CHADEMA walikuwa CCM-B kabla ya CUF.

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,017
7,220
Nimeguswa na aina mpya ya propaganda inayofanywa na Chadema ya kukiita chama cha wananchi CUF kuwa ni CCM-B. Hii ni kufumbia macho uhalisia wa hali ya kisiasa ya Zanzibar iliyopelekea kuwepo kwa muafaka. Hebu basi tupitie historia ili ituonyesha, ikiwa Chadema wangekuwa wamevaa viatu vya CUF wangefanya maamuzi gani?

Katika uchaguzi wa Madiwani uliofanyika tarehe 14 Desemba, 2006, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilipata Madiwani sita toka Chama cha Mapinduzi (CCM) na Madiwani saba toka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kwa vile CCM ilishinda pia kiti cha Ubunge cha Jimbo la Kigoma/Ujiji, Mbunge huyo aliongeza namba ya Wajumbe toka CCM kuwa saba na kufanya jumla ya wajumbe wa Halmashauri wa kuchaguliwa kuwa kumi na nne.

Baadaye Tume ya Uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 19 (1)(c) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na.8 ya 1984 iliwateua Wajumbe watatu (3) toka CCM na watatu toka CHADEMA kuwa Madiwani wa Viti Maalum vya Wanawake. Uteuzi huo wa Tume ya Uchaguzi ulifanya jumla ya Wajumbe wa Halmashauri ya Kigoma/Ujiji toka CCM kuwa kumi na wale wa kutoka CHADEMA kuwa kumi pia. Hivyo, idadi ya Wajumbe toka Vyama hivi ililingana na kufanya jumla ya Wajumbe wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma kuwa ishirini.

Hali ya Wajumbe toka Vyama vya CCM na CHADEMA kulingana ilifanya iwe vigumu kumpata Mwenyekiti wa Muda wa Kikao ambacho kingemchagua Meya na Naibu wa Meya. Kilichojitokeza ni kuwa pale Mjumbe toka CCM alipopendekeza jina la Mwenyekiti wa Muda, Wajumbe wote kumi toka CCM waliunga mkono na Wajumbe wote kumi wa CHADEMA walipinga. Vivyo hivyo hali hii ilijitokeza pale CHADEMA walipopendekeza jina na ndipo Viongozi wa Kitaifa wa Vyama walipoona umuhimu wa kuingilia kati suala hili.

Tarehe 26 Januari, 2006 Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya CCM na CHADEMA walifikia Makubaliano kuwa Uongozi katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji uwe wa kushirikiana.

Iliafikiwa kwamba, Awamu ya Kwanza kuanzia tarehe 9 Machi, 2006 hadi tarehe 30 Juni, 2008 Mheshimiwa Diwani Kitita Juma Magonjwa wa CHADEMA awe Meya na Mheshimiwa Diwani Yahya Liheye wa CCM awe Naibu wa Meya wa Manispaa. Aidha, Awamu ya Pili itakapoanza tarehe 1 Julai, 2008 hadi tarehe 28 Oktoba, 2008 Mheshimiwa Diwani Nashon Bidyanguze kutoka CCM aliteuliwa kuwa Meya na Mheshimiwa Diwani Shabaan Mambo kutoka CHADEMA awe Naibu wa Meya.

Labda niwakumbushe pia kuwa mgombea wa urais wa Chadema, Dr. Slaa, aliahidi kuunda serikali ya umoja wa kitaifa iwapo atashinda Urais. Alitoa ahadi hizo wakati muafaka na katiba mpya Zanzibar vilikuwa vimeshapitishwa. Swali ni je, alipanga kuunda serikali hiyo kwa ushirikiano na chama gani?
Je, Dr.Slaa alikuwa anaongelea kutengeneza CHADEMA-B, C etc.?
Je, Chadema ni chama kinachotekeleza yale kinachoyaongea?
 
ze marco..... chadema ilishafanya kile ilichofanya cuf.....CHADEMA NI CCM-B NAMBRI WAN....!
 
I am a great believer of the past to determine the future. Lakini not in this case; who cares what happened then. Tunakata kuongelea now mambo ya sasa and the future.. Please lets not live in the past
 
Wanachoniudhi ni unafiki wa kulaani vitu ambavyo wao huvifanya kila siku na kumake use of the the public ignorance/ lack of information.
They are just another bunch of politicians!
 
I am a great believer of the past to determine the future. Lakini not in this case; who cares what happened then. Tunakata kuongelea now mambo ya sasa and the future.. Please lets not live in the past

VOR,
Uko sahihi sana, nakunga mkono, lakin ili tuendelee na future juu ya hili inabidi Chadema na wafuasi wake wakiri kuwa kilichotokea Zanzibar ni political maturity na siyo swala la CUF kuwa CCM-B.
 
Kawaulize wakubwa wako CHADEMA ni nini? Tanzania kuna vyama vitatu tu vya upinzani, chadema ikiwemo. Rudi kamwulize makamba akuonyeshe mipango yote ya uanzishaji wa vyama vya upinzani, na majukumu aliyopewa kila mtu kwa nafasi yake. Au muulize Marando anafahamu zaidi ni kwanini alianzisha NCCR Mageuzi. Muulize Chief Fundikra (RIP) ni kwa nini hasa alianzisha chama. Pia kamuulize Edwini Mtei ni kwa vipi alianzisha CHADEMA.

Kwa taarifa yako vyama vingi vya upinzani vilianzishwa na serikali ya CCM kuitikia mwito wa umoja wa mataifa wa kuboresha demoncrasia. Chama kilichoanzishwa kwa misingi ya upinzani wa dhati ni CHADEMA, ambayo Edwini aliianzisha kumpinga Nyerere. Na alikuwa anamatumaini makubwa sana ya kuchukua nchi na kumtimulia vumbi Nyerere. Na kama utafuatilia kwa makini utajua ni kwanini Nyerere alikisifia CHADEMA siku za uhai wake. Alijua katika vyama vya upinzani vya kweli vyenye nguvu na vyenye uwezo wa kuongoza nchi ni CHADEMA pekee yenye sifa za kutosha. Kumbuka Nyerere hakuwa mnafiki.

Usijidanganye ndugu yangu chadema ni chama cha upinzani cha kweli kabisa, tofauti na NCCR, CUF au TLP.
 
Nimeguswa na aina mpya ya propaganda inayofanywa na Chadema ya kukiita chama cha wananchi CUF kuwa ni CCM-B. Hii ni kufumbia macho uhalisia wa hali ya kisiasa ya Zanzibar iliyopelekea kuwepo kwa muafaka. Hebu basi tupitie historia ili ituonyesha, ikiwa Chadema wangekuwa wamevaa viatu vya CUF wangefanya maamuzi gani?

Katika uchaguzi wa Madiwani uliofanyika tarehe 14 Desemba, 2006, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilipata Madiwani sita toka Chama cha Mapinduzi (CCM) na Madiwani saba toka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kwa vile CCM ilishinda pia kiti cha Ubunge cha Jimbo la Kigoma/Ujiji, Mbunge huyo aliongeza namba ya Wajumbe toka CCM kuwa saba na kufanya jumla ya wajumbe wa Halmashauri wa kuchaguliwa kuwa kumi na nne.

Baadaye Tume ya Uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 19 (1)(c) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na.8 ya 1984 iliwateua Wajumbe watatu (3) toka CCM na watatu toka CHADEMA kuwa Madiwani wa Viti Maalum vya Wanawake. Uteuzi huo wa Tume ya Uchaguzi ulifanya jumla ya Wajumbe wa Halmashauri ya Kigoma/Ujiji toka CCM kuwa kumi na wale wa kutoka CHADEMA kuwa kumi pia. Hivyo, idadi ya Wajumbe toka Vyama hivi ililingana na kufanya jumla ya Wajumbe wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma kuwa ishirini.

Hali ya Wajumbe toka Vyama vya CCM na CHADEMA kulingana ilifanya iwe vigumu kumpata Mwenyekiti wa Muda wa Kikao ambacho kingemchagua Meya na Naibu wa Meya. Kilichojitokeza ni kuwa pale Mjumbe toka CCM alipopendekeza jina la Mwenyekiti wa Muda, Wajumbe wote kumi toka CCM waliunga mkono na Wajumbe wote kumi wa CHADEMA walipinga. Vivyo hivyo hali hii ilijitokeza pale CHADEMA walipopendekeza jina na ndipo Viongozi wa Kitaifa wa Vyama walipoona umuhimu wa kuingilia kati suala hili.

Tarehe 26 Januari, 2006 Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya CCM na CHADEMA walifikia Makubaliano kuwa Uongozi katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji uwe wa kushirikiana.

Iliafikiwa kwamba, Awamu ya Kwanza kuanzia tarehe 9 Machi, 2006 hadi tarehe 30 Juni, 2008 Mheshimiwa Diwani Kitita Juma Magonjwa wa CHADEMA awe Meya na Mheshimiwa Diwani Yahya Liheye wa CCM awe Naibu wa Meya wa Manispaa. Aidha, Awamu ya Pili itakapoanza tarehe 1 Julai, 2008 hadi tarehe 28 Oktoba, 2008 Mheshimiwa Diwani Nashon Bidyanguze kutoka CCM aliteuliwa kuwa Meya na Mheshimiwa Diwani Shabaan Mambo kutoka CHADEMA awe Naibu wa Meya.

Labda niwakumbushe pia kuwa mgombea wa urais wa Chadema, Dr. Slaa, aliahidi kuunda serikali ya umoja wa kitaifa iwapo atashinda Urais. Alitoa ahadi hizo wakati muafaka na katiba mpya Zanzibar vilikuwa vimeshapitishwa. Swali ni je, alipanga kuunda serikali hiyo kwa ushirikiano na chama gani?
Je, Dr.Slaa alikuwa anaongelea kutengeneza CHADEMA-B, C etc.?
Je, Chadema ni chama kinachotekeleza yale kinachoyaongea?
marcopolo wape ukweli hao machadema ambao huwa wanaropoka bila kua nadata,wao wamekua sasa ndio wamechukua nafasi ya ccm kukosoa wapinzani,tena wanamageuzi wenzao wa cuf,mm nahisi wanaionea choyo nawivu cuf kwamafanikio iliyokua,chadema kwa sasa ndio hasa ccm b kwajinsi wanavoiandama cuf,ila wajue cuf majimarefu hawaiwez abadan,inauzoefu wasiasa zaharakati zaid ya miaka 20,sembuse wao kuvuma miaka2 washavimba vichwa.
 
Kawaulize wakubwa wako CHADEMA ni nini? Tanzania kuna vyama vitatu tu vya upinzani, chadema ikiwemo. Rudi kamwulize makamba akuonyeshe mipango yote ya uanzishaji wa vyama vya upinzani, na majukumu aliyopewa kila mtu kwa nafasi yake. Au muulize Marando anafahamu zaidi ni kwanini alianzisha NCCR Mageuzi. Muulize Chief Fundikra (RIP) ni kwa nini hasa alianzisha chama. Pia kamuulize Edwini Mtei ni kwa vipi alianzisha CHADEMA.

Kwa taarifa yako vyama vingi vya upinzani vilianzishwa na serikali ya CCM kuitikia mwito wa umoja wa mataifa wa kuboresha demoncrasia. Chama kilichoanzishwa kwa misingi ya upinzani wa dhati ni CHADEMA, ambayo Edwini aliianzisha kumpinga Nyerere. Na alikuwa anamatumaini makubwa sana ya kuchukua nchi na kumtimulia vumbi Nyerere. Na kama utafuatilia kwa makini utajua ni kwanini Nyerere alikisifia CHADEMA siku za uhai wake. Alijua katika vyama vya upinzani vya kweli vyenye nguvu na vyenye uwezo wa kuongoza nchi ni CHADEMA pekee yenye sifa za kutosha. Kumbuka Nyerere hakuwa mnafiki.

Usijidanganye ndugu yangu chadema ni chama cha upinzani cha kweli kabisa, tofauti na NCCR, CUF au TLP.

Mimi nakubali kuwa Chadema ni chama cha upinzani cha ukweli. Ila sikubaliani na wewe pamoja na wafuasi wengine wa Chadema mnaokipaka matope chama cha CUF kwa sababu ya muafaka wa Zanzibar, jambo ambalo hata Chadema wanatamani wangelipata. Na article hii ni ushahidi kuwa Chadema inatamani ingepata nafasi kama ya CUF.
 
ZeMarcopolo,

..yaani unalinganisha masuala ya halmashauri ya jiji na mambo yanayotokea bungeni?

..lini Chadema wakafanya vitimbi vya kitoto kama walivyofanya CUF walipokwenda kukaa sehemu wanayokaa wabunge wa Chadema wakati wa hotuba ya Kikwete bungeni?

..CUF wameshinda Pemba, huku Tanganyika wamepata majimbo mawili tu. kwanini CUF waanze kufanya vituko ndani ya bunge la muungano ambalo kwa kiasi kikubwa ndilo bunge la Tanganyika?
 
Kawaulize wakubwa wako CHADEMA ni nini? Tanzania kuna vyama vitatu tu vya upinzani, chadema ikiwemo. Rudi kamwulize makamba akuonyeshe mipango yote ya uanzishaji wa vyama vya upinzani, na majukumu aliyopewa kila mtu kwa nafasi yake. Au muulize Marando anafahamu zaidi ni kwanini alianzisha NCCR Mageuzi. Muulize Chief Fundikra (RIP) ni kwa nini hasa alianzisha chama. Pia kamuulize Edwini Mtei ni kwa vipi alianzisha CHADEMA.

Kwa taarifa yako vyama vingi vya upinzani vilianzishwa na serikali ya CCM kuitikia mwito wa umoja wa mataifa wa kuboresha demoncrasia. Chama kilichoanzishwa kwa misingi ya upinzani wa dhati ni CHADEMA, ambayo Edwini aliianzisha kumpinga Nyerere. Na alikuwa anamatumaini makubwa sana ya kuchukua nchi na kumtimulia vumbi Nyerere. Na kama utafuatilia kwa makini utajua ni kwanini Nyerere alikisifia CHADEMA siku za uhai wake. Alijua katika vyama vya upinzani vya kweli vyenye nguvu na vyenye uwezo wa kuongoza nchi ni CHADEMA pekee yenye sifa za kutosha. Kumbuka Nyerere hakuwa mnafiki.

Usijidanganye ndugu yangu chadema ni chama cha upinzani cha kweli kabisa, tofauti na NCCR, CUF au TLP.
subiri uone baada yamiaka 2 ndio utajua chadema ni chama cha upinzani au chakugombania ruzuku,we nahic huijui ccm ila ngoja utajionea na utakumbuka maneno yangu.
 
ZeMarcopolo,

..yaani unalinganisha masuala ya halmashauri ya jiji na mambo yanayotokea bungeni?

..lini Chadema wakafanya vitimbi vya kitoto kama walivyofanya CUF walipokwenda kukaa sehemu wanayokaa wabunge wa Chadema wakati wa hotuba ya Kikwete bungeni?

..CUF wameshinda Pemba, huku Tanganyika wamepata majimbo mawili tu. kwanini CUF waanze kufanya vituko ndani ya bunge la muungano ambalo kwa kiasi kikubwa ndilo bunge la Tanganyika?


Joka Kuu,
Mwizi akiiba shilingi elfu kumi haimaanishi kuwa akipata nafasi ya kuiba milioni ataiacha. Swali lako ni sawa na kuuliza kwa nini mwizi wa elfu kumi na milioni wote ni wezi.
Msingi wa article hii ni kuweka bayana kuwa kushirikiana baina ya vyama siyo kukifanya chama fulani kuwa B,C etc.
Maamuzi yaliyofanywa na CUF bungeni wameyafanya kama chama, na kama wameamua kushirikiana na chama kingine siyo jambo la ajabu kama jinsi tunavyoona Chadema walivyoamua kushirikiana na CCM.
 
Mimi nakubali kuwa Chadema ni chama cha upinzani cha ukweli. Ila sikubaliani na wewe pamoja na wafuasi wengine wa Chadema mnaokipaka matope chama cha CUF kwa sababu ya muafaka wa Zanzibar, jambo ambalo hata Chadema wanatamani wangelipata. Na article hii ni ushahidi kuwa Chadema inatamani ingepata nafasi kama ya CUF.

You know deep down I think Mtanzania Mlalahoi wa kweli hana Chama (hii sio kama simba na yanga). Mtanzania huyu yeye anataka Chama kitakachomwakilisha vema na kufanya maisha yake yawe bora, kwa sasa imetokea kwamba Watanzania wanataka yafuatayo:-
1. Maisha bora, na uwezo wa watoto wao kwenda shule na kutibiwa
2. Kuwabana mafisadi ambao wanafuja mali zetu
3. Kupunguza Matumizi ambayo hayana tija
4. Watu ambao watawabana Chama ambacho kipo madarakani since kimeshindwa kuleta mabadiliko (Je Chama hicho kitakuwaje CUF wakati zanzibar wameunda Serikali moja) huoni hapa kuna conflict of interest.
5. Katika vyama hivyo vyote ambavyo vipo sasa ukitumia mzani wa Bunge lililopita Chadema ndio waliokuwa mstari wa mbele kutoa uozo wa Mafisadi. Je? hivi vyama vingine havikujua au vilikuwa vinachuna tu.
 
You know deep down I think Mtanzania Mlalahoi wa kweli hana Chama (hii sio kama simba na yanga). Mtanzania huyu yeye anataka Chama kitakachomwakilisha vema na kufanya maisha yake yawe bora, kwa sasa imetokea kwamba Watanzania wanataka yafuatayo:-
1. Maisha bora, na uwezo wa watoto wao kwenda shule na kutibiwa
2. Kuwabana mafisadi ambao wanafuja mali zetu
3. Kupunguza Matumizi ambayo hayana tija
4. Watu ambao watawabana Chama ambacho kipo madarakani since kimeshindwa kuleta mabadiliko (Je Chama hicho kitakuwaje CUF wakati zanzibar wameunda Serikali moja) huoni hapa kuna conflict of interest.
5. Katika vyama hivyo vyote ambavyo vipo sasa ukitumia mzani wa Bunge lililopita Chadema ndio waliokuwa mstari wa mbele kutoa uozo wa Mafisadi. Je? hivi vyama vingine havikujua au vilikuwa vinachuna tu.

VOR,
1.Kama unadhani mtanzania mlalahoi ana chama basi tembelea vijiji vya kigoma utaona jinsi walalahoi walivyo na passion na vyama vyao.
2. Kana kuunda mfomu wa uongozi wa ushirikiano ni sababu ya kuwa na conflict of interest, Chadema wangekuwa na conflict of interest kwenye bunge lililopita.
3. Hii fikra kwamba kutoa uozo wa mafisadi ndio mahitaji makuu ya watanzania imetoka wapi?

narudia kusema kuwa lengo la kuanzisha hii thread ni kuleta changamoto ya fikra juu ya muafaka wa Zanzibar. Muafaka ni mojawapo ya mafanikio makubwa ya nchi yetu katika sekta ya kijamii. Hivyo basi mafanikio hayo tusiyabeze kwa kuwaita walioyakubali kuwa ni CCM-B. Tukiendelea kuwabeza tutafanya kazi ya utatuzi wa migogoro ya kisiasa siku za usoni kuwa haitekelezeki.
 
Nimeguswa na aina mpya ya propaganda inayofanywa na Chadema ya kukiita chama cha wananchi CUF kuwa ni CCM-B. Hii ni kufumbia macho uhalisia wa hali ya kisiasa ya Zanzibar iliyopelekea kuwepo kwa muafaka. Hebu basi tupitie historia ili ituonyesha, ikiwa Chadema wangekuwa wamevaa viatu vya CUF wangefanya maamuzi gani?

Katika uchaguzi wa Madiwani uliofanyika tarehe 14 Desemba, 2006, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilipata Madiwani sita toka Chama cha Mapinduzi (CCM) na Madiwani saba toka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kwa vile CCM ilishinda pia kiti cha Ubunge cha Jimbo la Kigoma/Ujiji, Mbunge huyo aliongeza namba ya Wajumbe toka CCM kuwa saba na kufanya jumla ya wajumbe wa Halmashauri wa kuchaguliwa kuwa kumi na nne.

Baadaye Tume ya Uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 19 (1)(c) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na.8 ya 1984 iliwateua Wajumbe watatu (3) toka CCM na watatu toka CHADEMA kuwa Madiwani wa Viti Maalum vya Wanawake. Uteuzi huo wa Tume ya Uchaguzi ulifanya jumla ya Wajumbe wa Halmashauri ya Kigoma/Ujiji toka CCM kuwa kumi na wale wa kutoka CHADEMA kuwa kumi pia. Hivyo, idadi ya Wajumbe toka Vyama hivi ililingana na kufanya jumla ya Wajumbe wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma kuwa ishirini.

Hali ya Wajumbe toka Vyama vya CCM na CHADEMA kulingana ilifanya iwe vigumu kumpata Mwenyekiti wa Muda wa Kikao ambacho kingemchagua Meya na Naibu wa Meya. Kilichojitokeza ni kuwa pale Mjumbe toka CCM alipopendekeza jina la Mwenyekiti wa Muda, Wajumbe wote kumi toka CCM waliunga mkono na Wajumbe wote kumi wa CHADEMA walipinga. Vivyo hivyo hali hii ilijitokeza pale CHADEMA walipopendekeza jina na ndipo Viongozi wa Kitaifa wa Vyama walipoona umuhimu wa kuingilia kati suala hili.

Tarehe 26 Januari, 2006 Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya CCM na CHADEMA walifikia Makubaliano kuwa Uongozi katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji uwe wa kushirikiana.

Iliafikiwa kwamba, Awamu ya Kwanza kuanzia tarehe 9 Machi, 2006 hadi tarehe 30 Juni, 2008 Mheshimiwa Diwani Kitita Juma Magonjwa wa CHADEMA awe Meya na Mheshimiwa Diwani Yahya Liheye wa CCM awe Naibu wa Meya wa Manispaa. Aidha, Awamu ya Pili itakapoanza tarehe 1 Julai, 2008 hadi tarehe 28 Oktoba, 2008 Mheshimiwa Diwani Nashon Bidyanguze kutoka CCM aliteuliwa kuwa Meya na Mheshimiwa Diwani Shabaan Mambo kutoka CHADEMA awe Naibu wa Meya.

Labda niwakumbushe pia kuwa mgombea wa urais wa Chadema, Dr. Slaa, aliahidi kuunda serikali ya umoja wa kitaifa iwapo atashinda Urais. Alitoa ahadi hizo wakati muafaka na katiba mpya Zanzibar vilikuwa vimeshapitishwa. Swali ni je, alipanga kuunda serikali hiyo kwa ushirikiano na chama gani?
Je, Dr.Slaa alikuwa anaongelea kutengeneza CHADEMA-B, C etc.?
Je, Chadema ni chama kinachotekeleza yale kinachoyaongea?


Hapo kuna makosa; nimefuatilia kwa 80% ya kampeni this year; sijawahi kusikia Dr Slaa anaongelea serikali ya kitaifa; alikuwa wazi akisema hawezi kuunda serikali ya kitaifa maana haelewi lengo la serikali ya kitaifa akihoji mtatumia katiba gani ili muonekane kweli mnaunda umoja wa kitaifa; aliamni ataunda serikali kwa kutumia makamanda ambao ni rahisi kuwatuma; naktk hilo aliwaomba wananchi wampe wabunge wengi kwa sababu hiyo hiyo; Ebu PITA tena huenda u lipitiwa au ni USHABIKI UNAKUPOFUSHA; Lipumba ndio wenye serikali y a kitaifa kote alisema alikokwenda (alikuwa akililia huruma ya ccm)
 
ZeMarcopolo said:
Joka Kuu,
Mwizi akiiba shilingi elfu kumi haimaanishi kuwa akipata nafasi ya kuiba milioni ataiacha. Swali lako ni sawa na kuuliza kwa nini mwizi wa elfu kumi na milioni wote ni wezi.
Msingi wa article hii ni kuweka bayana kuwa kushirikiana baina ya vyama siyo kukifanya chama fulani kuwa B,C etc.
Maamuzi yaliyofanywa na CUF bungeni wameyafanya kama chama, na kama wameamua kushirikiana na chama kingine siyo jambo la ajabu kama jinsi tunavyoona Chadema walivyoamua kushirikiana na CCM.

ZeMarcopolo,

..CUF ni chama cha Pemba peke yake. huku bara wanageresha tu.

..wangekuwa waungwana na kuwaachia Chadema na vyama vingine vya Tanganyika vishughulike na masuala yetu wa-Tanganyika.

..sijui kwanini wanganganie kuwa chama kikuu cha upinzani huku Tanganyika wakati hawana interest wala mandate na masuala ya wa-Tanganyika.
 
[/U][/I][/B]
Hapo kuna makosa; nimefuatilia kwa 80% ya kampeni this year; sijawahi kusikia Dr Slaa anaongelea serikali ya kitaifa; alikuwa wazi akisema hawezi kuunda serikali ya kitaifa maana haelewi lengo la serikali ya kitaifa akihoji mtatumia katiba gani ili muonekane kweli mnaunda umoja wa kitaifa; aliamni ataunda serikali kwa kutumia makamanda ambao ni rahisi kuwatuma; naktk hilo aliwaomba wananchi wampe wabunge wengi kwa sababu hiyo hiyo; Ebu PITA tena huenda u lipitiwa au ni USHABIKI UNAKUPOFUSHA; Lipumba ndio wenye serikali y a kitaifa kote alisema alikokwenda (alikuwa akililia huruma ya ccm)

Ngoja nikutafutie video ya mdahalo wa Moven pick. Amesema hilo bayana kabisa, wala halina ubishi.
 
ZeMarcopolo,

..CUF ni chama cha Pemba peke yake. huku bara wanageresha tu.

..wangekuwa waungwana na kuwaachia Chadema na vyama vingine vya Tanganyika vishughulike na masuala yetu wa-Tanganyika.

..sijui kwanini wanganganie kuwa chama kikuu cha upinzani huku Tanganyika wakati hawana interest wala mandate na masuala ya wa-Tanganyika.

Joka Kuu,
Hizi za kukiita chama fulani cha mahali fulani ni propaganda. Sikubaliani nazo. Chama cha Pemba hakiwezi kuwa na mbunge Lindi Mjini.
Swala la wao na Chadema kuachiana nafasi ya kugombea ni comical, kwa sababu kama Chadema philosophically wanaamini kushirikiana na CCM ni kuwa CCM-B, kwa nini waamini kuwa kushirikiana na Chadema is ok?
 
Back
Top Bottom