Hoja hii inaweza kutoka kwa mtu ambaye anathamini maslahi yake zaidi kuliko maslahi ya Taifa na si vinginevyo.
kwanini mkuu,au hampendi kukosolewa.unapaswa kumwelewesha kama kuna mahali kakosea.otherwise hakuna taasisi isiyo na mapungufu,hivyo chadema kama taasisi lazima ina mapungufu yake na hapa mleta mada ameonyesha moja ya mapungufu aliyoona ndani ya chadema.
Kama unataka kufukuzwa Chadema pinga mawazo ya Dr Slaa au Mbowe, muulize Kafulila.
Chagulani na Matata, nasikia leo wamekwenda mahakamani kupiga kuvuliwa uanachama, Wasukuma wa Mwanza wamejitolea kuwasaidia kuweka mawakili.
au tangaza nia ya kugombea urais ama uenyekiti wa chadema
Ritz hivi elimu yako ipoje? unaweza kutusaidia hata summary kidogo tu ya cv yako? Nasema hivi kwa kuwa always unapost upuuzi hapa kwenye jamvi na zaidi ya rejao hakuna anayeekunga mkono, Yaani madiwani wa Arusha waende kinyume na taratibu za chama waonywe wapewe muda wa kujieleza wakatae bado wavumiliwe tu?? CDM huwa inachukua hatua sio sawa na magamba akina Sitta na Nape walianzisha chama (CCJ) wakiwa ndani ya CCM mnawalea hadi leo
,CDM unafukuzwa then ukienda mahakamani ndio penyewe! Kolimba(R.I.P) alisema ccm haina dira yuko wapi leo??
Jumbe alihoji muungano nini kilitokea??Malecela akiwa waziri mkuu aliunga mkono serikali tatu nini kilimpata?hebu tuorodheshee huo udikteta wa CDM?halafu ndani ya CDM hakuna zidumu fikra za mwenyeketi!ukikosea unapigwa chini
Umesema Zitto alitaka kuvuliwa ubunge hebu tupatie minutes za hicho kikao inaelekea unaingia vikao vya cc ya CDM
Elimu yake ni sawa sawa na ya Mbowe lakini Ritz alijiendelezaendeleza hakuishia kujua kusoma na kuandika tu.
Mtu yoyote aliye makini na mwenye akili timamu ni lazima ahoji, serikali iwauwe viongozi wa Chadema kwa sababu ipi na kwa manufaa ya nani?