johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,852
- 141,786
Kiukweli japokuwa Chadema inafutika taratibu katika ramani ya siasa za Tanzania, lakini wengi tutaikumbuka kwa michango binafsi ya wabunge wake ndani na nje ya binge. Pamoja na ukweli kwamba baadhi ya wabunge walikuwa na Dada au watalaka wao ndani ya chama lakini waliendelea kubakia makini na wazalendo katika majukumu yao ya kibunge.
Historia itawakumbuka Dr Slaa, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na JJ Mnyika kwa jinsi walivyoifanya CCM na serikali take visilale usingizi. Historia itamkumbuka pia mbunge Sugu kwa jinsi alivyobebwa mzobe mzobe na askari wa bunge wakati akimtetea KUB Mbowe asitolewe ukumbini.
Inawezekana kabisa 2020 Chadema ikakosa wawakilishi bungeni kama ilivyo sasa kwa Cuf Kule Zanzibar katika BLW, lakini tutawakumbuka kwa michango chanya kwa taifa hili hata kama CAG bado ana mashaka kwa namna mlivyokuwa mnaifisadi ruzuku.
Ahsanteni!
Historia itawakumbuka Dr Slaa, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na JJ Mnyika kwa jinsi walivyoifanya CCM na serikali take visilale usingizi. Historia itamkumbuka pia mbunge Sugu kwa jinsi alivyobebwa mzobe mzobe na askari wa bunge wakati akimtetea KUB Mbowe asitolewe ukumbini.
Inawezekana kabisa 2020 Chadema ikakosa wawakilishi bungeni kama ilivyo sasa kwa Cuf Kule Zanzibar katika BLW, lakini tutawakumbuka kwa michango chanya kwa taifa hili hata kama CAG bado ana mashaka kwa namna mlivyokuwa mnaifisadi ruzuku.
Ahsanteni!