CHADEMA nao wasaka Spika

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).
KURUGENZI YA BUNGE NA HALIMASHAURI.
TAMKO KUHUSU ZOEZI LA UCHUKUAJI WA FOMU ZA NAFASI YA SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

Itakumbukwa kuwa kuna mchakato wa kumpata Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unaendelea ndani ya vyama vya Siasa .

CHADEMA tunapenda kuutangazia Umma wa wanachama wa CHADEMA kuwa mchakato huo umeanza rasmi leo ndani ya chama na kila mwanachama wa CHADEMA ambaye anasifa zinazostahili anatakiwa kuchukua fomu kwenye ofisi ya Katibu Mkuu wa chama .

Masharti kwa wagombea ni kama ifuatavyo;

1. Awe ni Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba na sheria za Bunge la Jamhuri ya Muungano.
3. Awe mwanachama wa CHADEMA .
4. Awe mtu mwenye mwenendo na maadili mema ndani ya jamii .

Gharama ya fomu hizo ni shilingi elfu hamsini tuu.

Zoezi la uchukuaji fomu linaendelea na mwisho wa kurejesha fomu hizo ni siku ya Jumatano tarehe 10/11/2010 saa kumi kamili jioni ofisi ya Katibu Mkuu.

Nawatakia kila la kheri katika zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo.

Imetolewa na ,


John Mrema .
Mkurugenzi wa Bunge na Halimashauri
 
Hakuna haja ya kuwa skeptical na machaguo ya ccm tunayoyasikia na kucomment huku ndani kila dakika, apatikane mtu mwenye vigezo toka Chadema, agombee, you never know!...wabunge wana siri moyoni!
 
Hakuna haja ya kuwa skeptical na machaguo ya ccm tunayoyasikia na kucomment huku ndani kila dakika, apatikane mtu mwenye vigezo toka Chadema, agombee, you never know!...wabunge wana siri moyoni!

Hili nalo neno mkuu
 
Spika si lazima awe mbunge (ila anatakiwa awe mtu mwenye sifa zinazostahiki )
 
kwa kifupi anatakiwa awe na sifa za kugombea ubunge. Hata kama si mbunge anaweza kugombea u-spika
 

Masharti kwa wagombea ni kama ifuatavyo;

1. Awe ni Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba na sheria za Bunge la Jamhuri ya Muungano.
3. Awe mwanachama wa CHADEMA .
4. Awe mtu mwenye mwenendo na maadili mema ndani ya jamii .

Hapo kwenye red, kumbe CHENGE angekuwa mwanachama wa CHADEMA hata tusingesumbuka kuumiza vichwa manake mfumo wa chama chetu wenyewe ungemtema nje mapemaaaaaa! Lakini huko Chama Cha Mafisadi anaweza kupenya!
 
Haaa jamani PCCB wamesema chenge hahusiki na mambo ya RADAR..teh teh TZ bana ni fulu komedi
 
Sioni namna yeyote kwa asiye wa ccm kushinda. Kama wapiga kura ni wabunge ambao zaidi ya nusu ni ccm unatakiwa kujua kama pi aka 22/7 kuwa CCM watamchagua CCM tu na ndo atashinda.

Wengine wataweka changamoto na kuonyesha demokrasia imechukua mkondo wake lakini haiwezi kubadili hali halisi kwa mazingira ya sasa. Tena wanakura za aina 2 za wazi na siri, wakiona mambo yanaweza haribika hupendekeza kura ya wazi ili kushinikiza ushindi kwao.
 
Tz aka Bongo, Full Usanii, kama ccm walivyo. Sintashangaa chenge kuwa spika kwa manufaa ya mafisadi
 
Chadema mnafaa mpelekwe kwenye hospitali ya wagonjwa wa akili ,madaktari wa magonjwa ya akili wanasema kila mtu ana matatizo ya akili kwa asilimia fulani nafikiri waChadema asilimia yao inatisha.
 
Sioni namna yeyote kwa asiye wa ccm kushinda. Kama wapiga kura ni wabunge ambao zaidi ya nusu ni ccm unatakiwa kujua kama pi aka 22/7 kuwa CCM watamchagua CCM tu na ndo atashinda.

Lakini inategemea pia CCM watampendekeza nani. kama wakifanya kosa tu, kuna wabunge wengi wa CCM ambao wako tayari kumpigia mtu mwingine kama chaguo la chama chao litakuwa bovu
 
Lakini inategemea pia CCM watampendekeza nani. kama wakifanya kosa tu, kuna wabunge wengi wa CCM ambao wako tayari kumpigia mtu mwingine kama chaguo la chama chao litakuwa bovu

Sijui tumpendekeze dr Slaa achukue fomu?
 
Sioni namna yeyote kwa asiye wa ccm kushinda. Kama wapiga kura ni wabunge ambao zaidi ya nusu ni ccm unatakiwa kujua kama pi aka 22/7 kuwa CCM watamchagua CCM tu na ndo atashinda.

Wengine wataweka changamoto na kuonyesha demokrasia imechukua mkondo wake lakini haiwezi kubadili hali halisi kwa mazingira ya sasa. Tena wanakura za aina 2 za wazi na siri, wakiona mambo yanaweza haribika hupendekeza kura ya wazi ili kushinikiza ushindi kwao.


Mkuu hizi kura hupigwa kwa siri, kwa hiyo lolote laweza kutokea. Na kwa bahati mbaya hapa hakuna uwezo wa mtu kuchakachua
 
Chadema mnafaa mpelekwe kwenye hospitali ya wagonjwa wa akili ,madaktari wa magonjwa ya akili wanasema kila mtu ana matatizo ya akili kwa asilimia fulani nafikiri waChadema asilimia yao inatisha.

mwiba a.k.a magugu magumu umeona ee!? Yan IQ ya chadema inatisha. Yan wako juu kinoma,ata yule mgonjwa wenu analitambua ndo mana kapokonya ushindi ili chadema wasijempeleka jela. Yan kila mtu wa ccm anaiogopa IQ ya chadema,naisi uwiano ni 89:18 ya ccm. IQ yao noma!
 
Takururu na chenge bdo sijawaelewa sijawaelewa kabisaaa!!!
hizo sifa ni zipi tumwagieni basi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom