CHADEMA ni wasanii! - Mtikila

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Mtikila adai Chadema inafanya usanii

Stella Nyemenohi
HabariLeo; Monday,October 01, 2007 @00:03

MWENYEKITI wa Democratic Party (DP), Christopher Mtikila ameibuka na kukishutumu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa kinafanya usanii wa kutumia majukwaa kujadili madai ya ufisadi dhidi ya viongozi wa Serikali kwa lengo la kufunika vyama vingine na kushika madaraka na siyo kuleta ukombozi kwa umma.

Mtikila, ambaye hata hivyo anaunga mkono madai hayo ya Chadema, alisema kitendo cha viongozi wa chama hicho kuacha kwenda mahakamani kinadhihirisha hawana nia thabiti ya kukabili tatizo, bali wanapoteza muda katika majukwaa kujipatia umaarufu.

“Hawa watu (Chadema) ni wasanii. Wanataka washangiliwe kwa gharama ya taifa. Mikataba ni suala la kisheria, haki ya kisheria haipatikani katika majukwaa. Wao hawataki mahakamani ambako ndiko wangepata haki?” Mtikila aliiambia HabariLeo jana.

Alisema kitendo cha baadhi ya viongozi waliotuhumiwa kuwa mafisadi kwenda mahakamani, ni mwelekeo wa kuzimaliza hoja hizo ambazo kama zingeshughulikiwa katika mkondo unaostahili, umma wa Watanzania ungeshuhudia mabadiliko.

Viongozi waliotangaza uamuzi wa kwenda mahakamani kumfungulia mashitaka Mbunge wa Karatu, Wilbrod Slaa, kwa madai ya kuitwa mafisadi ni Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Grey Mgonja na Katibu Mkuu, Wizara ya Maji, Patrick Rutabanzibwa.

“Kitendo cha walioshutumiwa kwenda mahakamani, hapo ndipo wamewabana. Lazima waanguke. Hapa suala la kujiuliza ni kwa nini Chadema hawakwenda wakati walikuwa na haki na hoja ni za kweli?” alihoji.

Kwa mujibu wa Mtikila, aliwashauri viongozi hao wa Chadema kufungua kesi kupitia mawakili watatu ambao kwa mujibu wake, walitaka walipwe Sh milioni 10 kwa kazi hiyo, lakini viongozi hao wakakataa.

Katika kile anachosisitiza kuwa ni usanii wa kutaka kutumia hoja hizo kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao, Mtikila alisema ushauri wake ulilenga kufungua kesi itakayotoa suluhu la ufisadi kwa upana, ikiwa ni pamoja na kuondoa kipengele cha usiri katika mikataba.

Mtikila aliendelea kukishutumu chama hicho cha upinzani kuwa kinafanya hivyo kujizoelea sifa kwa kutumia hoja ambazo siyo ngeni ili kukidhi matakwa ya wafadhili wao wanaowataka wahakikishe kinaingia madarakani katika uchaguzi ujao, na wala si kwa masilahi ya umma.

“Wanaposema Karamagi kasaini mkataba Uingereza, Chadema nao hawana tofauti naye. Hawa wana Barrick, wao wana Conservative, wamewaambia lazima waingie madarakani,” alidai Mtikila.

Akisisitiza kuwa shutuma hizo dhidi ya Chadema hazitokani na wivu wa siasa, Mtikila alisema, “vyama vya usanii vitanyauka. Ni mara ngapi tumekuwa tukitupwa gerezani, hata siku moja hawajawahi kuandamana kutetea haki zetu?”

Akizungumza kuhusu shutuma hizo za Mtikila, Mbunge wa Karatu, Dk. Slaa alisema, “anazungumza asichokijua. Suala siyo mahakama, kama ni taratibu, zote tulizifuata. Nikipeleka suala hili mahakamani, ujue majibu yake ni katika miaka 20. Sisi tumeamua tulipeleke kwa wananchi wenyewe ndiyo waamue.”

Katika kuzungumzia madai ya Mtikila kuhusu kuwatafutia mawakili, Dk. Slaa alidai kwamba Mwenyekiti huyo wa DP aliwaomba wamchangie Sh milioni 10 kwa ajili ya mawakili aliowaandaa. Hata hivyo, alisema hawakukubaliana naye kwa kuwa Dk. Slaa ana mawakili wanaomtetea bila gharama yoyote.

Kuhusu Chadema kubinafsisha hoja, Dk. Slaa alisema hoja hizo za ufisadi wa viongozi ni za vyama vyote. “Yeye (Mtikila) anataka aingie kwa nguvu,” alisema. Alikanusha madai ya kutumiwa na Conservative kwa kumtaka Mtikila aonyeshe ushahidi.

Wakati huo huo, Dk. Slaa amesema bomu alilokuwa ameahidi kulilipua wiki iliyopita, limeathiriwa na majibu ya serikali yaliyotolewa ambayo hata hivyo ameelezea kutoridhika nayo.

Ameitaka Serikali kutoa majibu ya hoja zake kwa kile alichodai majibu yaliyotolewa ni propaganda za siasa zisizowasaidia wananchi.
 
Mtikila bwana . Yaani madai haya yaende Mahakamani namna hii ?Hivi yale ya Mrema yalichukua muda gani kupata ufumbuzi ?Hivi tofauti ya Mahakama na Bunge ni ipi ? Maana Ditto kaua na mtu kalala kaburini lakini anapeta mtaani .Bora Chadema kuanzia nje then Mahakamani yote yanawezekana. Biashara naona aliitakam kuifanya Mtikila .
 
Right on Mtikila !

Hapa ndio utamu upo, ebu chekshia sinema hilo, yaani Mtikila anajiona anajua, huku Dr. Slaa hali kadhalika hiyo hiyo ! sasa sijui nani adui nani steringi ! bwana weeeh.

Lakini anyway i would care less about CHADEMA/CCM,MTIKILA/DR.SLAA and so forth, tunachotaka ni maendeleo kwa wananchi !
 
Ndugu zangu wa Ze Comedy wanasema Shuzi limepata Mjambaji. Lazima patatoka cheche hapo. Acha tuangalie...
 
Kupenda sometimes ni kilema; I wonder some guys are saying Mtikila is 60 pct right! Give me a break; Dr. Slaa is very very right; if this case is started by him will rot in the the court, that is a fact in a banana country like ours; now it is being started by themselves, maybe this will accerelate issues at the courts while the mass is already informed; keep-up Dr. slaa and the likes!

By the way, Mr. Mtikila stick to the murder case facing the CCM cadre, that one is already too heavy to handle for you; leave the CHADEMA boys and gals work on this; Bravo CHADEMA; just for now!!
 
Mbona shutuma zake kwa Sumaye hakuzipeleka mahakamani?

Au ndio kajua umuhimu wake sasa.
 
Mbinu ya CHADEMA ni sahihi kabisa, serikali ambayo imeweze kuliteka Bunge haishindwi na maamuzi ya mahakama.

Nini hatima ya kesi ya Mtikila juu ya mgombea binafsi? Maamuzi ya mahakama hayajatekelezwa hadi leo kwa vile maamuzi hayo yana athari kwao vigogo.CHADEMA imeona njia sahihi ni hiyo ya kushtaki kwa wananchi maana ndio wanaoibiwa.Mtikila anadhani ni fahari kila siku kuwa katika korido za mahakama ambazo hata ukishinda kesi unasifiwa tuu lakini maamuzi ya mahakama hayatekelezwi.

Lazima washtakiwe kwa wananchi ambao wengi wao walikuwa WANAPIGIKA bila kujua nini hasa chanzo na kuishia kusema Mipango ya MUNGU. Wacha wenye nchi yao wayasikie kwanza,waelewe na kuchukia kwa kufanywa wajinga kwa muda mrefu hivyo kuingia katika dimbwi la umaskini ndani ya nchi tajiri na yenye neema lukuki. Baada ya hapo wao ndio wataamua kuwatoa madarakani kidemokrasi (kama viongozi watakikubali kwa hiari uchaguzi huru) au kwa nguvu wakianza kuzuga.

Ya kuwa CHADEMA wanatumia nafasi hii kujijenga kisiasa,yeye alitegemea nini? Wafanye kazi ya kuitangaza DP? Wao kama chama cha siasa kila opportunity wanayoipata lazima waitumie. Asishangae kwa hilo maana hakuona jinsi CCM walivyo tumia Taifa Stars kujijenga?

Ni wajibu wetu sote hasa Watanzania,kuinga mkona hoja ya Slaa kwa faida ya nchi.
 
Somehow 60% Mtikila yupo sahihi!

FD,

Na mimi nakubaliana nawe kwamba aliyosema Mtikila yana ukweli. Ila tu CHADEMA na Mtikila wanaongea toka angle tofauti, strategies zao ziko tofauti.

Mtikila anataka ukombozi wa Mtanzania through haki na sheria. Binafsi ningependa ukombozi wa aina hii ili kuondoa uwezezekano wa kumuondoa fisadi mmoja na kumwingiza mwingine. Tatizo lake utekelezaji wake ni mgumu mno. Kwenda mahakamani kunahitaji resources nyingi na muda mrefu. Pia kwasababu CCM wameshika mpini basi hata huko mahakamani case nyingi zitatupwa kwa madai kwamba mahakama haina uwezo.

CHADEMA ni chama cha siasa, wanataka kutumia siasa kuingia madarakani, hilo la kumkomboa Mtanzania linakuja baadaye, ni mengineyo. Kwahiyo wao strategy yao sio kuisafisha CCM au kuwaondoa viongozi wabaya serikalini bali ni kuipaka matope CCM yote ili wananchi wachukie na uchaguzi ujao wawape wao madaraka. Wanaamini wakishika madaraka watakuwa na nafasi nzuri ya kubadili katiba, sheria na haki zingine za mwananchi, kwahiyo hapo ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Tatizo ni kwamba wakiingia madarakani, hawatataka kubadili sheria ambazo zitawasaidia kuwafanya waongoze kwa muda mrefu (mfano mzuri ni KIbaki na Chiluba).

Hizo ndio dilemma za wanasiasa na vyama vya siasa. Wengine yetu macho, kufarahi, kucheka na kununa. Katika mchezo huu wa siasa anayemumia ni nyasi, ni wale ndugu zetu kule vijijini ambao umaskini unazidi siku hadi siku.
 
FD,

Na mimi nakubaliana nawe kwamba aliyosema Mtikila yana ukweli. Ila tu CHADEMA na mtikila wanaongea toka angel tofauti, strategies zao ziko tofauti.

Mtikila anataka ukombozi wa Mtanzania through haki na sheria. Binafsi ningependa ukombozi wa aina hii ili kuondoa uwezezekano wa kumuondoa fisadi mmoja na kumwingiza mwingine. Tatizo lake utekelezaji wake ni mgumu mno. Kwenda mahakamani kunahitaji resources nyingi na muda mrefu. Pia kwasababu CCM wameshika mpini basi hata huko mahakamani case nyingi zitatupwa kwa madai kwamba mahakama haina uwezo.

CHADEMA ni chama cha siasa, wanataka kutumia siasa kuingia madarakani, hilo la kumkomboa Mtanzania linakuja baadaye, ni mengineyo. Kwahiyo wao strategy yao sio kuisafisha CCM au kuwaondoa viongozi wabaya serikalini bali ni kuipaka matope CCM yote ili wananchi wachukie na uchaguzi ujao wawape wao madaraka. Wanaamini wakishika madaraka watakuwa na nafasi nzuri ya kubadili katiba, sheria na haki zingine za mwananchi, kwahiyo hapo ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Tatizo ni kwamba wakiingia madarakani, hawatataka kubadili sheria ambazo zitawasaidia kuwafanya waongoze kwa muda mrefu (mfano mzuri ni KIbaki na Chiluba).

Hizo ndio dilemma za wanasiasa na vyama vya siasa. Wengine yetu macho, kufarahi, kucheka na kununa. Katika mchezo huu wa siasa anayemumia ni nyasi, ni wale ndugu zetu kule vijijini ambao umaskini unazidi siku hadi siku.


Mkuu mengine sawa,

Ila hilo hapo naona umeteleza kidogo, kuipaka matope manake wanaipakazia??? Mi nadhani hapa wanawaumbua siyo kuwapaka matope.

Mtikila kwa mtazamo wake kama mahakama ingekuwa huru sawa, ila kwa sasa hilo kwa Tanzania ni ndoto! Mhakama haina sauti/mamlaka hata! Kwahiyo walicho kifanya kina slaa ndo muafaka kwa hali ya mahakama za Tz!

Hata Hivo Mtikila hapaswi kubeza juhudi za wenziwe, naye kama ana uchungu bado hajazuiwa kwenda huko mahakamani! Asonge mbele tu alimradi yote ni kwania njema ya kuinasua Tanzania yetu katika makucha ya MAFISADI
 
naomba kuuliza waheshimiwa
fisadi kwa kiingereza ni nini? au kwa kamusi ya kiswahili fisadi ni nani?
 
"Wanaposema Karamagi kasaini mkataba Uingereza, Chadema nao hawana tofauti naye. Hawa wana Barrick, wao wana Conservative, wamewaambia lazima waingie madarakani," alidai Mtikila.

Reading between the lines, article nzima ya maoni Mtikila, yamekuwa fueled na wivu tu wa kisiasa,

However, swali langu kwa Mtikila, ipi ni afadhali, kutumiwa na viongozi wachache wa CCM kwa faida zao binafsi as he always do, au Chadema kutumiwa na conservative party ya UK kwa faida ya taifa zima?

Again this time Mtikila, ametumwa na nani Balali au Karamagi?
 
Reading between the lines, article nzima ya maoni Mtikila, yamekuwa fueled na wivu tu wa kisiasa,

However, swali langu kwa Mtikila, ipi ni afadhali, kutumiwa na viongozi wachache wa CCM kwa faida zao binafsi as he always do, au Chadema kutumiwa na conservative party ya UK kwa faida ya taifa zima?

Again this time Mtikila, ametumwa na nani Balali au Karamagi?

FM,
Sina hakika kama CHADEMA inatumiwa na Conservative. Lakini kama ni kweli basi sio kwa maslahi ya taifa zima. Kwani wanachokifanya ni kuhakikisha wana washirika, hata kama CCM ikiondoka basi CHADEMA itaendelea kutumikia maslahi ya hao hao kina Karamagi wanaowatumikia leo. Kwa minajili hiyo, wananchi ndio watakaoumia katika hili.
Kuna haja ya ukombozi wa kweli, hili linahitaji sana dhamira ya kweli ya viongozi wa CCM na vyama vya upinzani kwa upande mmoja na wananchi kwa upande mwingine. Vinginevyo kila mtu atakata kipande chake...matokeo yake itakuwa biashara ya papa sokoni, hata kipande kitaitwa papa.
 
Hapa mtikila kaniacha hoi bin taaban,je?alitaka milioni kumi ili atafute wanasheria kutoka wapi?ama alikuwa anataka kufanya kitu gani?

Mtikila hapo amekwenda kombo kwani alipaswa ama kukaa kimya ama vinginevyo naamini kuwa mtandao unawatumia baadhi ya watu ili kuuficha ukweli na hata leo nimesoma makala moja kwenye gazeti la mtanzania imeandikwa na mtu anayejiita naibu katibu mkuu wa UPDP.

hiki nacho ni chama cha siasa yeye alisema kuwa CHADEMA hawapaswi kuichafua serikali bali walipaswa kwenda kuzungumza nao, sasa hapa mwenye akili aweke conclusion yake.
 
FM,
Sina hakika kama CHADEMA inatumiwa na Conservative. Lakini kama ni kweli basi sio kwa maslahi ya taifa zima.

Mambo mengine kwa kweli either ni kuyakuza kisiasa au kutoelewa, Chadema kutotumiwa au kutumiwa, nafikiri tunachanganya mambo bila kuelewa,

Ninaamini kuwa Conservative Party, ya UK inashirikiana na Chadema, na pia ina-support msimamo wa Chadema, au haipendi baadhi ya mouvu yanayofanywa na CCM na serikali yetu, Scandanavians, pia waliwahi kufanya hayo baada ya kuchukizwa sana na serikali ya Mwinyi, waliamua kumsaidia Mrema, mpaka kupata ubunge wa Temeke, na pia walikuwa mbioni kumsaidia Mama Mongella, kugombea urais, wakulu wakafanya ujanja wakamlilia Mandela, ili ampe kazi ya Spika wa bunge la Africa, ili kumuondoa kinyemela,

Now, sio siri within CCM kuwa Chadema, inapata msaada gani na hao Conservative Party, ambao at one time walikuwa wakimdanganya Mkapa pia kuwa ni marafiki zake, the matter of fact wabunge wengi wa conservative party ni watu wa dini ya Dr. Slaa, ambao wanaamini kuwa muumini mwenzao Dr. Slaa anatekeleza kazi ya Mungu,

Kwa hiyo msaada wao kwa Dr. Slaa, ndio umeweza hata kumpa nguvu Dr. Slaa kusimama imara na kuyatoa maovu hadaharani na wote tumeyasikia, my point ni kwamba msaada wao yaani conservative kwa DR. Slaa/Chadema umekuwa ni msaada kwa taifa zima letu, kwa sababu whether you like it or not, political field ya bongo sasa hivi sio ile jana na juzi, leo CCM tuko kwenye defensive end kwa mara ya kwanza katika historia ya siasa Tanzania,

Regardless, kama hizo tuhuma ni za kweli au ni za uongo, so far I am not passing the hukumu, lakini they are very serious allegitions, kuaniza politically mpaka legally, sasa kama Dr. Slaa na Chadema wanasaidiwa na conservative party ya UK, basi this one ya orodha ya mafisadi ni good for our whole nation, kwa sababu in the process ya political scrumble inayoendelea sasa, wanaonufaika ni sisi wananchi kwamba for the first time in our nation's history we wananchi are taking a closer loook at how viongozi wetu wanavyo-operate, kwa mfano waziri wetu kwenda kusaini mkataba hotelini na kubeba mihuri ya taifa mfukoni mwake,

I mean what else can we ask from our opposition side na wanaowasaidia, in the wake ya orodha it does not matter nani anawasaidia Chadema, we as a nationa tunasubiri the results mahakamani?
 
Hivi mtu aweza kusimama yeye mwenyewe kwa kufuata principle zake au ni lazima awe na watu nyuma yake? Nilipoandika makala ya "mkapa azungumze" niliachiwa ujumbe mmoja kuwa "huyo aliyekutuma mwambie haogopwi, tena mwambie Bosi wako tunajua wanavyokutumia". Sasa, binafsi nilibakia kushangaa kwani nilidhani I am the boss!

Ni kweli kuna watu wanatumiwa (wenyewe wakijua au vinginevyo) and sometimes it is the nature of the beast... lakini kuna wakati watu husimama kwa kanuni wanazozijua wao. I hope behind everything else Dr. Slaa et al wanasimama kutokana na principles that are more noble, and beyond reproach than their own political ambitions and aspirations.
 
Back
Top Bottom