CHADEMA ni taasisi lakini linapokuja suala la Dr Slaa ni taasisi nyingine!

sixgates

JF-Expert Member
Mar 19, 2011
3,979
1,662
Habari za usiku wakuu.

Pamekua na mijadala mingi sana hapa jukwaani, mingi inazungumzia mustakabali wa taifa na duru za kisiasa hapa nchini. CDM kimekua ni chama ambacho bila kificho (existing perception) kimekua kikionekana kama ni chama kilichobeba cream ya wasomi,wanaharakati,vijana na bila kificho kimekua kikipokea mapokeo mazur kila kukicha. Nia yangu ni kukizungumzia hiki chama na mahusiano yake na uwepo wa Dr slaa.

Wengi mtakubaliana na mimi katik hii nchi Dr anaonekana kua na nguvu na pia ni big threat kwa chama chake cha zaman CCM na serikali kwa ujumla pengine sababu ni uwezo wake mkubwa katika kushawishi na misimamo yake,lakini kikubwa ni uwezo wa kupata serious information zinazohusu hili taifa(ilifikia mahali hapa JF akaitwa nusu usalama wa taifa)..CCM wamekua wakionesha wazi kutambua nguvu ya Dk na wengine kukiri wazi kabsa mf mh. Samweli sitta aliwahi kusema wazi pale CDM labda Dr ndo tishio,Mbowe anaweza tu kuongoza kumbi za starehe!

Mara nyingi tumekuwa tukiwasikia viongoz mbalimbali wakimzungumzia Dr slaa kama taasisi..mf jana wasira katika kipindi cha dkk 45 itv alisema wazi kua vyama vyote vya upinzani vimewapongeza(CCM) isipokua huyu Dr slaa ambae huwa haoni mazuri. Tafsiri yangu ni kwamba within CCM ni wazi Dr ndie tishio kubwa,within garvoo Dr ndie tishio. Dr slaa amekua na tabia ambayo ni tofauti na watanzania walio wengi, anapenda kushughulisha ubongo wake na anaamini jukumu lake sio kuisifia serikali pale inapotekeleza majukumu yake bali kuisukuma serikali kufanya yale ambayo inapaswa kufanya. Ana discipline anaheshimu maadili ya chama ndio maana vijana ambao wanaojiunga na CDM wenye njaa na tamaa humchukia na kumwita mkoloni(mf habibu mchange),haogopi mtu pale anapopigania haki (ndio maana said mwema anakua makini katika kuzima hoja za slaa).. Ukifuatilia vuguvugu la mabadiliko na vita dhidi ya ufisadi historia itamuheshimu Dr slaa kwa kuipressurelize serikali na kukijenga Chadema!

Haya ni maoni yangu, Dr is a mysterious creature you can add kama yapo unayohisi yanamfanya Slaa awe exceptional katika hili taifa!
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanatumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.
 
Dr Slaa ndiye Aliyeshinda urais 2010,that's why tunamkubali sana watanzania,naamini mpaka sasa fikra zake ndizo zinaongoza nchi na kuwaongoza magamba.Akili yote ya CCM ipo kwa dr hata Nape muda wote anamuwaza Slaa nimemsikia hata jana akimkashfu.but all in all watanzania tumeamua kufanya mapinduzi ya fikra.
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanaumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

Hapa ndio Dr slaa anapokua tofaut na watanzania wengi..Ritz u never think systematically kwani chama si kina mgawanyo wa majukumu?si kina mtunza hazina,kabla pesa haijatoka si zipo taratibu za kutoa fedha..ivi unafikiri kama hayo unayoyasema yangekuwepo chadema prof safari,tundu lissu,zitto kabwe,mnyika na wengine wenye uelewa wangebaki ndan ya hicho chama?? Amsha akili CCM janga njaa usikushushie uwezo wako wa kufikiri
 
Dr Slaa ndiye Aliyeshinda urais 2010,that's why tunamkubali sana watanzania,naamini mpaka sasa fikra zake ndizo zinaongoza nchi na kuwaongoza magamba.Akili yote ya CCM ipo kwa dr hata Nape muda wote anamuwaza Slaa nimemsikia hata jana akimkashfu.but all in all watanzania tumeamua kufanya mapinduzi ya fikra.

Hilo lipo wazi kabisa, ndo maana CCM wanamchukia
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanaumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

taasisi yenu ya sheh ponda vipi .... na mafunzo ya mad- rasta
 
habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanaumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye m4c wanakusanya mbowe na lema.

mzee naona umedandia gari kwa mbele ona sasa imekung'oa meno, pole yako, maana ata raisi wetu japo dhaifu, nnape, wasira wote wanamtaja dr wanataja chadema, we ujifunz tu? Aya endeleeni kuitegemea policcm labda itawakomboa
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanaumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

huchelewi leta kuchafua hewa kwa umbea.Hivi ukubwa wote na exposure ya discussions zote bado unaeneza huu chafu.Kweli unamdhalilisha Mungu kukup ubongo halafu huutumii.Hizo akili za JK zinakusaidia nini?Hembu thibitihsa uliyosema na si kwa umbea.
 
ninapomfikiria mtu ambaye anaweza kusimamia zoezi la kuisafisha nchi hii na laana iloletwa na ccm ilokengeuka na kuleta tena matumaini mapya kwa watz;NI DR. SLAA (rejea 'mahojiano' pale ITV wakati wa kampeni mwaka 2010 n.k)
 
ninapomfikiria mtu ambaye anaweza kusimamia zoezi la kuisafisha nchi hii na laana iloletwa na ccm ilokengeuka na kuleta tena matumaini mapya kwa watz;NI DR. SLAA (rejea 'mahojiano' yake pale ITV wakati wa kampeni mwaka 2010 n.k)
 
Dr Slaa ndiye Aliyeshinda urais 2010,that's why tunamkubali sana watanzania,naamini mpaka sasa fikra zake ndizo zinaongoza nchi na kuwaongoza magamba.Akili yote ya CCM ipo kwa dr hata Nape muda wote anamuwaza Slaa nimemsikia hata jana akimkashfu.but all in all watanzania tumeamua kufanya mapinduzi ya fikra.

Tatizo kubwa la Pro-Chadema JF ni ufahamu wao wa mambo hivi inaingia akilini upate wabunge 23 halafu ushinde kiti cha urais.
 
huchelewi leta kuchafua hewa kwa umbea.Hivi ukubwa wote na exposure ya discussions zote bado unaeneza huu chafu.Kweli unamdhalilisha Mungu kukup ubongo halafu huutumii.Hizo akili za JK zinakusaidia nini?Hembu thibitihsa uliyosema na si kwa umbea.

JF The home of Great Thinkers sio home of Chadema.

Hivi kweli kuna binadamu ambaye anaweza kudhalilisha Mungu.
 
Ni kweli dk slaa ni zaidi ya cdm, naanza kuamini aliyozungumza dk 2010 kwenye kampeni.mfano alizungumzia kushusha bei ya vifaa vya ujenzi, ccm walipuuza. Juzi kinana kaunga mkono. Vilevile alitoa ahadi ya Elimu bure,ccm wakaponda hoja hiyo,juzi lowasa kaunga mkono juu ya kutoa elimu bure.dk slaa na cdm ndio machaguo sahihi mwaka 2015 kwa ajili ya ukombozi wa kweli wa taifa letu!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Tatizo kubwa la Pro-Chadema JF ni ufahamu wao wa mambo hivi inaingia akilini upate wabunge 23 halafu ushinde kiti cha urais.

CCM janja yenu imegunduliwa CHADEMA si kwamba ilipata viti 23.Naamini na nitaendelea kuamini chadema ilishinda viti vingi lakini vilivyotangazwa na Tume ni hivyo unavyojua wewe,Jiulize ni kwa nini matokeo ya urais yalipigwa marufuku kutangazwa vituoni usiku? Jibu ni kwamba Kikwete alipata zero kwenye vituo vingi,ili kuepusha aibu wakapiga marufuku kwa amri ya TISS.mimi nilipita zaidi ya vituo 20 kikwete akijitahidi sana alikuwa anapata kura 7,sasa unataka kutuambia nini?
 
Ni ukweli kwa kila mkweli kuwa hata ndani ya CDM baada tu ya kumteua Dr. Slaa kugombea urais CDM kilitoka katk level moja hadi level ya juu zaidi. Ana kipaji (charisma) cha pekee kabisa. CCM wamecopy na kupaste fikra zake karibu zote. Wakati wote anaongea mambo aliyo na hakika nayo!!! Wanamtajataja kwa kuwa kweli ni tishio!!!
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanatumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

Ritz umesahau kutaja dini
 
Last edited by a moderator:
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanatumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

Hivi wewe ni mtu wa aina gani are you Hamasa or what yaani hueleweki kabisa yaani mtu kama wewe sifahamu akili zako ziko wapi maake kila leo pumba nyingi tu yaani haupo kwa Maslahi ya nchi sifahamu uko upande gani maake kila leo kikiongelewa kitu cha ukweli na cha maana kwa nchi nzima wewe unakuja na Pumba pumba eee bana wewe hebu ngoja usijeacha nipewa ban maake mtu kama wewe hautakiwi kuwepo ndani ya nchi yetu,nakupa warning ole wako
 
Habari za usiku nzuri mkuu, kimsingi Chadema ni taasisi ya watu fulani kutoka maeneo fulani ya nchi yetu. Wanatumia chama cha siasa kama njia ya kufanikisha maswala yao. Jiulize kwa nini pesa zote zinazochangwa na wananchi kwenye M4C wanakusanya Mbowe na Lema.

Mkuu unataka tumpe Kinana atukusanyie sadaka ya ukombozi, badala yake akasafirishie pembe za ndovu?
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom