Chadema Wafanye Mkutano mkubwa Dar Haraka maana karibia wakamatwe

Kwa vile dalilizote zinaonesha kuwa serikali ina lengo la kuwakamata Chadema kwa uhaini, ni vizuri wafanye mkutano mkubwa Dar es Salaam, wahamasishe peoples power ili pindi tu akikamatwa kiongozi yeyote wa Chadema, maandamano yaanzie hapohapo, vilevile naona serikali ya ccm inajiyafutia kifo chake yenyewe. Kwani Chadema hawajafanya uhaini wowote, wanachokiongea ni cha kawaida kabisa, sasa uhaini umetoka wapi? Hali ni mbaya kila mtu anaona. kwa hiyo ni dhambi kusema na kuwaeleza watanzania kuwa hali ni mbaya? Kwa nini watu hawataki kukosolewa? Anayesema hivyo nadhani hajaudhuria mkutano hata mmoja wa CDM. Mie sijaona baya lolote.

Sasa peoples powerrr iko hivi, mkijidanganya mkawakamata CDM, tunaanzia hapo kuingia barabarani nchi nzima. Naomba ufanywe nkutano mkubwa Dar fasta maana mambo yote yanaweza kuanzia hapo. Serikali muache vitisho ....... sasa wakamateni CDM muone .................cha .........moto.
CHADEMA wanakwenda kwa Ratiba na wana strategies. Hawakurupuki, hawaendeshwi na matukio.Kama Dar haipo kwenye ratiba yao kwa sasa hawawawezi kufanya.
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

Nyie watoto wa mafisadi naona msha anza kuchanganyikiwa kama wazazi wenu. Mlifikiri mtatesa siku zote kama Makamba na mwanaye, JK na RiZ1, akina Kingunge etc??? Kwa Taarifa yenu CDM hawana ubavu wa kuwaondoa kwa mtindo wa Tunisia na Egypt ila WATU ndiyo wenye nguvu hiyo. Kwa hiyo kama kazi yenu ni nzuri hamna haja ya kuwaogopa watu waliowachagua wazazi wenu waongoze nchi hii. PIPOOOOOOOOS POWER!!
 
Its true, hata mimi nimesikia huo mkutano haukuhudhuriwa na Rais yeyote zaidi ya JK!

labda alialikwa peke yake.halafu pia nilikuwa na swali wandugu mbona sisikii akitembelea nchi za afrika mashariki au hapa karibu huwa anatuma wawakilishi?
 
Keyboard warriors!

Jaribuni Dsm muone mziki wake na ndio mtajua JK anaungwa mkono kiasi gani.

Wachochezi wakubwa ninyi; Mlaaniwe popote mlipo!
 
Keyboard warriors!

Jaribuni Dsm muone mziki wake na ndio mtajua JK anaungwa mkono kiasi gani.

Wachochezi wakubwa ninyi; Mlaaniwe popote mlipo!


Yeah keyboards can produce wonders! Hii ni generation ya TEKNOHAMA mazee. So endelea kudharau nguvu ya keyboards afu mguu utaota tende!

Amandlah.
 
Dar ni sehemu yenye siasa za kinafiki sana, siwatukani wakazi wa Dar ila ukweli ni kwamba ni vigeugeu hata ndani ya sanduku la kura,<br />
Kuna jirani aliwahi kuniambia ukitaka kupigwa kubali kuwa wakala wa CUF kwenye uchaguzi lazma utaambiwa umeuza kura kumbe wana CUF wenyewe (Mbagala na Temeke) wakiingia ndani hawawapigii kura watu wao.<br />
<br />
Hamshangai CUF hawajai kuwa na mbunge Dar, Dar is all about CCM VOTERS hasa kwa wanaojiita wazawa, ubungo na Kawe kuna upinzani kwa kuwa kuna wahamiaji wengi wa miaka ya karibuni.<br />
<br />
STATERGICALLY DAR SIO MAHALI PA CDM wala CUF kuwekeza nguvu nyingi.
<br />
<br />
 
kwahiyo maandamano ndio njia ya kuingia ikulu au? maana cjapata hoja ya kunishawishi kuunga mkono maandamano haya.
ukiniambia lengo wanalotaraji kulifikia baada ya haya maandamano nitakuunga mkono
 
&lt;br /&gt;<br
Good Reasoning Martina,Dar is unpredictable when it comes to voting!!
Nakubaliana na wewe kwamba maeneo mengi ya Dar yanayokaliwa na "wazawa" kuna Unafiki mwingi,Nevertheless,tusife Moyo,hiki kizazi cha Wazawa kinazidi kuhamishwa and soon we shall observe change!!
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

Ushuziiiiiiii
 
Mpaka sasa sijaona mtu wa Dar anayeweza kuandamana kisa kiongozi fulani kakamatwa Arusha sawa sababu mnazijua. Kingine sioni chadema inachofanya katika maandamano kama kafulila alivyosema serikali inaifagilia chadema bure. chadema wanachojua ni lawama, dowans, epa na kutafuta kuonewa huruma, nasema hivi kwa kuwa sijawahisikia wakihamasisha watu kufanya kazi, wakihamasisha vijana kupambana na uhalifu hasa wanapokua wameajiriwa sehemu yoyote bila kujali itikadi zao, vijana kuungana kuikomboa nchi kutoka utumwani.

CHADEMA wajipange upya waje na new strategies za kupambana na malaghai yanayoiangamiza nchi yetu. Strategy ya kucheza na hisia za watanzania zinaanza kuwachosha watu na kuwafanya ccm wawe sugu. Waje na mbinu nyingine kuaibisha madhalimu. Mfano mzuri ni kutumia fedha wazotumia kwa maandamano kutunisha mifuko ya maendeleo katika majimbo yao kama walivyoanza Mh. Lema na baadhi ya wabunge wengine.

Umenifurahisha kweli hapo kwenye RED ulichokiongea ni sawa na kumwambia mtu amaasishe watu kula kuku samaki na maziwa wakati hata uwezo wa kula bamia hana! sasa wewe unaesema CHADEMA ihamasishe watu kufanya kazi unachekesha kweli kweli, ni nani anaehitaji kuhamasishwa kula? kazi zenyewe ziko wapi? wewe ni pimbi tu, ni mfu ingali upo hai.
 
kwahiyo maandamano ndio njia ya kuingia ikulu au? maana cjapata hoja ya kunishawishi kuunga mkono maandamano haya.
ukiniambia lengo wanalotaraji kulifikia baada ya haya maandamano nitakuunga mkono

Tarehe uliyojiunga JF tayari wazoefu wameshakuelewa, endelea tu kusubili jibu.
 
tatizo la serikali ya CCM ni kwamba wanapenda kuongoza watu wasiotambua haki zao pamoja na wenye uelewa mdogo au wapenda maslahi binafsi. Sasa kwa zama hizi za utandawazi na kizazi kipya cha miaka ya 80 ambacho ndo wengi kwa sasa hivi CCM ipo njia panda na ni suala la muda tu lazima itawekwa pembeni kwa njia halali kabisa wala siyo kwa fujo kama inavyo hofia.Mzoefu wa vurugu la fujo ni nani kama si CCM? Chama gani kililazimisha kushinda kwa nguvu mwaka jana 2010?
 
Ni kweli wewe sio JK lakini akili kama mnafanana vile

Pili tuambie wapi kanda ya ziwa umesikia uvunjifu wa amani baada ya polisi kukubali kulinda mkutano badala ya kuanzisha vurugu.

Chadema hawajaanzisha fujo popote na ushahidi upo, serikali ikijifanya kuwashugulikia yenyewe ndio itaanzisha fujo. Ni haki ya kikatiba ya chama cha siasa kufanya maandamano na mikutano ya siasa, ulikuwa hujui hilo tutakucheka.

Ni lipi kati ya wanayosema Chadema halina ukweli? Naomba unitajie. Dowans kampuni ya Kikwete na akina Rostam mtanzania gani anapenda ilipwe? , gharama za maisha hazijapanda?, uchumi haujaporomoka? ufisadi haujaongezeka?.

Wewe ni mtanzania kweli? Endelea kulala tukifika tutakuamsha.

1) Unafanya maandamno ili iwe nini? Kama ujumbe si umesha ufikisha? Au maandamano ya kila siku yanaashiria nini?

2)Ni haki ya kikatiba kufanya maandamano, hilo hakatai mtu, lakini kumbuka katiba hiyo hiyo mlisema ina mapungufu, sasa hiki kipengele cha haki ya maandamano hata kama yanaashiria uvunjifu wa amani inabidi serikali iliyopo madarakani ikishughulikie haraka sana. Na kwa sasa iamuwe kutokutoa vibali vya maandamano, si kila kitu kifanyiwe maandamano. Itakuwa nchi au uwanja wa maandamano.

3) Hayo yote ya dowans ni uzushi na uongo mtupu. ICC na majudge wa kimataifa wasione hayo unayosema wewe (mwenzangu na mie)?

Mbona wanaharakati wametumia njia za kisheria kutuwa mahakamani kuhusu dowans? Kwa sasa hicho cha dowans si kigezo tena cha maandamano, wacha uvivu wa kufikiri.

Mimi si mTanzania kama wewe ulivyo, kwani nna uhakika umezaliwa wakati Tanzania imeshaundwa. Mimi ni mTanganyika kabla ya Tanzania kuwepo.
 
serikali yenu omba-omba haina ubavu wa kukamata na kuwaweka vizuizini viongozi wa upinzani. labda mtu wenu awe ameacha mchezo wake wa kusafiri kila wiki kwenda kucheka-chaka na kina Sarkozy

Anadhani JK anapenda waaandamane?
Akiwa kataza atatembelea nchi gani sasa?

Labda Oman
 
1) Unafanya maandamno ili iwe nini? Kama ujumbe si umesha ufikisha? Au maandamano ya kila siku yanaashiria nini?

2)Ni haki ya kikatiba kufanya maandamano, hilo hakatai mtu, lakini kumbuka katiba hiyo hiyo mlisema ina mapungufu, sasa hiki kipengele cha haki ya maandamano hata kama yanaashiria uvunjifu wa amani inabidi serikali iliyopo madarakani ikishughulikie haraka sana. Na kwa sasa iamuwe kutokutoa vibali vya maandamano, si kila kitu kifanyiwe maandamano. Itakuwa nchi au uwanja wa maandamano.

3) Hayo yote ya dowans ni uzushi na uongo mtupu. ICC na majudge wa kimataifa wasione hayo unayosema wewe (mwenzangu na mie)?

Mbona wanaharakati wametumia njia za kisheria kutuwa mahakamani kuhusu dowans? Kwa sasa hicho cha dowans si kigezo tena cha maandamano, wacha uvivu wa kufikiri.

Mimi si mTanzania kama wewe ulivyo, kwani nna uhakika umezaliwa wakati Tanzania imeshaundwa. Mimi ni mTanganyika kabla ya Tanzania kuwepo.

Kumbe majibu unayo eh?
Ujumbe umefikishwa kwa njia gani?
Wangapi wamefikishiwa ujumbe huo,kanda ya ziwa tu mpaka sasa bado mikoa 23 mtakoma
 
Kwa vile dalilizote zinaonesha kuwa serikali ina lengo la kuwakamata Chadema kwa uhaini, ni vizuri wafanye mkutano mkubwa Dar es Salaam, wahamasishe peoples power ili pindi tu akikamatwa kiongozi yeyote wa Chadema, maandamano yaanzie hapohapo, vilevile naona serikali ya ccm inajiyafutia kifo chake yenyewe. Kwani Chadema hawajafanya uhaini wowote, wanachokiongea ni cha kawaida kabisa, sasa uhaini umetoka wapi? Hali ni mbaya kila mtu anaona. kwa hiyo ni dhambi kusema na kuwaeleza watanzania kuwa hali ni mbaya? Kwa nini watu hawataki kukosolewa? Anayesema hivyo nadhani hajaudhuria mkutano hata mmoja wa CDM. Mie sijaona baya lolote.

Sasa peoples powerrr iko hivi, mkijidanganya mkawakamata CDM, tunaanzia hapo kuingia barabarani nchi nzima. Naomba ufanywe nkutano mkubwa Dar fasta maana mambo yote yanaweza kuanzia hapo. Serikali muache vitisho ....... sasa wakamateni CDM muone .................cha .........moto.
Mbona Jk katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Feb 2011 amesema hali ni ngumu? au yeye tu ndio ana haki ya kusema hivyo na si wengine?
 
Kwa vile dalilizote zinaonesha kuwa serikali ina lengo la kuwakamata Chadema kwa uhaini, ni vizuri wafanye mkutano mkubwa Dar es Salaam, wahamasishe peoples power ili pindi tu akikamatwa kiongozi yeyote wa Chadema, maandamano yaanzie hapohapo, vilevile naona serikali ya ccm inajiyafutia kifo chake yenyewe. Kwani Chadema hawajafanya uhaini wowote, wanachokiongea ni cha kawaida kabisa, sasa uhaini umetoka wapi? Hali ni mbaya kila mtu anaona. kwa hiyo ni dhambi kusema na kuwaeleza watanzania kuwa hali ni mbaya? Kwa nini watu hawataki kukosolewa? Anayesema hivyo nadhani hajaudhuria mkutano hata mmoja wa CDM. Mie sijaona baya lolote.

Sasa peoples powerrr iko hivi, mkijidanganya mkawakamata CDM, tunaanzia hapo kuingia barabarani nchi nzima. Naomba ufanywe nkutano mkubwa Dar fasta maana mambo yote yanaweza kuanzia hapo. Serikali muache vitisho ....... sasa wakamateni CDM muone .................cha .........moto.

nitaishangaa serikali kwani ikiwakamata cdm ndo itakuwa inafanya uhaini kwa wananchi wapenda maendeleo!!!!
 
Back
Top Bottom