CHADEMA na ACT-Wazalendo mna wajibu mkubwa kwa wapiga kura wenu

KalamuTena

JF-Expert Member
Jul 7, 2018
13,189
17,157
CCM wamejipanga vizuri kupata ushindi, hata kama ni ushindi kwa njia isiyokuwa halali.

Miaka yote hii mitano, na kabla ya hapo, tumesikia manung'uniko yenu kuhusu ubovu wa usimamizi wa uchaguzi wetu unaowapendelea CCM. Miaka yote hii mmekuwa mkilalamika kuhusu jambo hili, lakini hatukuona mikakati yoyote mliyokuwa mkiiandaa kuzuia uharamia huu. Mmekuwa tu mkilalamika bila ya kutafuta suluhisho lake.

Huu uchaguzi mwingine unaokuja Oktoba, nao inaelekea kwamba matokeo ni yale yale na ulalamishi utaendelea vilevile.

Sasa tunawapa angalao pendekezo, ili msiendelee kuwa walalamishi tu, ni bora kujitayarisha vyema ili mlalamike mkiwa na ushahidi usiofichika kuhusu malalamiko yenu.

Haitoshi kulalamika tu, bila ya kuonyesha ushahidi wowote unaoonyesha malalamiko yenu kuwa ya msingi.

Ni lazima muwe na njia za kuweka ushahidi kamilifu zaidi katika kila jambo mtakalokuwa mmefanyiwa rafu. Tknologia zipo sasa za kukusanyia ushahidi wa uhakika utakaoonyesha wazi mnayoyalalamikia. Isiwe ni kulalamika tu, kama kule kwa Lowassa kudai kura milioni kadhaa bila ya ushahidi wowote.

Leo wakati mnaambiwa kwamba hata nakala za matokeo huenda msipewe, kwa nini nyinyi mkubali tu kauli hiyo hata bila ya kufanya juhudi za kuwa na uhakika wa kura zilizopatikana kituoni? Yaani haiwezekani kamwe kujua ni kura ngapi mmepigiwa na watu wenu, na juhudi zao hizi hata hamuwezi angalao kuonyesha ni kura ngapi walizowapa? Kwa nini muwakatishe tamaa wapiga kura wenu kiasi hiki.

Kazi yenu ya kwanza, mliyopaswa kuifanya tokea 2015, ni kuwa na watu wenu mnaoamini ni wanachama wenu wasiotetereka wala kuuza juhudi za wanachama wenzao huko waliko. Hawa ndio wanapaswa kuwa wasimamizi wenu katika vituo vyenu vyote vya kupigia na kuhesabu kura.

Haiwezekani watu wanaosimamia kazi mhimu kiasi hiki wawe ni wa kuokoteza tu mitaani siku chache kabla ya uchaguzi. Hawa ndio wanaouza kura za wapiga kura wenu na kuharibu juhudi zenu zote.

Kama kazi ya kuwatambua na kuwaanda hawa watu bado hamjaifanya hadi sasa, huo ni uzembe na mtastahili mtakachokipata.
 
Hilo ulilolizungumzia la kuokoteza watu nakubaliana na wewe, naamini sasa watakuwa wameshaliona na wamejifunza kutokana na hilo kosa siku zilizopita.

Jingine la mawakala kutokupewa matokeo hili naona ndio kubwa zaidi na ndilo litakaloenda kuleta vurugu wakati ukifika, nimemsikia Magufuli akisisitiza kuhusu uchaguzi wa kistaarabu usio na matusi, lakini kwangu huo ustaarabu ni pamoja na kufuata taratibu zote wakati wa uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kutoa nakala za matokeo kwa mawakala wa vyama husika.

Kama vyama marafiki wa CCM vilikubaliana na huo ujinga, Chadema waliukataa, na hii inaonesha dhahiri CCM pamoja na kelele zao zote hawajiamini, ni wepesi sana, ndio maana kila siku wanatengeneza vitu vya ajabu ili kujihakikishia ushindi kwa hila, safari hii wamefeli.
 
Hilo ulilolizungumzia la kuokoteza watu nakubaliana na wewe, naamini sasa watakuwa wameshaliona na wamejifunza kutokana na hilo kosa siku zilizopita.

Jingine la mawakala kutokupewa matokeo hili naona ndio kubwa zaidi na ndilo litakaloenda kuleta vurugu wakati ukifika, nimemsikia Magufuli akisisitiza kuhusu uchaguzi wa kistaarabu usio na matusi, lakini kwangu huo ustaarabu ni pamoja na kufuata taratibu zote wakati wa uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kutoa nakala za matokeo kwa mawakala wa vyama husika.

Kama vyama marafiki wa CCM vilikubaliana na huo ujinga, Chadema waliukataa, na hii inaonesha dhahiri CCM pamoja na kelele zao zote hawajiamini, ni wepesi sana, ndio maana kila siku wanatengeneza vitu vya ajabu ili kujihakikishia ushindi kwa hila, safari hii wamefeli.
Jambo linaloshangaza ni hilo la kutangaza mapema kabisa kwamba kuna uwezekano wa nakala kutotolewa!

Jambo la muhimu kama matokeo ya uchaguzi; kuna sababu zipi zinazoweza kuzuia nakala zisipatikane?

Hapa ndipo pa kuanzia. Sehemu zote ambazo nakala zitakuwa hazikupatikana, matokeo yake yanakuwa ya mashaka, kama sio batili moja kwa moja, na huko ndiko hivi vyama vya upinzani wanakotakiwa kuwekeza nguvu zaidi kuzuia uharamia.
 
Mkuu nakala kama hazitatolewa kwa wapinzani katika jimbo au majimbo lolote/yoyote Nchini basi matokeo yake ni BATILI.

Hapa ndipo pa kuanzia. Sehemu zote ambazo nakala zitakuwa hazikupatikana, matokeo yake yanakuwa ya mashaka, kama sio batili moja kwa moja, na huko ndiko hivi vyama vya upinzani wanakotakiwa kuwekeza nguvu zaidi kuzuia uharamia.
 
Jambo linaloshangaza ni hilo la kutangaza mapema kabisa kwamba kuna uwezekano wa nakala kutotolewa!

Jambo la muhimu kama matokeo ya uchaguzi; kuna sababu zipi zinazoweza kuzuia nakala zisipatikane?

Hapa ndipo pa kuanzia. Sehemu zote ambazo nakala zitakuwa hazikupatikana, matokeo yake yanakuwa ya mashaka, kama sio batili moja kwa moja, na huko ndiko hivi vyama vya upinzani wanakotakiwa kuwekeza nguvu zaidi kuzuia uharamia.
Hapa tusifiche kitu chochote, huku ni kutafutana uchokozi makusudi, huwezi kumnyima mtu haki yake bila sababu ya msingi halafu unamlazimisha atulie tu kwa kauli zao za hawataki vurugu wakati wa uchaguzi, wakati kimsingi wao ndio wanaoanzisha hizo vurugu.

Kama wanataka amani ya kweli wakati wa uchaguzi waondoe hizo sintofahamu zisizo na maana, hakuna mtu mwenye akili timamu wakuleta vurugu bila sababu kama chizi.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mkuu nakala kama hazitatolewa kwa wapinzani katika jimbo au majimbo lolote/yoyote Nchini basi matokeo yake ni BATILI.
Hili ndilo linalotakiwa wapinzani walisemee waziwazi watu wajue kungali mapema kabisa.

Haifai kunyamaza, halafu ghafla siku hiyo ya kura ndio wanaliamsha!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom