CHADEMA unganeni na ACT Wazalendo

Matusi yako wapi? Hizo kampeni unasubiri kutoka wapi kama hakutakuwa na tume huru ya uchaguzi?
Mpango wa kususia uchaguzi ni mwendelezo wa kuminya demokrasia ndani ya chama, maana hata bungeni ni jambo la kawaida.

Mtu mwenye tabia ya kususasusa kamwe hawezi kutoa ushirikiano, na akishirikiana ni kwa unafiki tu. Katika maisha ya binadamu huitwa MBEA
 
L
Kuna msemo unaosema ''HATA TAMU HUKINAI''. Msemo huu unamhusu Zitto kwa 100%. Watanzania wamemchoka sana zitto na ukitaka kuamini hilo fanya uchunguzi mdogo wa kufuatilia hoja anazozitoa zito kwa vyombo vya habari au katika mitandao ya kijamii. Zaidi ya asilimia 95 ya wachangiaji hawamuungi mkono. Hiyo ni dalili ya kuwa wamemchoka (amewakinai).



Sent using Jamii Forums mobile app

Acha upotoshaji, maoni ya Zito tunayaona na yanaungwa mkono na watu wengi. Sema matamanio yako ni watu wasimuunge mkono Zito.
 
Mpango wa kususia uchaguzi ni mwendelezo wa kuminya demokrasia ndani ya chama, maana hata bungeni ni jambo la kawaida.

Mtu mwenye tabia ya kususasusa kamwe hawezi kutoa ushirikiano, na akishirikiana ni kwa unafiki tu. Katika maisha ya binadamu huitwa MBEA

Kwa taarifa yako chama kama cha kinaweza kushiriki, ila sisi wapiga kura tunaojitambua hatutakuwa na muda wa kupoteza iwapo hakuna tume huru ya uchaguzi. Wao chama kama chama wanaweza kushiriki, ila sisi wapiga kura wao hatutakuwa na muda wa kushiriki huo upuuzi. Hakuna popote tunawaambia chama waache kushiriki, ila kama watakubali kushiriki wakati sisi wapiga kura hatuko tayari kushiriki uchaguzi chini ya tume isiyo huru hiyo ni juu yao. Wawaache Ccm na vyama vyake mapandikizi kama Cuf, NCCR, TLP nk washiriki.
 
Siasa haina adui wa kudumu mpendwa. Kuna mtu alinangwa na cdm kama Lowasa? Lakini hukumbuki huyo Lowasa aliyasahau yote na akawa mgombea urais kwa tiketi ya cdm?

Sent using Jamii Forums mobile app

Nani anakuambia Lowassa aliyasahau? Kuna mtu anasahau ukweli, yeye aliamua liwalo na liwe ili mradi atimize ndoto yake ya kuwa rais.
 
Usichokijua ni kwamba ili chama cha upinzani kifanikiwe Tanzania kwa sasa ni lazima kipendwe na Mungu wa miungu bwana wa mabwana alfa na omega nani kama yeye, ila vyama ulivyotaja hakuna hata kimoja kinachopendwa!
 
Chadema kimekuwa Chama cha kwenda kujiunga na Vyama vingine badala ya Vyama vingine vije kujiunga na Chadema haa!!

Na wanachama wake walivyokuwa wabishi, wanajaribu kukubali leo!!?

Mkuu, unamaanisha Kwamba Chadema Kwa sasa ndio Chama kidooogo kuliko ACT na Vyama vingine siyo?

Na nyinyi watu wa Chadema mnaounga mkono kwani mnaona Chama kinaenda shimoni siyo,

Ushauri wangu, Chadema haijachelewa kuchukua hatua madhubuti na kukirudisha Chama kwenye anga zake

Chadema inatatizo moja dooogo Sana, Ni mtu mmoja kukubali kwamba anafanya makosa katika Uongozi wake, kwani makosa yake ndiyo yamesababisha wengine nao wakaanza kutenda makosa, Mimi Naamini, wawili wanapokuwa kwenye ndoa, pale panopokosekana uwazi huwa wanaanza kuviziana,

Lakini uwazi ukitawala, kila kitu huenda Sawa,
 
Mkuu ni wendawazimu kushawishi watu wakapige kura ambazo haziheshimiwi. Hata hivyo nani kakuambia kuwa lazima ccm watoke madarakani kwa njia ya kura? Kwani wao ccm wanategemea njia ya kura kukaa madarakani? Kwa taarifa yako sio kwamba nashawishi, bali wengi wetu tumeshachukua maamuzi kuwa bila tume huru ya uchaguzi hatushiriki huo uhuni. Kama ulitarajia watu kwenda kujazana vituoni ili ccm wajitangaze kushinda kwa kishindo, basi umeumia.

Una uhakika na maneno yako.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi wapiga kura wa cdm hatujali hata ccm wakitangazwa washindi, tunajua fika hakuna uchaguzi. Hata kama watajitangaza washindi hatujali maana tunajua wako madarakani bila ridhaa yetu wala ushindi halali.

Nyie wangapi. Unajua unazungumza as if mko one million people. You are you. The only you. We toka lini ukawa CHadema. Usisemee nafsi. Kuwa kwanza na uhakika kama huyo unayeandika naye upamoja Ni ndugu yako kweli? Huwa nashangaa inawezekanaje mtu unaishi na mkeo unamlisha na kila kitu Lakini anachepuka na akirudi Home mahaba anakupa ya mwendo kasi. Ya moyoni ndo mtihani. So always talk about yourself and do not generalize.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie wangapi. Unajua unazungumza as if mko one million people. You are you. The only you. We toka lini ukawa CHadema. Usisemee nafsi. Kuwa kwanza na uhakika kama huyo unayeandika naye upamoja Ni ndugu yako kweli? Huwa nashangaa inawezekanaje mtu unaishi na mkeo unamlisha na kila kitu Lakini anachepuka na akirudi Home mahaba anakupa ya mwendo kasi. Ya moyoni ndo mtihani. So always talk about yourself and do not generalize.


Sent using Jamii Forums mobile app

Sina shaka na nilichokisema. Wananchi wengi ujinga umeshawatoka, hivyo wanajua kila kitu boss.
 
Zitto kama akikubali kufanya hivo nitamuona hamnazo kabisa. Kwa jinsi walivyomnanga kipindi kile afu Leo watake kuungana nae tena.?
Zitto usikubali kufanya huo ujinga hao wote walitaka upotee lakini ulipambana kiume sana hadi leo hii heshima imeanza kurudi.
Siyo Zitto tu, hata Maalim Seif hayuko tayari kujiunga na CDM ndomana hakukimbilia huko alipojiondoa CUF licha kukaribishwa kwa kuahidiwa "zawadi" ya kuwa mgombea urais na kuungwa mkono katika harakati zake dhidi ya Lipumba.
 
Msimamo wangu uko pale pale,chama kitakachopokea mamluki na wapiga dili wa sisiemu,kwangu mimi sio chama pinzani ni sisiemu B.
 
Back
Top Bottom