MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,173
Dk Slaa anena
Dk Slaa amesema chama hicho kinatarajia kuchimba visima vya maji 11 katika Wilaya ya Igunga mkoani Tabora ikiwa ni wiki takriban mbili tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa jimbo hilo uliofanyika Oktoba 2.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kukabidhi mchanganuo wa namna walivyogawa mradi wa utekelezaji wa visima 200, vilivyotolewa na Sabodo kwa lengo la kuchimbwa katika majimbo tofuati wanakotoka wabunge wa Chadema.
Alisema lengo la kutekeleza mradi huo wa maji katika Jimbo la Igunga limetokana na ziara aliyoifanya katika vijiji 98, vilivyopo katika jimbo hilo na kugundua wananchi wake wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji.
Katika mpango kazi wetu, tumepanga kuchimba visima 11 katika Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, hii imetokana na ziara yangu katika vijiji 98 ambapo niligundua kuwa wakazi hao wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji,alifafanua Dk Slaa.
Chadema kilishika nafasi ya pili katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, kwa aliyekuwa mgombea wake, Joseph Kashindye kupata kura 23,260 sawa na asilimia 44.3, nyuma ya mgombea wa CCM, Dalaly Kafumu aliyeshinda kwa kura 26,484 kati ya 52,487 halali zilizopigwa, sawa na asilimia 50.4.
Habari zinasemekana kuwa baada ya Kafumu wa CCM kushinda ubunge tayari ameisha weka makazi ya kudumu Mbezi beach Dar es Salaam na kuwaacha wananchi wa Igunga wakifa na njaa na kuhangaika huku na kule kutafuta maji,,,hiki kitendo kimefanya CHADEMA waamue kuanza kuwatekelezea mradi wa visima 11 vya maji wananchi wa Igunga japo hawakushinda ndani ya hilo jimbo kwani kipindi cha kampeni Dr Slaa aliona ni kiasi gani wanachi wa Igunga wanavyoteseka na uhaba wa maji..
Dk Slaa amesema chama hicho kinatarajia kuchimba visima vya maji 11 katika Wilaya ya Igunga mkoani Tabora ikiwa ni wiki takriban mbili tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa jimbo hilo uliofanyika Oktoba 2.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kukabidhi mchanganuo wa namna walivyogawa mradi wa utekelezaji wa visima 200, vilivyotolewa na Sabodo kwa lengo la kuchimbwa katika majimbo tofuati wanakotoka wabunge wa Chadema.
Alisema lengo la kutekeleza mradi huo wa maji katika Jimbo la Igunga limetokana na ziara aliyoifanya katika vijiji 98, vilivyopo katika jimbo hilo na kugundua wananchi wake wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji.
Katika mpango kazi wetu, tumepanga kuchimba visima 11 katika Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, hii imetokana na ziara yangu katika vijiji 98 ambapo niligundua kuwa wakazi hao wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji,alifafanua Dk Slaa.
Chadema kilishika nafasi ya pili katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, kwa aliyekuwa mgombea wake, Joseph Kashindye kupata kura 23,260 sawa na asilimia 44.3, nyuma ya mgombea wa CCM, Dalaly Kafumu aliyeshinda kwa kura 26,484 kati ya 52,487 halali zilizopigwa, sawa na asilimia 50.4.
Habari zinasemekana kuwa baada ya Kafumu wa CCM kushinda ubunge tayari ameisha weka makazi ya kudumu Mbezi beach Dar es Salaam na kuwaacha wananchi wa Igunga wakifa na njaa na kuhangaika huku na kule kutafuta maji,,,hiki kitendo kimefanya CHADEMA waamue kuanza kuwatekelezea mradi wa visima 11 vya maji wananchi wa Igunga japo hawakushinda ndani ya hilo jimbo kwani kipindi cha kampeni Dr Slaa aliona ni kiasi gani wanachi wa Igunga wanavyoteseka na uhaba wa maji..