Uchaguzi 2020 CHADEMA nawakumbusha sheria ya mita 200 bado ipo na haijabadilishwa!

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
51,961
41,438
Wasalaam!

Wanajamvi wasalaam

Bila shaka makamanda wa JF hasa wachadema ambao huu ni uwanja wao wa nyumbani na ni kama kituo chao cha kupigia kura!

Ni ukweli ulio wazi CHADEMA watashindwa uchaguzi kama ilivyo kawaida yao kwani CHADEMA hawajawai kujiandaa kushinda uchaguzi wa Tanzania hasa kwa ngazi ya Urais!

CHADEMA hasa mgombea wao wa Urais wamekuwa wakiwadanganya wafuasi wao kuwa watabaki vituoni kulinda kura wakati wanajua fika ni kinyume na sheria.

Sheria inawataka watu wote baada ya kupiga kura wanatakiwa kuondoka kituoni au kukaa nje ya kituo kwa mita 200 sawa na kukaa mbali wa viwanja viwili vya mpira wa miguu!

Hivyo wafuasi wa CHADEMA napenda kuwakumbusha kuwa mtatakiwa kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura!

CHADEMA mnatakiwa kuweka mawakala makini na wanaojua kusoma na kuandika bila kusahau kuhesabu!

Wasalaam wanajamvi
 
Bora umewakumbusha na pia mwaka 2015 kuna mdau alikwenda mahakamani akitaka mahakama itoe tafsiri sahihi juu ya kulinda kura. Chadema kama mnajidanganya mtakaa vituoni kulinda kura huo utahesabika kama KOSA LA KIUHALIFU
 
Mapoti wapo upande wa haki this time, na wale watakaozingua tutawafunza adabu, nguvu ya umma haijawahi kushindwa
 
Bora umewakumbusha na pia mwaka 2015 kuna mdau alikwenda mahakamani akitaka mahakama itoe tafsiri sahihi juu ya kulinda kura. Chadema kama mnajidanganya mtakaa vituoni kulinda kura huo utahesabika kama KOSA LA KIUHALIFU

Hakika
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom