Kiongozi mkuu2020
JF-Expert Member
- Aug 8, 2020
- 1,748
- 997
Sasa baada ya msomi ndugu bwana Vincent mashinji kutoka pale, nani mwanasayansi aliebaki pale?Ni ukweli ulio wazi kwamba kwenye mambo ya kuchanganua masuala ya fedha na ufisadi CHADEMA wako vizuri na tunawaheshimu katika hilo.
Ila kwenye eneo la kemia, baiolojia na famasia hawana uwezo nalo kabisa wanajaribu tu kujiingiza lakini wanafeli.
Hebu tuwaache CCM tuliwaamini na kuwapa uongozi wa nchi watuvushe katika hii sintofahamu ya Corona.
CHADEMA endeleeni kufuatilia mambo ya thamani ya fedha katika miradi mikubwa inayotekelexwa na serikali. Tunajua waasisi wa CHADEMA, Bob Makani RIP na mzee Mtei walikuwa wabobezi kwenye sekta hiyo.
Tuwaache wataalamu akina Dr Gwajima, Dkt. Mollel na hata yule Kigwangalla watupe mwongozo wa kuvuka salama chini ya Jemedari wetu Dkt. Magufuli akisaidiwa na Dkt. Hussein Mwinyi wa Zanzibar.
Kadhalika wabobezi wengine Dr Billal, Dr Shein na hata yule bingwa wa Baiolojia Prof. Kapuya.
CCM imesheheni wanasayansi tuwape nafasi.
Maendeleo hayana vyama!