Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni, baada ya kususa na kununia kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa wafuasi na viongozi wa CHADEMA sasa wamegeuka kuwa maripota wa matukio yanayojiri kwenye kampeni za uchaguzi zilizozinduliwa hapo jana.
Hii inadhihirisha kwamba maamuzi ya kususia na kununia uchaguzi ni ya kada wa CCM aliyepewa jukumu la kuingoza CHADEMA ndugu Mbowe na si ya wafuasi wa CHADEMA.
Ajizi nyumba ya njaa, ningeshauri tu wafuasi wa CHADEMA ili msiumie nafsi zenu ni bora mgesusia na kampeni yaani kila mkiangalia kampeni mnazidi kuathirika kisaikolojia.Kwanini hamkujifunza kwa Seif aliposusia uchaguzi Zanzibar, amepata faida gani zaidi ya kuwaathiri kisaikolojia wafuasi wake?
Nimalize kwa kusema, ''majuto mjukuu''.
Ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni, baada ya kususa na kununia kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa wafuasi na viongozi wa CHADEMA sasa wamegeuka kuwa maripota wa matukio yanayojiri kwenye kampeni za uchaguzi zilizozinduliwa hapo jana.
Hii inadhihirisha kwamba maamuzi ya kususia na kununia uchaguzi ni ya kada wa CCM aliyepewa jukumu la kuingoza CHADEMA ndugu Mbowe na si ya wafuasi wa CHADEMA.
Ajizi nyumba ya njaa, ningeshauri tu wafuasi wa CHADEMA ili msiumie nafsi zenu ni bora mgesusia na kampeni yaani kila mkiangalia kampeni mnazidi kuathirika kisaikolojia.Kwanini hamkujifunza kwa Seif aliposusia uchaguzi Zanzibar, amepata faida gani zaidi ya kuwaathiri kisaikolojia wafuasi wake?
Nimalize kwa kusema, ''majuto mjukuu''.