Uchaguzi 2020 CHADEMA, Wagombea wenu wanarejeshwa kugombea, mnajua mtapigwa wapi?

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Ujue Chadema mtafuta sana kura na mnakusanya watu, lakini mnafahamu tulimpoteza Aqwillina kwa sababu gani?

Mnawaandaje MAWAKALA wenu wa kuhesabu kura kuhusu kurubuniwa, kuoapishwa na kunyimwa forms?

Mnajua kua CCM wana options za mbinu zaidi ya 10 kuhakikisha kuwa wanashinda?

Mna kazi nzito sana mbeleni. Nawapa pole kubwa, mlipotoka ni rahisi sana kuliko mnajoelekea. Nadhani maneno ya NEC mmeyasikia kabisa ambayo kwa upande wangu ni biased kabisa.

Jipangeni sawasawa. Hili suala la watu wa kusimamia kura ni jambo gumu sana mpaka mpinzani ashinde.

MAWAKALA na WASIMAMIZI wa uchaguzi ndio watakaosababisha kushinda na kushindwa kwa mtu.

Take care!
 
Wakati huu hata waupande wao wamewachoka, hivyo naamini watatoa ushirikiano kuondoa dhulma zozote zilizopangwa dhidi za haki.
 
Mwananchi aliye well informed anatambua kwamba ana wajibu wa kulinda kura yake kwa gharama yoyote ile,

Ulinz wa kura na mengine yanayohusiana na hayo sio suala la viongozi wa Chama pekee bali la kila responsible citizen.
 
Inside person ameniambia kwamba moja ya mbinu ambayo itatumika siku ya uchaguzi ni kuleta watu wa kufanya fujo kwenye vituo vya kupigia kura. Mtu taingia na kumshambulia wakala wa chadema,aki-react kujibu mashambulizi basi anatolewa kwenye kituo na msimamizi wa uchaguzi kwa kufanya fujo kituoni.
 
Inside person ameniambia kwamba moja ya mbinu ambayo itatumika siku ya uchaguzi ni kuleta watu wa kufanya fujo kwenye vituo vya kupigia kura. Mtu taingia na kumshambulia wakala wa chadema,aki-react kujibu mashambulizi basi anatolewa kwenye kituo na msimamizi wa uchaguzi kwa kufanya fujo kituoni.
Naamini kuwa Kila binadamu Ana hali ya kupenda haki ndani yake,hata Kama ni katili kiasi gani, na vilevile naamini wapenda haki ni wengi kuliko wanaoangalia maslahi binafsi, Hivyo nawaomba wote wanaopenda haki wasimamie haki, na watakuwa nafuraha na amani ya kweli.
 
Naamini kuwa Kila binadamu Ana hali ya kupenda haki ndani yake,hata Kama ni katili kiasi gani, na vilevile naamini wapenda haki ni wengi kuliko wanaoangalia maslahi binafsi, Hivyo nawaomba wote wanaopenda haki wasimamie haki, na watakuwa nafuraha na amani ya kweli.
Pole mkuu,umeongea ukilengwa machozi kabisa...Jiandae tu kisaikolojia...ukweli utakuwa huo kwa 99%,kukiondoa chama tawala siyo mchezo,viashiria mbona vingi tu, mfano: Hotuba za Kilugha---Kienyeji/Kisukuma kikiwemo. Zinatoa picha ?etc.
 
Walishawaambia,watende haki tu basi.tofauti na hapo basi.RAIA Tupo zaidi ya million 30 wenye akili timamu.askari hawazidi laki 5 wenye akili mbovu.hivyo changanua mwenyewe.

Na Tanzania sio kisiwa cha mbali na Dunia. Me ngoja niishie hapo.

Ila na tume inajua nini kitatokea
 
Naamini mawakala wote wa CHADEMA watakua wamepata Elimu vizuri juu ya usimamizi wa kura, Hivyo ata watakaokuwa mawakala watakua wameandaliwa vizuri ili kuepuka rushwa ndani ya vyumba vya kupiga kura.
 
Hai chadema kama hawana pesa za kulipa mawakala waitishe michango wilaya kwa wilaya, tuchangue.

Hakuna maana kwenda kupiga kura halafu wakala anaachia mafisadi kufanya yao.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom