Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT, mkishindwa kuwa kitu kimoja na kuachiana majimbo mtawafaidisha CCM

Ni kweli, lakini kutoshiriki inaweza kuwa ni hasara zaidi kisiasa kwa hivi vyama.

Mkuu mimi bado msimamo wangu uko palepale, bila tume huru ya uchaguzi ni kupoteza Muda. Nilitarajia wapinzani kila wakisimama ni kuiponda tume, hadi tume ipoteze kujiamini na isiwe katika mazingira rahisi ya kuibeba ccm. Lakini naona wanaongelea uchaguzi tu, huku wakiiacha tume kama chombo sahihi cha kusimamia uchaguzi. Hii ya kuachiana sehemu uko sahihi, lakini kwa tume hii, hata chama kimoja kikijitoa na wanachama wake wote waende chama kimoja, bado hakuna lolote litakaloendelea.
 
Huu muungano kwenye kura za urais na mgombea urais ndipo penye walakini.

Kiukweli kwangu Membe sioni influence yake kabisa ukiacha hiyo mikoa ya kusini, sasa kipi bora;

(a) Kumsimamisha Membe asaidie wagombea ubunge mikoa ya kusini ambayo hatuna uhakika kama kweli ana hiyo influence?

Au

(b) Chadema imsimamishe mgombea urais wake ambae inaamini anaungwa mkono na kundi kubwa la watu Tanzania nzima kwa ujumla, na sio kanda fulani pekee?

Mleta mada umejaribu kusisitiza kwenye umoja ni vizuri, lakini pia tuangalie kwa jicho la pili nguvu za wagombea hasa wa Urais kutoka vyama vyote viwili, tusilazimishe tu bora fulani ana jina basi apewe hiyo nafasi, napenda hapa tutazame zaidi nguvu/uungwaji mkono wa wagombea wa hivyo vyama viwili.
 
Mkuu mimi bado msimamo wangu uko palepale, bila tume huru ya uchaguzi ni kupoteza Muda. Nilitarajia wapinzani kila wakisimama ni kuiponda tume, hadi tume ipoteze kujiamini na isiwe katika mazingira rahisi ya kuibeba ccm. Lakini naona wanaongelea uchaguzi tu, huku wakiiacha tume kama chombo sahihi cha kusimamia uchaguzi. Hii ya kuachiana sehemu uko sahihi, lakini kwa tume hii, hata chama kimoja kikijitoa na wanachama wake wote waende chama kimoja, bado hakuna lolote litakaloendelea.
Wewe ni mpiga debe tu wenye saccos wapo busy na watashiriki
Who are you?
 
Hawa wapinzai syo wakuwaamin kabisa ile 2015 walipoteza majimbo na kata kadhaa kwa uroho wao wa fedha na wakutoshiriana .
 
👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👏🏽👊🏽👊🏽👊🏽
Wanataka kurudia kosa lile lile la 2015 Chadema walipomkaribisha fisadi lowassa. Fool me once shame on you, fool me twice shame on ME.

Huu muungano umeingia shubiri Mara baada ya zitto kumtamani mwanachama Wa ccm aje aokoe jahazi LA kugombea urais kupitia Act kisha muungano huo.Zitto kwa hili kapotoka sana, membe aweza karibishwa upinzani ila sio kwa kugombea urais.
 
Nashauri ACT-WAZALENDO wasiwaamini hawa cdm wawaulize cuf walichofanyiwa 2015 jimbo la ukonga!!
 
Huu muungano kwenye kura za urais na mgombea urais ndipo penye walakini.

Kiukweli kwangu Membe sioni influence yake kabisa ukiacha hiyo mikoa ya kusini, sasa kipi bora;

(a) Kumsimamisha Membe asaidie wagombea ubunge mikoa ya kusini ambayo hatuna uhakika kama kweli ana hiyo influence?

Au

(b) Chadema imsimamishe mgombea urais wake ambae inaamini anaungwa mkono na kundi kubwa la watu Tanzania nzima kwa ujumla, na sio kanda fulani pekee?

Mleta mada umejaribu kusisitiza kwenye umoja ni vizuri, lakini pia tuangalie kwa jicho la pili nguvu za wagombea hasa wa Urais kutoka vyama vyote viwili, tusilazimishe tu bora fulani ana jina basi apewe hiyo nafasi, napenda hapa tutazame zaidi nguvu/uungwaji mkono wa wagombea wa hivyo vyama viwili.
Kwa mtazamo wangu,kwenye uraisi wamsimamishe Lissu na huyu Membe anaweza kutumika kumpigia kampeni katika hiyo mikoa ya kusini na kwingineko anakoweza kusaidia ila sio kuja kugombea uraisi kupitia upinzani.Hamahama imeshawavunja moyo wananchi na itakuwa kosa kubwa zaidi kurudia kitu kile kile hasa kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi.
 
Kwa mtazamo wangu,kwenye uraisi wamsimamishe Lissu na huyu Membe anaweza kutumika kumpigia kampeni katika hiyo mikoa ya kusini na kwingineko anakoweza kusaidia ila sio kuja kugombea uraisi kupitia upinzani.Hamahama imeshawavunja moyo wananchi na itakuwa kosa kubwa zaidi kurudia kitu kile kile hasa kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi.
Yes, especially ACT wakimsimamisha mgombea visiwani, basi Chadema wasimamishe mgombea bara.
 
Yes, especially ACT wakimsimamisha mgombea visiwani, basi Chadema wasimamishe mgombea bara.
Sasa CHADEMA nao wanasimamisha mgombea uraisi huko Zanzibar na teyari mmoja kashachukua fomu kama hiyo picha hapo juu kwenye mada inavyothibitisha.

Tatizo naloliona ni kila chama kina nia ya kujijenga bara na visiwani hivyo wanaona kutoshiriki ni kudumuza vyama vyao bila kujali watashinda au laa wakiamini kitendo cha kushiriki tu katika hizi chaguzi kinasaidia kujenga uhai wa chama hata kama hawatashinda.
 

Wanataka kurudia kosa lile lile la 2015 Chadema walipomkaribisha fisadi lowassa. Fool me once shame on you, fool me twice shame on ME.
Tuliwambia humu mkakaza shingo! Asiyesikia la mkuu huvunjika guu, sasa baada ya kuvunjika ndio akili zinawarudi,

Same kwa Mashinji tukiwaambia huyo jamaa hafai, bado mkajifanya much know,,
Yani nyie hat muwekewe kujifunza kwa picha hamuwezagi kuelewa kamwe

Sent from my SM-T585 using JamiiForums mobile app
 
Sijui nini kinaendelea kati ya CHADEMA na ACT juu ya kushirikiana katika uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu, ila napenda tu kuwatahadharisha kuwa wakishindwa kukaa pamoja na kuja na mpango mkakati wa pamoja juu ya namna bora ya kushirikiana katika uchaguzi huu,basi watakaofaidika na hali hii watakuwa ni CCM katika baadhi ya maeneo ambayo ACT watakuwa na nguvu na CHADEMA nao pia watakuwa na nguvu hata kama watakuwa wanazidiana kwa kiasi fulani.

Zanzibar
Huko ni bora CHADEMA wawaunge mkono ACT kwasababu ujio wa Maalim Seif umeipa nguvu ACT hivyo ni bora CHADEMA wawaunge mkono kuliko kugombea alafu wagawane kura ingawa hata pasipo kuungana, bado ACT itashinda kulinganisha na CHADEMA. Tutambue kuwa adui yetu mkubwa wa kisiasa ni CCM na si chama kingine chochote kile cha siasa.

View attachment 1498622

View attachment 1498597

kigoma
Katika mikoa ambayo ACT na CHADEMA wanaweza kugawana kura na matokeo yakawa ni wote kukosa kama siyo kupunguza majimbo ya kwenda upinzani,basi Kigoma inaweza kuwa ni mojawapo, hivyo ni vizuri washirikiane katika kusimamisha wagombea kwa maana ya kuachiana majimbo na kata za uchaguzi vinginevyo itakula kwao.

Mikoa ya kusini
Iwapo Membe atajiunga ACT bila kujali atagombea uraisi kupitia ACT au laa,kitendo tu cha Membe kujiunga ACT kitaipa nguvu ACT na kuongeza ushindani wa kisiasa baina ya vyama vitatu:CCM,ACT na CHADEMA.Kwa maana hiyo,wapinzani wakishindwa kuungana,CCM inaweza kufaidika ingawa ACT bado inaweza kushinda hata ikisimama peke yake ila hasara itakuja katika kura za mgombea uraisi iwapo hivi vyama kila kimoja kitasimamisha mgombea wake.

Ukiacha mikoa hiyo niliyoitaja pamoja na Zanzibar,athari za wapinzani kutoachiana majimbo na kata za uchaguzi zinaweza kuonekana pia katika maeneo mengine machache kama kwenye mikoa ya Tabora na Tanga, na lazima ieleweka athari za kugawana kura zitaweza hata kuathiri wagombea uraisi ikitokea kila chama kitasimamisha mgombea wake.

Hata kama watakuwa wamechelewa kuungana kisheria,swala la wao kushirikiana kwa kuachiana majimbo na kuamua kuwapigia debe wagombea wao haliwezi kuwa ni kosa kisheria zaidi tu ya kuhitaji dhamira ya kisiasa kutoka wahusika.

Ukweli ni kwamba,hata pasipo vyama hivi kuungana,CCM na wagombea wake ndio inayostahili kushika mkia kwenye matokeo ya uchaguzi ila ndio hiyo tena bado kuna baadhi ya watanzania wenzetu hawajielewi.

Muda wa nusu karne na zaidi kama umewashinda kubadili maisha ya watanzania,sioni ni sababu gani ya kuendelea kuwapa nafasi ya kuendelea kubaki madarakani.

CHADEMA mkijiona mna nguvu na mnaweza kusimama kivyenu katika kila sehemu ya nchi hii,basi matokeo yake mtakuja kuyaona;halikadhalika kwa ACT-Wazalendo.

Nukuu muhimu za wanasiasa zinazoendana na mada hii:


Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Wakati ni Huu! Wakati ni Sasa-Ismail Jussa on twitter.

Ni wajibu wetu sote kuonyesha dhamira zenu za kweli kwamba tunahitaji coalition. Wananchi wanafahamu kwamba wapo ambao wqnafanyabiashara katika hizi siasa. Nakubaliana na wewe Kaka Ismail Jussa kwamba hili lazima tusimame na tuhesabiwe-Patrick Ole Sosopi on twitter.

Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Ninaamini TUNAWEZA na TUTAWEZA-Zitto Kabwe on twitter.
Together we shall overcome
 
Sijui nini kinaendelea kati ya CHADEMA na ACT juu ya kushirikiana katika uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu, ila napenda tu kuwatahadharisha kuwa wakishindwa kukaa pamoja na kuja na mpango mkakati wa pamoja juu ya namna bora ya kushirikiana katika uchaguzi huu,basi watakaofaidika na hali hii watakuwa ni CCM katika baadhi ya maeneo ambayo ACT watakuwa na nguvu na CHADEMA nao pia watakuwa na nguvu hata kama watakuwa wanazidiana kwa kiasi fulani.

Zanzibar
Huko ni bora CHADEMA wawaunge mkono ACT kwasababu ujio wa Maalim Seif umeipa nguvu ACT hivyo ni bora CHADEMA wawaunge mkono kuliko kugombea alafu wagawane kura ingawa hata pasipo kuungana, bado ACT itashinda kulinganisha na CHADEMA. Tutambue kuwa adui yetu mkubwa wa kisiasa ni CCM na si chama kingine chochote kile cha siasa.

View attachment 1498622

View attachment 1498597

kigoma
Katika mikoa ambayo ACT na CHADEMA wanaweza kugawana kura na matokeo yakawa ni wote kukosa kama siyo kupunguza majimbo ya kwenda upinzani,basi Kigoma inaweza kuwa ni mojawapo, hivyo ni vizuri washirikiane katika kusimamisha wagombea kwa maana ya kuachiana majimbo na kata za uchaguzi vinginevyo itakula kwao.

Mikoa ya kusini
Iwapo Membe atajiunga ACT bila kujali atagombea uraisi kupitia ACT au laa,kitendo tu cha Membe kujiunga ACT kitaipa nguvu ACT na kuongeza ushindani wa kisiasa baina ya vyama vitatu:CCM,ACT na CHADEMA.Kwa maana hiyo,wapinzani wakishindwa kuungana,CCM inaweza kufaidika ingawa ACT bado inaweza kushinda hata ikisimama peke yake ila hasara itakuja katika kura za mgombea uraisi iwapo hivi vyama kila kimoja kitasimamisha mgombea wake.

Ukiacha mikoa hiyo niliyoitaja pamoja na Zanzibar,athari za wapinzani kutoachiana majimbo na kata za uchaguzi zinaweza kuonekana pia katika maeneo mengine machache kama kwenye mikoa ya Tabora na Tanga, na lazima ieleweka athari za kugawana kura zitaweza hata kuathiri wagombea uraisi ikitokea kila chama kitasimamisha mgombea wake.

Hata kama watakuwa wamechelewa kuungana kisheria,swala la wao kushirikiana kwa kuachiana majimbo na kuamua kuwapigia debe wagombea wao haliwezi kuwa ni kosa kisheria zaidi tu ya kuhitaji dhamira ya kisiasa kutoka wahusika.

Ukweli ni kwamba,hata pasipo vyama hivi kuungana,CCM na wagombea wake ndio inayostahili kushika mkia kwenye matokeo ya uchaguzi ila ndio hiyo tena bado kuna baadhi ya watanzania wenzetu hawajielewi.

Muda wa nusu karne na zaidi kama umewashinda kubadili maisha ya watanzania,sioni ni sababu gani ya kuendelea kuwapa nafasi ya kuendelea kubaki madarakani.

CHADEMA mkijiona mna nguvu na mnaweza kusimama kivyenu katika kila sehemu ya nchi hii,basi matokeo yake mtakuja kuyaona;halikadhalika kwa ACT-Wazalendo.

Nukuu muhimu za wanasiasa zinazoendana na mada hii:


Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Wakati ni Huu! Wakati ni Sasa-Ismail Jussa on twitter.

Ni wajibu wetu sote kuonyesha dhamira zenu za kweli kwamba tunahitaji coalition. Wananchi wanafahamu kwamba wapo ambao wqnafanyabiashara katika hizi siasa. Nakubaliana na wewe Kaka Ismail Jussa kwamba hili lazima tusimame na tuhesabiwe-Patrick Ole Sosopi on twitter.

Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Ninaamini TUNAWEZA na TUTAWEZA-Zitto Kabwe on twitter.
iseeee
 
Huu muungano umeingia shubiri Mara baada ya zitto kumtamani mwanachama Wa ccm aje aokoe jahazi LA kugombea urais kupitia Act kisha muungano huo.Zitto kwa hili kapotoka sana, membe aweza karibishwa upinzani ila sio kwa kugombea urais.
Yameshatimia sasa kwa Membe kujiunga ACT.
 
Kwa tume hii ya uchaguzi ni ngumu sana kutoboa!!!...Sijui kwa nini mnajisahaulisha

Kwa tume hii hii kusingetokea mtafaruku wa kipandikizi tokea kwa kina lipumba na mwenziwe slaa jiwe asingetoboa.

Hivyo hivyo bila mwungano Malawi, Mutharika angekuwa bado rais kule.

Mwungano kwanza mambo ya tume yanaweza rekebishika baadaye.
 
Back
Top Bottom