CHADEMA UK yazidi kuvurugika, M/kiti na Katibu vijana na Katibu muenezi waamua kumfuata Lukosi CCM

Kalenga-Iringa

JF-Expert Member
Nov 4, 2012
263
41
Kama ilivyotabiriwa Tsunami kubwa ya wafuasi wa chadema wameanza kuhamia CCM,
Leo hii tayari
mwenyekiti wa vijana
Katibu wa vijana
Katibu mwenezi
wote hawa wamechukizwa na siasa za kihuni za chadema za kufukuzana kama kuku na kuamua kumfuata kiongozi wao CHRIS LUKOSI CCM
Inasemekana kuwa wanachama wengi wamechukizwa sana na kitendo alichofanyiwa m,uasisi wao wa tawi la UK
Kma mnavyojua hakuna mwanaume alieweza kusimama na kusema anafungua tawi UK mpaka Lukosi alipofanya hivyo
Habari nyingi zinafuata kwani kwa taarifa zilizothibitishwa ni kuwa Lukosi atafanya press release jumamosi akiwa na kundi lake kubwa la wanachama na viongozi walioamua kurudi CCM.
wanachama+wapya+wakiwa+na+Makelele.JPG

ASILIMIA 75 YA UWAONAO HAPO JUU WAMELETWA NA LUKOSI CHADEMA
Mods hata mkifuta huu uzi haisaidii kwani tayari blogs zote zimepewa na zitaurusha usiku wa leo kwa hiyo ni bora muache tuu watu wasome, kufuta thread sio suluhisho. mbona ccm huwa inaumbuliwa hapa hamfutii?
 
Uko Uingereza kuna wachumia tumbo wengi sana,fanyeni kazi acheni ujinga.Kama ni siasa rudini numbani mkajenge nchi.Mna tabia za ukahaba wa kisiasa.Eti leo mko sijui chadema kesho ccm,halafu mnatujazia ***** wenu humu.Bakini na ujinga wenu huko huko uingereza.Kwanza ninavyofahamu mimi Uingereza ambapo nimeshawahi kuishi,huwa mna majungu sana na uswahili mwingi,kikawaida hampendani na watu mshachomeana sana.Sasa haya mambo ya chama ndiyo yameongezea tu,lakini ndivyo mlivyo.Mnaingia kwenye siasa kwa maslahi binafsi.Hovyo sana.Rudini nyumbani kama mnataka siasa.Huwezi kuwa nje ya nchi halafu bado ukawa na akili za kishibuda.Pambaff kabisa nyie.

Eti mmechukizwa na chadema,mlitegemea kupata nini chadema?Kama mlikuwa ccm,halafu mkaingia chadema,mmetumia umaarufu wa chama kupata umaarufu na sasa mnarudi kwenye matope yenu.Hamna misimamo,eti siasa za kihuni,ninyi ndo wahuni hamfai kabisa.
 
Kitu kinachomfanya mtu kuwa mwanachama wa chama fulani ni kule kuvutiwa na itikadi na sera za kile chama, bila kujali nani yumo ndani ya hicho chama. Hivyo basi kuondoka kwa mwanachama hakumfanyi mkereketwa wa chama husika naye kukihama. Kama atafanya hivyo, basi atakuwa amefuata tu mkumbo bila ya kuelewa malengo na nia ya chama kile kwa ujumla.
 
Kitu kinachomfanya mtu kuwa mwanachama wa chama fulani ni kule kuvutiwa na itikadi na sera za kile chama, bila kujali nani yumo ndani ya hicho chama. Hivyo basi kuondoka kwa mwanachama hakumfanyi mkereketwa wa chama husika naye kukihama. Kama atafanya hivyo, basi atakuwa amefuata tu mkumbo bila ya kuelewa malengo na nia ya chama kile kwa ujumla.
Wamefuata maslahi binafsi hakuna cha itikadi,maana ingekuwa hivyo wasingerudi ccm,bali wangebaki bila chama.Kama wanarudi ccm,waulize ni nini kimebadilika huko ccm ambacho kimewafanya waamuwe kurudi huko?Ndo akili za mbayu wayu hao.
 
Wamefuata maslahi binafsi hakuna cha itikadi,maana ingekuwa hivyowasingerudi ccm,bali wangeaki bila chama.Kama wanarudi ccm,waulize ni nini kimebadilika huko ccm ambacho kimewafanya waamuwe kurudi huko?Ndo akili za mbayu wayu hao.
Juzi juzi tu mlikua mnawaita makamanda na kuwamwagia sifa kibao leo wamekua hawafai. Siasa zitawashinda nyie.
 
Nirudie tu kwamba asilimia zaidi ya hamsini ya wapiga kura Tz siyo wanachama wa chama chochote cha siasa. Hawa ndiyo watakaoamua chama kipi kishike dola. Bahati nzuri wengi wa hili kundi ni understanding, hawayumbishwi na propaganda za vyama, ni Tanzania Kwanza.
 
Kitu kinachomfanya mtu kuwa mwanachama wa chama fulani ni kule kuvutiwa na itikadi na sera za kile chama, bila kujali nani yumo ndani ya hicho chama. Hivyo basi kuondoka kwa mwanachama hakumfanyi mkereketwa wa chama husika naye kukihama. Kama atafanya hivyo, basi atakuwa amefuata tu mkumbo bila ya kuelewa malengo na nia ya chama kile kwa ujumla.
Sasa ndio unajua kama watu wanafata mkumbo,endeleeni kujisifia watu wakija kwenye mikutano yenu.
 
Uko Uingereza kuna wachumia tumbo wengi sana,fanyeni kazi acheni ujinga.Kama ni siasa rudini numbani mkajenge nchi.Mna tabia za ukahaba wa kisiasa.Eti leo mko sijui chadema kesho ccm,halafu mnatujazia ***** wenu humu.Bakini na ujinga wenu huko huko uingereza.Kwanza ninavyofahamu mimi Uingereza ambapo nimeshawahi kuishi,huwa mna majungu sana na uswahili mwingi,kikawaida hampendani na watu mshachomeana sana.Sasa haya mambo ya chama ndiyo yameongezea tu,lakini ndivyo mlivyo.Mnaingia kwenye siasa kwa maslahi binafsi.Hovyo sana.Rudini nyumbani kama mnataka siasa.Huwezi kuwa nje ya nchi halafu bado ukawa na akili za kishibuda.Pambaff kabisa nyie.

Eti mmechukizwa na chadema,mlitegemea kupata nini chadema?Kama mlikuwa ccm,halafu mkaingia chadema,mmetumia umaarufu wa chama kupata umaarufu na sasa mnarudi kwenye matope yenu.Hamna misimamo,eti siasa za kihuni,ninyi ndo wahuni hamfai kabisa.

Ulikuwa wapi kuyasema haya yote wakati kina Chilisosi, wanafungua matawi ya Chadema Reading, Leicester, Milton Keynes, London.

Leo baada ya kuondoka ndio unaongea Chadema bana. Lema alipopiga picha na Chopa mliwasifia sana Chadema UK.
 
Last edited by a moderator:
kama ilivyotabiriwa tsunami kubwa ya wafuasi wa chadema wameanza kuhamia ccm,
leo hii tayari
mwenyekiti wa vijana
katibu wa vijana
katibu mwenezi
wote hawa wamechukizwa na siasa za kihuni za chadema za kufukuzana kama kuku na kuamua kumfuata kiongozi wao chris lukosi ccm
inasemekana kuwa wanachama wengi wamechukizwa sana na kitendo alichofanyiwa m,uasisi wao wa tawi la uk
kma mnavyojua hakuna mwanaume alieweza kusimama na kusema anafungua tawi uk mpaka lukosi alipofanya hivyo
habari nyingi zinafuata kwani kwa taarifa zilizothibitishwa ni kuwa lukosi atafanya press release jumamosi akiwa na kundi lake kubwa la wanachama na viongozi walioamua kurudi ccm.
wanachama+wapya+wakiwa+na+makelele.jpg

asilimia 75 ya uwaonao hapo juu wameletwa na lukosi chadema
mods hata mkifuta huu uzi haisaidii kwani tayari blogs zote zimepewa na zitaurusha usiku wa leo kwa hiyo ni bora muache tuu watu wasome, kufuta thread sio suluhisho. Mbona ccm huwa inaumbuliwa hapa hamfutii?

bwana lukosi,

kutumia id nyingi ni ujanja uliochakaa, kama kweli ulitaka kuhama, huna sababu ya kushinda kwenye mtambo kubuni majibu ionekane unaungwa mkono. Umefukuzwa njoo huku tujenge chama chetu cha mapinduzi.

Kajipange upya kaka, usipoteze muda wako.
 
Kwanza sioni umuhimu wa siasa za nje na kuna kipindi nilijiuliza sana kwa nini CCM na CDM vina concentrate kufanya siasa nje ya nchi hasa USA na UK????

Hawa jamaa wengi ni mamluki hivyo sitashangaa kama watatengeneza headline katika magazeti kwa ujira mdogo sana kama maskini wa kwetu kijijini.
 
Hawa hawana namna ni njaa zinawasumbua wameenda chadema kwa ajili ya mtu na mtu ameondoka nao wanaondoka
Nawasiwasi mambo ya visa nauli nje ya ccm vimewashinda kukabiliana na changamoto
chadema ni imani sio maigizo ya hawa maisha hapa yaliwashinda wakakimbilia kuwalamba wazungu miguu kama walisaliti tz sembuse chadema
 
Ulikuwa wapi kuyasema haya yote wakati kina Chilisosi, wanafungua matawi ya Chadema Reading, Leicester, Milton Keynes, London.

Leo baada ya kuondoka ndio unaongea Chadema bana. Lema alipopiga picha na Chopa mliwasifia sana Chadema UK.
Jiulize ni kwanini hawakufunguwa matawi ya ccm?

Ni hapo watu wanapotaka kufanya siasa kama mtaji wa biashara,waliona tayari ccm ni soko ambalo walishawahi wenzao(Kina Susan Mzee),wakaingia na gia ya kufunguwa matawi ya chadema(soko jipya),sasa kiumaarufu kidogo tu ndo haoo,wanajiona eti ni wanasiasa wa maana,dhumuni lao lilikuwa ni kupata attention kutoka ccm,hawana nia ya kukomboa nchi hao.

Huko ccm waliporudi hawatapata maslahi,kwasababu tayari kuna wenyewe,na wengine wanasubiria na wameshajipanga,hakuna lolote kama unaingia kwenye siasa kwa maslahi binafsi na akili fupi.Wasubiri wataona.Na wala mimi sijawahi kuwasifia hao chadema Uingereza,fuatilia wewe hujui kitu.Ulishawahi kuniona kwenye zile thread hata siku moja?
 
Kwanini hawkfunguwa matawi ya ccm?Ni hapo watu wanapotaka kufanya siasa kama mtaji wa biashara,waliona tayari ccm ni soko ambalo walishawahi wenzao(Kina Susan Mzee),wakaingia na gia ya kufunguwa matawi ya chadema(soko jipya),sasa kiumaarufu kidogo tu ndo haoo,wanajiona eti ni wanasiasa wa maana,dhmuni lao lilikuwa ni kuepwa attention na ccm,hawana nia ya kukomboa nchi hao.Huko ccm waliporudi hawatapata maslahi,kwasababu tayari kuna wenyewe,na wengine wanasubiria,hakuna lolote kam unaingia kwenye sias kwa masahi binafsi na akili fupi.Wasubiri wataona.Na wala mimi sijawahi kuwasifia hao chadema Uingereza,fuatilia wewe hujui kitu.
Leo unaturuka mkuu? hata wewe msee wangu?
 
Matawi na wanachama wote a CCM na CDM waste of time na kuendekeza njaa tu. Manake hata kupiga kura hampigi. BOKSI likizidi ndo wengine wanaona siasa ni short cut
 
Jiulize ni kwanini hawakufunguwa matawi ya ccm?

Ni hapo watu wanapotaka kufanya siasa kama mtaji wa biashara,waliona tayari ccm ni soko ambalo walishawahi wenzao(Kina Susan Mzee),wakaingia na gia ya kufunguwa matawi ya chadema(soko jipya),sasa kiumaarufu kidogo tu ndo haoo,wanajiona eti ni wanasiasa wa maana,dhumuni lao lilikuwa ni kupata attention kutoka ccm,hawana nia ya kukomboa nchi hao.

Huko ccm waliporudi hawatapata maslahi,kwasababu tayari kuna wenyewe,na wengine wanasubiria na wameshajipanga,hakuna lolote kama unaingia kwenye siasa kwa maslahi binafsi na akili fupi.Wasubiri wataona.Na wala mimi sijawahi kuwasifia hao chadema Uingereza,fuatilia wewe hujui kitu.Ulishawahi kuniona kwenye zile thread hata siku moja?
Mushi ndugu yangu utajitetea sana tu hapa,haya yote hukuyaona awali? Jamaa mlivyo kua mnawasifia leo hii wamekua hawafai?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom