Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,389
- 31,335
- Thread starter
- #721
Nafasi yetu kama Raia ni kubwa sana, tunachotofuatiana ni jinsi gani wananchi watumie nafasi hiyoNimekupata Mkuu.
Nikijibia swali lako kama tuna instructors na kama wanajua wajibu wao na kuuwajibikia. Ni wazi nafasi yao ipo, na wenyewe waliojivika kofia hizo wapo, lakini wanachofanya ni Ubatili. Hivyo tunaweza sema ni Watu Hewa.
Swali, ni je huo ndio ukomo wa ndoto za wananchi wetu? Je, Hatima ya umma wetu inabebwa na hilo tu, kiasi hatuwezi kufanikiwa katika lolote pasipo wao?
Nafikiri huo ndio msingi wa hoja ya Mwalimu, IPI I NAFASI YETU KAMA RAIA KATIKA KUONDOA UNYONGE WETU? Nafikiri huo ndio mwanzo wa UTAMBUZI wa kweli.
Kama ulinisoma mwanzo niliporudisha bandiko hili la miaka mingi, nilisema ni makosa makubwa wananchi kulaumu CCM na Serikali yao wakiwa hawafanyi tofauti au lolote
Nilirudia kuonyesha udhaifu ulioifikisha CUF ilipo, nikaenda kwa Chadema
Udhaifu unao onekana unafumbiwa macho na wanachama wa vyama hivyo
Hoja ikawa huwezi kulaumu CCM kwa uzembe uliotufikisha hapa ukatamani kuiondoa kwa kutumia taasisi dhaifu ulizoshindwa kujirekebisha, zilizoshindwa kuongoza umma
Hilo ni kukwepa jukumu ''kutafuta mchawi katika paa ukiacha majoka uvunguni''
Nafasi ya wananchi inaanzia katika vyama.
Midhali kuna 'watu hewa' kabla ya kushambulia wa CCM, fanya jambo na hewa ulio nao.
Wajibu wetu kama wananchi ni kuhakikisha tunajenga taasisi imara ili ziongoze kwa wakati, kutuheshimu na kujenga kuheshimiana
Ni kwa msingi huo nikasema Chadema kama chama kikuu cha upinzani kianze kujisafisha Wanachama wachukue hatua za dharura na za lazima dhidi ya viongozi wanaozembea
Hiyo ni sehemu ya nafasi ya majukumu ya wananchi yasohitaji subra wala ruhusua
Hatuishii hapo, ACT wazalendo,TPP n.k nao wajisafishe kama kuna matatizo ili tuwe na taasisi tofauti zikiwa na something in common, usafi na kuwajibika.
Tujenge utamaduni wa kuwajibisha wazembe
Tuliobaki tutimize wajibu kwa kushea tulicho nacho kidogo sana, hiyo ndiyo nafasi yetu
Katika kutimiza wajibu tusione haya, tusistahamiliane kinafiki, tusionee au kuonewa
Tuite kole kwa jina lake na si kijiko kikubwa.
Ninawanasihi wengine kusimama katika kujitambua, si siku ya uchaguzi, si kunyooshea kidole CCM bali kujitakasa huko CUF, Chadema, ACT na kwingineko kwanza
Nipo katika rekodi nikiudhi watu kwa ukweli kuwa kazi tuliyo nayo wananchi ni ngumu
Yaliyotokea Chadema wiki iliyokwisha, sisiti kusema siioni kesho ya matumaini
Ndio msingi wa kusema, ni wakati uongozi ukae pembeni kutoa fursa ya fikra mpya
Tusemezane