CHADEMA, tumsamehe Zitto tusonge mbele; awe mtu asiye na madhara kama Shibuda!

Kasimba G

JF-Expert Member
Jan 19, 2011
3,428
2,609
Tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokuwa vikitokea kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yangu hata Zitto asamehewe hata kabla hajawaza wala kusema kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kuwa sidhani kama Zitto mwenyewe atakuwa tayari kuomba msamaha, Tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.
 
Nasema tumsamehe, tulikula naye nasema tumsamehe, Tumetoka naye Mbali nasema tumsamehe, Hiki ndo kipimo cha uungwana wetu nasema Tumsamehe, Chondechonde tusiwape faida wabaya wetu nasema tumsamehe, Hii ni kamba anavuta tunavuta matokeo yake itakatika, nasema tumsamehe.


Ndugu yangu Mbowe umemtoa Mbali kijana huyu, mwenyewe pia amesema hivyo mara kadhaa,naomba tumsamehe, nasema 7 mara 70 tumsamehe, chondechonde babangu mzee wangu Dk Slaa nasema ni mwenzetu tumsamehe,tukumbuke wema wake. Tuwaonee huruma watanzania walio jawa tumaini, uungwana ni vitendo nasema tumsamehe Mandela pamoja na kufungwa miaka 27 nakutemewa mate kwenye kikombe chake cha uji, na kila aina ya mabaya yasiyo stahiki kufanyiwa na binadamu lakini aliwasamehe Makaburu tena msamaha wa kweli. nasema Tumuenzi Mzee wetu Mandela kwa kwa kumsamehe Zitto.


Nasema tumsamehe pasipo masharti, pasipo kujali itikadi zetu , neno moja tu nasema tumsamehe, nasema tukimsamehe naamini aweza kuwa kiongozi mwema na muadilifu,mwaminifu na akawa mfano wa kuigwa. Wabaya wetu wanacheka wana furahi a tunavyo vuana nguo mitaani, wanacheka wanasema kimenuka, wabaya wetu sasa wamejazana baa wanakesha huku wakishikana mikono na kutosi wanasema safi sana.


Nasali usiku kucha nasema Mungu inusuru Chadema na watanzania, Mbowe tunatambuwa vyema mmewekeza nguvu,mali na kila namna ya kukijenga chama, lakini jambo kubwa nalo ni hili la watanzanini walio wekeza matumaini yao kuwa chadema ndo mkombozi, pia wako watanzania wanao amini kuwa Keki ya Taifa wataila kupitia Chadema, tuwaonee huruma. Asubuhi kunakucha naomba tuite vyombo vya habari tusiseme mengi bali neno moja tu kuwa tumemsamehe mwezetu tena kwa msamaha wa kweli, Watanzania watafurahi wakisikia tumemsamehe Mh Zitto.


Zitto si mwizi, si jambazi, si mkwapuaji,si kibaka nasema tumsamehe,tena pasipo kuhesebu makosa yake wala umri wa makosa yake, ni mwanzetu ni kijana wetu amejikwaa, alilpotea, tumrudishe kundini tena tumwandalie Karamu tule naye tunywe naye tumkumbatie tena hadhara, wabaya wetu waone kuwa tumemsamehe mwenzetu na tunampenda. Mh Tundu Lissu na Mh Myika na wengine wote nasema Tumsamehe kwa moyo wa dhati tuweke masilahi ya taifa mbele.
Hakika watanzania wenye mapenzi mema na Chama hata wasio wanachama watafurahi kusikia au kuona tukimsamehe mwenzetu, yatupasa kuamini kuwa naye ni binadamu anastahiki kusamehewa, katu hatutolaumiwa kwa msamaha huu kwa mwenzetu. Chonde chonde, kazi iliyofanyika kuijenga chadema nikubwa kuliko, ya kutaka kuibomoa inayofanyika sasa.

Mwisho kabisa naomba namba ya ndgu Mh Mbowe na Mh Mzee wetu Dk Slaa ninalo neno la kuwaambia.
Napatikana kwa namba hii. 0773 944 944


NB
Namalizia kwa kusema katika kutatua tatizo unaweza kusababisha tatizo lingine likawa kubwa kuliko la awali, lakini pia tukumbuke katika nia njema kabisa ya kutenda mema makosa yanaweza kufanyika, tutangulize umakini katika utatuzi wa jambo hili, lakini pia tutangulize umakini ktika ujenzi wa taifa letu.
Mungu Tubariki sote
 
kama kakutuma mwambie asiwe na shaka PIA anastahili kusamehewa baada ya kufanya yafuatayo BILA KUSITA NA KWA NIA YA DHATI YA MOYO WAKE...

Naamini huko aliko hana furaha hata kidogo na anajutia nafsi yake hasa anapokuwa peke yake. Nashauri afanye haya ili apate msamaha wa kweli toka kwa wazee wake walomlea na kumkuza kisiasa sasa anataka kuchana mbeleko..asipokuwa makini RADHI ya mzazi inamuandama muda si mrefu.

1- Aombe yeye mwenyewe msamaha kwa kauli yake na mbele ya vyombo vya habari na kina shonza wasihusike na uitishwaji wa mkutano huo
2- Ataje na kuyajutia makosa yoote anayoamini anahitaji kusamehewa kwakuwa aliyatenda
3- Ataje waliomshawishi na kwa gharama kiasi gani na pia mwa manufaa ya nani alikubali kuyafanya hayo yoote ambayo kwayo anajutia na anaomba msamaha wa dhati

Tunajuwa kuwa mtoto akinyea mkono wa mama sio kuwa unakatwa na kutupwa bali husafishwa na mtoto pia husafishwa..ila mtu mzima anaponyea mkono wa mzazi wake hana budi kupewa adhabu kali ili watoto wakikuwa wasijekufanya kama hayo aliyoyafanya yule mkubwa.

SASA ZZK AAMUE KUWA MTOTO WATU WASAFISHE MKONO NAYE PIA ASAFISHWE AU AENDELEE KUWA MTU MZIMA APATE RUNGU LA ADHABU.

NI AYO TUUU.
 
kama kakutuma mwambie asiwe na shaka PIA anastahili kusamehewa baada ya kufanya yafuatayo BILA KUSITA NA KWA NIA YA DHATI YA MOYO WAKE...

Naamini huko aliko hana furaha hata kidogo na anajutia nafsi yake hasa anapokuwa peke yake. Nashauri afanye haya ili apate msamaha wa kweli toka kwa wazee wake walomlea na kumkuza kisiasa sasa anataka kuchana mbeleko..asipokuwa makini RADHI ya mzazi inamuandama muda si mrefu.

1- Aombe yeye mwenyewe msamaha kwa kauli yake na mbele ya vyombo vya habari na kina shonza wasihusike na uitishwaji wa mkutano huo
2- Ataje na kuyajutia makosa yoote anayoamini anahitaji kusamehewa kwakuwa aliyatenda
3- Ataje waliomshawishi na kwa gharama kiasi gani na pia mwa manufaa ya nani alikubali kuyafanya hayo yoote ambayo kwayo anajutia na anaomba msamaha wa dhati

Tunajuwa kuwa mtoto akinyea mkono wa mama sio kuwa unakatwa na kutupwa bali husafishwa na mtoto pia husafishwa..ila mtu mzima anaponyea mkono wa mzazi wake hana budi kupewa adhabu kali ili watoto wakikuwa wasijekufanya kama hayo aliyoyafanya yule mkubwa.

SASA ZZK AAMUE KUWA MTOTO WATU WASAFISHE MKONO NAYE PIA ASAFISHWE AU AENDELEE KUWA MTU MZIMA APATE RUNGU LA ADHABU.

NI AYO TUUU.

Mkuu hayo masharti ni magumu, mbona Shibuda huwa tunamsamehe kabla hata hajasema wala kufanya chochote? Mie naona Zitto nae apewe nafasi kama ya Shibuda, awe anasamehewa kabla ya kusema wala kufanya chochote kwa afya ya chama, sio kwamba anaweza kuleta madhala lakini tumsamehe!

Mbona Mungu mwenyewe huwa anatusamehe, na sisi tuonyeshe upevu, tumsameha, najua atakuwa ameishaaanza kuelewa anavyotakiwa kuwa!
 
'Kumsamehe' Zitto ni kuhatarisha Nafasi ya Mbowe kwenye Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema hapo June 2014.
 
'Kumsamehe' Zitto ni kuhatarisha Nafasi ya Mbowe kwenye Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema hapo June 2014.

According to you? Labda mje mpige kura nyie maCCM! Zitto kwa sasa kesha jiharibia saana
 
mkuu hayo masharti ni magumu, mbona shibuda huwa tunamsamehe kabla hata hajasema wala kufanya chochote? Mie naona zitto nae apewe nafasi kama ya shibuda, awe anasamehewa kabla ya kusema wala kufanya chochote kwa afya ya chama, sio kwamba anaweza kuleta madhala lakini tumsamehe!

Mbona mungu mwenyewe huwa anatusamehe, na sisi tuonyeshe upevu, tumsameha, najua atakuwa ameishaaanza kuelewa anavyotakiwa kuwa!

mkuu sijaona sharti lolote gumu kwa ndugu zzk...huwezi kumsamehe mtu kosa asilolijuwa..na pia kukiri kuwa kakosea na kuahidi kutorudia makosa.

Mfano wa john ccm shibuda ni case tofauti kabsaaa na kijana zzk..john ni mtoto wa jirani alikuja kuomba kuishi kwetu pia tunaamini alitumwa aje kuishi kwetu ili tukimkataa jirani apate la kutusemea duniani...sie wabaguzi mara chama cha wachaga..ila zzk ni mwanetu wa damu ni wajibu wa mzazi kumlea na kumrejesha kwenye mstari kila anapoonekana kukosea na hasa anapotambua kuwa kakosea....

John ccm shibuda ni sawa na mtu mwenye shari na hila kwa hiyo tunamwangalia afanye afanyavyo ila hatutomgusa wala kumsemesha na ndio maana hutokaa usikie shibuda kupewa hata ujumbe wa nyumba 5 za chadema...

Ila kumbuka zzk ni naibu katibu mkuu...nchi kama china kwa haya anayoshutumiwa kuyafanya alikuwa keshanyongwa zamaniiii...imeandikwa kwenye maandiko "musizifanye shingo zenu ngumu........toba ya kweli huendana na majuto ya moyoni ya mkosefu na msamaha utolewao huwa ni wa kweli na dhahiri.

Mwambie kijana afanye toba ya kweli ili apate msamaha wa kweli.
 
mkuu sijaona sharti lolote gumu kwa ndugu zzk...huwezi kumsamehe mtu kosa asilolijuwa..na pia kukiri kuwa kakosea na kuahidi kutorudia makosa.

Mfano wa john ccm shibuda ni case tofauti kabsaaa na kijana zzk..john ni mtoto wa jirani alikuja kuomba kuishi kwetu pia tunaamini alitumwa aje kuishi kwetu ili tukimkataa jirani apate la kutusemea duniani...sie wabaguzi mara chama cha wachaga..ila zzk ni mwanetu wa damu ni wajibu wa mzazi kumlea na kumrejesha kwenye mstari kila anapoonekana kukosea na hasa anapotambua kuwa kakosea....

John ccm shibuda ni sawa na mtu mwenye shari na hila kwa hiyo tunamwangalia afanye afanyavyo ila hatutomgusa wala kumsemesha na ndio maana hutokaa usikie shibuda kupewa hata ujumbe wa nyumba 5 za chadema...

Ila kumbuka zzk ni naibu katibu mkuu...nchi kama china kwa haya anayoshutumiwa kuyafanya alikuwa keshanyongwa zamaniiii...imeandikwa kwenye maandiko "musizifanye shingo zenu ngumu........toba ya kweli huendana na majuto ya moyoni ya mkosefu na msamaha utolewao huwa ni wa kweli na dhahiri.

Mwambie kijana afanye toba ya kweli ili apate msamaha wa kweli.

Sasa mtoto wa ndani amekuwa na dalili za mtoto haramu unafanyaje? Tufanye kama hatujui tumsamehe na tujue na yeye ni kama wa nyumba ya jirani mkuu!
 
tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokkuwa vikitoke kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema kitu wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yagu naona hata zitto asamehewe hata kabla hajawaza kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kauwa sidhani kama atakuwa tayari kuomba msamaha, tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.

nini makosa ya zitto kati ya haya?

1.kuhoji matumizi ya ruzuku ya chama?
2.kuhoji kuhusu ukaguzi wa ruzuku?
3.kukataa posho?
4.kutaka kugombea uenyekiti?
5.kuto watonya?
6.kuandaliwa na wakina kitila kuwa kiongozi kama mtei alivyo kuwa ana muandaa arfi?
 
nini makosa ya zitto kati ya haya?

1.kuhoji matumizi ya ruzuku ya chama?
2.kuhoji kuhusu ukaguzi wa ruzuku?
3.kukataa posho?
4.kutaka kugombea uenyekiti?
5.kuto watonya?
6.kuandaliwa na wakina kitila kuwa kiongozi kama mtei alivyo kuwa ana muandaa arfi?

Wewe kuna vitu huelewi na havijawekwa wazi kwa manufaa ya chama, usiwe mshabiki kipofu kama hivyo!

1. Kuchukua hela toka kwa mahasimu
2. Kuwa na mashabiki wa kutoka yanga wakati wewe uko simba
3. Kuandaliwa vikao na viongozi wa Yanga wakati wewe uko simba
4. Kuchukua vijisenti toka taasisi ambazo inabidi uzisimamie n.k
 
Unawezaje kumsamehe mtu anayetoboa jahazi ambalo wote mnasafiria katikati ya bahari yenye masavimbi na manchemba...

Zitto has to go. Nobody is bigger than CHADEMA
 
Tumekuwa na mihemko na hasira muda mrefu na vitu vilivyokkuwa vikitoke kwenye chama chetu, sasa naona ni muda muafaka kumsamehe huyu bwana na tusonge mbele. Shibuda huwa tunakuwa tumemsamehe kabla hata hajasema kitu wala hajafanya kitu, mimi kwa mapendekezo yagu naona hata Zitto asamehewe hata kabla hajawaza kitu!

Tumsamehe tuu pamoja na kauwa sidhani kama atakuwa tayari kuomba msamaha, Tumsamehe na tujenge chama kwa upya kwa spidi isiyo ya kawaida.

Kwani amefanya kosa gani?si nyie mlisema kaonewa?utamsamehe vipi mtu ambaye hajakukosea?kiiimyaaa!!
 
Unawezaje kumsamehe mtu anayetoboa jahazi ambalo wote mnasafiria katikati ya bahari yenye masavimbi na manchemba...

Zitto has to go. Nobody is bigger than CHADEMA

Mkuu tunamnyang'anya bisibisi zoote alizokuwa anatumia kutoboa boti, akitaka labda atoboe kwa makucha yake jambo ambalo hataliweza
 
Kwani amefanya kosa gani?si nyie mlisema kaonewa?utamsamehe vipi mtu ambaye hajakukosea?kiiimyaaa!!

Mke akiwa na tabia ya kujikojolea kitandani huwa hatutangazi, sisi tunajua kosa lake wewe wa CCM huwezi kujua na hatutakuambia!
 
Unawezaje kumsamehe mtu anayetoboa jahazi ambalo wote mnasafiria katikati ya bahari yenye masavimbi na manchemba...

Zitto has to go. Nobody is bigger than CHADEMA

Nope mkuu, we need to carry each others burdens sometimes! We forgive him, but set him pending so that he can realize what he has done! it will be a big lesson for the rest of us!
 
Nope mkuu, we need to carry each others burdens sometimes! We forgive him, but set him pending so that he can realize what he has done! it will be a big lesson for the rest of us!
Mkuu mtu kama anatoboa jahazi mnalosafiria maana yake ni kuwa wote mnazama maji yakianza kuingia. Toka enzi na enzi soma stori zote za wavuvi, mtu anayetoboa jahazi mnalosafiria dawa huwa inakuwa ni moja tu, KUTOSWA...
 
Back
Top Bottom