ilboru1995
JF-Expert Member
- Oct 4, 2007
- 2,329
- 268
Hata mkipotezea mada kivipi...CDM itamtema ili mumtumie vizuri kutetea serikali mbili...
Watanzania wenzangu kwanza natoa salaam zangu za heri ya mwaka mpya.
Napenda kutumia jukwaa hili kutoa maoni yangu juu ya sakata hili lililopo mbele yetu kati ya Zitto na CHADEMA kwa ujumla wake.
Kwa ufupi ni kuwa sakata hili limetikisa chama na wanachama wake wote! na ukweli umejaribu kuwekwa hadharani na mwenye macho kaona mwenyewe na kusikia mwenyewe. Sasa kuendelea kutunishiana msuli huku kila mtu akitaka kuonesha ni nani zaidi, sioni kama ni jambo muafaka kwa sasa. Kuna haja ya kukaa chini kama binadamu na kuonyana na wale wote ambao wamekwenda kinyume na Katiba wakili na waombe msamaha.
Zitto wewe bado ni kijana mdogo sana na kete yako ya kufika mbali bado ipo wazi kabisa, hivi kama ni uongozi ni kitu gani kinachokusukuma kwa nguvu namna hiyo kana kwamba dunia inapinduka kesho na usipoongoza leo utakufa????!!
Je, ni wangapi ndani ya CCM waliambiwa kuwa hawana hadhi hata ya kuwa wajumbe wa nyumba kumi lakini leo ndio wanaotuongoza?
Je, umewahi kujitafakalisha ni jinsi gani walivyoamini kuwa bila Nyerere na Tanzania itakwisha lakini bado tunadunda ki mtindo?!
Je, kwa nini usivute subira na ukatumia muda mwingi kujenga matakwa yako kwa wananchi ambao sasa muda wao wa kushika hatamu unawadia (kwa mujibu wa Katiba mpya) ambapo tutakuwa na mandeti ya kuongozwa na tunaemtaka?
Mambo yapo mengi sana ya kuainisha katika kufikia mustakabali wa jambo hili, ila kwa ufupi tu naomba tuingie mwaka mpya kwa mambo mapya ya ujenzi wa chama kwa nguvu mpya.
Naomba Kamati kuu mtakapoingia kwenye kikao chenu hapo kesho kutwa isiwe ni kwa kumkamia Zitto, bali iwe ni jinsi gani ya kumtengeneza upya ahesabike kuwa mtoto ndani ya familia ya CDM.
Nawe Zitto, ukweli ni kuwa umekuwa na mambo mengi sana ambayo kwa macho hata ya upofu yanionesha kwenda kinyume na mipango mikakati ya chama, kama kweli unataka kubaki ndani ya CDM jifanye mdogo nasi tunaokuangalia tutakuinua hata kwa maombi yetu.
Je, nani angejua kuwa ipo siku moja sauti ya wanyonge itasimamam na kusema tunataka hili katika katiba yetu na likasikilizwa?! Je, mbona leo ipo hivo?
HIZI NDIO SALAAM ZANGU ZA MWAKA MPYA.
TAFAKARINI.
hahaaaahaaah CDM hatugombani, Zitto atajadiliwa sanjari na mambo mengine..!Nakipenda sana chama changu za cdm, kwa kuwa hakina mbadala katika kutetea Taifa hili, kimevumilia mengi, kimepita mabonde na milima, wanachama wetu wamemwaga damu katika juhudi hizi za ukombozi wa pili.
hata hivyo ninajua kuwa kamati kuu inakutana wiki end hii na kuwa agenda ni kuwavua uanachama wasaliti, sina kinyongo katika hili, ila NAOMBA KUTOA TAHADHARI, KILA JAMBO NA WAKATI WAKE, HUU NI WAKATI WA KUJADILI KATIBA MPYA NA MUSTAKABALI WA NCHI YETU, WENZENU CCM WANASUBIRI KWA HAMU MLIANZISHE NA ZITO WALICHOCHEE KAMA KAWAIDA NA BAADA YA HAPO WAIKARABATI RASIMU WANAVYOPENDA WENYEWE, MKIMALIZA UGOMVI TAYARI MTAKUWA MMECHELEWA.
KILLERS KISS GUY, kusema kweli you are one sick individual...kilaza asiyeweza kuandika hata sentense moja iliyonyoka kwa lugha ya taifa...words fail me! Hivi katika karne hii watu wa aina yako bado wapo ndani ya Tanzania hii. Eti hata wewe unathubutu kutoa ushauri kwa Chadema, are you kidding me? JF kila siku inazidi kuwa kama kokoro, inazoa kila kitu...duh, kaazi kweli kweli!katika harakati za kuadai haki na kuwakomboa wananchi umakini ni kitu cha msingi hasa katika kufanya maamuzi chadema inapoenda kufanya maamuzi kuhusu akina zitto iwe makini kwani umakini ukikosekana katika maamuzi macccm watatumia mwanya huo kukichafua chadema,,,,,moja kuwafukauza akina zitto italeta au itakuza dhana ya ukanda na ukabila ambayo ni kik kwa ccm hasa kwa wale wavivu wa kufikiri,..mbili akina zitto wanaweza kutumiwa na macccm kukichafua zaidi chadema hivyo dhana ya ukanda, udini na ukabila ukiwa ni moja ya kik kwa ccm.......tatu...chadema kiachane na baadhi ya wachungaji wanaokuja kugombea ubunge kama ni mchungaji aachane na uchungaji kwanza ndo ajiunge na chadema hii itasaidia kuondoa dhana ya udini na kuwafanya ccm wakose kik ya kuongelea na na hivyo kuwafanya waislaam waamini chadema kuwa ndo mkombozi wao.....mwisho taasisi yoyote ile na chadema ikiwemo haiwezi kukosa mawazo kinzani ndani ya chma je kila atakaye pingana na uongozi ni lazima afukuzwe, kwa hili chadema muwe siyo kila mtu mwenye mawazo negative lazima afukuzwe coz hakuna chama chochote cha siasa dunian ambacho hakina upinzani wa ndani,,,,,.ni hayo tu wadau......ni mawazo yangu kwa chama changu chademaaaaaaaaaaaaaaaaa
KILLERS KISS GUY, kusema kweli you are one sick individual...kilaza asiyeweza kuandika hata sentense moja iliyonyoka kwa lugha ya taifa...words fail me! Hivi katika karne hii watu wa aina yako bado wapo ndani ya Tanzania hii. Eti hata wewe unathubutu kutoa ushauri kwa Chadema, are you kidding me? JF kila siku inazidi kuwa kama kokoro, inazoa kila kitu...duh, kaazi kweli kweli!
..mimi wala simtetei Zito ila kinachonishangaza ni 'utaratibu'unaotumika. zito 'anatuhuma' kamati kuu imeshamhukumu kwa kumvua nafasi zake za uongozi na wanafikiria kumvua na uanachama , bila hata kusubiri rufani ya zito au kumpa barua ya kuhitaji utetezi wake chama sasa kinatumia nguvu zake zote ktk kampeni ya kumpaka Zito matope!
sasa ninashangaa mno kuona kila mdau anaongea habari ya 'maccm' badala ya kuuliza hivi:- ni zipi hasa tuhuma zinazomkabili huyu mwanachama? na je, asili ya hizi tuhuma ni wapi, je mwanachama alipoelezwa alijitetea vipi ? na je kulingana na huo utetezi je hukumu iliyotolewa iko sawa? je huyu mwanachama amepewa haki ya kukata rufaa kwenye ngazi inayofuata? je chama kimeweza kumtendea mwanachama 'haki' ya kumpa uhuru wa kujitetea ktk vikao vyote husika kabla hakijamtangaza mwanachama kua mtu hatari?
je kama zito atatoa ushahidi wa uaminifu wake kwa 'chama' siyo kwa watu chama kitaweza kuzunguka nchi nzima kumsafisha?
ni busara tukajua kua tunaongea kuhusu haki za mwanachama yeyote, na kwamba namna tunavyofanya leo itawezekana pia kwa mwanachama mwingine yeyote?
Ni mawazo yako.
Yanaheshimiwa, ila dawa ya jino bovu ni kuling'oa, heri maumivu ya
wakati wa kuling'oa kuliko maumiu endelevu ya kila siku. Hapo kwenye
wachungaji sijakuelewa, ina maana unapendekeza MTU YEYOTE MWENYE WADHIFA
WA KIDINI AWE MCHUNGAJI, PADRE, SHEIKH, KUHANI e.t.c ama!? na kwa nini
CHADEMA tu na sio kwingineko!?
hiyu kijana ataendelea kung'ara kisiasa coz makosa yake yametengenezwa'too mathematically'nt concrete beyond natural reasonable dought.
KILLERS KISS GUY, kusema kweli you are one sick individual...kilaza asiyeweza kuandika hata sentense moja iliyonyoka kwa lugha ya taifa...words fail me! Hivi katika karne hii watu wa aina yako bado wapo ndani ya Tanzania hii. Eti hata wewe unathubutu kutoa ushauri kwa Chadema, are you kidding me? JF kila siku inazidi kuwa kama kokoro, inazoa kila kitu...duh, kaazi kweli kweli!
Hili ndo gojwa lenu kubwa kuamini kila anaemsupport zitto ni ccm kwan zitto hana suport ndani ya chadema tumieni akili mtakuja shituka mmekwisha.
Kama kila anayetoa mawazo ya njia mbadala wa kuushughulikia na kuutatua mtafaruku ulioisibu CHADEMA ataitwa msaliti basi tuna safari ndefu sana kuifikia demokrasia! Pamoja na mtafaruku huu kuwa na mkono wa maCCM, wapo wana CDM wenye uchungu na chama wanaobezwa katika kila watakalolizungumza, hii yote ni kwa faida ya CCM! Yaani CCM baada ya kuzusha varangati wametuachia CHADEMA wenyewe tujimalize!
Wito: Ni lazima busara itumike, si wote wanaotoa maoni ni wa buku 7! Tutafakari na tuchukue hatua. Hata mimi nasema Zitto si tishio kihivyo maadamu tumeshamwelewa na yeye na wenzake wanaweza kabisa rekebishika na wakawa wenye manufaa kwa CHADEMA. Huu ni wakati wa kuimarisha safu za mapambano na si kujifhoofisha kama wanavyotaka maCCM.
Nakipenda sana chama changu za cdm, kwa kuwa hakina mbadala katika kutetea Taifa hili, kimevumilia mengi, kimepita mabonde na milima, wanachama wetu wamemwaga damu katika juhudi hizi za ukombozi wa pili.
hata hivyo ninajua kuwa kamati kuu inakutana wiki end hii na kuwa agenda ni kuwavua uanachama wasaliti, sina kinyongo katika hili, ila NAOMBA KUTOA TAHADHARI, KILA JAMBO NA WAKATI WAKE, HUU NI WAKATI WA KUJADILI KATIBA MPYA NA MUSTAKABALI WA NCHI YETU, WENZENU CCM WANASUBIRI KWA HAMU MLIANZISHE NA ZITO WALICHOCHEE KAMA KAWAIDA NA BAADA YA HAPO WAIKARABATI RASIMU WANAVYOPENDA WENYEWE, MKIMALIZA UGOMVI TAYARI MTAKUWA MMECHELEWA.