Elections 2010 CHADEMA: Serikali ilaani vurugu Ivory Coast

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,172
CHADEMA: Serikali ilaani vurugu Ivory Coast


na Juma Kasesa


amka2.gif
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka serikali kulaani hadharani matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya demokrasia ya kimataifa unaofanywa na Rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na wafuasi wake nchini humo.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya chama hicho ilisema, Rais Jakaya Kikwete anatakiwa kutamka hadharani kumtambua Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo na kulaani vitendo vinavyofanywa na Gbagbo na wafuasi wake.
“Inashangaza kwamba wakati Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU) na serikali za nchi mbalimbali ndani na nje ya Afrika zimetoa matamko ya wazi serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya diplomasia ya kimya.
“Hii ni tofauti kabisa na wakati Mwalimu Nyerere ambapo Tanzania ilikuwa mstari wa mbele na kutoa misimamo ya wazi ya kukemea vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza CHADEMA inatambua kwamba Rais Kikwete alizungumzia kidogo matatizo ya Ivory Coast wakati akihutubia Mkutano wa Kimataifa wa Amani katika eneo la Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika hivi karibuni nchini Zambia.
Katika mkutano huo Rais Kikwete alieleza kwamba suala la Ivory Coast linashughulikiwa na mikono salama na akaonyesha matumaini yake kwamba pande mbili zenye mgogoro zitafikia makubaliano.
“Kauli hii ya Rais Kikwete inalea vitendo vya ukiukwaji wa misingi ya demokrasia vinavyofanywa na Laurent Gbagbo na wafuasi wake kwa kuwa inatoa fursa kwa mgombea ambaye taasisi zote huru zimetamka kuwa ameshindwa katika uchaguzi kuanza majadiliano na aliyeshinda badala ya kumpisha katika uongozi wa nchi,” ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilisema serikali ya Tanzania inatakiwa kueleza msimamo wake kwa uwazi, ili kuondoa mashaka kwamba ukimya wake unatokana na Rais Kikwete kukosa uhalali wa kimaadili wa kukemea vitendo vya ukiukwaji wa demokrasia na mchakato wa uchaguzi uliomuingiza madarakani kuhojiwa kutokana na tuhuma za matokeo ‘kuchakachuliwa’ katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
 
Safi sana hii, anaogopa ile verse ya kitabu kitakatifu inayosema kabla ya kutoa kibanzi kwenye jicho la mwenzio kwanza uondoe boriti kwenye jicho lako. Raisi anayeongoza taifa kwa hila katika chaguzi hawezi kukemea mwenzie. Nini kilichotokea haoa Tanzania kwani kinacholeta tofauti na Ivory Cost kwani, wabunge wangapi wameibiwa kura mchana kweupe kwa nguvu? Ole wao wafanyao haya, mwisho wao utakuwa wa kusaga meno
 
Safi sana hii, anaogopa ile verse ya kitabu kitakatifu inayosema kabla ya kutoa kibanzi kwenye jicho la mwenzio kwanza uondoe boriti kwenye jicho lako. Raisi anayeongoza taifa kwa hila katika chaguzi hawezi kukemea mwenzie. Nini kilichotokea haoa Tanzania kwani kinacholeta tofauti na Ivory Cost kwani, wabunge wangapi wameibiwa kura mchana kweupe kwa nguvu? Ole wao wafanyao haya, mwisho wao utakuwa wa kusaga meno

He doesnt have moral authority to do that.
 
CHADEMA: Serikali ilaani vurugu Ivory Coast


na Juma Kasesa


amka2.gif
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka serikali kulaani hadharani matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya demokrasia ya kimataifa unaofanywa na Rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na wafuasi wake nchini humo.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya chama hicho ilisema, Rais Jakaya Kikwete anatakiwa kutamka hadharani kumtambua Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo na kulaani vitendo vinavyofanywa na Gbagbo na wafuasi wake.
“Inashangaza kwamba wakati Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU) na serikali za nchi mbalimbali ndani na nje ya Afrika zimetoa matamko ya wazi serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya diplomasia ya kimya.
“Hii ni tofauti kabisa na wakati Mwalimu Nyerere ambapo Tanzania ilikuwa mstari wa mbele na kutoa misimamo ya wazi ya kukemea vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza CHADEMA inatambua kwamba Rais Kikwete alizungumzia kidogo matatizo ya Ivory Coast wakati akihutubia Mkutano wa Kimataifa wa Amani katika eneo la Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika hivi karibuni nchini Zambia.
Katika mkutano huo Rais Kikwete alieleza kwamba suala la Ivory Coast linashughulikiwa na mikono salama na akaonyesha matumaini yake kwamba pande mbili zenye mgogoro zitafikia makubaliano.
“Kauli hii ya Rais Kikwete inalea vitendo vya ukiukwaji wa misingi ya demokrasia vinavyofanywa na Laurent Gbagbo na wafuasi wake kwa kuwa inatoa fursa kwa mgombea ambaye taasisi zote huru zimetamka kuwa ameshindwa katika uchaguzi kuanza majadiliano na aliyeshinda badala ya kumpisha katika uongozi wa nchi,” ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilisema serikali ya Tanzania inatakiwa kueleza msimamo wake kwa uwazi, ili kuondoa mashaka kwamba ukimya wake unatokana na Rais Kikwete kukosa uhalali wa kimaadili wa kukemea vitendo vya ukiukwaji wa demokrasia na mchakato wa uchaguzi uliomuingiza madarakani kuhojiwa kutokana na tuhuma za matokeo ‘kuchakachuliwa’ katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Hiki ni bonge la kitanzi watajioondoaje,shingo imebana
 
JK hawezi kutoa tamko la namna hiyo bila ya kujiuma midomo, kwani hadi sasa chama chake kinaendeleza unporaji, au tuseme unyang'anyi wa halmashauri mbali mbali hapa nchini. Labda akishamaliza shughuli hiyo ndiyo atatamka.
 
Kiranja mkuu hana amani moyoni. Anajua mwenzie akinyolewa,tia maji kichwani. Siku ya uhuru akatoroka na hotuba kwenye mfuko wa koti itakuwa vp atoe tamko zito kama ilo. Hana ujanja!
 
Hata weza kutamka lolote maana anajua kuwa atapa kigugumizi hasa kuhusiana na uporaji wa halmashauri unaofanywa na chama chake rejea uchaguzi wa mayor wa Arusha na Mwanza.

Hii inaonyehsa kukosa ujasiri wa kukemea maswala ambayo chama chake nacho kimefauta mkondo huohuo.
 
He doesnt have moral authority to do that.

Kwa kweli ni ndoto kali sana. Ila kwa unafiki wa viongozi wetu their do not have such a thing called moral authority. They are typical immoral and out of their upuuzi utasikia wanalaani wakati na wao wamepitia mlango huo huo.
 
Laurent Gbagbo na Jakaya Kikwete ni sawa na idential twins!!wote ni wezi wa kura na wizi wao unafanana!!
 
Hivi CHADEMA mnaitambua serikali ya Jakaya Kikwete ? Nawashangaa sana kwa ombi hili zidi ya serikali ya Mheshimiwa Jakaya. Inaelekea kabisa hamjui mtendalo.
 
CHADEMA: Serikali ilaani vurugu Ivory Coast


na Juma Kasesa


amka2.gif
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka serikali kulaani hadharani matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya demokrasia ya kimataifa unaofanywa na Rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na wafuasi wake nchini humo.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya chama hicho ilisema, Rais Jakaya Kikwete anatakiwa kutamka hadharani kumtambua Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo na kulaani vitendo vinavyofanywa na Gbagbo na wafuasi wake.
"Inashangaza kwamba wakati Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU) na serikali za nchi mbalimbali ndani na nje ya Afrika zimetoa matamko ya wazi serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya diplomasia ya kimya.
"Hii ni tofauti kabisa na wakati Mwalimu Nyerere ambapo Tanzania ilikuwa mstari wa mbele na kutoa misimamo ya wazi ya kukemea vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza CHADEMA inatambua kwamba Rais Kikwete alizungumzia kidogo matatizo ya Ivory Coast wakati akihutubia Mkutano wa Kimataifa wa Amani katika eneo la Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika hivi karibuni nchini Zambia.
Katika mkutano huo Rais Kikwete alieleza kwamba suala la Ivory Coast linashughulikiwa na mikono salama na akaonyesha matumaini yake kwamba pande mbili zenye mgogoro zitafikia makubaliano.
"Kauli hii ya Rais Kikwete inalea vitendo vya ukiukwaji wa misingi ya demokrasia vinavyofanywa na Laurent Gbagbo na wafuasi wake kwa kuwa inatoa fursa kwa mgombea ambaye taasisi zote huru zimetamka kuwa ameshindwa katika uchaguzi kuanza majadiliano na aliyeshinda badala ya kumpisha katika uongozi wa nchi," ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, taarifa hiyo ilisema serikali ya Tanzania inatakiwa kueleza msimamo wake kwa uwazi, ili kuondoa mashaka kwamba ukimya wake unatokana na Rais Kikwete kukosa uhalali wa kimaadili wa kukemea vitendo vya ukiukwaji wa demokrasia na mchakato wa uchaguzi uliomuingiza madarakani kuhojiwa kutokana na tuhuma za matokeo ‘kuchakachuliwa' katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Mh! Akitamta lolote kuhusu Ivory coast nitaamini kuwa nyani haoni kundule! Achilia mbali ya uchaguzi mkuu ulopita lakini hili la Arusha litamsuta.
 
Si Tunaona Jinsi Gani Tanzania Inashindwa Kujihusisha na Maswala ya Afrika? JK Anaweza Kumwambia Dikteta Gbagbo Chochote? Alichokifanya Huyu Gbagbo Si Ndicho Kikwete Kafanya? Utakuwa Ujinga na Mimi Namshauri JK Akae Kimya Kama Anavyofanya It's Good Strategy. Hata Mugabe, Museven, Kibaki, Mubarak Tunawaona Wapo Kimya Wanajua Wanachokifanya Nchini Kwao. JK Amechukua Exactly Playbook ya Gbagbo na Mugabe Kuongoza Tanzania na Sita Shangaa JK Anawasiliana na Mugabe kwa Simu Kila Siku. Mpaka Leo Zimbabwe Hawana Katiba na Tanzania CCM Wanasema Hawataki Katiba, Imetoka Wapi?
 
...we kilaza mwiba kunywa maziwa fasta utapike hiyo sumu inayokuua ya propaganda za magazeti ya RA na Uhuru et al kwamba CDM hawamtambui Rais wa JMT!!!! Rais anatambulika kisheria lakini mchakato uliomuweka madarakani unatufanya tumuone illigitimate Presidaa. Kwanza JK akemee kitendo cha kumwaga damu ya Hon. G. Lema na kupora halmashauri ya arusha mjini.
 
Back
Top Bottom