CHADEMA na CCM, Watu wangapi wamekufa katika harakati zenu za siasa?

Alexism

JF-Expert Member
Aug 14, 2011
3,423
2,045
Kama mtanzania mwenye upendo na mzalendo wa nchi na watu wake ningependa kujua idadi ya wananchi ambao wamekufa kwa kuuwawa na polisi wakati harakati za kisiasa baina ya CHADEMA na CCM.

Swala ili ni muhimu tukalijua ili tuweza kufaham nani wakulaumiwa na nani anabidi awajibishwe katika mauaji ya watanzania wasio na hatia. Kama utakuwepo uwezekano kabisa na ninao uhakika upo wakuwajibisha watu waliousika moja kwamoja.

Naomba wahusika kama polisi au vyama tajwa watoe taarifa kwa umma hasa kwakutumia mtandao huu ili umma uweze kujua na kufanya mahamzi dhidi ya vitendo hivi vinavyo endelea kila kukicha.
 
Unachanganya mambo, Muuaji anajulikana, Bwana mipango wa mauaji anajulikana. Tuna TISS na Polisi hao ndi wa kuwauliza kama kazi yao wanaifahamu sawasawa.
 
Heading yako umekosea andika CCM kwa kushirikiana na Polisi Mmeua wana CDM wangapi katika harakati zao za kisiasa?
Kwani katika matukio yote ya mauaji na ukandamizaji juu ya Demokrasia hakuna sehemu ambayo wana CCM walivamiwa na polisi isipokuwa ni kwa CDM tu.
 
Hili swali ungeuliza Polisi,kuna kila dalili za Polisi kuvuruga utulivu wetu kwa mabavu yasiyo na msingi.Kuna uelekeo wa kuishiwa uvumilivu nchi ilipuke.fanyeni mizaha na hali halisi ukiwaka umewaka kweli kweli,waoneni Wananchi ni wajinga tu!
 
Cha msingi si kutafuta wa kulaumiwa, bali Tutafute jinsi ya kuzuia mauaji zaidi yasitokee. Mimi naamini 100%, chama changu hakiwezi kutuma chombo chochote cha dola kuua. Mauaji hutokea pasipo dhamira ya chama chochote, isipokuwa tuombe vyombo vya dola, visiingilie uhuru na haki za vyama kufanya kazi zao za kuhamasisha jamii. Naamini mauaji ni mbinu chafu za baadhi ya watendaji wanao simamia vyombo vya dola, katika kumharibia Mkuu wangu wa kaya asipate nishani ya Mo Ibrahimu, ambayo kiukweli alistahili.
 
Dr Slaa ana list yote na malengo yake mpaka jinsi nchi itakavoingia katika machafuko.
 
Kama mtanzania mwenye upendo na mzalendo wa nchi na watu wake ningependa kujua idadi ya wananchi ambao wamekufa kwa kuuwawa na polisi wakati harakati za kisiasa baina ya CHADEMA na CCM.

Swala ili ni muhimu tukalijua ili tuweza kufaham nani wakulaumiwa na nani anabidi awajibishwe katika mauaji ya watanzania wasio na hatia. Kama utakuwepo uwezekano kabisa na ninao uhakika upo wakuwajibisha watu waliousika moja kwamoja.

Naomba wahusika kama polisi au vyama tajwa watoe taarifa kwa umma hasa kwakutumia mtandao huu ili umma uweze kujua na kufanya mahamzi dhidi ya vitendo hivi vinavyo endelea kila kukicha.

Waulize CDM kwa uchu wao wa madaraka wamepanga kuua watu wangapi mpaka kufanikiwa watakacho? kwenye bendera wameweka hata rangi yao nyekundu kuwa sera yao ni kumwaga damu na kutofuata utawala wa sheria. CDM ni janga la kitaifa na dunia

 
Waulize CDM kwa uchu wao wa madaraka wamepanga kuua watu wangapi mpaka kufanikiwa watakacho? kwenye bendera wameweka hata rangi yao nyekundu kuwa sera yao ni kumwaga damu na kutofuata utawala wa sheria. CDM ni janga la kitaifa na dunia


Unarukaruka kila hoja, jibu hoza unazoziacha nyuma kwa kila hoja unayoitibulia na kuichafua na kurukia nyingine.


Kuwa mungwana.
 
Unarukaruka kila hoja, jibu hoza unazoziacha nyuma kwa kila hoja unayoitibulia na kuichafua na kurukia nyingine.


Kuwa mungwana.

Haya ww ni kada kufa wa cdm, rangi nyekundu ina maana gani ? tujuze hapa jamvini

 
Haya ww ni kada kufa wa cdm, rangi nyekundu ina maana gani ? tujuze hapa jamvini



Mimi nitaanza kukuuliza maswali uliyotakiwa utupatie majibu kwenye hoja ulizorukaruka, nitakuuliza hapa kwa sababu amejitokeza hapa, japo haiendani na hoja tuliyonayo. Nakuomba tu tuendeleze huu mdahalo kwa maana ya uelewa, weka papara pembeni na chambua haya mambo kama great thinker no magumashi tunapodebeti.


1. Kunahoja ulisema kifo cha kujitakia, hebu tueleze ulikuwa unamanisha nini, na nani alijitakia kifo hadi akajiuwa?


2. Kwenye hoja ilele ukasema, alie uwa anapaswa kuuwawa kwa majibu wako na kwamba ndivyo mungu anavotaka. nikasema kwa mujibu wa sheria za mwanadamu za kimahakama mtu anahukumiwa kunyongwa ikithibitika pasipo kuacha shaka.

Maswali yangu yalikuwa hivi.

i) Mungu anaruhusu mwanadamu kuhukumu kwaniaba yake? kivipi na kwa nini?

ii) Kama ndivyo i) hapo juu, je mungu hanauwezo hata mwanadamu amsaidie kuhukumu? na kama ndivyo elezea udhaifu wa mungu kukosa uwezo uko wapi hata asaidiwe kuhukumu?

iii) Siku ya kiama ipo? na jehanamu ipo?
-kama jibu ni ndio, je hukumu atakayotoa mungu (Allah) siku hiyo inauhusiano wowote na hukum ulioisema kwamba alieua kwa makusudi yampasa kuuwawa kwa amri ya mwanadamu?



RANGI NYEKUNDU.

Mara nyingi rangi nyekundu huchukuliwa kama inshara ya hari ya hatari, lakini pia wapendanao huitumia rangi hiyo kwa maana ya upendo na haishii hapo itategemeana piwa na maamuzi ya mtumiaji. (mimi naelewa hivyo sijuwi wewe unaelewaje?)

Matumizi ya rangi hii ni lazima yawe sahihi, kwa maana ya haki na kukubaliwa na wahusika wa pande mbili (kama ni kwa maana ya hatari, au upendo au maana nyingine yeyote)

Tofauti na matumizi ya haki, hata mbwa unaemfuga na kumlisha kila siku usipomtendea haki na kumkandamiza ukamuumiza atakung'ata na anaweza kukuuwa. Hivyo, heshima ya utu na thamani kwa maana ya sheria kutoka katiba mama lazima kuzingatiwa ilikupata matokeo sahihi kwa watawala.

Usitegemee kupanda umaskini, chuki na udharirishaji miongoni mwa raia wako ukitegemea kuvuna, utulivu, amani na upendo.
 
Nilitaka nikukumbushe pia mauaji ya CCM na CUF kule Zenji 95/96 had watu wakaenda uhamishoni SHIMONI na wamerudi juzi tu...na baaada ya hapo sasa tuongee ili uone nani muuaji wa wananchi....

Kama mtanzania mwenye upendo na mzalendo wa nchi na watu wake ningependa kujua idadi ya wananchi ambao wamekufa kwa kuuwawa na polisi wakati harakati za kisiasa baina ya CHADEMA na CCM.

Swala ili ni muhimu tukalijua ili tuweza kufaham nani wakulaumiwa na nani anabidi awajibishwe katika mauaji ya watanzania wasio na hatia. Kama utakuwepo uwezekano kabisa na ninao uhakika upo wakuwajibisha watu waliousika moja kwamoja.

Naomba wahusika kama polisi au vyama tajwa watoe taarifa kwa umma hasa kwakutumia mtandao huu ili umma uweze kujua na kufanya mahamzi dhidi ya vitendo hivi vinavyo endelea kila kukicha.
 
Mimi nitaanza kukuuliza maswali uliyotakiwa utupatie majibu kwenye hoja ulizorukaruka, nitakuuliza hapa kwa sababu amejitokeza hapa, japo haiendani na hoja tuliyonayo. Nakuomba tu tuendeleze huu mdahalo kwa maana ya uelewa, weka papara pembeni na chambua haya mambo kama great thinker no magumashi tunapodebeti.


1. Kunahoja ulisema kifo cha kujitakia, hebu tueleze ulikuwa unamanisha nini, na nani alijitakia kifo hadi akajiuwa?


2. Kwenye hoja ilele ukasema, alie uwa anapaswa kuuwawa kwa majibu wako na kwamba ndivyo mungu anavotaka. nikasema kwa mujibu wa sheria za mwanadamu za kimahakama mtu anahukumiwa kunyongwa ikithibitika pasipo kuacha shaka.

Maswali yangu yalikuwa hivi.

i) Mungu anaruhusu mwanadamu kuhukumu kwaniaba yake? kivipi na kwa nini?

ii) Kama ndivyo i) hapo juu, je mungu hanauwezo hata mwanadamu amsaidie kuhukumu? na kama ndivyo elezea udhaifu wa mungu kukosa uwezo uko wapi hata asaidiwe kuhukumu?

iii) Siku ya kiama ipo? na jehanamu ipo?
-kama jibu ni ndio, je hukumu atakayotoa mungu (Allah) siku hiyo inauhusiano wowote na hukum ulioisema kwamba alieua kwa makusudi yampasa kuuwawa kwa amri ya mwanadamu?



RANGI NYEKUNDU.

Mara nyingi rangi nyekundu huchukuliwa kama inshara ya hari ya hatari, lakini pia wapendanao huitumia rangi hiyo kwa maana ya upendo na haishii hapo itategemeana piwa na maamuzi ya mtumiaji. (mimi naelewa hivyo sijuwi wewe unaelewaje?)

Matumizi ya rangi hii ni lazima yawe sahihi, kwa maana ya haki na kukubaliwa na wahusika wa pande mbili (kama ni kwa maana ya hatari, au upendo au maana nyingine yeyote)

Tofauti na matumizi ya haki, hata mbwa unaemfuga na kumlisha kila siku usipomtendea haki na kumkandamiza ukamuumiza atakung'ata na anaweza kukuuwa. Hivyo, heshima ya utu na thamani kwa maana ya sheria kutoka katiba mama lazima kuzingatiwa ilikupata matokeo sahihi kwa watawala.

Usitegemee kupanda umaskini, chuki na udharirishaji miongoni mwa raia wako ukitegemea kuvuna, utulivu, amani na upendo.

Hata Red Cross kazi yao ni kumwaga damu?
 
Kama mtanzania mwenye upendo na mzalendo wa nchi na watu wake ningependa kujua idadi ya wananchi ambao wamekufa kwa kuuwawa na polisi wakati harakati za kisiasa baina ya CHADEMA na CCM.

Swala ili ni muhimu tukalijua ili tuweza kufaham nani wakulaumiwa na nani anabidi awajibishwe katika mauaji ya watanzania wasio na hatia. Kama utakuwepo uwezekano kabisa na ninao uhakika upo wakuwajibisha watu waliousika moja kwamoja.

Naomba wahusika kama polisi au vyama tajwa watoe taarifa kwa umma hasa kwakutumia mtandao huu ili umma uweze kujua na kufanya mahamzi dhidi ya vitendo hivi vinavyo endelea kila kukicha.

Kama Wewe Sio Mnafiki unge-kuwa based kwa CHADEMA tu; kama kweli Unapenda haki na ni free haupendelei Upande wowote

Ungebadilisha Tittle na kuuliza CHADEMA wamepoteza watu wangapi kwa NGUVU za CCM? CCM inatumia NGUVU za POLISI na

SHERIA kukandamiza USAWA na haki za kisheria...

Sasa, Umeona Mkutano wowote wa Nnape Nnauye Umeingiliwa na FFU? hata siku Moja? Wewe hata Mkutano wa USA - DMV

Bado CCM wanasema CHADEMA wanahonga wana CCM; Unaona hakuna HAKI na USAWA.... PLEASE BE FAIR...

"
Emancipate yourselves from mental slavery, none but ourselves can free our minds!"

 
Cha msingi si kutafuta wa kulaumiwa, bali Tutafute jinsi ya kuzuia mauaji zaidi yasitokee. Mimi naamini 100%, chama changu hakiwezi kutuma chombo chochote cha dola kuua. Mauaji hutokea pasipo dhamira ya chama chochote, isipokuwa tuombe vyombo vya dola, visiingilie uhuru na haki za vyama kufanya kazi zao za kuhamasisha jamii.

Naamini mauaji ni mbinu chafu za baadhi ya watendaji wanao simamia vyombo vya dola,

katika kumharibia Mkuu wangu wa kaya asipate nishani ya Mo Ibrahimu, ambayo kiukweli alistahili
.

Mkuu, hapo kwenye red mwanzoni ni mwendelezo wa propaganda chafu na za kijinga za kujaribu kumtenganisha Mkulu na maovu, uchafu na udhaifu wa watendaji wake zinazoenezwa na ccm wakidhani wanamsaidia kumbe ndio wanadhihirisha udhaifu wake kiutendaji. Na bahati mbaya ni kwamba zimegeuka kuwa wimbo usiotamanisha kuusikia tena!

Red ya chini ni upuuzi kabisa kufikiria hilo maana wanaotoa zawadi hawaangalii rais aliyefanya safari nyingi za nje bali yule aliye mbunifu na kwa ubunifu wake ameliletea taifa lake demokrasia ya kweli na maendeleo katika nyanja za kielimu, kisiasa, kiuchumi, kiuongozi, kiufundi na kijamii. Mambo ambayo jamaa'ako ameshindwa kabisa!
 
Mkuu, hapo kwenye red mwanzoni ni mwendelezo wa propaganda chafu na za kijinga za kujaribu kumtenganisha Mkulu na maovu, uchafu na udhaifu wa watendaji wake zinazoenezwa na ccm wakidhani wanamsaidia kumbe ndio wanadhihirisha udhaifu wake kiutendaji. Na bahati mbaya ni kwamba zimegeuka kuwa wimbo usiotamanisha kuusikia tena!

Red ya chini ni upuuzi kabisa kufikiria hilo maana wanaotoa zawadi hawaangalii rais aliyefanya safari nyingi za nje bali yule aliye mbunifu na kwa ubunifu wake ameliletea taifa lake demokrasia ya kweli na maendeleo katika nyanja za kielimu, kisiasa, kiuchumi, kiuongozi, kiufundi na kijamii. Mambo ambayo jamaa'ako ameshindwa kabisa!
Hapo kwenye red, Mkulu amepungukiwa lipi????? Tuache siasa, tuhukumu watu kwa haki. najua yapo ambayo yamekuwa kasoro kwake. mfano swala la mabwepande limemchafua sana, swala la kufungia gazeti la mwana halisi ni kasolo kubwa, mauaji ya Arusha, mauaji ya jana, morogoro - hayo ni baadhi ya mambo ambayo yamemchafua, ingawa naamini ni upotofu wa vyombo vilivyo chini yake, na vimetenda bila kumhusisha. Toa maoni kiukomavu, na sio kwa wingi wa matusi na kashfa, haisaidii.
 
Back
Top Bottom