Tawi la chadema SAUT limejipanga kutumika kama kichaka cha kuficha aibu, ufisadi na uchu wa madaraka wa Mwenyekiti wa chadema taifa Nd. Freeman Mbowe. Matumizi ya tawi hili yamekuja siku chache baada ya tamko lililotolewa na mwenyekiti wa matawi ya Chadema Mwanza Mh. Gwanchele, tamko anbalo lilikemea ufisadi na uchu wa madaraka ndani ya chama ambapo tamko liliwataja Mbowe na Slaa kama vinara wa ufisadi huo wa chama na kuwataka wasikanyage mwanza kama hawapo tayari kujihuzuru na kupisha uchunguzi wa matumizi ya pesa za chama. Pia tamko la mwenyekiti wa matawi lilipinga maamuzi ya kamati kuu kuhusu kuwavua uongozi kinyume cha katiba: Kitila mkumbo, Mwigamba na Zitto Kabwe.
KWANINI MBOWE KAKIMBILIA CHADEMA SAUT
Mbowe ameona aitumie chadema SAUT kama kichaka chake cha kujifichia kwasababu ameshaona kuwa wananchi na wanachama wa chadema wameshagundua ufisadi unaoendelea katika chama, kwakuwa Mbowe anaamini kuwa wananchi huamini wasomi ndio maana mbowe ameamua kuwatumia viongozi wa chadema SAUT na hili limewezekana kwasababu tu mwenyekiti wa Chadema SAUT ni mchaga ambaye anaamini kuwa chadema si chama cha siasa balini CHAGA DEVELOPMENT MACHAME. Tayari wanafunzi wa vyuo vikuu wanaojitambua walishatoa tamko la kukataa ufisadi wa mbowe na kupinga maamuzi ya kamati kuu kuwafukuza watu kwa maslahi binafsi tamko ambalo lilitolewa na viongozi wa wanachama wa chadema vyuo vikuu (CHASO).
UTOFAUTI WA CHADEMA SAUT NA CHADEMA VYUO VIKUU VINGINE
- Chadema SAUT ni tawi pekee linalounga mkono hatua ya Mbowe kunyofoa kinyemela kifungu cha ukomo wa uongozi wa chama kwenye katiba chadema.
- Chadeama SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa mtu anayekosoa maovu yanayotendeka kwenye chama anatumiwa na ccm.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa ili ufike mbali kwenye chadema ni lazima unyenyekee na ujipendekeze kwa viongozi.
- Chadema SAUT ni tawi pekee lenye washabiki na wafuasi wengi wa Mbowe kuliko wanachama hai wa chadema.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa chadema haiwezi kuwepo bila mbowe kutokana na ukabila wa mweyekiti wake.
- Chadeama SAUT ni tawi pekee linalounga mkono Ruzuku ya chama kutumika makao makuu tu.
- Chadema SAUT ni tawi linaloongoza kwa usahaulifu kwani mara zote limekuwa likiheshimiwa na kutembelewa na viongozi pale tu wanapokuwa na shida zao binafsi au linapowataka wanafunzi hao kwenda kusimamia kura.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini chadema itashinda kwa upepo tu.
NAMNA CHADEMA SAUT INAVYOTUMIKA
· December 8 Viongozi wa Chadema SAUT walihongwa pesa na timu ya Mbowe ili waite vyombo vya habari (Press conference) na kuutangazia umma kuhusu ziara ya mbowe Mwanza, pia waliagizwa kumpiga mkwara Mwenyekiti wa matawi ya chadema Mwanza Ngd Gwanchele kwa kumtishia kumshitaki, pia waliambiwa wasema kuwa watu wa mwanza wapo tayari kumpokea mbowe, wanaunga mkono maamuzi ya kamati kuu na kwamba watu hawataandamana kumpimga mbowe kama matamko yanavyosema. Hili lilifanyika na habari hii ilitangazwa kwenye vyombo vya habari ikiwemo Channel 10 habari Tarehe 9/12.2013 saa 1 na dk 3 usiku. Umeona wapi ziara ya kimkoa kwenye mkoa fulani ikitangazwa na viongozi wa tawi?
· Viongozi wa Chadema SAUT wahongwa pesa za kuandaa mkutano wa kumsafisha Mbowe atakapokuja Mwanza. Mkutano huo utafanyika jumamosi tarehe 15/12.2013 ambapo mbowe atakuwepo mkutanoni. Katika mkutano huo viongozi wa chadema SAUT watatakiwa kutoa tamko la kumuunga mkono mbowe na maamuzi yake pia kupinga tamko la kiongozi wa umoja wa matawi ya chadema Mwanza. Viongozi wa chadema SAUT watatakiwa kuwathibitishia wananchi imani yao kwa chama na pia kuunga mkono maamuzi yote ambayo yamefanywa na chama.
· Viongozi wa chadema SAUT wameahidiwa donge nono ikiwa watafanikiwa kumlinda mbowe asianikwe, kuchafuliwa na kuzomewa katika ziara yake ya Mwanza kama inavyotokea kwa Dr. Slaa huko Kigoma. Tayari viongozi wa Chadema SAUT wameshaandaa watu wa kumshangilia mbowe kwenye mkutano washangiliaji ambao watashangilia kila kitakachosemwa na mbowe hata kama hakina mantiki.
Ikumbukwe kuwa ni Chadema SAUT iliyopewa pesa ya kulipa vyombo vya habari tarehe 28/11/2013 ili watoe tamko la kuunga mkono maamuzi yaliyofanywa na kamati kuu, kupinga tamko la CHASO na kupinga matamko yote yaliyotolewa na wanamwanza kuhusu kuandamana kupinga maamuzi ya kamati kuu na ufisadi ndani ya chama. Tamko hilo lilitolewa tarehe 29/11/2013.
Hawa ndio wasomi wetu, watu wanaotegemewa kuwa dira na mwanga kwa wananchi ambao hawakupata bahati ya kwenda shule. Kama wao wanaweza kuburuzwa namna hii tutegemee nini miaka 10-20 ijayo chama kikiwa chini ya viongozi kama hawa?
Zoezi hili linaendeshwa na viongozi wa Chadema SAUT wakiongozwa na Kitaly Wilhad (Mwenyekiti), Lang'o Jackson (Katibu) na Nick Kilunga (Mpambe).
KWANINI MBOWE KAKIMBILIA CHADEMA SAUT
Mbowe ameona aitumie chadema SAUT kama kichaka chake cha kujifichia kwasababu ameshaona kuwa wananchi na wanachama wa chadema wameshagundua ufisadi unaoendelea katika chama, kwakuwa Mbowe anaamini kuwa wananchi huamini wasomi ndio maana mbowe ameamua kuwatumia viongozi wa chadema SAUT na hili limewezekana kwasababu tu mwenyekiti wa Chadema SAUT ni mchaga ambaye anaamini kuwa chadema si chama cha siasa balini CHAGA DEVELOPMENT MACHAME. Tayari wanafunzi wa vyuo vikuu wanaojitambua walishatoa tamko la kukataa ufisadi wa mbowe na kupinga maamuzi ya kamati kuu kuwafukuza watu kwa maslahi binafsi tamko ambalo lilitolewa na viongozi wa wanachama wa chadema vyuo vikuu (CHASO).
UTOFAUTI WA CHADEMA SAUT NA CHADEMA VYUO VIKUU VINGINE
- Chadema SAUT ni tawi pekee linalounga mkono hatua ya Mbowe kunyofoa kinyemela kifungu cha ukomo wa uongozi wa chama kwenye katiba chadema.
- Chadeama SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa mtu anayekosoa maovu yanayotendeka kwenye chama anatumiwa na ccm.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa ili ufike mbali kwenye chadema ni lazima unyenyekee na ujipendekeze kwa viongozi.
- Chadema SAUT ni tawi pekee lenye washabiki na wafuasi wengi wa Mbowe kuliko wanachama hai wa chadema.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini kuwa chadema haiwezi kuwepo bila mbowe kutokana na ukabila wa mweyekiti wake.
- Chadeama SAUT ni tawi pekee linalounga mkono Ruzuku ya chama kutumika makao makuu tu.
- Chadema SAUT ni tawi linaloongoza kwa usahaulifu kwani mara zote limekuwa likiheshimiwa na kutembelewa na viongozi pale tu wanapokuwa na shida zao binafsi au linapowataka wanafunzi hao kwenda kusimamia kura.
- Chadema SAUT ni tawi pekee linaloamini chadema itashinda kwa upepo tu.
NAMNA CHADEMA SAUT INAVYOTUMIKA
· December 8 Viongozi wa Chadema SAUT walihongwa pesa na timu ya Mbowe ili waite vyombo vya habari (Press conference) na kuutangazia umma kuhusu ziara ya mbowe Mwanza, pia waliagizwa kumpiga mkwara Mwenyekiti wa matawi ya chadema Mwanza Ngd Gwanchele kwa kumtishia kumshitaki, pia waliambiwa wasema kuwa watu wa mwanza wapo tayari kumpokea mbowe, wanaunga mkono maamuzi ya kamati kuu na kwamba watu hawataandamana kumpimga mbowe kama matamko yanavyosema. Hili lilifanyika na habari hii ilitangazwa kwenye vyombo vya habari ikiwemo Channel 10 habari Tarehe 9/12.2013 saa 1 na dk 3 usiku. Umeona wapi ziara ya kimkoa kwenye mkoa fulani ikitangazwa na viongozi wa tawi?
· Viongozi wa Chadema SAUT wahongwa pesa za kuandaa mkutano wa kumsafisha Mbowe atakapokuja Mwanza. Mkutano huo utafanyika jumamosi tarehe 15/12.2013 ambapo mbowe atakuwepo mkutanoni. Katika mkutano huo viongozi wa chadema SAUT watatakiwa kutoa tamko la kumuunga mkono mbowe na maamuzi yake pia kupinga tamko la kiongozi wa umoja wa matawi ya chadema Mwanza. Viongozi wa chadema SAUT watatakiwa kuwathibitishia wananchi imani yao kwa chama na pia kuunga mkono maamuzi yote ambayo yamefanywa na chama.
· Viongozi wa chadema SAUT wameahidiwa donge nono ikiwa watafanikiwa kumlinda mbowe asianikwe, kuchafuliwa na kuzomewa katika ziara yake ya Mwanza kama inavyotokea kwa Dr. Slaa huko Kigoma. Tayari viongozi wa Chadema SAUT wameshaandaa watu wa kumshangilia mbowe kwenye mkutano washangiliaji ambao watashangilia kila kitakachosemwa na mbowe hata kama hakina mantiki.
Ikumbukwe kuwa ni Chadema SAUT iliyopewa pesa ya kulipa vyombo vya habari tarehe 28/11/2013 ili watoe tamko la kuunga mkono maamuzi yaliyofanywa na kamati kuu, kupinga tamko la CHASO na kupinga matamko yote yaliyotolewa na wanamwanza kuhusu kuandamana kupinga maamuzi ya kamati kuu na ufisadi ndani ya chama. Tamko hilo lilitolewa tarehe 29/11/2013.
Hawa ndio wasomi wetu, watu wanaotegemewa kuwa dira na mwanga kwa wananchi ambao hawakupata bahati ya kwenda shule. Kama wao wanaweza kuburuzwa namna hii tutegemee nini miaka 10-20 ijayo chama kikiwa chini ya viongozi kama hawa?
Zoezi hili linaendeshwa na viongozi wa Chadema SAUT wakiongozwa na Kitaly Wilhad (Mwenyekiti), Lang'o Jackson (Katibu) na Nick Kilunga (Mpambe).