Ule mkakati unaoratibiwa na John Heche wa kushawishi CHADEMA wasishiriki katika chaguzi pamoja na kujiweka upande wa Magufuli zoezi lililoanzia katika ziara ya Heche Kusini linaelekea kutopata mafanikio baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe kupingana vikali na mawazo hayo ya John Heche.
Mbowe amehoji kuwa Chama kinaoneka hakina ajenda kwa wakati huu kumsifia Magufuli dhidi ya Rais Samia kitawaondolea Popularity ni bora wakaelekeza nguvu zaidi kwenye mambo mengine na si hoja ya kulala mbele na wafuasi wa magufuli ambao kimsingi ni suala la hovyo kwao na halitawapa upepo wowote wa kisiasa.
Hoja ya Mbowe imeungwa mkono na Makamu mwenyekiti wa Chama Tundu Antipass Lissu kwa kumkaripia vikali Godbless Lema na Heche kuwa uwezo wa CHADEMA haupimwi kwenye ajenda ndogondogo au matakwa ya watu binafsi “Lissu aligusia kwa kusema kuwa kama mnaona CHADEMA kushabikia utawala wa Magufuli ni Sawa wakumbuke kuhusu September 7, Wamkumbuke kamanda Mawazo, Wamkumbuke Daniel Luena waangalie miaka mitano nyuma wao kama chama walikuwa katika hali gani?”
Mkakati wa John Heche pamoja na wanachadema wanaoshinda kwenye mitandao walikubaliana kwenda kwa Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe kuhusu kufanya ziara katika mikoa ya kusini na kuwaanda Wananchi kuvuruga ziara kuwapandisha Wananchi morali kusema wanaibiwa kwenye Gesi aliyeanza ziara alikuwa katibu Mkuu wa chama hicho Mnyika pili akafuatia John Heche na kuwaanda Wananchi na Mabango jambo ambalo halikufanikiwa na kwenye Mwenyekiti amewataka wajitathimini.
Mbowe amegusia kusema chama hakipaswi kuwa kama Bondia Mandonga kuwa tunafanya ziara na hakuna jambo lolote linatokea hicho si chama cha siasa! Mbowe amekichukulia chama chake na msemo wa Mandonga kuwa wapo kama hawapo (Akipigwa Sawa na Akipiga Sawa) na kutokuwa na mipango kutakivunja chama vipande si kila mjumbe anaweza kuaamua wafanye nini..
Wana CHADEMA wa Kusini walioweka mabango yaliyoandaliwa na Heche kwa ajili ya ziara hiyo waliyapuuzia na kuhudhuria kwenye mikutano iliyoandaliwa na CCM wenyewe bila kikwazo kwa kumshangilia kiongozi aliyewatembelea.
Shuhuda wa habari hizi ambaye ni mimi mwenyewe nimeshuhudia Mbowe na Lissu wakitoa msimamo mkali kwa Heche na wenzie kuwa CHADEMA imejengwa kwenye misingi ya misimamo hawapaswi kufuata misimamo ya watu wengine ambao wanaweza kuwa mtego kwao.
John Heche alipoulizwa na Wazee wa CHADEMA kuhusu msimamo wake alidai kuwa wanaunga mkono hoja za Bashiru na Polepole sababu wanapata taarifa za ndani za uwepo wa kundi linalomuunga mkono Marehemu linaweza kuwa mtaji wao.
Wazee wa CHADEMA wametoa karipio kwa Vijana na kuwauliza kama hoja wanazozipigia kelele ni za dharura itakuwaje mustakabali wa Chama Chao ni kuonekana wamekosa ajenda kama chama cha Upinzani kuwa Makasuku. Hivyo hawapo tayari kupokea watu kama walivyofanya kwa Lowassa na Sumaye.
Wazee wameenda mbali zaidi na kuuliza juu ya hoja zao kuhusu Maji na Umeme zitawapeleka CHADEMA wanapotaka..? Alihoji Abduel Kileo Mzee Kileo amesisitiza Vijana wajikite zaidi kwenye madai ya msingi na ya muda mrefu na siyo kuwa wadangaji wa hoja.
Wazee wamkumbuka Dkt. Slaa. Katika hali isiyotegemewa Wazee wamemuomba mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe kama kuna uwezekano wa kumrudisha Dkt Wilbroad Slaa basi na wafanye hivi kwasababu wanaimani ni mtu mwenye misimamo katika hoja na si mtu ambaye anarukaruka na ajenda za kutafuta Umaarufu wa kisiasa.
Vijana wahofia CHADEMA kupoteza Mvuto wanafunzi wa vyuo Vikuu mbalimbali wanasema kwa hali iliyopo hivi sasa hairidhishi kuwa CHADEMA ni chama cha upinzani chenye ajenda ya kuchukua nchi, Vijana wahitimu wa vyuo vikuu mbalimbali wanasema zamani ilikuwa ni fahari kujiunga na CHADEMA lakini kwasasa hakuna ufahari huo kutokana na Chama hicho kukosa ajenda makini za kuwasemea Wananchi na wamekuwa watu wa kukaa mitandaoni na kudandia ajenda pamoja na kutengeneza akaunti Feki zenye taarifa za kugushi.
Kijana aliyejitambulisha kwa jina BIG muhitumu wa shahada ya istilahi ya kompyuta amesema kwa mfano ukiangalia katika mtandao wa Twitter kuna akaunti ambazo zimekuwa zikihisiwa ni za watu wa CHADEMA zenye kuwa na taarifa nyingi za uongo na story za kubumba. Big ameenda mbali kwa kusema kuwa Vijana hivi sasa wana taarifa nyingi kama mtu anataka kuleta taarifa ambazo ni za siri basi wahakikishe taarifa hizi zinakuwa genuine na si chai za mitaani, hivyo CHADEMA hawawezi kujenga ushawishi kwa namna hii watajikuta mtandaoni wanapoteza pamoja na mitaani wanakosa watu.
Baadhi ya makamanda wakilalamika KUSALITIWA na wenzao ambapo wanasema kuwa kuna Vijana wenzao hawapaswi kuwa kwenye harakati zao kwa kipindi hiki kwasababu hawawezi kupamba kwenye mambo waliyotaita ya msingi.
Vijana ambao wameitwa ni wasaliti wameibuka na kuhoji kuwa kama sisi ni wasaliti Jiulizeni hiki Chama chenye viongozi wanaodangia hoja ni chama…? Kwanza Tunalia ni Viongozi wetu walitudanganya kuhusu Wabunge 19 ila hali mmoja wa Viongozi mke wake ni Mbunge miongoni mwa Wabunge 19 na ni Naibu Katibu Mkuu sasa hapo kuna Chama kweli alihoji mmoja wa kijana ambaye hakutaka jina lake liwekwe mitandaoni.
Vijana wamesema kuwa wataendelea kumuhitaji Mbowe kama mwenyekiti kwasababu hawauoni uhai wa chama kwa mwingine yoyote, kuna Tetesi kuwa John Heche amejipanga kugombea nafasi ya Mwenyekiti katika uchaguzi Mkuu ujao wa chama hicho.
Mbowe amehoji kuwa Chama kinaoneka hakina ajenda kwa wakati huu kumsifia Magufuli dhidi ya Rais Samia kitawaondolea Popularity ni bora wakaelekeza nguvu zaidi kwenye mambo mengine na si hoja ya kulala mbele na wafuasi wa magufuli ambao kimsingi ni suala la hovyo kwao na halitawapa upepo wowote wa kisiasa.
Hoja ya Mbowe imeungwa mkono na Makamu mwenyekiti wa Chama Tundu Antipass Lissu kwa kumkaripia vikali Godbless Lema na Heche kuwa uwezo wa CHADEMA haupimwi kwenye ajenda ndogondogo au matakwa ya watu binafsi “Lissu aligusia kwa kusema kuwa kama mnaona CHADEMA kushabikia utawala wa Magufuli ni Sawa wakumbuke kuhusu September 7, Wamkumbuke kamanda Mawazo, Wamkumbuke Daniel Luena waangalie miaka mitano nyuma wao kama chama walikuwa katika hali gani?”
Mkakati wa John Heche pamoja na wanachadema wanaoshinda kwenye mitandao walikubaliana kwenda kwa Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe kuhusu kufanya ziara katika mikoa ya kusini na kuwaanda Wananchi kuvuruga ziara kuwapandisha Wananchi morali kusema wanaibiwa kwenye Gesi aliyeanza ziara alikuwa katibu Mkuu wa chama hicho Mnyika pili akafuatia John Heche na kuwaanda Wananchi na Mabango jambo ambalo halikufanikiwa na kwenye Mwenyekiti amewataka wajitathimini.
Mbowe amegusia kusema chama hakipaswi kuwa kama Bondia Mandonga kuwa tunafanya ziara na hakuna jambo lolote linatokea hicho si chama cha siasa! Mbowe amekichukulia chama chake na msemo wa Mandonga kuwa wapo kama hawapo (Akipigwa Sawa na Akipiga Sawa) na kutokuwa na mipango kutakivunja chama vipande si kila mjumbe anaweza kuaamua wafanye nini..
Wana CHADEMA wa Kusini walioweka mabango yaliyoandaliwa na Heche kwa ajili ya ziara hiyo waliyapuuzia na kuhudhuria kwenye mikutano iliyoandaliwa na CCM wenyewe bila kikwazo kwa kumshangilia kiongozi aliyewatembelea.
Shuhuda wa habari hizi ambaye ni mimi mwenyewe nimeshuhudia Mbowe na Lissu wakitoa msimamo mkali kwa Heche na wenzie kuwa CHADEMA imejengwa kwenye misingi ya misimamo hawapaswi kufuata misimamo ya watu wengine ambao wanaweza kuwa mtego kwao.
John Heche alipoulizwa na Wazee wa CHADEMA kuhusu msimamo wake alidai kuwa wanaunga mkono hoja za Bashiru na Polepole sababu wanapata taarifa za ndani za uwepo wa kundi linalomuunga mkono Marehemu linaweza kuwa mtaji wao.
Wazee wa CHADEMA wametoa karipio kwa Vijana na kuwauliza kama hoja wanazozipigia kelele ni za dharura itakuwaje mustakabali wa Chama Chao ni kuonekana wamekosa ajenda kama chama cha Upinzani kuwa Makasuku. Hivyo hawapo tayari kupokea watu kama walivyofanya kwa Lowassa na Sumaye.
Wazee wameenda mbali zaidi na kuuliza juu ya hoja zao kuhusu Maji na Umeme zitawapeleka CHADEMA wanapotaka..? Alihoji Abduel Kileo Mzee Kileo amesisitiza Vijana wajikite zaidi kwenye madai ya msingi na ya muda mrefu na siyo kuwa wadangaji wa hoja.
Wazee wamkumbuka Dkt. Slaa. Katika hali isiyotegemewa Wazee wamemuomba mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe kama kuna uwezekano wa kumrudisha Dkt Wilbroad Slaa basi na wafanye hivi kwasababu wanaimani ni mtu mwenye misimamo katika hoja na si mtu ambaye anarukaruka na ajenda za kutafuta Umaarufu wa kisiasa.
Vijana wahofia CHADEMA kupoteza Mvuto wanafunzi wa vyuo Vikuu mbalimbali wanasema kwa hali iliyopo hivi sasa hairidhishi kuwa CHADEMA ni chama cha upinzani chenye ajenda ya kuchukua nchi, Vijana wahitimu wa vyuo vikuu mbalimbali wanasema zamani ilikuwa ni fahari kujiunga na CHADEMA lakini kwasasa hakuna ufahari huo kutokana na Chama hicho kukosa ajenda makini za kuwasemea Wananchi na wamekuwa watu wa kukaa mitandaoni na kudandia ajenda pamoja na kutengeneza akaunti Feki zenye taarifa za kugushi.
Kijana aliyejitambulisha kwa jina BIG muhitumu wa shahada ya istilahi ya kompyuta amesema kwa mfano ukiangalia katika mtandao wa Twitter kuna akaunti ambazo zimekuwa zikihisiwa ni za watu wa CHADEMA zenye kuwa na taarifa nyingi za uongo na story za kubumba. Big ameenda mbali kwa kusema kuwa Vijana hivi sasa wana taarifa nyingi kama mtu anataka kuleta taarifa ambazo ni za siri basi wahakikishe taarifa hizi zinakuwa genuine na si chai za mitaani, hivyo CHADEMA hawawezi kujenga ushawishi kwa namna hii watajikuta mtandaoni wanapoteza pamoja na mitaani wanakosa watu.
Baadhi ya makamanda wakilalamika KUSALITIWA na wenzao ambapo wanasema kuwa kuna Vijana wenzao hawapaswi kuwa kwenye harakati zao kwa kipindi hiki kwasababu hawawezi kupamba kwenye mambo waliyotaita ya msingi.
Vijana ambao wameitwa ni wasaliti wameibuka na kuhoji kuwa kama sisi ni wasaliti Jiulizeni hiki Chama chenye viongozi wanaodangia hoja ni chama…? Kwanza Tunalia ni Viongozi wetu walitudanganya kuhusu Wabunge 19 ila hali mmoja wa Viongozi mke wake ni Mbunge miongoni mwa Wabunge 19 na ni Naibu Katibu Mkuu sasa hapo kuna Chama kweli alihoji mmoja wa kijana ambaye hakutaka jina lake liwekwe mitandaoni.
Vijana wamesema kuwa wataendelea kumuhitaji Mbowe kama mwenyekiti kwasababu hawauoni uhai wa chama kwa mwingine yoyote, kuna Tetesi kuwa John Heche amejipanga kugombea nafasi ya Mwenyekiti katika uchaguzi Mkuu ujao wa chama hicho.