CHADEMA ni chachu tu, haiwezi kuikomboa Tanzania

Bayana

JF-Expert Member
Sep 25, 2012
433
69
Kama kuna jambo ambalo ni dhahiri kwa sasa kwa Tanzania, ni hamu ya watanzania kupata mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi. Lakini pengo kubwa linaloonekana ni kukosekana kwa nguvu na sauti moja ambayo itaungwa mkono na watanzania kutoka makundi yote ya kijamii bila kujali makabila yao, dini zao, rangi zao, jinsia n.k.

Wakati ikionekana ni wazi kuwa CCM ni chama ambacho watanzania wangependa kikae chonjo ili kupisha mabadiliko na kujikarabati upya, hakuna chama cha upinzani ambacho kinawaunganisha watanzania kufikia malengo hayo kwa mujibu wa tofauti zao. Hii ni kutokana na kasoro mbali mbali zikiwemo za kuzuwa na nyingine ni za kweli ambazo kwa kiasi kikubwa zimeweza kuaminiwa na baadhi ya wananchi walio wengi.

Vyama vingi viliibuka na kufifia mfano TLP na NCCR kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubinafsi wa viongozi waliovianzisha, migogoro ya kimaslahi na mapandikizi kutoka chama tawala. Mfano wa udhaifu katika vyama vya upinzania hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:

1) CHADEMA
Kwa sasa ndicho chama ambacho kinaonekana kuwa na nguvu kubwa kama chama kikuu cha upinzani.

Hata hivyo kinakabiliwa na shutuma zifuatazo:
i)Ukabila na ukanda
ii)Ukosefu wa maadili kwa watendaji wake wakuu
iii)Kutokuaminiana kati ya viongozi wake wakuu ikidhaniwa kwamba baadhi ni mapandikizi kutoka chama tawala.
iv)Dhana ya CHADEMA kwamba vyama vyote vya upinzani ni mapandikizi ya CCM, hivyo kukataa ushirikiano na vyama vingine.
v)Udini

2)CUF
Ni chama ambacho ni cha pili cha upinzani baada ya CHADEMA. Hata hivyo kinashutumiwa kwa mambo yafuatayo:
i) Udini
ii) Usultani wa viongozi wakuu kuhodhi madaraka na kutokuwapisha wengine kukamata nafasi kubwa za uongozi
iii) Kuwa na nguvu upande mmoja wa muungano

3) NCCR: Huko mwanzo kilishawahi kuhusishwa na ukanda na ukabila. Hata hivyo kwa sasa madai haya hayasikiki kwa vile nguvu zake zimepungua kama ilivyo TLP.
4) Vyama vingine vilivyobaki vinachukuliwa kama NGOs za kujipatia mapato kwa waliovianzisha.
Hizi shutma iwe zina uhakika au ni za kukisia, tukubali kuwa ni pengo kwa ukombozi wa kweli wa Tanzania na ni ngumu kuziondoa kwa sasa kwa vile jamii imeshagawanywa kwa misingi hiyo.

HITIMISHO:

Ili kukata kiu ya mabadiliko ya watanzania, ni vyema wasomi mbalimbali maarufu wanaokubalika wasiohusika na kashfa hizo hapo juu kuungana na kuanzisha chama ambacho kitakubalika na watanzania walio wengi. Vugu vugu hili la mabadiliko ya kweli litafaa zaidi kama litaanzia kwenye taasisi za elimu ya juu.

Tukifika hapo TZ in 2015 ni vifijo na nderemo! Kinyume chake, tusahau kuingóa CCM madarakani kutokana na advantage ya mgawanyiko kutokana na tofauti tajwa hapo juu. Weka ushabiki wa chama pembeni unapochangia hii thread! Mihemko ikikuzidi, fanya kama vile hujaiona hii thread!
 
Tuhuma za CHADEMA kuwa kina udini na ukabila ni nadharia tu zilizopandikizwa na CCM. Ni za kufikirika tu. Hazipo. Pia conclusion yako ni irrelevant hasa unaposema kianzishwe chama kipya na wasomi wa elimu ya juu. Kumbuka uchaguzi wa 2015 upo karibu sana kisiasa. Chama kinatakiwa kipange sera zake, kisimike viongozi wake mpaka vijijini, kieneze itikadi zake, etc. Haiwezekani kwa sasa. Pia hakuna ushahidi wowote wa kisiasa wala wa kisayansi kwamba chama kilichonzishwa na wasomi au wanazuoni ndicho hufanikiwa kuchukua dola. Mimi ningependa watanzania waachane na propaganda chafu za CCM kwa wapinzani na badala yake waunganishe nguvu zao kwa pamoja na waki-support chama cha upinzani chenye bright vision na mission kuhusiana na nchi hii.
 
We mleta mada danganya wajinga lakini kwa watu wenye kuona mbali watajua kwamba wewe ni mmoja wawaeneza propanganda za CCM za kusema chama fulani ni cha kidini au kabila fulani. Hiyo propaganda ya udini umeiingiza kijanja lakini nimekushitukia. Tumia mbinu nyingine
 
Kama kuna jambo ambalo ni dhahiri kwa sasa kwa Tanzania, ni hamu ya watanzania kupata mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi. Lakini pengo kubwa linaloonekana ni kukosekana kwa nguvu na sauti moja ambayo itaungwa mkono na watanzania kutoka makundi yote ya kijamii bila kujali makabila yao, dini zao, rangi zao, jinsia n.k.
Wakati ikionekana ni wazi kuwa CCM ni chama ambacho watanzania wangependa kikae chonjo ili kupisha mabadiliko na kujikarabati upya, hakuna chama cha upinzani ambacho kinawaunganisha watanzania kufikia malengo hayo kwa mujibu wa tofauti zao.
Hii ni kutokana na kasoro mbali mbali zikiwemo za kuzuwa na nyingine ni za kweli ambazo kwa kiasi kikubwa zimeweza kuaminiwa na baadhi ya wananchi walio wengi.
Vyama vingi viliibuka na kufifia mfano TLP na NCCR kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubinafsi wa viongozi waliovianzisha, migogoro ya kimaslahi na mapandikizi kutoka chama tawala.
Mfano wa udhaifu katika vyama vya upinzania hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:

1) CHADEMA
Kwa sasa ndicho chama ambacho kinaonekana kuwa na nguvu kubwa kama chama kikuu cha upinzani.

Hata hivyo kinakabiliwa na shutuma zifuatazo:
i)Ukabila na ukanda
ii)Ukosefu wa maadili kwa watendaji wake wakuu
iii)Kutokuaminiana kati ya viongozi wake wakuu ikidhaniwa kwamba baadhi ni mapandikizi kutoka chama tawala.
iv)Dhana ya CHADEMA kwamba vyama vyote vya upinzani ni mapandikizi ya CCM, hivyo kukataa ushirikiano na vyama vingine.
v)Udini

2)CUF
Ni chama ambacho ni cha pili cha upinzani baada ya CHADEMA. Hata hivyo kinashutumiwa kwa mambo yafuatayo:
i) Udini
ii) Usultani wa viongozi wakuu kuhodhi madaraka na kutokuwapisha wengine kukamata nafasi kubwa za uongozi
iii) Kuwa na nguvu upande mmoja wa muungano

3) NCCR: Huko mwanzo kilishawahi kuhusishwa na ukanda na ukabila. Hata hivyo kwa sasa madai haya hayasikiki kwa vile nguvu zake zimepungua kama ilivyo TLP.
4) Vyama vingine vilivyobaki vinachukuliwa kama NGOs za kujipatia mapato kwa waliovianzisha.
Hizi shutma iwe zina uhakika au ni za kukisia, tukubali kuwa ni pengo kwa ukombozi wa kweli wa Tanzania na ni ngumu kuziondoa kwa sasa kwa vile jamii imeshagawanywa kwa misingi hiyo.

HITIMISHO:

Ili kukata kiu ya mabadiliko ya watanzania, ni vyema wasomi mbalimbali maarufu wanaokubalika wasiohusika na kashfa hizo hapo juu kuungana na kuanzisha chama ambacho kitakubalika na watanzania walio wengi.
Vugu vugu hili la mabadiliko ya kweli litafaa zaidi kama litaanzia kwenye taasisi za elimu ya juu.
Tukifika hapo TZ in 2015 ni vifijo na nderemo! Kinyume chake, tusahau kuingóa CCM madarakani kutokana na advantage ya mgawanyiko kutokana na tofauti tajwa hapo juu.
Weka ushabiki wa chama pembeni unapochangia hii thread! Mihemko ikikuzidi, fanya kama vile hujaiona hii thread!


UKOMBOZI toka kwa NANI?
Kama kawaida ya Wasio jua DEMOKRASIA Unahusisha CHAMA cha CHADEMA na UDINI; UHAKIKA wako UKO WAPI wakati ina Wabunge; Madiwani wa DINI MBALIMBALI?

Dr. Slaa; Mbowe; Zitto - Hao wote watatu wako DINI tofauti na Dr. Slaa na Mbowe wako Madhehebu Mbalimbali
Sasa UDINI wako UNAUTOA WAPI?

Kwasababu inaonyesha UNAONGEA kama Rais KIKWETE alipokuwa anagombea URAIS 2010; Alihusisha CHADEMA na UDINI na UKABILA lakini hakuwa na UTHIBITISHO - Na Sasa yanamtokea ya UAMSHO na SHEIKH PONDA

Kama Unaweka HOJA ni bora UWE NA UTHIBITISHO wa Kauli zako Unazozitoa; TUSITAFUTE UMASHUHURI
 
Tuhuma za CHADEMA kuwa kina udini na ukabila ni nadharia tu zilizopandikizwa na CCM. Ni za kufikirika tu. Hazipo. Pia conclusion yako ni irrelevant hasa unaposema kianzishwe chama kipya na wasomi wa elimu ya juu. Kumbuka uchaguzi wa 2015 upo karibu sana kisiasa. Chama kinatakiwa kipange sera zake, kisimike viongozi wake mpaka vijijini, kieneze itikadi zake, etc. Haiwezekani kwa sasa. Pia hakuna ushahidi wowote wa kisiasa wala wa kisayansi kwamba chama kilichonzishwa na wasomi au wanazuoni ndicho hufanikiwa kuchukua dola. Mimi ningependa watanzania waachane na propaganda chafu za CCM kwa wapinzani na badala yake waunganishe nguvu zao kwa pamoja na waki-support chama cha upinzani chenye bright vision na mission kuhusiana na nchi hii.

Mleta mada nae ni mwizi ndani ya serikali ndo maana anaeneza propaganda za udini, ukabila na ukanda. Achana nae
 
Tuhuma za CHADEMA kuwa kina udini na ukabila ni nadharia tu zilizopandikizwa na CCM. Ni za kufikirika tu. Hazipo. Pia conclusion yako ni irrelevant hasa unaposema kianzishwe chama kipya na wasomi wa elimu ya juu. Kumbuka uchaguzi wa 2015 upo karibu sana kisiasa. Chama kinatakiwa kipange sera zake, kisimike viongozi wake mpaka vijijini, kieneze itikadi zake, etc. Haiwezekani kwa sasa. Pia hakuna ushahidi wowote wa kisiasa wala wa kisayansi kwamba chama kilichonzishwa na wasomi au wanazuoni ndicho hufanikiwa kuchukua dola. Mimi ningependa watanzania waachane na propaganda chafu za CCM kwa wapinzani na badala yake waunganishe nguvu zao kwa pamoja na waki-support chama cha upinzani chenye bright vision na mission kuhusiana na nchi hii.

Kwanza huyo jamaa mimi namuona yeye ndiyo mbaguzi kwa nini aseme kianzishwe chama cha wasomi ina maana wasio wasomi hawana nafasi ya kuchangia mabadiliko wakiwa wanachama??? Nadhani hata uelewa wake una kasoro na kama kapita shule basi alinunua mitihani kwa kutumia pesa ya ada ya shule au pocket money alopewa na wazazi wake shame on him/her
 
Tuhuma za CHADEMA kuwa kina udini na ukabila ni nadharia tu zilizopandikizwa na CCM. Ni za kufikirika tu. Hazipo. Pia conclusion yako ni irrelevant hasa unaposema kianzishwe chama kipya na wasomi wa elimu ya juu. Kumbuka uchaguzi wa 2015 upo karibu sana kisiasa. Chama kinatakiwa kipange sera zake, kisimike viongozi wake mpaka vijijini, kieneze itikadi zake, etc. Haiwezekani kwa sasa. Pia hakuna ushahidi wowote wa kisiasa wala wa kisayansi kwamba chama kilichonzishwa na wasomi au wanazuoni ndicho hufanikiwa kuchukua dola. Mimi ningependa watanzania waachane na propaganda chafu za CCM kwa wapinzani na badala yake waunganishe nguvu zao kwa pamoja na waki-support chama cha upinzani chenye bright vision na mission kuhusiana na nchi hii.

Hakuna Bright vision na mission kama HAKI SAWA KWA WOTE! na mahala pake ni CUF!
 
Mtoa Uzi naona umelewa kimba la udini la 2010 la kikwete. endelea hivyo hivyo maana ndo upeo wa akili yako ulivyo.
 


UKOMBOZI toka kwa NANI?
Kama kawaida ya Wasio jua DEMOKRASIA Unahusisha CHAMA cha CHADEMA na UDINI; UHAKIKA wako UKO WAPI wakati ina Wabunge; Madiwani wa DINI MBALIMBALI?

Dr. Slaa; Mbowe; Zitto - Hao wote watatu wako DINI tofauti na Dr. Slaa na Mbowe wako Madhehebu Mbalimbali
Sasa UDINI wako UNAUTOA WAPI?

Kwasababu inaonyesha UNAONGEA kama Rais KIKWETE alipokuwa anagombea URAIS 2010; Alihusisha CHADEMA na UDINI na UKABILA lakini hakuwa na UTHIBITISHO - Na Sasa yanamtokea ya UAMSHO na SHEIKH PONDA

Kama Unaweka HOJA ni bora UWE NA UTHIBITISHO wa Kauli zako Unazozitoa; TUSITAFUTE UMASHUHURI

Slaa ni Katibu Mkuu wa CDM, Mke wake ni mbunge mteule!, hawara ake anataka kugombea ubunge Ubungo na ni kada wa cdm!, Mtei ni mwanzilishi na mlezi wa CDM, Mkwe wake Mbowe ni Mwenyekiti wa chama!, Ndesamburo ni muasisi wa CDM na Mbunge wa M.Mjini, mtoto wake ni mbunge wa CDM!

Sasa ukiacha mbali udini uliopo CDM kwa Mapadre na Maaskofu kuipigia debe uchaguzi 2010! kumbuka Askofu Kakobe!
Ukanda na ukabila ndio kama huo wa CDM kuongozwa na familia za kichagga!
 
Anzisha chama chako basi ukomboe nchi

Mtoa mada anawashwa washwa nini?katibu wetu angekuwa sio msomi angepata u dr?prof safari,lissu,kitila na wengineo weeeengi,kajipange tena propaganda zako hapa sio mahali pake,gamba mkubwa wewe.
 
TAHADHARI

kuna watu wameona sasa ni dili kujipatia fedha kupitia mapambano dhidi ya Chadema (DEMOKRASI)!!! Tutafakari kwa kina NA kwa tahadhari kubwa matumizi ya fedha za Serikali kwa kisingizio cha kupambana na CHADEMA!!! Kuna wizi mpya umezuka wa kisingizio cha kupambana na chadema kumbe ndo watu wanakwapua!!!
 
Mleta mada nae ni mwizi ndani ya serikali ndo maana anaeneza propaganda za udini, ukabila na ukanda. Achana nae

Kuna points kama tano hivi ambazo ni shutma dhidi ya CDM fafanua moja moja ili upewe base ya moja baada ya nyingine.
 
Mtoa mada anawashwa washwa nini?katibu wetu angekuwa sio msomi angepata u dr?prof safari,lissu,kitila na wengineo weeeengi,kajipange tena propaganda zako hapa sio mahali pake,gamba mkubwa wewe.

I dont want to be personal. Katibu wenu sawa ni msomi ni DR wa nini na ameipata wapi? Maana kusema kweli sijui. Mbowe ana elimu gani? Hata hivyo bado sio tatizo kubwa sana, tatizo ni hizo propaganda nyingine ambazo walio wengi wanaziamini na zinaathiri ukuaji wa chama!
 
mkuu mi nashukuru kwanza kwa kutambua chadema kuwa ni chachu, lakini usisahau kuwa chachu kidogo tu huchachusha donge nzima, mabadiliko ni lazima na yataanza na wewe endapo utachukua hatua, kujiandikisha, na kupiga kura yenye lengo la mabadiliko, nina hakika watanzania walio wengi hawanufaiki na rasilimali ya nchi hii, lakini watanzania walio wengi wanadanganyika na furaha ya siku moja ambayo itamgarimu miaka mitano.Tukatae tufanye mabadiliko, tuone, tusilalamike kura yako inauwezo wa kukukomboa kama utamaanisha, chukua hatua fanya maamuzi magumu hatakama umekula pesa za waliozoea kununua haki, lakini kura ni siri yako, na hiyo pesa haina lawama maana ni kodi yako. na jasho lako, kula ukishiba amua, utaniambi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom