Chadema sasa ipo tayari kuongea na serikali...........

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Gazeti la the Citizen linatupasha ya kuwa uongozi wa Chadema upo tayari kuongea na serikali juu ya kumaliza mgogoro wa kisiasa uliotokana na mapungufu ya uchaguzi wa Uraisi...................gazeti hilo limeweka kichwa cha habari kisemacho....................."Chadema now ready to talk to government."

Pia katika ufumbuzi hizo ni pamoja na kuitunga upya katiba yetu..........tume huru ya uchaguzi.....serikali nayo ipo tayari kwa masharti ya Chadema kufuata taratibu zilizopo.......
 
MHHHHHH, kama kweli serikali iko tayari! ni ushindi mkubwaaaaaaa kwa wapenda mabadilikoooo
 
hakuna kuongea nao..kura zihakikiwe upya ndo mzungumzo yafanyike
 
Gazeti la the Citizen linatupasha ya kuwa uongozi wa Chadema upo tayari kuongea na serikali juu ya kumaliza mgogoro wa kisiasa uliotokana na mapungufu ya uchaguzi wa Uraisi...................gazeti hilo limeweka kichwa cha habari kisemacho....................."Chadema now ready to talk to government."

Pia katika ufumbuzi hizo ni pamoja na kuitunga upya katiba yetu..........tume huru ya uchaguzi.....serikali nayo ipo tayari kwa masharti ya Chadema kufuata taratibu zilizopo.......

Serikali wao wapo tayari kwa CHADEMA kufuata taratibu za kiserikali na sio wao wanavyotaka. Na mbowe ameisha sema wao hawasemi uchaguzi urudiwe na wala Slaa atangazwe kuwa Rais. Hii ina maana kuwa wameisha kubali kuwa JK ndio Rais. Na hapa maneno ya JK yanaanza kutimia kuwa' WATAKWENDA WATARUDI KWAKE KWANI YEYE NDIO MWENYE MAMLAKA YA KUWATIMIZIA HAYO WAYATAKAYO'

 
hakuna kuongea nao..kura zihakikiwe upya ndo mzungumzo yafanyike

kwenye madai ya CHADEMA hakuna dai la kura kuhesabiwa upya, CHADEMA wanachohitaji ni KATIBA, TUME HURU YA UCHAGUZI, NA TUME YA UCHUNGUZI KUHUSU UCHAGUZI MKUU
 
hakuna kuongea nao..kura zihakikiwe upya ndo mzungumzo yafanyike

itakuwa ngumu baadhi ya maeneo mfano jimbo la shinyanga mjini kura zilichomwa na usalama wa ccm baada ya kubwagwa vibaya.pia ushauri wa bure kwa wabunge wa ccm waliopewa ubunge kwa njia ya uchakachuzi achane kuwazomea wabunge wetu mnazidi kututia hasira
 
Gazeti la the Citizen linatupasha ya kuwa uongozi wa Chadema upo tayari kuongea na serikali juu ya kumaliza mgogoro wa kisiasa uliotokana na mapungufu ya uchaguzi wa Uraisi...................gazeti hilo limeweka kichwa cha habari kisemacho....................."Chadema now ready to talk to government."

Pia katika ufumbuzi hizo ni pamoja na kuitunga upya katiba yetu..........tume huru ya uchaguzi.....serikali nayo ipo tayari kwa masharti ya Chadema kufuata taratibu zilizopo.......
Nahisi hata hii kauli imechakachuliwa...! Kwa maana hadi CHADEMA wafikie maamuzi yao ya kutomtambua Rais ni matokea ya serikali kususia mazungumzo haya....! Na badala yake mimi nahisi Serikali ndio imekuwa tayari kuzungumza na CHADEMA, hivyo ingekaa hivi; "The Government now ready to talk to CHADEMA". Lakini kwangu mimi mwenye uwezo wa kusoma message na kupata ujumbe hiyo siijali hata kidogo, maana wakisema watakavyosema bado meza ni ileile, na mantiki ni yaleyale...! Hivyo, hii ni kuwafumba mambumbumbu macho waone upende mwingine wa sarafu, japo lengo litabaki kama ilivyokusudia....!
 
hakuna kuongea nao..kura zihakikiwe upya ndo mzungumzo yafanyike

Chini ya sheria uchaguzi ni mahakama tu yenye mamlaka ya kuagiza kura kurudiwa kuhesabiwa na chadema hawataki kwenda mahakamani.....................
 
Nahisi hata hii kauli imechakachuliwa...! Kwa maana hadi CHADEMA wafikie maamuzi yao ya kutomtambua Rais ni matokea ya serikali kususia mazungumzo haya....! Na badala yake mimi nahisi Serikali ndio imekuwa tayari kuzungumza na CHADEMA, hivyo ingekaa hivi; "The Government now ready to talk to CHADEMA". Lakini kwangu mimi mwenye uwezo wa kusoma message na kupata ujumbe hiyo siijali hata kidogo, maana wakisema watakavyosema bado meza ni ileile, na mantiki ni yaleyale...! Hivyo, hii ni kuwafumba mambumbumbu macho waone upende mwingine wa sarafu, japo lengo litabaki kama ilivyokusudia....!

You could be right......hili ni gazeti linalomilikiwa na CCM..........................lakini la msingi hapa pande mbili zaona umuhimu kumaliza tofauti zao kwa njia ya mazungumzo.....na hiyo ndiyo demokrasia pia.......................
 
itakuwa ngumu baadhi ya maeneo mfano jimbo la shinyanga mjini kura zilichomwa na usalama wa ccm baada ya kubwagwa vibaya.pia ushauri wa bure kwa wabunge wa ccm waliopewa ubunge kwa njia ya uchakachuzi achane kuwazomea wabunge wetu mnazidi kututia hasira

Hakuna nguvu ya kisheria kuhakiki kura ila kwa kibali cha mahakama..................
 
Mimi nimemsikia Mbowe asubuhi kwenye WAPO radio alipokuwa akihojiwa.
Kafafanua vizuri sana kuhusu position ya Chadema - hawawezi kisheria na kiutendaji kupingana na maamuzi ya katiba iliyopo, which means chama chake hakiwezi ku-reverse matokeo ya u-rais yaliyotangazwa.

Kwa hiyo hoja ya Chadema, alisikika akisema, ni kupinga ectoral process, NEC na katiba mbovu.
Aka-conclude kuwa the recent ("infamous") walk-out ilikuwa ni method ya kuonyesha protest yao ili the whole world itambue kuwepo kwa matatizo hayo ya msingi na kwamba Chadema imedhamiria kuhakikisha haya yanakuwa addressed.
For starters, akasema, Chadema inataka iundwe tume huru ya uchunguzi ili kufukunyua details za matokeo ya kura za u-rais. Kifuatacho ni kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya.

Baada ya kuulizwa uwezekano wa kukutana na JK, Mbowe kasema JK (kama taasisi ya u-rais) ndiye anayewajibika kukutana na wananchi (wakiwemo Chadema) na kwamba wao (Chadema) watakuwa tayari kukutana naye kama wananchi wengine na watatumia opportunity hiyo kusisitiza hayo madai yao.

Source: WAPO radio leo asubuhi.
 
Gazeti la the Citizen linatupasha ya kuwa uongozi wa Chadema upo tayari kuongea na serikali juu ya kumaliza mgogoro wa kisiasa uliotokana na mapungufu ya uchaguzi wa Uraisi...................gazeti hilo limeweka kichwa cha habari kisemacho....................."Chadema now ready to talk to government."

Pia katika ufumbuzi hizo ni pamoja na kuitunga upya katiba yetu..........tume huru ya uchaguzi.....serikali nayo ipo tayari kwa masharti ya Chadema kufuata taratibu zilizopo.......

.... na pia katika hayo, kwenye sheria inayohusu vyama vya siasa, suala la UMAMLUKI, au kwa kudhungu, deliberate, premediatated and all acts of sabotage perpetrated by a PARTY or PARTIES against another PARTY or PARTIES liangaliwe kwa kina kudhibiti UPUUZI unaofanywa wakati huu na kina CCM na baadae wapuuzi wa namna hiyo kuharibu democratic process na kukiuka HAKI za wengine ili kuendeleza HEGEMONY yao. It is really sickening!

I am lost for words to describe positions, views, mentallity, perceptions etc maintained and held by party stalwarts in the likes of Chiligatis, Makambas, the Tambwes, Simbas to name but a few among the current CCM lot. I percieve that lot as essentially LOATHSOME and that at the expense of PROGRESS, LIGHT in Tanzania, they remain at the core and epicenter of the darkness which has continously engulfed this nation. A luta continua!
 
Rutashubanyuma: You could be right......hili ni gazeti linalomilikiwa na CCM..........................lakini la msingi hapa pande mbili zaona umuhimu kumaliza tofauti zao kwa njia ya mazungumzo.....na hiyo ndiyo demokrasia pia.......................

The Citizen halimilikiwi na CCM..mmliki wake ni Nation Media Group ya Kenya, ambayo inamilikiwa na His Highness Aga Khan
 
Mimi nimemsikia Mbowe asubuhi kwenye WAPO radio alipokuwa akihojiwa.
Kafafanua vizuri sana kuhusu position ya Chadema - hawawezi kisheria na kiutendaji kupingana na maamuzi ya katiba iliyopo, which means chama chake hakiwezi ku-reverse matokeo ya u-rais yaliyotangazwa.

Kwa hiyo hoja ya Chadema, alisikika akisema, ni kupinga ectoral process, NEC na katiba mbovu.
Aka-conclude kuwa the recent ("infamous") walk-out ilikuwa ni method ya kuonyesha protest yao ili the whole world itambue kuwepo kwa matatizo hayo ya msingi na kwamba Chadema imedhamiria kuhakikisha haya yanakuwa addressed.
For starters, akasema, Chadema inataka iundwe tume huru ya uchunguzi ili kufukunyua details za matokeo ya kura za u-rais. Kifuatacho ni kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya.

Baada ya kuulizwa uwezekano wa kukutana na JK, Mbowe kasema JK (kama taasisi ya u-rais) ndiye anayewajibika kukutana na wananchi (wakiwemo Chadema) na kwamba wao (Chadema) watakuwa tayari kukutana naye kama wananchi wengine na watatumia opportunity hiyo kusisitiza hayo madai yao.

Source: WAPO radio leo asubuhi.

Hayo maelezo ya kamanda Mbowe ni crystal clear..
Sijui chiligati na cronies wenzake next watasemaje baada ya huu ufafanuzi, maana wanapanga mbinu chafu kutaka kuwafukuza CDM bungeni
 
Chadema inabidi iangalie kitengo chake cha PR, kuhusu utoaji wa taarifa sahihi na kwa wakati..hilo ni muhimu sana kama wanataka wananchi wawachukulie seriously.
 
Mimi nimemsikia Mbowe asubuhi kwenye WAPO radio alipokuwa akihojiwa.
Kafafanua vizuri sana kuhusu position ya Chadema - hawawezi kisheria na kiutendaji kupingana na maamuzi ya katiba iliyopo, which means chama chake hakiwezi ku-reverse matokeo ya u-rais yaliyotangazwa.
Tatizo la Chadema ni kutotafuta ushauri wa kisheria juu ya tafsir sahihi ya Ibara ya Na. 41(5) ambayo imeitaka NEC kuhakikisha inafuata taratibu zote zilizoainishwa kwenye sheria ya uchaguzi wakati wanamtangaza Raisi ili Mahakama au chombo kinginecho kiweze kuzuiwa kuwa kuhoji matamshi ya NEC ya kumtangaza Raisi..........................

Mimi ninaanza kuwa na wasiwasi wa kuwa huenda chadema hawana ushahidi wa kuhoji NEC kama kweli ilifuata au haikufuata sheria ya uchaguzi katika kumtangaza JK kuwa Raisi na ndiyo maana wanagwaya kwenda mahakamani kwa visingizio vya katiba Ibara ya 41(7) ndiyo kikwazo kwao.................kama kweli wana matokeo yote kutoka vituoni na ambayo yalitangazwa na Wasimamizi wa majimbo nchi nzima na NEC hawakuyafuata katika kumtangaza JK kuwa ni Raisi na hivyo kukiukwa Ibara ya 41 (5) ya katiba yetu........hivi ni nini kinawazuia kwenda mahakamani......wakati matokeo ambayo hayawezi kuchunguzwa na Mahakama ni yale tu ambayo yametangazwa kwa kuzingatia Ibara nzima ya 41 na hii Ibara ndogo ya 41(5) imo?

Hawa chadema are playing with us but the question has to be for how long?
 
Nadhani CHADEMA wako kwenye move nzuri mpaka sasa,hawajakosea mahali popote.wasiojua sheria na katiba ndo wanaoropoka hovyo humu.
Ila kazi tunayo ya kuhakikisha tunawaelimisha watu wote ambao Katiba na Sheria ya Tanzania inawapiga chenga na ndio walio wengi sana Tanzania.
Shida kubwa imeanza kwenye kujua HAKI YA KILA RAIA.
Haki raia wa Tanzania imeporwa na wageni hili si jambo la kuficha tena mpaka sasa.Lazima tuwe wawazi bila hivyo wasomi wa Tanzania watakuwa wakulaumiwa mpaka mwisho.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom