Chadema Wafanye Mkutano mkubwa Dar Haraka maana karibia wakamatwe

Ta Muganyizi

R I P
Oct 19, 2010
5,361
2,734
Kwa vile dalilizote zinaonesha kuwa serikali ina lengo la kuwakamata Chadema kwa uhaini, ni vizuri wafanye mkutano mkubwa Dar es Salaam, wahamasishe peoples power ili pindi tu akikamatwa kiongozi yeyote wa Chadema, maandamano yaanzie hapohapo, vilevile naona serikali ya ccm inajiyafutia kifo chake yenyewe. Kwani Chadema hawajafanya uhaini wowote, wanachokiongea ni cha kawaida kabisa, sasa uhaini umetoka wapi? Hali ni mbaya kila mtu anaona. kwa hiyo ni dhambi kusema na kuwaeleza watanzania kuwa hali ni mbaya? Kwa nini watu hawataki kukosolewa? Anayesema hivyo nadhani hajaudhuria mkutano hata mmoja wa CDM. Mie sijaona baya lolote.

Sasa peoples powerrr iko hivi, mkijidanganya mkawakamata CDM, tunaanzia hapo kuingia barabarani nchi nzima. Naomba ufanywe nkutano mkubwa Dar fasta maana mambo yote yanaweza kuanzia hapo. Serikali muache vitisho ....... sasa wakamateni CDM muone .................cha .........moto.
 
Kwanini serikali mnaogopa kama mna uhakika kwamba hamjawakosea wananchi??? ahaghgggggggggggghh
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

serikali yenu omba-omba haina ubavu wa kukamata na kuwaweka vizuizini viongozi wa upinzani. labda mtu wenu awe ameacha mchezo wake wa kusafiri kila wiki kwenda kucheka-chaka na kina Sarkozy
 
kuna quote moja kwenye gazeti la mtanzania la leo ni nzuri sana (iko kwenye ukurasa wa mbele)nikilipata nitaanzisha thread. ok by the way kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake,hivyo basi kwa kuwakamata viongozi wa chadema kutachochoa machafuko zaidi na kusababisha vurugu zisizo na maana,kwa kuwa chadema wanaongelea hali halisi ya watanzania kwa nini viongozi wetu wanakwepa hoja na kujaribu kukemea na kukurupuka.
 
serikali yenu omba-omba haina ubavu wa kukamata na kuwaweka vizuizini viongozi wa upinzani. labda mtu wenu awe ameacha mchezo wake wa kusafiri kila wiki kwenda kucheka-chaka na kina Sarkozy
Kwani ameonana na Sarkozy....!!!!!!,sidhani.....huyo rais Sarkozy ana kazi nyingi sana siyo kuhudhuria mikutano ya NGOs
 
Dar ni sehemu yenye siasa za kinafiki sana, siwatukani wakazi wa Dar ila ukweli ni kwamba ni vigeugeu hata ndani ya sanduku la kura,
Kuna jirani aliwahi kuniambia ukitaka kupigwa kubali kuwa wakala wa CUF kwenye uchaguzi lazma utaambiwa umeuza kura kumbe wana CUF wenyewe (Mbagala na Temeke) wakiingia ndani hawawapigii kura watu wao.

Hamshangai CUF hawajai kuwa na mbunge Dar, Dar is all about CCM VOTERS hasa kwa wanaojiita wazawa, ubungo na Kawe kuna upinzani kwa kuwa kuna wahamiaji wengi wa miaka ya karibuni.

STATERGICALLY DAR SIO MAHALI PA CDM wala CUF kuwekeza nguvu nyingi.
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

Ni kweli wewe sio JK lakini akili kama mnafanana vile

Pili tuambie wapi kanda ya ziwa umesikia uvunjifu wa amani baada ya polisi kukubali kulinda mkutano badala ya kuanzisha vurugu.

Chadema hawajaanzisha fujo popote na ushahidi upo, serikali ikijifanya kuwashugulikia yenyewe ndio itaanzisha fujo. Ni haki ya kikatiba ya chama cha siasa kufanya maandamano na mikutano ya siasa, ulikuwa hujui hilo tutakucheka.

Ni lipi kati ya wanayosema Chadema halina ukweli? Naomba unitajie. Dowans kampuni ya Kikwete na akina Rostam mtanzania gani anapenda ilipwe? , gharama za maisha hazijapanda?, uchumi haujaporomoka? ufisadi haujaongezeka?.

Wewe ni mtanzania kweli? Endelea kulala tukifika tutakuamsha.
 
Wewe naona ni wale wale, Chama cha siasa chochote makini kama kilivyo CDM ni kuhuhubiri siasa. Kwa chama cha cha upinzani kazi yake kubwa ni kuikosoa serikali iliyoko madarakani. Siyo kazi ya upinzani kuisifia serikali iliyoko madarakani.

Ili uongee na wanachama huwezi kuwafuata mmoja mmoja nyumbani, ni lazima uwakusanye, uwahamasishe na uwaeleze madhaifu ya serikali iliyoko madarakani. Taabu chama tawala kilizoea siasa za wakati wa uchaguzi tu, kinaachwa kipindi chote hiki kinafanya kinavyotaka. Uwajibikaji kwa waajiri wao - yaani wananchi unakuwa hakuna.

Siasa ni kuvumiliana, na hasa kwa chama kilichoko madarakani lazima wakubali kukosolewa na yule anayewakosoa asionekane kama mhaini, kwanza anawasaidia kujirekebasha.

Hayati Mwl Nyerere aliwahi kusema enzi za uhai wake kwamba: Vyama vya Upinzani ni VIOO vya ccm. Inajiangalia kupitia ukosoaji na kutumia muda huo kujirekebisha.

Vyama vya upinnzani ni sawa na mcheza mpira aliyeko Benchi. Ukivurunda tu unaona mtu "ana-troti",(anapiga jaramba), ndivyo CDM wanavyofanya, cha msingi ccm wakaze buti kutatua kero za msingi za waTZ, wanaweza wakacheza hadi dk ya 90. Vinginevyo wachezaji wa akiba tunao wengi, na pengine ni wazuri kuliko waliomo uwanjani kwa sasa.
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

Akupe nani uongozi wakati wewe ni kipofu?
 
Mpaka sasa sijaona mtu wa Dar anayeweza kuandamana kisa kiongozi fulani kakamatwa Arusha sawa sababu mnazijua. Kingine sioni chadema inachofanya katika maandamano kama kafulila alivyosema serikali inaifagilia chadema bure. chadema wanachojua ni lawama, dowans, epa na kutafuta kuonewa huruma, nasema hivi kwa kuwa sijawahisikia wakihamasisha watu kufanya kazi, wakihamasisha vijana kupambana na uhalifu hasa wanapokua wameajiriwa sehemu yoyote bila kujali itikadi zao, vijana kuungana kuikomboa nchi kutoka utumwani.

CHADEMA wajipange upya waje na new strategies za kupambana na malaghai yanayoiangamiza nchi yetu. Strategy ya kucheza na hisia za watanzania zinaanza kuwachosha watu na kuwafanya ccm wawe sugu. Waje na mbinu nyingine kuaibisha madhalimu. Mfano mzuri ni kutumia fedha wazotumia kwa maandamano kutunisha mifuko ya maendeleo katika majimbo yao kama walivyoanza Mh. Lema na baadhi ya wabunge wengine.

Muda wa majungu ya siasa umepita sasa tutumie majungu ya kisayansi kuijenga nchi na kuaibisha madhalimu. kwa mfano tufanye liwezalo kumsahuri rais katika kupata wakurugenzi wa idara nyeti kwa kutumia misingi ya kitaalamu na siyo kisiasa kama kiongozi wa TAKUKURU, Usalama wa Taifa (CID), Tume ya mipango, tume ya haki za binadamu, tume ya uchaguzi, msajili wa vyama vya siasa nk pia kuondoa taasisi zisizokua na sababu ya kuwepo yaani zinazofanya kazi zinazoingiliana kama mkukuta, mkurabita nk. pia kwa maslahi ya nchi katika kupanga muundo wa serikali, muundo wa mahakama. Haya yote ni hujuma kwa madhalimu na mwisho wake ni kuwadhalilisha bila kujali wanatokea chama gani cha kisiasa maana wanasiasa wote lao sawa ila mipango ndiyo tofauti.
 
Hakuna kitu kama hicho kwani wakamatwe kwa kosa gani? dar tutafanya maandamano tu kufuatana na ratiba yeu!
 
duh kwa hali hii mie naona watz wakubali tu kwamba ni maskini basi. Msijitingishe kaeni hivyo hivyo. Acheni wenye kula wale, ukipata nafasi pa kuitafuna nchi tafuneni maana watu kama wameridhika na hali iliyopo aghhhhh.
 
Ikiwa viongozi wa Chadema turufu yao wanayoitumia ni maandamano basi wajuwe hawana ubunifu wala muelekeo.

Kwa upande wangu, naona hata JK bado anawabembeleza sana. Laiti ningekuwa mimi ndie nnaongoza, saa hizi kusingekuwa na kiongozi wa Chadema anatembea mitaani kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Ingekuwa kweli wanayoyasema yote yana ukweli wangetumia njia za amani na si hizi za kuandamanisha watu kwa majungu.

Nasema, serikali iwashughulikie kisheria hawa waanzisha fujo haraka iwezekanavyo. Kwa nini inawaona wanaanzisha maandamano yasiyo na maana yoyote halafu inawaacha tu waendelee? Serikali iwafungulie mashitaka ya uvunjaji wa amani haraka iwezekanavyo.

Katika yoote uliyoongea nimekuheshimu sana penye red. Kikwete ndo anataka kuvunja amani ya nchi hii, sisi tuna sheria zetu akitokea mtu anahatarisha amani yetu apelekwe mahakamani kujibu makosa yake kisheria siyo malalamiko utadhani mwimbaji wa taarabu, kikwete ana ni-let down mwanaume mwenzake
 
dar cha mtoto bana kwenye kupiga kura hawana lolote hakuna umuhimu wa kufanya mkutano dar vijijini ndo wanahitaji kuamshwa sasa maana bado kuna watu wanajua ccm ni ya nyerere ndo mana wanaichagua so big up cdm kazeni buti kuwaamsha hao wa mashambani kitaeleweka tuuu!!
 
Mpaka sasa sijaona mtu wa Dar anayeweza kuandamana kisa kiongozi fulani kakamatwa Arusha sawa sababu mnazijua. Kingine sioni chadema inachofanya katika maandamano kama kafulila alivyosema serikali inaifagilia chadema bure. chadema wanachojua ni lawama, dowans, epa na kutafuta kuonewa huruma, nasema hivi kwa kuwa sijawahisikia wakihamasisha watu kufanya kazi, wakihamasisha vijana kupambana na uhalifu hasa wanapokua wameajiriwa sehemu yoyote bila kujali itikadi zao, vijana kuungana kuikomboa nchi kutoka utumwani.

CHADEMA wajipange upya waje na new strategies za kupambana na malaghai yanayoiangamiza nchi yetu. Strategy ya kucheza na hisia za watanzania zinaanza kuwachosha watu na kuwafanya ccm wawe sugu. Waje na mbinu nyingine kuaibisha madhalimu. Mfano mzuri ni kutumia fedha wazotumia kwa maandamano kutunisha mifuko ya maendeleo katika majimbo yao kama walivyoanza Mh. Lema na baadhi ya wabunge wengine.

Muda wa majungu ya siasa umepita sasa tutumie majungu ya kisayansi kuijenga nchi na kuaibisha madhalimu. kwa mfano tufanye liwezalo kumsahuri rais katika kupata wakurugenzi wa idara nyeti kwa kutumia misingi ya kitaalamu na siyo kisiasa kama kiongozi wa TAKUKURU, Usalama wa Taifa (CID), Tume ya mipango, tume ya haki za binadamu, tume ya uchaguzi, msajili wa vyama vya siasa nk pia kuondoa taasisi zisizokua na sababu ya kuwepo yaani zinazofanya kazi zinazoingiliana kama mkukuta, mkurabita nk. pia kwa maslahi ya nchi katika kupanga muundo wa serikali, muundo wa mahakama. Haya yote ni hujuma kwa madhalimu na mwisho wake ni kuwadhalilisha bila kujali wanatokea chama gani cha kisiasa maana wanasiasa wote lao sawa ila mipango ndiyo tofauti.


Nadhani umejaza maneno mengi tu...ngoja nikusasahishe, hayo hayo uliyonena kwa ujumla wake ndio katiba mpya ambayo CHADEMA ndio vinara wa kuilazimisha serikali ifanye mchakato wa kuipata kwa manufaa ya wananchi wote...we vipi bana!!!!
 
Kwani kazi ya chama cha upinzani ni nini? Sio kuikosoa serikali, na pale inapoonekana haiwezi, kuishinikiza ijiuzulu?

CDM ina wajibu, wa kikatiba, kuikosoa serikali ya CCM, na pale inapoonekana serikali haikosoleki, kuishinikiza ijiuzulu.

Njia ya kawaida ya amani, ya chama cha upinzani kuishinikiza serikali iachie ngazi (kama serikali ikionekana kushindwa kuongoza), ni ipi? Sio maandamano ya amani?

Naona wanaopinga maandamano ya amani ya CDM wana lao. Wanataka kuleta vurugu.
 
CDM wakamatwe kwani wamekosa nn?? Wanaongea na wananchi kuhusu natatizo yao na jinsi serikali inavyotakiwa kuyashughilikia. Mbona ccm mnaogopa kivuli chenu?? CCM wamezoea kuwadanganya wananchi sasa wanapoona wanaelezwa ukweli wanachachawa.
Go go gooooooooooo CDM
 
Back
Top Bottom