CHADEMA na dhana ya usaliti na pandikizi katika chaguzi za ndani

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Wascotland wana methali inayosema"Give a Dog an ill Name, and he'll soon be hanged’’.

Hii methali imekuwa ikitumiwa sana wakati wa harakati za uchaguzi ndani ya CHADEMA kwa wagombea ambao malengo na mitazamo yao inapingana na uongozi wa juu wa chama.

Mwanachama ambaye anaonekana kuwa na malengo na mitazamo tofauti ndani ya CHADEMA amekuwa akipewa na viongozi wa juu majina ya PANDIKIZI au MSALITI huku wakishirikiana na kundi walilounda halafu baadaye wanachama wengine wanaaminishwa kama ni pandikizi au msaliti ili wamshughulikie.

Tuliona mwaka 2013/14 ilivyokuwa wakati wa harakati za uchaguzi ndani ya CHADEMA ambapo Zitto Kabwe alionyesha nia ya kutaka kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa ambapo alipewa jina la PANDIKIZI na MSALITI na akashughulikiwa kweli kweli mpaka akaamua kukimbia kabla hajafukuzwa rasmi.

Kwenye maandalizi ya uchaguzi ndani ya CHADEMA tuliambiwa CHADEMA inamuhitaji sana Mbowe wakati huo kwa sababu chama kiko kwenye mafanikio makubwa ambapo kinaenda kitachukua dola kwenye Uchaguzi Mkuu 2015. Tukaambiwa Zitto ni PANDIKIZI na MSALITI kwa sababu ametumwa na CCM ili kuhakikisha CHADEMA haishiki dola mwaka 2015.

Kama ilivyo methali, Zitto alinyongwa kisiasa mpaka kuimbia CHADEMA na mengine ni historia!

Kwa njia ileile iliyotumika kumnyonga Zitto kisiasa, ndivyo hivyo kwa sasa inatumika kumnyonga Cecil Mwambe na kundi lake baada ya kuonyesha nia ya kugombea nafasi ya juu ndani ya CHADEMA huku akionekana kuwa na malengo na mitazano tofauti na uongozi wa sasa wa juu wa CHADEMA.

Sumaye baada ya kuonja joto la Mbowe na kundi lake mapema ameamua kukimbia haraka kabala ya kuitwa MSALITI.

Tunaambiwa Mwambe ni PANDIKIZI kwa sababu ametumwa na CCM ili kuiua CHADEMA.Yaleyale kama methali ya Wascotland inavyosema, "Give a Dog an ill name, and he'll soon be hanged’’.

Baada ya kumnyonga kisiasa Mwambe, kundi la Mbowe linawaaminisha wanachama kuwa CHADEMA inamuhitaji sana Mbowe muda huu kuliko wakati wowote kwa sababu bila Mbowe basi CHADEMA itakufa. Kwa maana nyingine, kiboko cha CCM ya sasa ni Mbowe!

Mwaka 2014 wanachama waliambiwa wamchague Mbowe kwa sababu ‘’imemla ng’ombe mzima na amebakiza mkia’’. Kwamba wamchague Mbowe kwa sababu amekifikisha chama katika hatua ya mwisho ya kuchukua dola mwaka 2015.

Mwaka huu wanachama wanaambiwa wamchague Mbowe kwa sababu ni yeye pekee anaweza kupambana na kuishinda CCM ya awamu ya Tano! Kama watamchagua mwanachama mwingine basi CHADEMA itakufa!

Dhana ya USALITI na PANDIKIZI ni silaha ambayo imekuwa ikimpa ushindi Freeman Mbowe kila baada ya miaka mitano na mwaka huu inaelekea kutoa tena ushindi!

Mbowe and his stooge are giving Mwambe a bad name and hang him! He’s finished!
 
Binafsi sio mdau hasa wa chama ila huwa naona mabandiko hapa kwahiyo napata idea ya kinachokuwa kinaendelea.
Sasa ninachokiona mimi hayo majina mabaya wanayopata watu uliowataja ni kufuatana na aina ya harakati zao wanapotaka kuichukua nafasi ya uenyekiti, inaonekana wengi hawajimini na wanamuogopa mwnyekiti kwahiyo inapofikia kutaka sasa kumchallenge inabidi kufanya harakati nyingi za chinichini kwanza ambazo zikinaswa sas na intelejensia ya viongozi automatic hao watu lazima wataonekana wana nia ovu
 
G.Man,
Inawezekana unachosema ni kweli lakini kama hiyo ndio sababu kuu, unadhani mwenyekiti hafanyi harakati za chini chini ili abakie kwenye nafasi ya uongozi?
 
Ule mpango wa kina Zitto na Kitila wa pindua Mbowe 2014 hukuwahi kuufahamu?, hawakuonewa na mtu yeyote, walitaka kutumia mbinu haramu kumpindua Mbowe na kwa hilo walistahili kukutwa na yaliyowakuta. Bado uongezee ile mikutano ya Zitto na JK mafichoni halafu Zitto anatoka huko anakuja kutaka uenyekiti wa chama, utaweza vipi kumpa uenyekiti mtu wa aina hiyo?!

Suala la Mwambe kunyongwa kisiasa huo ni mtazamo wako tu, Mwambe hajanyongwa na yeyote, huyo bado mchanga, only four years ndani ya chama!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ule mpango wa kina Zitto na Kitila wa pindua Mbowe 2014 hukuwahi kuufahamu?, hawakuonewa na mtu yeyote, walitaka kutumia mbinu haramu kumpindua Mbowe na kwa hilo walistahili kukutwa na yaliyowakuta. Bado uongezee ile mikutano ya Zitto na JK mafichoni halafu Zitto anatoka huko anakuja kutaka uenyekiti wa chama, utaweza vipi kumpa uenyekiti mtu wa aina hiyo?!
Mbinu za ''kiharamu'' katika siasa ni sehemu ya siasa kwa sababu siasa mara nyingi hazina sheria au kanuni na kama zipo basi huwa hazifuatwi na wanasiasa wote. Hata Mbowe ukichunguza utagundua hutumia pia mbinu ''haramu'' katika kazi zake za siasa ndani na nje ya CHADEMA. Hawawezi kumnyoshea kidole mwanasiasa mwingine kwa kosa ambalo na wao hulitenda!

Kama nilivyosema, hiyo ilikuwa ni mbinu ya ''give a dog a bad name and hang him''

Suala la Mwambe kunyongwa kisiasa huo ni mtazamo wako tu, Mwambe hajanyongwa na yeyote, huyo bado mchanga, only four years ndani ya chama!.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwambe ameishanyongwa kisiasa na kinachosubiriwa kwa sasa ni kuzikwa kisiasa ndani ya CHADEMA!

Nina uhakika wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CHADEMA wameishaaminishwa kuwa ni PANDIKIZI na hafai kupewa uongozi wa juu ndani ya CHADEMA!
 
Mkuu mbona unaumia sana kuliko sisi wanachadema wenye chama? Haya wewe umekoti watu wa Scotland na mimi na koti watu wa hapahapa yani waswahili, "Pilipili iko shamba wewe inakuwashia nini?".

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli CHADEMA ni pilipili iko shambani lakini kumbuka mkulima ni mimi na wewe ambao kodi zetu inazitumia katika kujiendesha!
 
Mbinu za ''kiharamu'' katika siasa ni sehemu ya siasa kwa sababu siasa mara nyingi hazina sheria au kanuni na kama zipo basi huwa hazifuatwi na wanasiasa wote. Hata Mbowe ukichunguza utagundua hutumia pia mbinu ''haramu'' katika kazi zake za siasa ndani na nje ya CHADEMA. Hawawezi kumnyoshea kidole mwanasiasa mwingine kwa kosa ambalo na wao hulitenda!

Kama nilivyosema, hiyo ilikuwa ni mbinu ya ''give a dog a bad name and hang him''


Mwambe ameishanyongwa kisiasa na kinachosubiriwa kwa sasa ni kuzikwa kisiasa ndani ya CHADEMA!

Nina uhakika wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CHADEMA wameishaaminishwa kuwa ni PANDIKIZI na hafai kupewa uongozi wa juu ndani ya CHADEMA!
Hebu wacha kupotosha watu, inajulikana wazi kila taasisi ina katiba, na sheria ndogondogo walizojiwekea, sasa kama wanachama wanajambo lao kuhusu uongozi taratibu za kufuatwa zimeainishwa huko, sio kuibuka na njia za ajabu ajabu kutaka kuuondoa uongozi halali uliowekwa na wanachama kwa kisingizio eti njia haramu zinafuatwa kwasababu ni sehemu ya siasa!, are you serious?!

Suala la Mwambe kunyongwa kiasiasa narudia tena ni mtazamo wako, wajumbe ni watu wazima wenye akili zao timamu wana maamuzi yao, Mwambe kajipima kajiona anastahili kuwa mwenyekiti wa CDM hivyo asubiri kupigiwa kura, suala la kusema wajumbe wamelishwa maneno ni hoja nyepesi sana, wale sio watoto wadogo, wanapima wenyewe wanajua wanamuhitaji yupi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom