EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
SIKU moja baada ya kuwepo taarifa kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, anahaha kutafuta suluhu baina yake na mbunge wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere, kwa familia ya Mwalimu Julius Nyerere, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kiongozi huyo anapaswa kurudi Arumeru Mashariki na kuomba radhi mbele ya wananchi kwa uongo aliousema.
Kutokana na tuhuma hizo, CHADEMA kimewataka wakazi wa Arumeru na Watanzania kwa ujumla kuwa makini na CCM, kwani kimekuwa kikitumia mbinu zisizo halali kuendelea kutawala ikiwemo kuwarubuni, kulaghai na kusema uongo.
Akizungumza na waandishi wa habari na baadhi ya wananchi wa Arumeru jana, meneja kampeni wa CHADEMA, Mchungaji Israel Natse, alisema kuwa kama kweli Mkapa anataka kujisafisha kwa uongo aliosema mbele ya wananchi, dawa pekee inayoweza kumsaidia ni kurudi na kuwaomba radhi.
Unajua tunapowaambia wananchi kuwa wawe makini na CCM na viongozi wake mifano sahihi ndiyo hii kama mwenyekiti mstaafu anaweza kusema uongo kama huo mbele za watu sasa itakuwaje kwa watendaji wa chini yake, itakuwaje kwa wanachama wa kawaida, chama hiki kimefika mwisho, hakiwezi tena kusimama mbele ya wananchi na hapa Arumeru itakuwa ni moja ya fundisho kuwa zama zao, alisema.
Naye Vicent Nyerere amemtaka Mkapa akamwonyeshe ukoo alikozaliwa baada ya kuutangazia umma kuwa hatoki katika familia ya Mwalimu Nyerere.
Unajua mimi nashangaa kwa mtu mzima kusema uongo mbele ya wananchi, tena kiongozi anayepaswa kuaminiwa na watu anaowaongoza. Alipofariki baba yangu ambaye alikuwa rafiki yake na Mkapa pia, alikuja nyumbani kwetu kwenye msiba hata rambirambi alinikabidhi mimi.
Sasa kwa kuwa kasema mimi si familia ya Nyerere, anipeleke huko kwenye hiyo familia nyingine, alisema Nyerere.
Kutokana na tuhuma hizo, CHADEMA kimewataka wakazi wa Arumeru na Watanzania kwa ujumla kuwa makini na CCM, kwani kimekuwa kikitumia mbinu zisizo halali kuendelea kutawala ikiwemo kuwarubuni, kulaghai na kusema uongo.
Akizungumza na waandishi wa habari na baadhi ya wananchi wa Arumeru jana, meneja kampeni wa CHADEMA, Mchungaji Israel Natse, alisema kuwa kama kweli Mkapa anataka kujisafisha kwa uongo aliosema mbele ya wananchi, dawa pekee inayoweza kumsaidia ni kurudi na kuwaomba radhi.
Unajua tunapowaambia wananchi kuwa wawe makini na CCM na viongozi wake mifano sahihi ndiyo hii kama mwenyekiti mstaafu anaweza kusema uongo kama huo mbele za watu sasa itakuwaje kwa watendaji wa chini yake, itakuwaje kwa wanachama wa kawaida, chama hiki kimefika mwisho, hakiwezi tena kusimama mbele ya wananchi na hapa Arumeru itakuwa ni moja ya fundisho kuwa zama zao, alisema.
Naye Vicent Nyerere amemtaka Mkapa akamwonyeshe ukoo alikozaliwa baada ya kuutangazia umma kuwa hatoki katika familia ya Mwalimu Nyerere.
Unajua mimi nashangaa kwa mtu mzima kusema uongo mbele ya wananchi, tena kiongozi anayepaswa kuaminiwa na watu anaowaongoza. Alipofariki baba yangu ambaye alikuwa rafiki yake na Mkapa pia, alikuja nyumbani kwetu kwenye msiba hata rambirambi alinikabidhi mimi.
Sasa kwa kuwa kasema mimi si familia ya Nyerere, anipeleke huko kwenye hiyo familia nyingine, alisema Nyerere.