Uchaguzi 2020 CHADEMA Tunduma: Wananchi wakimsindikiza Mwakajoka kuchukua fomu za Ubunge

Huwa tathimini yangu nilioipiga nimeona nikama mikoa ya mbeya songwe chadema niwengi kuliko mikoa mingine yote

Ni kweli kabisa Mbeya na Songwe ccm ilikufa zamani sana. Kwanza kunapakana na nchi ambazo zimekomaa kidemocrasia kama vile Malawi, Zambia na DRC
 
Yapo majinga mengi yalitia Nia ccm, na Pasco Mayala akiwemo, kwa kudhani kuw a CCM itawabeba kiulaini. lakini shughuli ya October hata kasimu majaliwa huenda asirudi bungeni
Ka-simu ameanza vituko vya kuteka watu!
 
Hivi hawa hawana habari za ndege kununua kwa cash? Hawajui SGR?
Mbona wako hivi hawa? Jee hawana habari za kuunga mkono juhudi kwa kina Nasari, Gekule, Silinde, na madiwani wengi tuu? Hata daraja la mfugale ambalo ni la aina yake barani Afrika?
Hawa ni wapiga dili
 
13 August 2020
Tunduma, Tanzania

UMATI WA WATU WAMPELEKA MWAKAJOKA KUCHUKUA FORM YA KUGOMBEA UBUNGE.


Source: DSS Tunduma

Tuliwaambia CCM Mpya wananchi wanataka sera bora zitakazowafanya wawe watu huru katika kujiletea Maendeleao ya Watu.

Mfano wa Maendeleo ya Watu kwa mtu huru ni serikali kuweka mazingira bora katika kilimo. Siyo wao wanalima Korosho kama watoto yatima halafu siku ya mavuno serikali inakuja kuyanyakuwa kwa mkopo wakati wamefanya kazi kwa bidii na jingi bila msaada wa Mkuu wa wilaya DC, RC, Waziri wa Kilimo, Ofisi ya Waziri Mkuu wala Ofisi ya Rais. Huo ni mfano mmoja wa unyanyasaji.

Wananchi wanaona unyanyasaji wa wazi kwa wabunge wao waliowatuma huko ndani ya Bunge na nje ya Bunge. Chaguzi ndogo kati ya 2015-2019 zilizofanyika kukuta Ofisi ya Mkurugenzi imefungwa! Mwaka 2019 November Uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijiji wagombea wa upinzani kunyimwa fomu au kuenguliwa kihuni wananchi waliona. Vyombo vya habari kutishwa kurusha habari za wapinzani...

Wananchi wanalipa kodi lakini viongozi wanasema wazi na kwa vitendo vya kibaguzi kuwa hawatapata barabara kwa vile wamechagua viongozi bora ambao wametokana na upande mbadala ambao licha ya kuwa unatambulikana kisheria kupitia katiba lakini wanaadhibiwa na CCM Mpya kwa kunyimwa huduma muhimu za Maendeleo ya Watu.

Sasa wananchi wameamua kusema basi!

Ushauri : Mgombea wa ccm Tunduma ajitoe .
 
Watu walikuwa wagonjwa,wanaugulia ndani ya nafsi zao. Tume isiingize siasa kupitisha wagombea;kusiwe na double standard,vinginevyo vichaa watakuwa wengi,,,sonona. Tunahitaji umoja wa kitaifa,hoja zitawale,hatutaki matusi
 
jiwe awaze mambo mengine ya maendeleo, aache kupoteza muda na pesa kujaribu kuua upinzani...haiwezekani watz wote KAMWE hatuwezi woote kuwa CCM, hata kama mabomba ya maji yangetoa maziwa nchi nzima!.
 
Hapo unakuta wanaopiga kura ni wachache tu
mkuu kuwa honest kwenye nafsi yako, hebu jiulize inawezekana vp pamoja na mazingira ya upinzani kubanwa sana awamu hii lakini kumbe bado wapo tu kwa wingi hivyo?!. na hapo hakuna cha wasanii wa muziki wala wananchi kusombwa kwa mabasi/malori!!.
 
Kati ya makosa makubwa CCM watajilaumu kumuacha akazuia Shughuli za Vyama vya siasa na kudhulumu uchaguzi wa Serikali za mitaaa mwaka jana ndio matokeo yake tunayaona leo
WANANCHI KOTE NCHINI BARA NA VISIWANI WAMEKUA NA SHAUKU KUBWA SANA YA KUWASIKILIZA WAPINZANI KINYUME KABISA NA MAWAZO KUWA WANGEKATA TAMAA

Kiukweli kupitia hili ccm wajifunze ;ingekua wapinzani wanapata muda wa kusema miaka mitaano hii bila kunyanyaswa leo hawangekua na la kuwaambia watu

Binadamu huna jipya la kuwafanyia au kuwapa ; WAPE KILA KITU ILA USIWANYIME MDOMO KUSEMA NA MASIKIO KUSIKIA ......Dola na Vyama vyenye Nguvu duniani zilifanya Maendeleo makubwa Lakini zilianguka kwa sababu tu waliziba watu midomo ...

Leo CCM haipo kwa watu kabisa zaidi ya kwenye Dola tena kwenye dola sio wote bali wale wenye mamlaka

Wanamikakati wa CCM wamempotosha Sana Mwenyekiti

Mwaka Huu ni maeneo machache Sana ccm inaweza kushinda kihalali Hii ni tofauti kabisa na miaka mitano nyuma Pamoja na kazi nzuri iliyofanywa

SEKRETARIET ya CCM imeuwa Chama kwenye mioyo ya watu !!!!!

Baada ya uchaguzi Huu lazima mabadiliko makubwa yafanyike kwenye sekretariet ya CCM ile ya kina Kinana na Nape was far better kwakua ilikua na approach ya kutumia siasa zaidi kuliko kutegemea kubebwa na Dola nzima .
 
Kati ya makosa makubwa CCM watajilaumu kumuacha akazuia Shughuli za Vyama vya siasa na kudhulumu uchaguzi wa Serikali za mitaaa mwaka jana ndio matokeo yake tunayaona leo
WANANCHI KOTE NCHINI BARA NA VISIWANI WAMEKUA NA SHAUKU KUBWA SANA YA KUWASIKILIZA WAPINZANI KINYUME KABISA NA MAWAZO KUWA WANGEKATA TAMAA

Kiukweli kupitia hili ccm wajifunze ;ingekua wapinzani wanapata muda wa kusema miaka mitaano hii bila kunyanyaswa leo hawangekua na la kuwaambia watu

Binadamu huna jipya la kuwafanyia au kuwapa ; WAPE KILA KITU ILA USIWANYIME MDOMO KUSEMA NA MASIKIO KUSIKIA ......Dola na Vyama vyenye Nguvu duniani zilifanya Maendeleo makubwa Lakini zilianguka kwa sababu tu waliziba watu midomo ...

Leo CCM haipo kwa watu kabisa zaidi ya kwenye Dola tena kwenye dola sio wote bali wale wenye mamlaka

Wanamikakati wa CCM wamempotosha Sana Mwenyekiti

Mwaka Huu ni maeneo machache Sana ccm inaweza kushinda kihalali Hii ni tofauti kabisa na miaka mitano nyuma Pamoja na kazi nzuri iliyofanywa

SEKRETARIET ya CCM imeuwa Chama kwenye mioyo ya watu !!!!!

Baada ya uchaguzi Huu lazima mabadiliko makubwa yafanyike kwenye sekretariet ya CCM ile ya kina Kinana na Nape was far better kwakua ilikua na approach ya kutumia siasa zaidi kuliko kutegemea kubebwa na Dola nzima .
Magufuli hakushauriwa na yeyote , aliamua mwenyewe binafsi kwa kudhani ana akili kuliko wengine , Sisi wengine tulijua kitakachotokea
 
Back
Top Bottom