadi achukuliwe hatua stahiki. Vinginevyo, kuendelea kumwita fisadi na hamchukui hatua ni kutueleza kuwa hamfuati sheria na hamchukii ufisadi km mnavyojitapa.
 
Huyu ni msomi anaye tegewa Lumumba......tuambie vyama vingine kwenye hizo chaguz vilipata kura ngap ....? kufikia kwenye uchumi wa viwanda kwa mbumbu kama hawa wakiwa ndio wakurugenzi ni ndoto....
 
Chadema chama cha mafisadi kwa sasa ndiyo maana mambo yao yote kwa sasa lazima yaamuliwe na mafisadi.
Huwa najiuliza fisadi mmoja kuhamia chama kingine kinakuwa chama cha mafisadi. Je wale wenye mtambo wa kuzalisha na kulea mafisadi tuwaiteje? LOL.
 
Back
Top Bottom