Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Hakuna raia wa Tanzania anaependa mtu kuonewa au kufanyiwa unyama ambao upo kinyume na sheria za nchi hii.
Ndio maana hata polisi wanapofanya makosa na kuvunja haki za binadamu kila mtu hulaani.
Hata Mh Rais katika maadhimisho ya sheria ya mwaka huu 2020 amesisitiza juu ya vyombo vyote vinavyosimamia sheria kutenda haki na kuzingatia maadili.
Viongozi wenu walivamia eneo nyeti na kufanya vurugu kwa mujibu wa kamanda Mambosasa, mlitegemea nini? Askari magereza waliwatuliza na kuwakamata kwa mujibu wa sheria. Mliemfuata ametoka na sasa yupo kwake anakula bata. Kwa nini msingemsubiri nje?
Sasa mnataka huruma kwa wananchi ili iweje? Badala muwe na mikakati ya kujiimarisha maana uchaguzi umefika (japokuwa kiti cha urais mmeshashindwa) mnabaki kutafuta huruma kwa wananchi baada ya kupigwa virungu.
Hivi mbona mmepwaya sana toka Dk Slaa aondoke!
Ndio maana hata polisi wanapofanya makosa na kuvunja haki za binadamu kila mtu hulaani.
Hata Mh Rais katika maadhimisho ya sheria ya mwaka huu 2020 amesisitiza juu ya vyombo vyote vinavyosimamia sheria kutenda haki na kuzingatia maadili.
Viongozi wenu walivamia eneo nyeti na kufanya vurugu kwa mujibu wa kamanda Mambosasa, mlitegemea nini? Askari magereza waliwatuliza na kuwakamata kwa mujibu wa sheria. Mliemfuata ametoka na sasa yupo kwake anakula bata. Kwa nini msingemsubiri nje?
Sasa mnataka huruma kwa wananchi ili iweje? Badala muwe na mikakati ya kujiimarisha maana uchaguzi umefika (japokuwa kiti cha urais mmeshashindwa) mnabaki kutafuta huruma kwa wananchi baada ya kupigwa virungu.
Hivi mbona mmepwaya sana toka Dk Slaa aondoke!